Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 25,258
- 48,589
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 22
"Larah..."aliita Mr.Romy kwa upole huku zile hasira zote akiziweka pembeni, Larah mwenyewe alibaki kumtazama.
"Naomba nikwambie kitu...zile chuki na hasira zote ziweke pembeni. Najua nimekosea na sikupaswa kufanya hayo niliyofanya na pia najutia kwa hilo, naomba unisamehe na tuanze upya. Naahidi kukusafisha kama ulivyofanya wewe leo hii, nipo tayari kwa kila kitu Larah " maneno hayo kutoka kwa Mr.Romy yalimfanya Larah afurahie kwenye nafsi yake huku akiona kua kazi kiupande wake imekua nyepesi tofauti na alivyodhani.
Hakuishia hapo tu Mr.Romy alishindwa kustahamili kuona machozi ya Larah yakimwagika mbele yake, alisimama na kumuinua kisha akamkumbatia kwa upendo mkubwa huku akimpigapiga mgongoni kumfariji.
Naam penzi jipya lilizaliwa kati yao, Larah aliamua kujiachia mazima ili aweze kulipiza kisasi chake kirahisi, hadi kufikia hapo kwa kitendo ambacho kiliendelea kati yao basi kilimhakikishia kua Mr.Romy ndie mhusika wa tukio lile na ndio maana kakubali kwa urahisi.
Zile picha na video ambazo zilitumwa kupitia account zake walizifanyia utaratibu na kuzifuta zote, licha ya kwamba watu walikua wanazo. Baada ya hapo Larah alirudi kwenye majukumu yake ya kawaida huku akimuacha boss ofisini kwake, hakuondoka hivi hivi bali alimuaga kwa busu zito ambalo aliamini litazidisha mahaba.
Mara tu baada ya kutoka Mr.Romy alipokea simu kutoka kwa mamaake Madam Ziya, hapo alizopokea ni lawama tu kutokana na kile ambacho alikiona kwenye vyombo vya habari. Madam Ziya hakua tayari kuona mahusiano ya kijana wake na binti wa mtaani ambae ndie aliyepelekea taasisi yao kuyumba. Hakuishia hapo tu baada ya kuona Mr.Romy kashikilia msimamo wake wa kua na Larah basi alimsisitiza amfanyie uchunguzi wa kina kuanzia maisha yake na watu ambao wanamzunguka ili wasije kuangukia tena kwenye mambo makubwa kama yaliyojitokeza.
**********
Jioni ilipotimia Larah alijisogeza maeneo ya kwao akitokea ofisini, njiani alipopita story zilikua ni kumuhusu yeye na kile ambacho alikizungumza asubuhi na kuenea kwenye mitandao ya kijamii , wapo waliompongeza kwa ujasiri wake na pia wapo ambao walimbeza na kumuona kua sio wa thamani tena. Hayo hata hakuyatia akilini alichojali yeye ni furaha ya maisha yake na sio wengine.
Alisogea hadi kwenye chumba chao ambacho walipanga, taratibu huku akiweka sura ya tabasamu aliingia ndani na kukutana na kitu ambacho kiliipoteza furaha yake, kwa mwendo wa haraka alimsogelea mwanamke aliyekaa pembeni ya mamaake wakitia story.
"Niffa naomba utoke" hii kauli kutoka kinywani mwa Larah iliwaacha wazi midomo wale waliokua kando yake.
"Laarah waungwana wakikutana hujuliana hali kwanza!!" Niffa alizungumza kwa upole kama sio yeye ambae alitakiwa kutoka, Mama Larah yeye hakutia neno alibaki kumtazama bintie kwa masikitiko.
"Kuna muda baadhi ya vitu vinakua havina umuhimu wa kuwepo, kiswahili changu nafikiri kinaeleweka sihitaji uwepo wako hapa" Larah alizungumza hayo akionekana wazi hakua kwenye matani.
Niffa alishangazwa na hali hiyo , hata mama yake na yeye alizidi kumshangaa bintie na tabia zake , Niffa alitamani kumtukana ila alijizuia alipogundua uwepo wa mtu anaemheshimu eneo lile. Kwa ukaribu zaidi alimsogelea Larah na kumburuza hadi nje .
"Sipo hapa kwa ajili ya shari , naomba unigaie muda wako kidogo tu" aliomba Niffa huku akiweka sura ya msisitizo
"Hivi hufahamu kuwa muda ni mali? Sipaswi kuongea na watu pale tu ninapokuwa na muda, bali natakiwa kutengeneza muda wa kuongea na watu. Niffa....sikuhitaji na wala sina muda mchafu wa kupoteza na wewe" maneno hayo kutoka kinywani kwa Larah yalimduwaza Niffa na kumfanya asiamini alichosikia. Alipotaka kujiweka vyema ili atoe jibu alimshuhudia Larah akipiga hatua kuuelekea mlango. Kamwe hakutaka hilo litokee hivyo alimuwahi na kumvutia nje kwa mara nyingine.
" Larah....JITAMBUE. Anza kwa kuufahamu utu wako mwenyewe , jitahidi kuwa na mtazamo wa wazi wa utu wako, ikiwa ni pamoja na uwezo, udhaifu, mawazo, imani, misukumo na hisia zako. Larah kujitambua ni raha sana maana kunakupa kuelewa watu wengine, jinsi gani wanakuona wewe, mtazamo wako na majibu yako kwao katika wakati husika. KWAHERI"
Niffa alimaliza kuzungumza na kuanza kupiga hatua kuondoka , Larah uso chini huku maneno mazito kutoka kwa Niffa yakimuelemea. Alitamani hata arejeshe muda nyuma ili amsikilize ila haikuwezekana tena maana wakati sio gari kama linaweza kwenda na kurudi.
Hali ya majuto ilimzidi na kuanza kumvaa, alibaki kizingitini akiilaumu nafsi yake kwa kushindwa kutenga muda wa kumsikiliza rafiki yake. Hakupaswa kamwe kumfikiria kua yeye ndie chanzo cha matatizo yaliyomkumba kwa maana kila kinachotokea basi kilipangwa na Mungu kitokee.
"Kivyovyote vile sipaswi kuwasahau wale walionisaidia na wakasimama nami katika nyakati za shida na nyakati ngumu za majaribu. Niffa wewe ndio chanzo cha yote ila wema wako kwangu bado utaniazibu....hapana sistahili kukumbatia!! Yafaa nikuweke kando na kukukwepa kabisa " Larah alijisemea mwenyewe ni kama vile alichanganikiwa.
Larah aliingia ndani akiwa vilevile mwenye hasira na majuto ndani yake. Aliona aibu kumsogelea hata mamaake hivyo alikaa kando na kisirani chake akisubiri kusomewa mashtaka yake. Siku hiyo mama Larah alijitahidi kudhibiti ulimi wake maana hakusema neno kabisa , alimuacha bintie aendelee na kiburi chake.
************
Siku , wiki na miezi ilipepea kama upepo hadi kufikia miezi mitatu tokea picha na video chafu za Larah na Mr.Romy kuachiwa mtandaoni. Perfect Advertising ilijua kujiinua upya kwa mara nyingine. Larah na wafanya kazi wote waliungana kuitengeneza upya taasisi hiyo. Penzi kati ya Mr.Romy na Larah lilizidi kukuwa huku kila mmoja akiiva kiimani juu ya mwenzie hata zile tofauti ambazo walikua nazo basi zilionekana kufifia, hisia za upendo zilizaliwa na walipendeza sana maana kila sehemu walikua pamoja yaani kiufupi hakuna Larah bila Mr.Romy.
