Single mother tumeanza kushindwana na kutishiana maisha kisa mwanaye

Ni rahisi kumrekebisha mtoto wako kuliko mtoto wa mtu mwingine. Asikudanganye mtu. Na kama mama yake hayupo kwenye uelekeo wako mtagombana bure tu. Wewe umesoma ukaelewa msimamo au mtizamo wa mama wa mtoto?
 
Ni rahisi kumrekebisha mtoto wako kuliko mtoto wa mtu mwingine. Asikudanganye mtu. Na kama mama yake hayupo kwenye uelekeo wako mtagombana bure tu. Wewe umesoma ukaelewa msimamo au mtizamo wa mama wa mtoto?
Huyo mwanamke hakuwa tayari mwanae kuwa na baba wa kambo na Jamaa hakuwa tayari kuwa baba wa kambo ila walitakana wao na wakalazimisha mambo. Wamefanya sahihi kuachana.
 
Anataka baba wa kambo jukumu lake liwe ni kutoa hela tu mtoto akitaka hiki au kile. Kwenye kunyoosha tabia anaona mtoto wake ananyanyasika ujinga tu
Mimi hata watoto wa ndugu zangu.
Mwanao akae hapa ila atafuata utaratibu wa hapa.
Usinipe mtoto nikae nae kwa kufuata katiba zako.
Kwako halali mchana hapa kwangu atalala.
Kwako hafanyi usafi chumbanj kwake sijui kuosha vyombo hapa atafanya!
kwako humuadhibu akikosea hapa ataadhibiwa.

Hiyo ni likizo!
Na ninawakusanyaga hatari, !
Sembuse mtoto wa partner natakiwa kumlea, ah weeee!
Mtu asitarajie nchi ya maziwa na asali ili usione simpendi.
if by disciplining kids ni kutokuwapenda then wacha iwe, beba mwanao na wewe mwenyewe!
tusichoshane!
 
Kulea mtoto wa mtu mwingine, ni RAHISI tu IWAPO MZAZI ANAKURUHUSU UMLEE KATIKA NJIA IPASAYO!

hakuna mtu mgumu kulea mtoto naye kama mzazi(wa kiume au wa kike) asiyeamini katika your parenting style!
hakiiii nakwambia huwezi!
 
Reactions: Tsh
Kulea mtoto wa mtu mwingine, ni RAHISI tu IWAPO MZAZI ANAKURUHUSU UMLEE KATIKA NJIA IPASAYO!

hakuna mtu mgumu kulea mtoto naye kama mzazi(wa kiume au wa kike) asiyeamini katika your parenting style!
hakiiii nakwambia huwezi!
Na ni ujinga sana wewe una mtoto halafu unaenda kuanzisha mahusiano na mtu ambaye hatamuongoza mwanao katika njia unayoamini kuwa ni sahihi. Tatizo watu wanaingia kwenye mahusiano kwa sababu wanazozijua wao mioyoni mwao ila si familia.
 
Unalea mtoto kwa mapenzi na umama/ubaba hasa anakuja mwenzio '' eti vumilia angekuwa babako yupo hai angekununulia''
mxxxxxxieee!
Mimi ni mwanamke, nimesikia hasira!
Manake anakuona you are less of a man unajua?
Aiseeh hapana
 
Na ni ujinga sana wewe una mtoto halafu unaenda kuanzisha mahusiano na mtu ambaye hatamuongoza mwanao katika njia unayoamini kuwa ni sahihi. Tatizo watu wanaingia kwenye mahusiano kwa sababu wanazozijua wao mioyoni mwao ila si familia.
Kabisa.
Yani ukishakuwa na watoto na huishi na mwenzi uliyezaa nae.
Kigezo cha kwanza kabisa kwa mwenzi anayefuata ni yule
ATAKAYEKUBALI NA KUWEZA KUWA BABA/MAMA kwa watoto wako.
Mengine yanafuata!
kinyume na hapo kila siku itakuwa ni changamoto!
 
Reactions: Tsh
Mtu mpaka aliamua ajifie kuepuka shida ...yeye anaenda kujibebea...
Shida siku hizi tuonaoana kisa utamu wa kitandani tu labda kidogo na mezani.

Kijana akishapewa mapenzi tuu . huyu Sasa ndio mwanamke. Anasahau mambo muhimu kama utulivu wa akili na mawazo, ukarimu, lugha njema, usafi na nidhamu..

Acha tupigike na ujinga
 
Kabisa.
Yani ukishakuwa na watoto na huishi na mwenzi uliyezaa nae.
Kigezo cha kwanza kabisa kwa mwenzi anayefuata ni yule
ATAKAYEKUBALI NA KUWEZA KUWA BABA/MAMA kwa watoto wako.
Mengine yanafuata!
kinyume na hapo kila siku itakuwa ni changamoto!
Kabisa. Usiokoteze okoteze tu ili uonekane una mtu.
 
kweli kabisa.
Ubaya hata hizo values zenyewe za kutizama in a partner ili awe a spouse watu hawazijui.
mradi ana hips na bmw na analipa kodi yake. ah huyu mume /mke tayari.
Kumbe kuna watu hata namna ya kutoa sahani mezani ni tatizo!
Sijui tunakuza aina ipi ya wanadamu!
 
Nimesoma nimegundua bibi yake huyo mtoto anajua kulea sana. Changamoto huyo demu wako

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
Huyo mwanamke hata asingekuwa na mtoto jamaa huenda wangesumbuana.

Huyo mwanamke anahitaji mwanaume mwenye uzoefu na maisha sio kijana anayeanza kuijenga kesho yake. Wote watatumia mihemko tu kwenye maamuzi.
 
Naona kijana utam wa bed haumzuzui ila wengi mauno yanawachanganya mpaka wanafanyiwa mambo ya hovyo na aibu na hawaoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…