Ndugu yetu, tazama majibu na matusi uliyopewa. Ninaamini kuwa hakuna kosa lisilosameheka, lakini kweli waweza fanya kosa la namna hii na ukaja ukalianika kwenye mtandao? Uaminifu ni hazina, lakini ukishindwa kuwa mwaminifu angalau tumia busara. Yaani hata kumlinda kidogo huyo mr. wako haujaona umuhimu? Katika karne hii mbona hakuna haja ya kwenda nje, tena peku, na kusema ati "tumetoka naye mbali".
Usikubali kuonekana mwanamume anakudai bwana, kwani thamani yako ni kubwa kuliko huto tuvitu alivyokudanganyia navyo. Ulikuwa peke yako, sasa wewe umekua, tena hata una mme, basi uwe na swaga la mtu mwenye mume bwana. Utamlipa hadi lini? mara ngapi?
Pili, ukikosea, pata ushauri kwa faragha, namna hii umedhalilisha wanawake wote. (Hata mimi nimejisikia kuchefukwa na kudhalilika). Tatu, pole sana, utapata mtoto ambaye daima atakukumbusha matendo yako, na hata siku akiumwa ikatakiwa damu, baba akipimwa ili amtolee mtoto, au mambo mengine ya kiafya, sijui utafanyaje. Akiambiwa kwa majibu haya ya damu haiwezekani wewe uwe baba yake, je ndio utakwenda kwa huyo mwizi wako? Utamwambiaje mtoto? kweli ya ngoswe mwachieni ngoswe!
Jibu langu kama daktari: kwa hayo uliyoandika huwezi kuwa na uhakika mtoto ni wa nani. Unaweza kufanya paternity test mtoto akizaliwa. Au, iwapo daktari akijua blood group yako, ya mtoto, ya Mr, na ya yule ndugu, kuna uwezekano wa kutambua kuwa mtoto ni wa nani, iwapo group zao zitakuwa hazifanani.