Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 25,258
- 48,589
Siku zote changamoto ndio zinatufanya nini tuamue kwenye maisha yetu, kwenye maamuzi hayo tunatakiwa tuwe na umakini wa kutoathiri hisia za wengine. Binadamu tunakosea mno kuishi kwa kukariri, usimhukumu mtu bila kujua chanzo cha kosa! kuuliza sio ujinga na kukaa kimya sio dawa ya kuuwepuka ujinga.
Naam nakukaribisha kwenye kisa hiki cha kusisimua, kisa ambacho nina imani kitakwenda kukuburudisha, kukusisimua na kukufunza mengi.KARIBU.
SEHEMU YA 1
Ni asubuhi tulivu ambayo jua lilianza kutoa mwanga kwa wanamtaa wa Geza, mtaa ambao ulisifika kwa idadi kubwa ya watu ambao hawakuyapatia maisha, ndio hawakuyapatia maisha ila hilo halikuwafanya kukata tamaa ya kuyapambania maisha yao na ndio maana isingekua ajabu alfajiri kukuta umati wa watu kwenye soko lao kuu la JIZOLEE , naam hao ndio Wanageza ambao waliyazowea maisha yao japo kuwa hayakuzoweleka, hadi kufikia saa kumi na mbili za asubuhi kunguru na ndege kadhaa angani walionekana wakirukaruka na kutoa kelele, kelele ambazo bila ya shaka zilikwenda kuwaibua vitandani wale walioendekeza usingizi.
Ndani ya chumba kimoja ambacho kimuonekano kilidhihirisha wakaazi wa humo hali yao ya uchumi ilikua duni , alionekena binti wa miaka 18 akijiangalia kwenye pande la kioo lililokuwa dirishani, alijitahidi kuzisuka nywele zake nyingi ambazo zilimpa shida mpaka kufikia hatua ya kukasirika na kuanza kutafuta kitu kwenye meza ndogo iliyokuwa chumbani humo.
" Laarah , natamani mikono yangu ingekua na nguvu nikakusaidia kuziweka vyema nywele zako ila ndio hivyo... " sauti kutoka nyuma yake iliyojaa maumivu ilimfanya aache kutafuta alichokusudia na kumfuata alietamka maneno yale, hakua mwingine bali ni mamaake aliyekua kitandani.
"Mamaa.....hupaswi kuongea yote hayo, mimi ni mkubwa sasa hivyo kuna mambo napaswa kuyafanya mwenyewe, tena pale nilikuwa natafuta mkasi ili nizipunguze hizi nywele" kwa sauti yake ya upole aliongea huku mikono yake ikiwa kwenye paji la uso ikipapasa chunusi zilizoisumbua sura yake.
Tabasamu mwanana ambalo bila ya shaka lilibeba hisia za maumivu alilionyesha kwa mtoto wake, alimtaka bintie alale kifuani kwake huku taratibu akijaribu kuchana kipande kidogo cha shuka kwa mkono wake wa kushoto, haikushangaza kuchanika maana shuka lenyewe lilikua laini kutokana na uchakavu, alijaribu kuzifunga nywele zile ila mikono illimsaliti kwa wakati huo.
"Mama unafanya nini? Mikono yako haina nguvu tena ya kufunga nywele zote hizii, ndio maana nataka kuzipunguza " alilalamika Larah kwa sauti yake ya upole iliyojaa deko.
"Utapunguza urembo wako binti yangu, naomba uziache!
"Heheee mama... urembo bila pesa? Umasikini wetu ndio unaficha vitu vingi vizuri tunavyofanya, hemu ona leo hii, masikini ukimsaidia ajiwezae basi utaambiwa unajipendekeza , kama hiyo haitoshi basi ukimpenda mwenye vyake pia utashukiwa uchawi au una tamaa ya mali, hivyo mamaangu mimi sijaona faida ya uzuri huu..... " Larah aliongea akionekana kuchukizwa na jinsi ambavyo watu waliwachukulia.
"Mwanangu hao ndio walimwengu na hayo hayapo kwao tu matajiri hata sisi masikini tumejivika hiyo tabia, Imani yangu inanituma ya kwamba utapata mtu sahihi katika maisha yako ambae hatakupenda kwa uzuri wako tu bali pia jinsi mwenyewe ulivyo"
"Mamaaa, ukianza kuuhubiri uzuri wangu najua hutomaliza, sasa mimi ndio hivyo kumekucha wacha niwahi sokoni " maneno hayo yaliambata na mfungo wa nywele zake kwa kutumia kipande kilekile cha shuka ambacho mamaake alichana, ingawa hazikukaa vyema ila alibana.
