Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

Google mzee au nenda wizara ya mambo ya nje kaulizie ila jua tu alikuwa mmama jina lake sitaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uhalisia ndo ulikuwa huo ila vinena zinaacha zinaongoza chumvi nyingiiiii ila mauji ilikuwa kama tu po jahanamu vile.
Hii story kama sinema vile kila hatua inaleta hamu ya kujua ya mbeleni.

Kuna CD jina nimesahau inaelezea mauaji ya watutsi daah baba mmoja mhutu akapoteza mke na watoto kisa mke ni mtutsi

Wanafunzi wakachapwa risasi darasa zima kisa watutsi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda alikuwa akiongea na mbobezi wa nchi ya Rwanda wa wakati huo yaani waziri wa mambo ya nchi za nje kumlalamikia kile wanachokifanya watu wake kwenye ubalozi wa Tanzania.
Baadae nilikuja gundua kuwa alikuwa anaongea na mkuu wa interahamwe ( jina lake nimelisahau jamaa babe liuaji hatari sijui kama bado lipo hai, kama bado yupo hai hajasakwa na kufikishwa ICC basi haina haja ya kuendelea kuwahukumu wengine) ila jamaa hilo ndo lilikuwa kama Li-mkuu la majeshi kigali nzima huyo ndo top akisema ua umekwisha akisema acha umepona, unajua mabalozi lazima wawe na koneksheni kubwa sanaa wakati mwingine kwa upande wa serikali, waasi (kama wapo) na wapinzani. Mtakufa wote lakini balozi atapona, atalindwa atasindikizwa na kuwekwa sehemu salama. Nyinyi mnahenyeka tuu na vipassport vyenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hapo uliposema wadada wa kitutsi walivokimbilia ubalozi wetu nimekumbuka nilihadithiwa ubalozi pale ulipo tayari inatambulika kama vile ni sehemu ya ile nchi iko pale, hata inapotokea tatizo ukikimbilia pale basi umeingia nchi nyingine
 
umemaliza udbs wewe?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inawezekana unachosema coz kuna watu hawapendi kusikia ukweli huu kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Humu kuna wasomali (anaebisha huwa hao wasomali wanaongea hadi hicho kisomali humu) ,kuna Warundi, Wanyarwanda etc mataifa yanayoongea kiswahili wamo humu

Kigoma wahutu ni wengi lazima wawatetee wahutu wenzao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jifunze kuandika mkuu, mwandiko wako unatia aibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naungana na wewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wahutu mpo wengi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mhutu kama sio interahamwe huyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bossless usimalize story mapema maana kipindi hiki Cha Kwaresma tumeachana na uzi wa kula tunda kimasihara. Kipindi hicho ukiwa mkoa wa Kagera ndege zilipishana angani kama daladala. Baadae ilianzishwa kambi ya Burigi na mpaka leo bado watusi masalia wapo.
 
Inaendelea.....

Niwakumbushe tu kuwa tayari nimeshazitaja dalili mbili za kuingia kwenye machafuko rasmi sasa twende na dalili ya mwisho ambayo KUOGOPANA.

KUOGOPANA, hii maanake nini? Iko hivi ukiona yule jirani au majirani mnaanza kuogopana yani kila mtu yupo kivyake ujue sasa hali imefika mwisho kilichobaki ni kila mtu kumuwahi mwenzake ili abaki salama yeye hakuna namna.sasa hapo naomba nizungumzie jambo kabla sijaendelea.vita vya ukabila vikawa vimekufa rasmi ikaibuka vita nyingine mbaya ya njaa hapo tena ikawa haangaliwi mtusi au mhutu .ukiwa na chochote hata gunia la sembe la Kilo kumi watu wakajua utake usitake utatoa tu mgawane hapo ndo iliibuka dhana ya kuogapana yani ukija kwangu utajua na nini? Ukitoka unaenda kuwaambia wengine usiku mnanivamia mnachukua chakula ukileta ubishi mapanga ni halali yako.

Watu wakawa hawaaminiani tena siku zikawa inasonga kila mtu kivyake hakuna ujamaa wala undugu kila mtu la kwake ,maduka yakavunvwa wakapora vitu mji mzima chakula kikageuka kuwa almasi, watu wakaanza kuchunguzana kwa siri ukiwa na chakula upo hatarini kupotea au kuuawa kabisa tena na majirani hao njaaaa.....ikachukua nafasi si kwa wenyeji au wageni vita mipakani inaendelea unachinja kuku unamla siku 4 ,ana chacha wala husikii harufu ya kuchacha mambo yanazidi kuwa mabaya zaidi mpaka ikawa imefikia mwezi wa pili mwishoni 1994 sasa kila kitu kikawa wazi kuwa rwanda imebakia sekundi izame. propaganda zilipungua redioni wale wasemaji wasemaji wakawa hawasikiki tena mambo yanakwenda mrama(wameshakimbia) kigali inabaki tupu wale magwii wa siasa za propaganda wakapotea ghafla redio siku nzima inapiga muziki wa chama.

Watumishi wote tukaamriwa tureport ubarozini hakuna kutoka nilichukua begi langu hadi ubalozini nikawa sikumbuki tena mapenzi yangu na yule binti maanake nini tupo hatua mbaya na ya mwisho ya uharibifu hapo hakuna unachokifiria zaidi ya nafsi yako pekee unawaza unatoka aje salama hapo.

Kufika ubalozini nikakuta watu kibao (watanzania) waloikuwa rwanda aise watu wamejazana halafu eneo dogo ukiangalia wengine wamekuja na wake zao wakitisu kabisa na watoto wao Watusi pure aise
Nikajisemea leo balaa tusipouwa basi ,balozi akawa kama kapigwa na ganzi akiwaangalia wale watu ikawa ni kujieleza kila moja na watu wake hiyo ndo ikawa kazi yetu tunawahojimtu na mkewe. Daahh

Hesabu ikaonyesha kuwa watanzania tupo kiasi ila watoto na akina mama ambao ndo wengi halafu haiba yao ya kitusi pure ikaja tunafanya aje? Tuwafukuze au tufanyeje tukampa taarifa rasmi balozi yeye akawa yupo ofisini anaongea na watu kwa sauti ya chinichini sanaa tukawa hatuelewi tukawa tumekaa tu yeye yupo ofisini. Sasa angalia cha ajabu.

Kulikuwa kuna walinzi wawili pale getini wa kampuni ya pale pale kigali ghafla bila kutarajia jamaa wakayeyuka ghafla haijulikani walienda wapi? hiyo wasiwasi wangu walihofia ile hali sasa tukabaki hatuna ulinzi geti jeupeeeeee....yani unajiingilia tu.

Kufika midaa kama saa kumi na mbili ikaja landrover(defenda)nyeupe ikiwa na tinted full ikapaki getini ilionekana kama imetokea safari, balozi akatoka akawapokea hao jamaa, mapande ya majitu yaliyoshiba yamejazia vizuri kabisa walikuwa 7 wakashuka na maboksi flani hawakutaka mtu yeyote awasaidie kushusha wakawa wameingia ndani sasa kukawa kuna Mazungumzo yanaendelea hatukuja nini kinaendelea. Usiku ukafika tukalala kuamka asubuhi hatukiwaona tena hao jamaa ikawa sasa kila mtu na hisia zake, ila kuna mfanyakazi akawa anasema amesikia ndani wanaongea kiswahili. Sasa ntaelezea baadae ni akina nani hao na tulikutana tena boda ya burundi na rwanda wakiwa full ..........


Itaendelea..... Jioni.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Okay... Tukutane jioni mzee baba.
Imeishia patamu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…