Hili jambo lilimkosesha sana amani Niffa maana kila alipojaribu kuweka ukaribu na watu hao basi ilishindikana. Hakuna aliyetaka kumsikiliza kati yao hata mama Larah pia na yeye alimfukuza Niffa pale alipokwenda kwa lengo la kutaka ukaribu wa mazungumzo. Naam hawa ndio wanadamu ambao siku zote wakipata basi huwasahau hata wale waliokua nao kwenye nyakati ngumu.
Larah aliishi maisha mengine kabisa , alikua ni sio yule Larah wa kulalia uji au wali mkavu. Huyu alikua ni Larah aliyeishi na kuogelea kwenye utajiri. Alihama uswahilini na kuishi ushuwani kulingana na hadhi yake. Hakuna asiyemjua mlimbwende Larah, juhudi na bidii za kufanya matangazo mengi yenye ubora ndio yaliyomfanya kuwa hapo alipo.
Katika chumba cha kifahari chenye kila aina ya mapambo Larah alionekana akiwa kalala fofofo, akiwa kwenye usingizi huo mzito alishtuliwa na mlio wa simu iliyokua kando yake, mlio ule ulimkera na kupelekea kuachia msonyo mkali huku akijinyongoa na kuyafikicha macho yake. Alizidisha hasira pale alipoona jina la aliyepiga simu .
"Huyu nae hajui kupuuzwa? Larah aliropoka huku akiiacha simu ile iite hadi ilipokata.
Hiyo haikua dawa kabisa maana mpigaji aliendelea kupiga simu ile bila kukoma. Kwa hasira aliipokea na kuiweka sikioni kwake huku uso wake ukiwa umewiva. Ni kama aliisusia maana aliacha aliyepiga azungumze alichokusudia huku yeye akiubana kimya.
"Naona unajisahaulisha wewe ni nani kwangu! usisahau ulipotoka na wala usimsahau aliyekurusha hapo ulipo. Nikuone getoni kwangu sasa hivi" sauti ya Meddy ilinguruma kutoka kwenye simu iliyokua sikioni kwa Larah, alichukia ila hakua na namna.....itaendeleaaaaaa
"Larah..."aliita Mr.Romy kwa upole huku zile hasira zote akiziweka pembeni, Larah mwenyewe alibaki kumtazama.
"Naomba nikwambie kitu...zile chuki na hasira zote ziweke pembeni. Najua nimekosea na sikupaswa kufanya hayo niliyofanya na pia najutia kwa hilo, naomba unisamehe na tuanze upya. Naahidi kukusafisha kama ulivyofanya wewe leo hii, nipo tayari kwa kila kitu Larah " maneno hayo kutoka kwa Mr.Romy yalimfanya Larah afurahie kwenye nafsi yake huku akiona kua kazi kiupande wake imekua nyepesi tofauti na alivyodhani.
Hakuishia hapo tu Mr.Romy alishindwa kustahamili kuona machozi ya Larah yakimwagika mbele yake, alisimama na kumuinua kisha akamkumbatia kwa upendo mkubwa huku akimpigapiga mgongoni kumfariji.
Naam penzi jipya lilizaliwa kati yao, Larah aliamua kujiachia mazima ili aweze kulipiza kisasi chake kirahisi, hadi kufikia hapo kwa kitendo ambacho kiliendelea kati yao basi kilimhakikishia kua Mr.Romy ndie mhusika wa tukio lile na ndio maana kakubali kwa urahisi.
Zile picha na video ambazo zilitumwa kupitia account zake walizifanyia utaratibu na kuzifuta zote, licha ya kwamba watu walikua wanazo. Baada ya hapo Larah alirudi kwenye majukumu yake ya kawaida huku akimuacha boss ofisini kwake, hakuondoka hivi hivi bali alimuaga kwa busu zito ambalo aliamini litazidisha mahaba.