Alihakikisha anamuacha mamaake katika mazingira mazuri na salama kwa afya yake , kila kitu ambacho kingehitajika wakati yeye akiwa hayupo alimuwekea karibu yake, kwa upendo alimsogelea mamaake na kumbusu kwenye paji la uso na kuondoka kwa kumpungia mkono.
Safari yake aliipa kituo cha kwanza mbele ya chumba cha jirani yao ambae alikuwa akifua, hakuacha kumuachia maagizo mafupi na kuomba kutupiwa macho mamaake hadi pale ambapo angerudi kwenye mihangaiko yake, kwa vile waliishi vyema na majirani zao basi wala hakusumbuka sana, alijuwa mamaake yupo mikono salama.
**********
Nje ya soko kuu la JIZOLEE alikuwepo kijana ambae alionekena kumsubiri mtu kwa muda mrefu, macho yake hayakuacha kuangaza usawa wa njia kuu ambayo vyombo vya usafiri havikuchoka kupita, ghafla kijana yule sura yake ilichanua ua la tabasamu, tabasamu ambalo lilikwenda kuibua hisia za furaha kwa yule ambae alimtunuku, hata hivyo kijana yule hakuweza kustahamili kuwa pale hivyo aliona ni bora amfuate yule ambae alimzawadia tabasamu muda mfupi uliopita.
Kumbatio ndio ilikuwa salamu yao endapo wawili hao wangekutana , hawakujali macho ya watu waliokuwa pembeni mwao ila wao waliziendekeza hisia kufanya kile walichoamini kinawapa furaha, kwao tabasamu ilikuwa silaha kuu wakiamini ndio chaka la kuficha machungu wanayopitia, kwa vile muda ulikuwa umepotea kijana yule alikumbuka kujitoa mbio kwenye kumbatio lile na kuanza kumtazama binti aliyekuwa usoni kwa macho ya kugombeza, Larah alisanuka!
"Samahani sana Meddy , najua imekua kawaida ila unadhani nitafanya nini na ndio hali halisi ya maisha yangu" alijitetea Larah huku akiweka tabasamu zito la ulaghai mbele ya mwanaume yule ambae sura yake aliikunja kwa hasira.
"Tatizo nakuchekea Larah ndio maana unanipa hii adhabu, kamwe matatizo yako yasikufanye ukashindwa kujipangia muda mzuri wa kufanya kazi , heshimu sana kile ambacho kitakufanya uyafute hayo matatizo uliyonayo , hemu nihurumie na unipe moyo mimi ninaekupigania " Meddy aliongea kwa kumgombeza.
"Lakini Meddy na mamaangu ni muhimu pia , hivi unadhani bila yeye ningekuwa hapa leo hii? Mama ana nafasi kubwa mno kuliko haya matatizo ninayopitia, kumbuka mimi ndio kila kitu kwake" Larah alizidi kujitetea.
"Sijakataa hilo, ila unadhani usipofanya kazi utamhudumia vipi! Kula, kodi na dawa utapata wapi?...." aliuliza Meddy ila hakuna jibu alilopewa zaidi ya ukimya.
"Ok...tuachane na hayo, leo hakuna kukaa kwa mama Pili ukanuka masufuria ya ubwabwa , hata vijana wa Geza waliozowea kukutania basi leo hawatakuona, kuna sehemu mpya nakwenda kukupeleka, huko sitaki uzembe Larah! ni mwendo wa kuchapa kazi ili mifuko ivimbe" Meddy alitoa maelekezo.
"Weweeh! kwa maana leo miguu yangu haitosalia ndani ya soko hili la JIZOLEE ? Kwa tabasamu Larah alihoji na kulinyooshea mkono soko lililokuwa mbele yao.
"Kabisaaaa! Ila chonde mama, machachari yako yaweke kando , Larah nareje tena mapepe sitaki, kinachotakiwa ni kazi tu! " aliongea Meddy akionekana kuwa serious.
"Meddy mbona unasisitiza sana hadi nimeanza kuogopa! hii kazi ya safari hii ni kazi gani?" Larah alihoji kwa wasiwasi.
