Kizzy Wizzy
JF-Expert Member
- Aug 2, 2013
- 3,280
- 3,789
Kwanini ulimtelekeza mpenzi wako jamani, inaniskitishaa... ungejitahidi kuangalia namna ya kumuokoa.
Maskini sijui kama alipona.
Sent using Jamii Forums mobile app
Maskini sijui kama alipona.
Inaendelea.....
Niwakumbushe tu kuwa tayari nimeshazitaja dalili mbili za kuingia kwenye machafuko rasmi sasa twende na dalili ya mwisho ambayo KUOGOPANA.
KUOGOPANA, hii maanake nini? Iko hivi ukiona yule jirani au majirani mnaanza kuogopana yani kila mtu yupo kivyake ujue sasa hali imefika mwisho kilichobaki ni kila mtu kumuwahi mwenzake ili abaki salama yeye hakuna namna.sasa hapo naomba nizungumzie jambo kabla sijaendelea.vita vya ukabila vikawa vimekufa rasmi ikaibuka vita nyingine mbaya ya njaa hapo tena ikawa haangaliwi mtusi au mhutu .ukiwa na chochote hata gunia la sembe la Kilo kumi watu wakajua utake usitake utatoa tu mgawane hapo ndo iliibuka dhana ya kuogapana yani ukija kwangu utajua na nini? Ukitoka unaenda kuwaambia wengine usiku mnanivamia mnachukua chakula ukileta ubishi mapanga ni halali yako.
Watu wakawa hawaaminiani tena siku zikawa inasonga kila mtu kivyake hakuna ujamaa wala undugu kila mtu la kwake ,maduka yakavunvwa wakapora vitu mji mzima chakula kikageuka kuwa almasi, watu wakaanza kuchunguzana kwa siri ukiwa na chakula upo hatarini kupotea au kuuawa kabisa tena na majirani hao njaaaa.....ikachukua nafasi si kwa wenyeji au wageni vita mipakani inaendelea unachinja kuku unamla siku 4 ,ana chacha wala husikii harufu ya kuchacha mambo yanazidi kuwa mabaya zaidi mpaka ikawa imefikia mwezi wa pili mwishoni 1994 sasa kila kitu kikawa wazi kuwa rwanda imebakia sekundi izame. propaganda zilipungua redioni wale wasemaji wasemaji wakawa hawasikiki tena mambo yanakwenda mrama(wameshakimbia) kigali inabaki tupu wale magwii wa siasa za propaganda wakapotea ghafla redio siku nzima inapiga muziki wa chama.
Watumishi wote tukaamriwa tureport ubarozini hakuna kutoka nilichukua begi langu hadi ubalozini nikawa sikumbuki tena mapenzi yangu na yule binti maanake nini tupo hatua mbaya na ya mwisho ya uharibifu hapo hakuna unachokifiria zaidi ya nafsi yako pekee unawaza unatoka aje salama hapo.
Kufika ubalozini nikakuta watu kibao (watanzania) waloikuwa rwanda aise watu wamejazana halafu eneo dogo ukiangalia wengine wamekuja na wake zao wakitisu kabisa na watoto wao Watusi pure aise
Nikajisemea leo balaa tusipouwa basi ,balozi akawa kama kapigwa na ganzi akiwaangalia wale watu ikawa ni kujieleza kila moja na watu wake hiyo ndo ikawa kazi yetu tunawahojimtu na mkewe. Daahh
Hesabu ikaonyesha kuwa watanzania tupo kiasi ila watoto na akina mama ambao ndo wengi halafu haiba yao ya kitusi pure ikaja tunafanya aje? Tuwafukuze au tufanyeje tukampa taarifa rasmi balozi yeye akawa yupo ofisini anaongea na watu kwa sauti ya chinichini sanaa tukawa hatuelewi tukawa tumekaa tu yeye yupo ofisini. Sasa angalia cha ajabu.
Kulikuwa kuna walinzi wawili pale getini wa kampuni ya pale pale kigali ghafla bila kutarajia jamaa wakayeyuka ghafla haijulikani walienda wapi? hiyo wasiwasi wangu walihofia ile hali sasa tukabaki hatuna ulinzi geti jeupeeeeee....yani unajiingilia tu.
Kufika midaa kama saa kumi na mbili ikaja landrover(defenda)nyeupe ikiwa na tinted full ikapaki getini ilionekana kama imetokea safari, balozi akatoka akawapokea hao jamaa, mapande ya majitu yaliyoshiba yamejazia vizuri kabisa walikuwa 7 wakashuka na maboksi flani hawakutaka mtu yeyote awasaidie kushusha wakawa wameingia ndani sasa kukawa kuna Mazungumzo yanaendelea hatukuja nini kinaendelea. Usiku ukafika tukalala kuamka asubuhi hatukiwaona tena hao jamaa ikawa sasa kila mtu na hisia zake, ila kuna mfanyakazi akawa anasema amesikia ndani wanaongea kiswahili. Sasa ntaelezea baadae ni akina nani hao na tulikutana tena boda ya burundi na rwanda wakiwa full ..........
Itaendelea..... Jioni.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app