Nimeusikiliza wimbo wa Mwanza uliofungiwa na basata kwa Makini na nikafuatalia mashairi yake moja baada ya jingine kwa ukweli sijaona mahali penye kosa.!
Wimbo huu unaanza na kibwagizo kinachosifia moja kati ya maeneo ya Jiji la Mwanza Nchini Tanzania. "Nyegezi" na msanii huyu anaimba kwa madaha akijivunia kwao Mwanza " Nyegezi"! Akiimba kwa kukatisha "Nyege Nyegeee kwetu Mwanza Nyegezi "...
Beti la kwanza pamoja na maneno mengine anasema anaogopa "Central mambo ya Amber ruty" bila shaka akiwa anamaanisha anaheshimu sheria kwa mambo yaliyo kinyume na jamii...
Ukiendelea mbele sioni tatizo la kimashairi la wimbo huu. Kwa kazi ya sanaa.
Labda Basata watuambie kuwa Neno "Nyegezi" ni tusi kwa kiswahili
Na kwa maana hiyo ikitokea mtu kaimba. Kima.. kimaa akimaanisha " kimara" Dar es salaam ni tusi, vivyo akiima Tundu.. tunduu akimaanisha Tunduma mkoa wa Songwe naye tumfungie..
Mwisho ninachokiona ni chuki binafsi ama wivu usio kuwa na tija kwa baadhi ya wasanii. Mfano kuna sehemu Bwana mwingereza amenukuliwa na Global online Tv akisema "Yeye Diamond ni nani?".......
Kwa kauli hii tu inaonesha kuna namna ya ushindani wa kimamlaka pale mmoja anapotaka kuonesha nguvu yake ya kimamlaka.!
BASATA wangefungia pia Nyimbo kama "Mtalimbo umelala dolo" au " Mhogo wa Jang'ombe" ama "huo mtende wachanua"
Ama kachili kachili . Na nyinginezo nyingi ambazo zilikuwa na ujumbe mkali na wenye kuhamasisha ngono.
Nadiriki kusema BASATA mna nia ovu kwa msanuu huyu. Sio kuwa mnatimiza sheria la hasha. Nakumbuka hata mimi mlivyonisumbua mwaka 2005 mpaka 2009 nilipokuwa nataka kusajili kampuni yangu mpaka nikaamua kuwaachia zile document. Na kuendelea na maisha mengine. Acheni njaa zenu.