Sintosahau nilichokishuhudia kwa macho yangu nchini Rwanda wakati wa vita vya kikabila 1994 hadi naingia kaburini

😀 😀 😀 😀 😀
Jf kuna watu wamepinda, eti atawakuta njiani. Na wamembembeleza amekubali, atakuja kuendeleza mlipoishia.
 
Mkuu kwa mitihani uliyopitia najua hauwezi kubabaishwa na kelele za watu wenye kashfa hapa jukwaani, najua yale uliyoyaona maana binafsi nimetembelea sana hizo nchi Rwanda,Burundi na Congo, hakika wewe ni mwanaume unapaswa kupuuzia vitu vidogo kama hivi.

Leta stori mkuu
 
Shida ya watu wengi wanatabia ya kujiona special na wanahitaji kubembelezwa...

Anyways, hongera kwa kubadilika. Upinzani upo sehemu zote na kwa kila kitu na mtu.

Hata ukiwa mwenyewe kuna muda unakuwa unajipinga baadhi ya vitu.

Usiwe na soft heart Mkuu.
 
Ulitaka uingie ahera!!? Kaburini utalalaa ti
 
Kwa watu wengine ile tu kushuhudia yale mauaji ya kutisha kwa macho ingetosha kabisa kuwapa ujasiri wa kuhimili vishindo vya dharau, matusi, njaa, kukatishwa tamaa n.k. Mleta mada kwa yale mauaji aliyoshuhudia hakupaswa kuwa mtu wa kukatishwa tamaa kirahisi rahisi. Ila ni maamuzi yake binafsi japo stori ilikuwa nzuri na yenye mwelekeo wa kusisimua sana.
 
umeandika vizuri hili zoezi lako la kuandika riwaya umepasi.
 
Unaongelea Rwanda ya mwaka gani? Tuanzie hapo? Halafu ntakujibu wakati unatoka Boda kwa miaka hiyo ya 1989 kulikuwa kuna vizuizi zaidi ya 50 kila kilometer 10 ...mnakuta barrier mnasachiwa kuanzia mabegi hadi buti ya gari. Kwa kukumbusha kipindi hicho ndo vuguvugu LA uvamizi lilikuwa limeanza kukawa kuna mashambulizi madogo madogo yapa na pale kutoka kwa waasi. Ntakupa mfano mdogo kama wewe. Ni msafiri kweli hebu niambie kutoka kasubalesa to Lubumbashi kuna berrier ngapi? Unajua kwanini? Waasi baba serikali haimini MTU tena ndivyo Rwanda ilivyokuwa miaka hiyo sasa unahisi utafika kwa hayo Masaa yako matatu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu mzee anatuangusha wazee wa rika lake!..

Hivi miaka 55 ndio sababu ya kumfanya mzee aliyekwepa mishale mingi kuondoshwa kwenye reli ya mada aliyoishuhudia kwa macho yake? tena kataka mwenyewe kutushirikisha bila ya mtu kumlazimisha... 😳 Mimi siamini utetezi wake huu, labda tatizo ni kifaa anachotumia hakina uwezo mkubwa au sio chake.

Naishauri JF au hata ndugu yetu Paschal Mayalla wainunue simulizi hii kisha ichapishwe kama makala hapa JF au majarida mengine... Hii habari ya ITAENDELEA mara sitaki tena kuendeleza simulizi ni utoto ukubwani unaopaswa kuadhibiwa na uongozi wa jukwaa hili.😡
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…