Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 25,258
- 48,589
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 17
Tayari siku mpya iliwasili ndani ya mtaa wa Geza, tunawajua jinsi walivyo watu wa mtaa huu, kabla jua halijachomoza wao tayari walitawanyika kwenye pembe nne za dunia kwenda kujitafutia kile ambacho wamekipanga, kupata ama kukosa hayo waliyachukulia kama majaliwa ya Mungu. Larah alimaliza kumuweka sawa mamaake na yeye mwenyewe, alimsogelea na kumkumbatia kama wafanyavyo siku zote.
"Mwanangu, furaha uliyonayo usoni mwako naomba idumu siku zote, nafurahi sana kuona mafanikio yako huku na mimi nikiwa hai, najivunia uwepo wako maana umeweza kuipigania afya yangu. Mheshimu sana Meddy maana yeye ndie ambae kila siku amekua mstari wa mbele kwetu, nakutakia kila la kheri kwenye kazi zako...Mungu awe mbele yako binti yangu" Mama Larah aliongea hayo kwa sauti iliyosheheni furaha.
"Usijali mama, nakuahidi mimi binti yako nitabaki kua mwema kwako na yeyote yule aliyeshiriki kunishika mkono wakati wa dhiki" Larah na yeye aliahidi huku akimimina mabusu usoni kwa mamaake.
Huyu mama na yeye hajui tu kama mwanawe tayari keshazagamuliwa zaidi ya mara tano, huyo Meddy anayemsemea aheshimiwe bintie tayari kafanya mume. Au inawezekana pia huyo mama Larah anaelewa kinachoendelea kati yao lakini tu anajizima data😄
Mguu mosi mguu pili hatimae alizipata hatua ambazo zilimsogeza hadi nje ya nyumba ambayo walipanga, akiwa hapo alibahatika kuona kundi la watu likiwa limeduwaa mbele yake likimtazama , kundi hilo liliongozwa na wapangaji wenziwe, mwanzo alidhani labda ni kwa namna ambavyo amevaa , alijikagua na kujiridhisha kua hakua na kasoro yoyote katika mpangilio wa mavazi yake licha ya kwamba yalikua ya kisasa zaidi, bado kundi lile liliendelea kumpa hofu maana nyuso zao zilionekana kuwa na hasira huku nyingine zikionekana kutibuliwa, hawakuishia hapo tu kundi lile lilionekana likionyeshana jambo kwenye simu zao za kisasa huku mikono yao ikiwa kwenye midomo yao wakionekana kushaangaa kitu..
Alijipa matumaini ya kua pengine mpango wake na Meddy utakua umeshakamilishwaa, alifurahi kwenye moyo wake licha ya kwamba hofu juu ya zile nyuso ilimrejesha nyuma, aliamua kusogeza hatua zake mbele ili kuwakaribia kwa ukaribu zaidi ila alisita baada ya kuona sura ya Meddy ikichomoza mbele yake tena ikiwa haina nuru ya tabasamu hata kidogo, haraka sana alimsogelea kwa hofu maana kengele ya hatari iligonga kichwani mwake.
"Meddy kuna nini mbona sielewi? Kwani umefanikiwa kufanya lile jambo? Na kama umefanya mbona jamii yangu inaonekana kuwa na nyuso zilizokosa tabasamu dhidi yangu?" aliuliza Larah kwa hofu huku akimkokota Meddy pembeni .
"Larah, usijitoe akili ! Hivi umewaza nini kabla ya kuachia huo upuuzi wako?" Meddy aliuliza hayo kwa sauti ya ukali.
"Upuuzi gani Meddy? Nyoosha maelezo usinivuruge na wewe! Kwani si tuliamua pamoja " Larah aliuliza kwa hofu kubwa maana hakua akijua kosa lake.
"Pamoja na nani ? Usiniigizie Larah, mimi ndio nilikua na wewe pale kitandani? tayari video na picha zako za utupu ukiwa kitandani na Romy zinasambaa kwenye mitandao yote ya kijamii, nadhani umefakiwa kuonyesha uhodari wako kama mwanamke kabla ya kilele chako kufika...." Meddy alifoka kwa hasira.
Taarifa hiyo ilimshtua mno Larah, hakutegemea kamwe kama siku yake ambayo aliikaribisha kwa tabasamu inaenda kuangukia kwenye dimbwi la huzuni, moyo ulimuenda kasi na kumfanya akae chini bila kutaka. Aliwaza mengi kwenye akili yake hadi alihisi kuvurugwa.
"Meddy, kweli mimi naweza kufanya hivyo? Huyo atakua Romy tu ........nakuapia" kwa sauti ya kilio Larah alijitetea.
"Romy eeeh....inawezekana ikawa kweli ni yeye maana hata account zako umeamua kumpa yeye adhihirishe mahaba yenu ? Kwanini usingesubiri tumalize tulichokipanga? Umejidhalilisha mno na umenivunja moyo, tayari unaangukia kwenye sifa mbaya na kutupiwa kila aina ya matu...." kabla Meddy hajamaliza maneno yake alishtukia Larah akimalizia kuanguka chini kama mzigo.
Kundi ambalo lilikuwa pembeni yao liliwasogelea kwa ukaribu zaidi, Meddy hakujisumbua kumnyanyua zaidi ya kuondoka bila kutoa msaada wowote , watu ambao walimzunguka walibaki wakichukua picha na video ili wapate kuendeleza story ambayo ilibamba mitandaoni. Wale wasiokua na simu basi waliona ule ulikua ni muda sahihi wa kumtupia Larah matusi na laana kibao.
Kwenye wabaya siku zote na mwema huwa hakosekanani, sote tunamkumbuka shogaake aliyeitwa Niffa, huyu ndie ambae kwa muda ule alikua ni msaada kwake, Niffa alibeba jukumu la kumkokota Larah na kumuingiza chumbani kwao, huko alifanikiwa kumkuta mama Larah akiwa kwenye majonzi mazito, hii ilidhihirisha wazi kuwa masikio yake yaliweza kunasa kelele na maneno ambayo yalikua yakiendelea kutupwa huko nje, alimhurumia bintie huku akimshukuru Niffa kwa wema wake.
**********
Kiti chake kwa siku hiyo alikichukia maana hakua na hamu hata ya kukaa, hasira zilimvaa hadi uso wake uliiva na kuzidisha wekundu kwenye pua yake ndefu, Ngumi zisizo na idadi aliamua kuzibamiza kwenye ukuta wa ofisi yake hali iliyopelekea mikono yake kuanza kuvuja damu, alilia na kujilaumu katika nafsi yake. Kichwani mwake yalizunguka maswali ambayo hakua na uwezo wa kuyajibu maana hakuwa na kumbukumbu ya tukio ambalo linaendelea kutapakaa kwenye mitandao, anaikumbuka vyema siku ambayo aliingia na Larah moja ya hotel kubwa Geza ila hakuwa na kumbukumbu ya yeye kushiriki tendo wala kurikodi tukio lolote, nani alifanya? kwanini video iachiwe siku ile?
"Kwanini Larah! kumbe wewe ni nyoka eeeh? Sikuwahi kufikiria kamwe kama unaweza kufanya upuuzi kama huu! Sawa mimi na wewe hatukua sawa lakini ndio ulipize namna hii tena kuelekea siku muhimu ambayo Geza nzima inatutazama? Nitakutafuta na lazima utalipia kwa hili , nataka nijue nani yupo nyuma yako kwenye hili? " Romy alibwata kwa hasira machozi yakiwa usoni mwake.
Hakika ungemuona basi moyo wa huruma ungekuingia, Romy alijiweka kipembeni na kuinamisha uso wake kwenye mapaja yake akilia kwa hasira, alijuta kumfahamu Larah kwenye maisha yake, alijilaumu kwanini alimuamini kupitiliza . Hakua na habari ya mlango wa ofisi yake kugongwa mfululizo, mamaake aliita kila jina ila hakuna alichoambulia zaidi ya ukimya ambao ulimtia mashaka, uamuzi aliochukua ni kuwaita walinzi ambao walianza kuuvunja mlango.
Ule usemi wa uchungu wa mwana aujuae mzazi ulionekana kwa Madam Ziya, hakujali kabisa mazingira machafu ya ofisi ambayo alikumbana nayo , yeye alimsogelea kijana wake ambae bado alijikunyata huku mikono yake ikiwa imerowana damu, alimkumbatia na kunyanyua pale alipokaa huku akimtaka waondoke eneo lile kuepuka mapaparazi ambao walijaa kutafuta taarifa za undani wa tukio ambalo lilijitokeza .
******
"DEAL DONE" hayo yalikua ni maandishi mekundu makubwa yaliyoonekana kwenye ukuta mkubwa mweupe ambao ulipatikana ndani ya chumba ambacho kilikua na vijana wawili wa kiume. Maandishi hayo yalionekana kuchorwa muda mfupi uliopita maana rangi yake ilionekana kuchuruzika na kufanya michirizi.
"Nadhani mpango huu umekamilika, kinachofuata sasa ni kuendelea kuharibu imani zao kwa kuwaendesha vile ambavyo mimi nataka, nitahakikisha hakuna amani kati yao na jina la kampuni yao linakufa kama ambavyo alikufa baba yangu" maneno yenye hisia zito yalitolewa kinywani kwa sauti iliyojaa hasira huku akimgeukia mwenziwe.
Licha ya sura yake kuonyesha hasira lakini mavazi yake yalionekana wazi kabisa kuwa ni mtu aliyejiweza kiuchumi , muonekano wake kwa wakati ule ulionekana kubadilika kabisa! Naam huyu ndie Meddy 🙄 laiti mngemuona basi mngesema hakua yule Meddy wa Larah 😀 wala Meddy ambae alionekana na Wanageza akiranda ovyo mitaani ila ukweli hauwezi kujificha siku zote. Itawashangaza! ndio yeye kabisa .
Tayari siku mpya iliwasili ndani ya mtaa wa Geza, tunawajua jinsi walivyo watu wa mtaa huu, kabla jua halijachomoza wao tayari walitawanyika kwenye pembe nne za dunia kwenda kujitafutia kile ambacho wamekipanga, kupata ama kukosa hayo waliyachukulia kama majaliwa ya Mungu. Larah alimaliza kumuweka sawa mamaake na yeye mwenyewe, alimsogelea na kumkumbatia kama wafanyavyo siku zote.
"Mwanangu, furaha uliyonayo usoni mwako naomba idumu siku zote, nafurahi sana kuona mafanikio yako huku na mimi nikiwa hai, najivunia uwepo wako maana umeweza kuipigania afya yangu. Mheshimu sana Meddy maana yeye ndie ambae kila siku amekua mstari wa mbele kwetu, nakutakia kila la kheri kwenye kazi zako...Mungu awe mbele yako binti yangu" Mama Larah aliongea hayo kwa sauti iliyosheheni furaha.
"Usijali mama, nakuahidi mimi binti yako nitabaki kua mwema kwako na yeyote yule aliyeshiriki kunishika mkono wakati wa dhiki" Larah na yeye aliahidi huku akimimina mabusu usoni kwa mamaake.
Huyu mama na yeye hajui tu kama mwanawe tayari keshazagamuliwa zaidi ya mara tano, huyo Meddy anayemsemea aheshimiwe bintie tayari kafanya mume. Au inawezekana pia huyo mama Larah anaelewa kinachoendelea kati yao lakini tu anajizima data😄
Mguu mosi mguu pili hatimae alizipata hatua ambazo zilimsogeza hadi nje ya nyumba ambayo walipanga, akiwa hapo alibahatika kuona kundi la watu likiwa limeduwaa mbele yake likimtazama , kundi hilo liliongozwa na wapangaji wenziwe, mwanzo alidhani labda ni kwa namna ambavyo amevaa , alijikagua na kujiridhisha kua hakua na kasoro yoyote katika mpangilio wa mavazi yake licha ya kwamba yalikua ya kisasa zaidi, bado kundi lile liliendelea kumpa hofu maana nyuso zao zilionekana kuwa na hasira huku nyingine zikionekana kutibuliwa, hawakuishia hapo tu kundi lile lilionekana likionyeshana jambo kwenye simu zao za kisasa huku mikono yao ikiwa kwenye midomo yao wakionekana kushaangaa kitu..
Alijipa matumaini ya kua pengine mpango wake na Meddy utakua umeshakamilishwaa, alifurahi kwenye moyo wake licha ya kwamba hofu juu ya zile nyuso ilimrejesha nyuma, aliamua kusogeza hatua zake mbele ili kuwakaribia kwa ukaribu zaidi ila alisita baada ya kuona sura ya Meddy ikichomoza mbele yake tena ikiwa haina nuru ya tabasamu hata kidogo, haraka sana alimsogelea kwa hofu maana kengele ya hatari iligonga kichwani mwake.
"Meddy kuna nini mbona sielewi? Kwani umefanikiwa kufanya lile jambo? Na kama umefanya mbona jamii yangu inaonekana kuwa na nyuso zilizokosa tabasamu dhidi yangu?" aliuliza Larah kwa hofu huku akimkokota Meddy pembeni .
"Larah, usijitoe akili ! Hivi umewaza nini kabla ya kuachia huo upuuzi wako?" Meddy aliuliza hayo kwa sauti ya ukali.
"Upuuzi gani Meddy? Nyoosha maelezo usinivuruge na wewe! Kwani si tuliamua pamoja " Larah aliuliza kwa hofu kubwa maana hakua akijua kosa lake.
"Pamoja na nani ? Usiniigizie Larah, mimi ndio nilikua na wewe pale kitandani? tayari video na picha zako za utupu ukiwa kitandani na Romy zinasambaa kwenye mitandao yote ya kijamii, nadhani umefakiwa kuonyesha uhodari wako kama mwanamke kabla ya kilele chako kufika...." Meddy alifoka kwa hasira.
Taarifa hiyo ilimshtua mno Larah, hakutegemea kamwe kama siku yake ambayo aliikaribisha kwa tabasamu inaenda kuangukia kwenye dimbwi la huzuni, moyo ulimuenda kasi na kumfanya akae chini bila kutaka. Aliwaza mengi kwenye akili yake hadi alihisi kuvurugwa.
"Meddy, kweli mimi naweza kufanya hivyo? Huyo atakua Romy tu ........nakuapia" kwa sauti ya kilio Larah alijitetea.
"Romy eeeh....inawezekana ikawa kweli ni yeye maana hata account zako umeamua kumpa yeye adhihirishe mahaba yenu ? Kwanini usingesubiri tumalize tulichokipanga? Umejidhalilisha mno na umenivunja moyo, tayari unaangukia kwenye sifa mbaya na kutupiwa kila aina ya matu...." kabla Meddy hajamaliza maneno yake alishtukia Larah akimalizia kuanguka chini kama mzigo.
Kundi ambalo lilikuwa pembeni yao liliwasogelea kwa ukaribu zaidi, Meddy hakujisumbua kumnyanyua zaidi ya kuondoka bila kutoa msaada wowote , watu ambao walimzunguka walibaki wakichukua picha na video ili wapate kuendeleza story ambayo ilibamba mitandaoni. Wale wasiokua na simu basi waliona ule ulikua ni muda sahihi wa kumtupia Larah matusi na laana kibao.
Kwenye wabaya siku zote na mwema huwa hakosekanani, sote tunamkumbuka shogaake aliyeitwa Niffa, huyu ndie ambae kwa muda ule alikua ni msaada kwake, Niffa alibeba jukumu la kumkokota Larah na kumuingiza chumbani kwao, huko alifanikiwa kumkuta mama Larah akiwa kwenye majonzi mazito, hii ilidhihirisha wazi kuwa masikio yake yaliweza kunasa kelele na maneno ambayo yalikua yakiendelea kutupwa huko nje, alimhurumia bintie huku akimshukuru Niffa kwa wema wake.
**********
Kiti chake kwa siku hiyo alikichukia maana hakua na hamu hata ya kukaa, hasira zilimvaa hadi uso wake uliiva na kuzidisha wekundu kwenye pua yake ndefu, Ngumi zisizo na idadi aliamua kuzibamiza kwenye ukuta wa ofisi yake hali iliyopelekea mikono yake kuanza kuvuja damu, alilia na kujilaumu katika nafsi yake. Kichwani mwake yalizunguka maswali ambayo hakua na uwezo wa kuyajibu maana hakuwa na kumbukumbu ya tukio ambalo linaendelea kutapakaa kwenye mitandao, anaikumbuka vyema siku ambayo aliingia na Larah moja ya hotel kubwa Geza ila hakuwa na kumbukumbu ya yeye kushiriki tendo wala kurikodi tukio lolote, nani alifanya? kwanini video iachiwe siku ile?
"Kwanini Larah! kumbe wewe ni nyoka eeeh? Sikuwahi kufikiria kamwe kama unaweza kufanya upuuzi kama huu! Sawa mimi na wewe hatukua sawa lakini ndio ulipize namna hii tena kuelekea siku muhimu ambayo Geza nzima inatutazama? