Sintofahamu kuhusu hali ya Wanajeshi Wetu DRC: Ni muhimu ifanyike Cabinet Reshuffle haraka sana.

Sintofahamu kuhusu hali ya Wanajeshi Wetu DRC: Ni muhimu ifanyike Cabinet Reshuffle haraka sana.

Katika reshuffle hiyo....
Waziri wa ulinzi abaki yule mama...naibu Waziri ulinzi Apewe Juliana Shonza, Mkuu wa Majeshi apewe yule ADC/Mpambe wa mama, IGP mwanamke , DGIS/Mkurugenzi usalama apewe yule mama Afisa kipenyo ambaye ni katibu wa bunge, yaani safu yote pale juu wawaweke wanawake ..halafu waanze vita ..wawachambeer m23 mpaka wafweeee.....
hahahaaaaa serikali ya wanawake, aisee kama nchi tuko pabaya kwa kweli na kikwete anafurahia kwa kutoa ushauri eth samia agombee tena sielewi ana nia gani aisee! Tunadhalilishwa na nchi kama rwanda? Watanzania roho inauma jk please fanya mabadiliko tunakuomba.
 
Sawa, sikukatalii. Mimi mwenyewe napenda sana uwazi.

Lakini bado hujaelewa point yangu.

Unategemea vipi mabadiliko ya kutoa habari zaidi yaje kwa kumbadilisha waziri wakati tatizo ni kuwa na serikali ambayo kwa makusudi kabisa inafanya usiri?

Huoni kwamba ikiwa ni kweli serikali inataka usiri, hili si tatizo la waziri wa sasa, na hata ukimbadilisha, huyo mwingine mpya itambidi afanye kazi kwa usiri huo huo, na hivyo zoezi lako la kutaka waziri abadilishwe litakuwa halina maana?

Huoni kwamba unajaribu kutibu dalili ya ugonjwa wa Kifua Kikuu ya kukohoa kwa kumpa mgonjwa dawa ya kupooza kikohozi ya Cofta, wakati hujatibu igonjwa wenyewe wa Kifua Kikuu, na kwa hivyo, dalili ya kikohozi itaendelea tu, kwa sababu ugonjwa wa msingi haujatibiwa?

Wewe unafikiri kweli hawa mawaziri ndio wanaamua watoe habari au wasitoe?
Kwa uelewa wangu. Mawaziri ndo washauri wakuu wa mamlaka.

Waziri anapaswa kuwa mtu mwenye uelewa mkubwa sana na maarifa makubwa sana na sekta anayoiongoza na changamoto zake hivyo kuweza kushauri ipasavyo a best way forward hasa kwenye crisis.

Kinachoendelea saivi inamaanisha kuwa something is wrong somewhere. It's either we are compromised or we don't have competent people huko juu!

SADC/ EAC/ AU have proved that they have failed to manage the Congo crisis. So we need people who can think and decide correctly. Ubaya wa haya yanayoendelea, Kagame anazidi kutengeneza kutengeneza kukubalika kwa hoja zake! Anazidi kutengeneza relevancy kwake na kuondoa relevancy ya hoja zetu. Matokeo ya hiki sio mazuri huko mbeleni.
 
Basi tutakuwa tuna tatizo kubwa kuliko tunavyodhani. We are compromised and fucked up!

But Why CDF asisimame kumwambia ukweli Rais?
Si alishamwambia mchana kweupeeee.... Kuwa Kuna viongozi wengi sana sio raia katika Serikali....aseme mara ngapi Mkuu...
 
Hapa at least umeongea jambo. ila pale nyuma ulikengeuka.

Nakubaliana na wewe kuwa something must be done either na wananchi or vyombo vya usalama against CCM.

Kwa upande wa Wananchi ni ngumu ila kwa upande wa vyombo vya ulinzi na usalama uwezo huo wanao. Ni kufanya maamuzi magumu tu kwa maslahi ya Taifa.
Hakuna chombo cha ulinzi na usalama kinachoweza kufanya hicho unachokishauri kifanye hakipo... Wao wakae tu wasubiri Chadema wakiamdaa maandamano waingie barabarani kufanya usafi na mazoezi ya utayari .Hilo wanaweza vizuri sana ...lakini unalotaka walifanye kamwe hawawezi
 
hahahaaaaa serikali ya wanawake, aisee kama nchi tuko pabaya kwa kweli na kikwete anafurahia kwa kutoa ushauri eth samia agombee tena sielewi ana nia gani aisee! Tunadhalilishwa na nchi kama rwanda? Watanzania roho inauma jk please fanya mabadiliko tunakuomba.
Wakati mwenzako JK ndio anazidi kumwaga maganda ya ndizi Ili aendelee kuteleza bila mkwamo .....
 
