Singida: Tundu Lissu aongea na Waandishi wa Habari wa Ndani na wa Kimataifa

Singida: Tundu Lissu aongea na Waandishi wa Habari wa Ndani na wa Kimataifa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu ataongea na Waandishi wa Habari huko Singida, Mkutano uliopangwa kufanyika kwenye Ukumbi wa Kanisa Katoliki.

Inatarajiwa Mtikisiko Mkubwa sana kutokea Nchini Tanzania.

Taarifa ya Chama chake iliyosambazwa kote Duniani Hii hapa

Screenshot_2024-11-11-21-56-12-1.png
 
Kesho nitakuwepo hapo. Jamaa mjanja mjana sana kachagua venue neutral 😀😀😀
 
Uchafuzi wa mchakato mzima wa uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 kumeleta kitu kinchoitwa aibu kubwa kwa taifa

Chama dola kongwe pamoja na umri wake mkubwa kilijigamba kuwa makada wake wasimamizi wakuu wakurugenzi maDED na wasimamizi wasaidizi wamekula kiapo cha kutenda haki, lakini kama kesi ya wananchi watatu mwanaharakati Dr. Annanilea Nkya, Buberwa Kaiza mwandishi nguli mkongwe na Bob Chacha Wangwe walivyosema katika kesi kwa niaba yetu raia wote wa Tanzania kuwa serikali ya CCM ina maslahi mgongano.

Pia kuwa TAMISEMI haina utashi, uwezo na nia ya kutenda haki, Bunge la chama kimoja CCM kujiburuza kutunga sheria INEC isimamie uchaguzi wa 2024, na Mahakama ikapinga hoja za raia 3 ikitaka ushahidi kwa kusema tusubiri tuone kwa kuwa imefungwa mikono na sheria za bunge la CCM , lakini Mungu si Athumani mambo hadharani mkwe wa mheshimiwa rais wa Tanzania aliye pia mwenyekiti wa CCM chama dola na TAMISEMI wamevurunda mapema kweupe
 
Samia anajiharibia mwenyewe hana wa kumlaumu heshima yote imeharibiwa na aliowaamini pamoja nayeye mwenyewe kifupi inaonekana 4R ni utapeli tu na huu UCHAGUZI ndio umefanya serikali na ccm kuchukiwa mara dufu ! Speech ya Katibu wa TEC imehuzunisha wengi sana hata wanaoiunga mkono hiyo serikali.
 
Kwanini wasifanyie huo mkutano msikitini?
Ni chama cha wagalatia bwashee
Mapadri na maaskofu wanaikumbatia chadema, mikutano ya chadema yote inafanyika kanisani
Sasa hapo tusemeje zaidi ya kuwa chama cha wagalatia ,
Wakitafutwa wahojiwe wanakimbilia kanisani, misikitini aaaa, halafu mnataka kura za waislamu? Never
 
Back
Top Bottom