Mara tu baada ya kutoka Mr.Romy alipokea simu kutoka kwa mamaake Madam Ziya, hapo alizopokea ni lawama tu kutokana na kile ambacho alikiona kwenye vyombo vya habari. Madam Ziya hakua tayari kuona mahusiano ya kijana wake na binti wa mtaani ambae ndie aliyepelekea taasisi yao kuyumba. Hakuishia hapo tu baada ya kuona Mr.Romy kashikilia msimamo wake wa kua na Larah basi alimsisitiza amfanyie uchunguzi wa kina kuanzia maisha yake na watu ambao wanamzunguka ili wasije kuangukia tena kwenye mambo makubwa kama yaliyojitokeza.
**********
Jioni ilipotimia Larah alijisogeza maeneo ya kwao akitokea ofisini, njiani alipopita story zilikua ni kumuhusu yeye na kile ambacho alikizungumza asubuhi na kuenea kwenye mitandao ya kijamii , wapo waliompongeza kwa ujasiri wake na pia wapo ambao walimbeza na kumuona kua sio wa thamani tena. Hayo hata hakuyatia akilini alichojali yeye ni furaha ya maisha yake na sio wengine.
Alisogea hadi kwenye chumba chao ambacho walipanga, taratibu huku akiweka sura ya tabasamu aliingia ndani na kukutana na kitu ambacho kiliipoteza furaha yake, kwa mwendo wa haraka alimsogelea mwanamke aliyekaa pembeni ya mamaake wakitia story.
"Niffa naomba utoke" hii kauli kutoka kinywani mwa Larah iliwaacha wazi midomo wale waliokua kando yake.
"Laarah waungwana wakikutana hujuliana hali kwanza!!" Niffa alizungumza kwa upole kama sio yeye ambae alitakiwa kutoka, Mama Larah yeye hakutia neno alibaki kumtazama bintie kwa masikitiko.
"Kuna muda baadhi ya vitu vinakua havina umuhimu wa kuwepo, kiswahili changu nafikiri kinaeleweka sihitaji uwepo wako hapa" Larah alizungumza hayo akionekana wazi hakua kwenye matani.
Niffa alishangazwa na hali hiyo , hata mama yake na yeye alizidi kumshangaa bintie na tabia zake , Niffa alitamani kumtukana ila alijizuia alipogundua uwepo wa mtu anaemheshimu eneo lile. Kwa ukaribu zaidi alimsogelea Larah na kumburuza hadi nje .
"Sipo hapa kwa ajili ya shari , naomba unigaie muda wako kidogo tu" aliomba Niffa huku akiweka sura ya msisitizo
"Hivi hufahamu kuwa muda ni mali? Sipaswi kuongea na watu pale tu ninapokuwa na muda, bali natakiwa kutengeneza muda wa kuongea na watu. Niffa....sikuhitaji na wala sina muda mchafu wa kupoteza na wewe" maneno hayo kutoka kinywani kwa Larah yalimduwaza Niffa na kumfanya asiamini alichosikia. Alipotaka kujiweka vyema ili atoe jibu alimshuhudia Larah akipiga hatua kuuelekea mlango. Kamwe hakutaka hilo litokee hivyo alimuwahi na kumvutia nje kwa mara nyingine.
" Larah....JITAMBUE. Anza kwa kuufahamu utu wako mwenyewe , jitahidi kuwa na mtazamo wa wazi wa utu wako, ikiwa ni pamoja na uwezo, udhaifu, mawazo, imani, misukumo na hisia zako. Larah kujitambua ni raha sana maana kunakupa kuelewa watu wengine, jinsi gani wanakuona wewe, mtazamo wako na majibu yako kwao katika wakati husika. KWAHERI"
Niffa alimaliza kuzungumza na kuanza kupiga hatua kuondoka , Larah uso chini huku maneno mazito kutoka kwa Niffa yakimuelemea. Alitamani hata arejeshe muda nyuma ili amsikilize ila haikuwezekana tena maana wakati sio gari kama linaweza kwenda na kurudi.