Kizazi hiki uzembe umetuzidi. Ya mwaka 1964 makubwa sana kwa huyu. Huyu alikuwa wa kuambiwa tu akiwa nyumbani kwake kuwa kuanzia sasa wewe siyo rais (kama alivyofanyiwa Mugabe).
Kafulila aliwahi sema inawezekana tukawa na kizazi bora makabulini kuliko tulichonaso sasa.
 
Kafulila aliwahi sema inawezekana tukawa na kizazi bora makabulini kuliko tulichonaso sasa.
Kafulila alikuwa sahihi sana. Nyerere alipokuwa akifundisha pale Pugu akiwa ofisi moja na wazungu huku akiwa anamiliki baiskeli, ingelikuwa ndiyo kizazi hiki angeanza kuwalingishia wenzake na kuwa chawa wa wazungu. Lkn Nyerere alipambana na mfumo kandamizi wa wazungu kwa maslahi mapana ya taifa lake.

Kumbuka miaka ya 1960, mzungu alifananishwa na Mungu. Na kumiliki baiskeli ni sawa na kumiliki BMW miaka hii.
 
Kwa uelewa wangu. Mawaziri ndo washauri wakuu wa mamlaka.

Waziri anapaswa kuwa mtu mwenye uelewa mkubwa sana na maarifa makubwa sana na sekta anayoiongoza na changamoto zake hivyo kuweza kushauri ipasavyo a best way forward hasa kwenye crisis.

Kinachoendelea saivi inamaanisha kuwa something is wrong somewhere. It's either we are compromised or we don't have competent people huko juu!

SADC/ EAC/ AU have proved that they have failed to manage the Congo crisis. So we need people who can think and decide correctly. Ubaya wa haya yanayoendelea, Kagame anazidi kutengeneza kutengeneza kukubalika kwa hoja zake! Anazidi kutengeneza relevancy kwake na kuondoa relevancy ya hoja zetu. Matokeo ya hiki sio mazuri huko mbeleni.
Waziri hawezi kushauri lolote kwenye suala la serikali kuacha kuwa na utamaduni wa usiri.

Mpaka mtu kuwa Waziri maana yake ashausoma mchezo na kujua sheria zake, moja ya sheria ni kutoshauri kitu ambacho hakikubaliki na kinaweza kukuondoa kwenye uwaziri.

Hujasikia Waziri wa Elimu analalamika anabaniwa hata kupata muda wa kuongea na rais tu?

Haya mambo mengine hata rais Samia hawezi kubadilisha kirahisi ni utamaduni uliojengwa kwa miaka na miaka.

Inaonekana unavyofikiri serikali inafanya kazi na jinsi serikali inavyofanya kazi ni vitu viwili tofauti.

Unategemea vipi Waziri abadilishe suala lililojengeka kiutamaduni kwa miaka na miaka?

Kuna watu wameanzisha online archive za Dr. Salim Ahmed Salim. Walikuwa wanataka kuziweka nyaraka za kawaida kabisa za Dr. Salim alivyokuwa anafanya kazi. Walipata tabu sana kwa sababu serikali ya Tanzania ina over classify kila kitu, halafu haina utamaduni wa ku declassify hata baada ya miaka mingi sana.

Hili ni suala la utamaduni wa serikali, si suala la kubadilishwa na waziri.

 
..tatizo ni uwezo mdogo wa Mama Abduli.

..hakuwahi kufikiria, na hakuna mtu alikuwa anamfikiria, kuwa atakuwa Raisi.

..ameshabadilisha wakurugenzi wa Tiss watatu, mnataka ambadilishe na aliyeko sasa hivi?
Sasa anataka kukuthibitishia, baada ya hiyo October 2025 kwamba haya yote uyaandikayo wewe hapa hayana ukweli wowote (bila kujali jinsi gani itakayo muwezesha kubaki madarakani).

"... kubadilisha wakurugenzi", na wengi wengine alio wapanga wamsafishie yeye njia badala ya kusaidia nchi, ndio mkakati muhimu ulio mhakikishia maslahi yake na ndiyo njia itakayo hakikisha anaendelea kuwepo kutawala.
 
