Sio JF pekee itakuunganisha na mwanamke jaribu na nja hii..

Sio JF pekee itakuunganisha na mwanamke jaribu na nja hii..

Huyo simtaki .wazee Wana matatizo mengi
😂😂😂😂😂😂wakukuletea ni huyo link😂😂😂😂😂😂chagua hadi ujichagulie😂😂😂😂wengine tuna nuksi ya kukutana nao wanamiliki wasiojulikana nyingi
 
Hahahaha!
Click tu ujionee mkuu.
Inawezekana tunakacha vitu vizuri pasipo kujua.
Link za NGO na Charity organisation😂😂😂Hakawii kukumbilia click yangu😂😂😂Nilitumia tumbo kuclick
 
Tunawatakia ndio Njema Shetani akijiinua tutakuja kumuaga

Jinsi ya Kufanikiwa Katika Ndoa ya Kikristo​


“Kila mtu mmoja-mmoja kati yenu na ampende hivyo mke wake kama vile anavyojipenda mwenyewe; . . . mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.”—EFE. 5:33.
NYIMBO: 87, 3

UNGEJIBUJE?​

  • Mungu aliwapa waume na wake majukumu gani?
  • Kwa nini upendo na wororo ni muhimu sana katika ndoa?
  • Biblia inaweza kutoa msaada gani ikiwa kuna matatizo katika ndoa?
1. Ingawa ndoa huwa na furaha mwanzoni, wale wanaofunga ndoa wanapaswa kutarajia nini? (Tazama picha mwanzoni mwa makala hii.)
BIBI-ARUSI mrembo anaposimama kando ya bwana-arusi mtanashati siku yao ya arusi, wao huwa na furaha isiyo na kifani. Wakati wa uchumba, upendo wao ulikua sana hivi kwamba sasa wako tayari kuweka nadhiri kuwa watakuwa waaminifu katika ndoa yao. Bila shaka, wanahitaji kufanya mabadiliko kwa kuwa wameunganisha maisha yao na kuanzisha familia mpya. Lakini Neno la Mungu linatoa ushauri wenye hekima kwa wote wanaotaka kufunga ndoa, kwa kuwa Mwanzilishi wa ndoa mwenye upendo anataka zifanikiwe na ziwe na furaha. (Met. 18:22) Hata hivyo, Maandiko yanatuambia wazi kwamba wanadamu wasio wakamilifu wanaofunga ndoa “watakuwa na dhiki katika mwili wao.” (1 Kor. 7:28) Dhiki hiyo inaweza kupunguzwa jinsi gani? Ni nini kitakachofanya ndoa za Wakristo zifanikiwe?
2. Wenzi wa ndoa wanapaswa kuonyeshana aina zipi za upendo?
2 Biblia inakazia umuhimu wa upendo. Upendo mwororo (Kigiriki, phi·liʹa) unahitajika katika ndoa. Upendo wa kimahaba (eʹros) huleta raha, na upendo kuelekea watu wa familia (stor·geʹ) ni muhimu watoto wanapozaliwa. Hata hivyo, upendo unaoongozwa na kanuni (a·gaʹpe) ndio unaofanikisha ndoa. Mtume Paulo aliandika hivi kuhusu upendo huo: “Kila mtu mmoja-mmoja kati yenu na ampende hivyo mke wake kama vile anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.”—Efe. 5:33.

WENZI WA NDOA WANA MAJUKUMU GANI HASA?​

3. Upendo unapaswa kuwa wenye nguvu kadiri gani katika ndoa?
3 Paulo aliandika hivi: “Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu, kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake.” (Efe. 5:25) Kuiga mfano wa Yesu kunamaanisha kwamba wanafunzi wake wanapaswa kupendana kama alivyowapenda. (Soma Yohana 13:34, 35; 15:12, 13.) Hivyo, wenzi wa ndoa Wakristo wanapaswa kupendana sana hivi kwamba kila mmoja wao awe tayari kufa kwa ajili ya mwenzake hali ikilazimu. Lakini huenda ikawa vigumu kufanya hivyo matatizo makubwa ya kutoelewana yanapotokea. Hata hivyo, upendo wa a·gaʹpe “huhimili mambo yote, huamini mambo yote, hutumaini mambo yote, huvumilia mambo yote.” Naam, “upendo haushindwi kamwe.” (1 Kor. 13:7, 8) Wenzi wa ndoa wanaomwogopa Mungu wakikumbuka nadhiri walizotoa kwamba watapendana na kuwa waaminifu katika ndoa, watajitahidi kufuata kanuni bora za Yehova kutatua matatizo yoyote yanayoweza kutokea.
4, 5. (a) Mume ana jukumu gani akiwa kichwa cha familia? (b) Mke anapaswa kuuonaje ukichwa? (c) Wenzi fulani wa ndoa walihitaji kufanya mabadiliko gani?
4 Paulo aliandika hivi kuhusu majukumu ya kila mwenzi wa ndoa: “Wake na wajitiishe kwa waume zao kama kwa Bwana, kwa sababu mume ni kichwa cha mke wake kama vile Kristo pia alivyo kichwa cha kutaniko.” (Efe. 5:22, 23) Mpango huo haumfanyi mke awe duni kuliko mume wake. Badala yake, unamsaidia kutimiza jukumu ambalo Mungu alikuwa nalo kuelekea mke, aliposema hivi: “Si vema huyo mwanamume [Adamu] aendelee kuwa peke yake. Nitamfanyia msaidizi, awe kikamilisho chake.” (Mwa. 2:18) Mume Mkristo anapaswa kutumia ukichwa wake kwa upendo jinsi ambavyo Kristo, “kichwa cha kutaniko,” anaonyesha upendo. Anapofanya hivyo, mke wake anahisi salama na anafurahia kumwonyesha heshima, kumuunga mkono, na kujitiisha.
5 Cathy [1] anakiri kwamba lazima ufanye mabadiliko unapofunga ndoa. Anasema hivi: “Nilipokuwa mseja, nilijitegemea na nilijitimizia mahitaji yangu. Nilihitaji kufanya mabadiliko baada ya kuolewa kwa kuwa nilijifunza kumtegemea mume wangu. Haijawa rahisi sikuzote, lakini kuishi kulingana na kanuni za Yehova kumetusaidia kuwa na uhusiano wa karibu zaidi.” Mume wake anayeitwa Fred, anasema hivi: “Haijawahi kuwa rahisi kwangu kufanya maamuzi. Na katika ndoa, inakuwa vigumu hata zaidi unapohitaji kufanya maamuzi yanayohusu watu wawili. Lakini ninapotafuta mwongozo wa Yehova kwa kusali na kusikiliza kwa makini mapendekezo ya mke wangu, inakuwa rahisi zaidi. Ninahisi kwamba kwa kweli tunakamilishana!”
 
Back
Top Bottom