Hali ya majuto ilimzidi na kuanza kumvaa, alibaki kizingitini akiilaumu nafsi yake kwa kushindwa kutenga muda wa kumsikiliza rafiki yake. Hakupaswa kamwe kumfikiria kua yeye ndie chanzo cha matatizo yaliyomkumba kwa maana kila kinachotokea basi kilipangwa na Mungu kitokee.
"Kivyovyote vile sipaswi kuwasahau wale walionisaidia na wakasimama nami katika nyakati za shida na nyakati ngumu za majaribu. Niffa wewe ndio chanzo cha yote ila wema wako kwangu bado utaniazibu....hapana sistahili kukumbatia!! Yafaa nikuweke kando na kukukwepa kabisa " Larah alijisemea mwenyewe ni kama vile alichanganikiwa.
Larah aliingia ndani akiwa vilevile mwenye hasira na majuto ndani yake. Aliona aibu kumsogelea hata mamaake hivyo alikaa kando na kisirani chake akisubiri kusomewa mashtaka yake. Siku hiyo mama Larah alijitahidi kudhibiti ulimi wake maana hakusema neno kabisa , alimuacha bintie aendelee na kiburi chake.
************
Siku , wiki na miezi ilipepea kama upepo hadi kufikia miezi mitatu tokea picha na video chafu za Larah na Mr.Romy kuachiwa mtandaoni. Perfect Advertising ilijua kujiinua upya kwa mara nyingine. Larah na wafanya kazi wote waliungana kuitengeneza upya taasisi hiyo. Penzi kati ya Mr.Romy na Larah lilizidi kukuwa huku kila mmoja akiiva kiimani juu ya mwenzie hata zile tofauti ambazo walikua nazo basi zilionekana kufifia, hisia za upendo zilizaliwa na walipendeza sana maana kila sehemu walikua pamoja yaani kiufupi hakuna Larah bila Mr.Romy.
Hili jambo lilimkosesha sana amani Niffa maana kila alipojaribu kuweka ukaribu na watu hao basi ilishindikana. Hakuna aliyetaka kumsikiliza kati yao hata mama Larah pia na yeye alimfukuza Niffa pale alipokwenda kwa lengo la kutaka ukaribu wa mazungumzo. Naam hawa ndio wanadamu ambao siku zote wakipata basi huwasahau hata wale waliokua nao kwenye nyakati ngumu.
Larah aliishi maisha mengine kabisa , alikua ni sio yule Larah wa kulalia uji au wali mkavu. Huyu alikua ni Larah aliyeishi na kuogelea kwenye utajiri. Alihama uswahilini na kuishi ushuwani kulingana na hadhi yake. Hakuna asiyemjua mlimbwende Larah, juhudi na bidii za kufanya matangazo mengi yenye ubora ndio yaliyomfanya kuwa hapo alipo.
Katika chumba cha kifahari chenye kila aina ya mapambo Larah alionekana akiwa kalala fofofo, akiwa kwenye usingizi huo mzito alishtuliwa na mlio wa simu iliyokua kando yake, mlio ule ulimkera na kupelekea kuachia msonyo mkali huku akijinyongoa na kuyafikicha macho yake. Alizidisha hasira pale alipoona jina la aliyepiga simu .
"Huyu nae hajui kupuuzwa? Larah aliropoka huku akiiacha simu ile iite hadi ilipokata.
Hiyo haikua dawa kabisa maana mpigaji aliendelea kupiga simu ile bila kukoma. Kwa hasira aliipokea na kuiweka sikioni kwake huku uso wake ukiwa umewiva. Ni kama aliisusia maana aliacha aliyepiga azungumze alichokusudia huku yeye akiubana kimya.
"Naona unajisahaulisha wewe ni nani kwangu! usisahau ulipotoka na wala usimsahau aliyekurusha hapo ulipo. Nikuone getoni kwangu sasa hivi" sauti ya Meddy ilinguruma kutoka kwenye simu iliyokua sikioni kwa Larah, alichukia ila hakua na namna.....itaendeleaaaaaa