Hadi sasa kuna taarifa kinzani kuhusu hali za Wanajeshi wetu waliopo nchini Congo (DRC).

Hadi sasa ni nchi ya Afrika Kusini tu inayotoa status kwa wananchi wake kuhusu hali ya wapiganaji wao waliopo nchini humo.

Juzi Media za Kimataifa zilisema kuhusu Wanajeshi wa Tanzania, Malawi na Afrika Kusini waliojeruhiwa kurudishwa makwao ambapo walikwama kwa saa kadhaa nchini Rwanda.

Wakati Media za Afrika Kusini zikiwataarifu wananchi kuhusu wapiganaji wao majeruhi kurudi nyumbani hali imekuwa tofauti hapa nyumbani. Hadi sasa hatujui kama Wapiganaji wetu wamerudi nyumbani au la. Hadi sasa hatufahamu kama majeruhi wetu walifika salama au bado wamekwama Rwanda. Hadi sasa hatufahamu vikosi vyetu vilivyopo nchini DRC vipo kwenye hali gani?

Tofauti na inavyotokea siku zote ambapo wananchi huwa tunapewa taarifa kuhusu Wanajeshi wetu tunaowapenda sana, kwa sasa hatupewi taarifa hizo.

Kutokupata taarifa sahihi kumezidi kumpa kichwa Kagame na vyombo vyake vya propaganda vilivyojaa kwenye social media mbalimbali ambao wamekuwa wakisambaza taarifa za kutekwa kwa Wanajeshi wetu.

Kutokana na Nchi yetu kuwa kimya sana, hii inaweza kutafsiriwa kuwa kwa sasa tumemezwa na Kagame na kuwa kama watumwa wake. Hii inaweza kutafsiriwa kuwa kwenye nafasi za juu hatuna watu competent wanaoweza ku counter propaganda machinery ya Rwanda iliyofanikiwa kuwa chanzo pekee cha taarifa ya yanayotokea Mashariki mwa Congo.

Kwangu mimi hali hii naitafsiri kama incompetence kwa waliopo Serikalini sasa kudeal na Kagame na watu wake.

Ili kurekebisha haya. Napendekeza yafuatayo:

1. Yafanyike Mabadiliko ya Baraza la Mawaziri ambapo Waziri wa Ulinzi abadilishwe. Achukuliwe Mwanasiasa Mzoefu ikiwemo aliyeserve na kustaafu Jeshini mwenye uzoefu na vita pamoja na propaganda ateuliwe kuwa Waziri wa Ulinzi.- Hapa tuna kina Kanali Kinana, Simbakalia na Wengineo.

2. Kutokana na udharula warudishwe retired competent TPDF Officers kuhandle hii crisis. Kwenye hili nasita kupendekeza Mabadiliko ya CDF ila ikiwezekana ateuliwe mzoefu na competent mmoja (Either retired Ganeral au Retired Leuternant General kuwa CDF). Kwenye hili hata Trump amefanya juzi kwa kumteua Retired Luteni Generali kuwa CDF. Kwa haraka sana hapa napendekeza Mella, Makakala na Mwakibolwa wafikiriwe ili kuhande this crisis.

3. Yafanyike mabadiliko ya DGIS. Ikiwezekana ateuliwe yule aliyemgomea Magufuli kumpa Taarifa za Kiusalama mbele ya Waandishi wa habari kipindi Magufuli alipofanyq ziara Airport ( Nadhani jina lake Madafa) kuwa DGIS.



Lord denning
Dubai.
Wanajeshi wetu warudi
 
Basi tutakuwa tuna tatizo kubwa kuliko tunavyodhani. We are compromised and fucked up!

But Why CDF asisimame kumwambia ukweli Rais?
Unasahau Raisi ana nguvu ya kuteuwa,na baada ya kukupiga chini anatuma chawa wake wakutukane na kukuaribia CV kwa jamii mpaka uonekane si chochote kabisa
 
Nimeona leo kwenye taarifa ya Habari ya Azam TV , CDF ametembelea familia ya mwanajeshi aliyeuwawa Congo na kusema alishaagwa tangu tarehe 13 Februari 2025.

Hongera CDF kwa kuanza kuchukua hatua. Hii ndo namna Jeshi letu shupavu linapaswa kufanya kazi na sio kuwa kimya kwenye mambo haya hadi propagandist wa Rwanda wanawachafua kwenye mitandao na tunashindwa kuelewa kipi ni kipi.
 
Back
Top Bottom