Meddy alisogeza mdomo wake sikioni kwa bibie Larah na kuanza kunong'ona maneno machache ambayo yalikwenda kuibua mshangao kwenye uso wa Larrah, alionekena wazi kushtuka huku wapita njia wakianza kumshangaa kutokana na mshangao aliouonyesha.........itaendeleaaaaaa.
Naam nakukaribisha kwenye kisa hiki cha kusisimua, kisa ambacho nina imani kitakwenda kukuburudisha, kukusisimua na kukufunza mengi.KARIBU.
SEHEMU YA 1
Ni asubuhi tulivu ambayo jua lilianza kutoa mwanga kwa wanamtaa wa Geza, mtaa ambao ulisifika kwa idadi kubwa ya watu ambao hawakuyapatia maisha, ndio hawakuyapatia maisha ila hilo halikuwafanya kukata tamaa ya kuyapambania maisha yao na ndio maana isingekua ajabu alfajiri kukuta umati wa watu kwenye soko lao kuu la JIZOLEE , naam hao ndio Wanageza ambao waliyazowea maisha yao japo kuwa hayakuzoweleka, hadi kufikia saa kumi na mbili za asubuhi kunguru na ndege kadhaa angani walionekana wakirukaruka na kutoa kelele, kelele ambazo bila ya shaka zilikwenda kuwaibua vitandani wale walioendekeza usingizi.
Ndani ya chumba kimoja ambacho kimuonekano kilidhihirisha wakaazi wa humo hali yao ya uchumi ilikua duni , alionekena binti wa miaka 18 akijiangalia kwenye pande la kioo lililokuwa dirishani, alijitahidi kuzisuka nywele zake nyingi ambazo zilimpa shida mpaka kufikia hatua ya kukasirika na kuanza kutafuta kitu kwenye meza ndogo iliyokuwa chumbani humo.
" Laarah , natamani mikono yangu ingekua na nguvu nikakusaidia kuziweka vyema nywele zako ila ndio hivyo... " sauti kutoka nyuma yake iliyojaa maumivu ilimfanya aache kutafuta alichokusudia na kumfuata alietamka maneno yale, hakua mwingine bali ni mamaake aliyekua kitandani.
"Mamaa.....hupaswi kuongea yote hayo, mimi ni mkubwa sasa hivyo kuna mambo napaswa kuyafanya mwenyewe, tena pale nilikuwa natafuta mkasi ili nizipunguze hizi nywele" kwa sauti yake ya upole aliongea huku mikono yake ikiwa kwenye paji la uso ikipapasa chunusi zilizoisumbua sura yake.
Tabasamu mwanana ambalo bila ya shaka lilibeba hisia za maumivu alilionyesha kwa mtoto wake, alimtaka bintie alale kifuani kwake huku taratibu akijaribu kuchana kipande kidogo cha shuka kwa mkono wake wa kushoto, haikushangaza kuchanika maana shuka lenyewe lilikua laini kutokana na uchakavu, alijaribu kuzifunga nywele zile ila mikono illimsaliti kwa wakati huo.
"Mama unafanya nini? Mikono yako haina nguvu tena ya kufunga nywele zote hizii, ndio maana nataka kuzipunguza " alilalamika Larah kwa sauti yake ya upole iliyojaa deko.
"Utapunguza urembo wako binti yangu, naomba uziache!
"Heheee mama... urembo bila pesa? Umasikini wetu ndio unaficha vitu vingi vizuri tunavyofanya, hemu ona leo hii, masikini ukimsaidia ajiwezae basi utaambiwa unajipendekeza , kama hiyo haitoshi basi ukimpenda mwenye vyake pia utashukiwa uchawi au una tamaa ya mali, hivyo mamaangu mimi sijaona faida ya uzuri huu..... " Larah aliongea akionekana kuchukizwa na jinsi ambavyo watu waliwachukulia.
"Mwanangu hao ndio walimwengu na hayo hayapo kwao tu matajiri hata sisi masikini tumejivika hiyo tabia, Imani yangu inanituma ya kwamba utapata mtu sahihi katika maisha yako ambae hatakupenda kwa uzuri wako tu bali pia jinsi mwenyewe ulivyo"
"Mamaaa, ukianza kuuhubiri uzuri wangu najua hutomaliza, sasa mimi ndio hivyo kumekucha wacha niwahi sokoni " maneno hayo yaliambata na mfungo wa nywele zake kwa kutumia kipande kilekile cha shuka ambacho mamaake alichana, ingawa hazikukaa vyema ila alibana.
Alihakikisha anamuacha mamaake katika mazingira mazuri na salama kwa afya yake , kila kitu ambacho kingehitajika wakati yeye akiwa hayupo alimuwekea karibu yake, kwa upendo alimsogelea mamaake na kumbusu kwenye paji la uso na kuondoka kwa kumpungia mkono.
Safari yake aliipa kituo cha kwanza mbele ya chumba cha jirani yao ambae alikuwa akifua, hakuacha kumuachia maagizo mafupi na kuomba kutupiwa macho mamaake hadi pale ambapo angerudi kwenye mihangaiko yake, kwa vile waliishi vyema na majirani zao basi wala hakusumbuka sana, alijuwa mamaake yupo mikono salama.
**********
Nje ya soko kuu la JIZOLEE alikuwepo kijana ambae alionekena kumsubiri mtu kwa muda mrefu, macho yake hayakuacha kuangaza usawa wa njia kuu ambayo vyombo vya usafiri havikuchoka kupita, ghafla kijana yule sura yake ilichanua ua la tabasamu, tabasamu ambalo lilikwenda kuibua hisia za furaha kwa yule ambae alimtunuku, hata hivyo kijana yule hakuweza kustahamili kuwa pale hivyo aliona ni bora amfuate yule ambae alimzawadia tabasamu muda mfupi uliopita.
Kumbatio ndio ilikuwa salamu yao endapo wawili hao wangekutana , hawakujali macho ya watu waliokuwa pembeni mwao ila wao waliziendekeza hisia kufanya kile walichoamini kinawapa furaha, kwao tabasamu ilikuwa silaha kuu wakiamini ndio chaka la kuficha machungu wanayopitia, kwa vile muda ulikuwa umepotea kijana yule alikumbuka kujitoa mbio kwenye kumbatio lile na kuanza kumtazama binti aliyekuwa usoni kwa macho ya kugombeza, Larah alisanuka!
"Samahani sana Meddy , najua imekua kawaida ila unadhani nitafanya nini na ndio hali halisi ya maisha yangu" alijitetea Larah huku akiweka tabasamu zito la ulaghai mbele ya mwanaume yule ambae sura yake aliikunja kwa hasira.
"Tatizo nakuchekea Larah ndio maana unanipa hii adhabu, kamwe matatizo yako yasikufanye ukashindwa kujipangia muda mzuri wa kufanya kazi , heshimu sana kile ambacho kitakufanya uyafute hayo matatizo uliyonayo , hemu nihurumie na unipe moyo mimi ninaekupigania " Meddy aliongea kwa kumgombeza.
"Lakini Meddy na mamaangu ni muhimu pia , hivi unadhani bila yeye ningekuwa hapa leo hii? Mama ana nafasi kubwa mno kuliko haya matatizo ninayopitia, kumbuka mimi ndio kila kitu kwake" Larah alizidi kujitetea.
"Sijakataa hilo, ila unadhani usipofanya kazi utamhudumia vipi! Kula, kodi na dawa utapata wapi?...." aliuliza Meddy ila hakuna jibu alilopewa zaidi ya ukimya.
"Ok...tuachane na hayo, leo hakuna kukaa kwa mama Pili ukanuka masufuria ya ubwabwa , hata vijana wa Geza waliozowea kukutania basi leo hawatakuona, kuna sehemu mpya nakwenda kukupeleka, huko sitaki uzembe Larah! ni mwendo wa kuchapa kazi ili mifuko ivimbe" Meddy alitoa maelekezo.
"Weweeh! kwa maana leo miguu yangu haitosalia ndani ya soko hili la JIZOLEE ? Kwa tabasamu Larah alihoji na kulinyooshea mkono soko lililokuwa mbele yao.
"Kabisaaaa! Ila chonde mama, machachari yako yaweke kando , Larah nareje tena mapepe sitaki, kinachotakiwa ni kazi tu! " aliongea Meddy akionekana kuwa serious.
"Meddy mbona unasisitiza sana hadi nimeanza kuogopa! hii kazi ya safari hii ni kazi gani?" Larah alihoji kwa wasiwasi.
Meddy alisogeza mdomo wake sikioni kwa bibie Larah na kuanza kunong'ona maneno machache ambayo yalikwenda kuibua mshangao kwenye uso wa Larrah, alionekena wazi kushtuka huku wapita njia wakianza kumshangaa kutokana na mshangao aliouonyesha.........itaendeleaaaaaa.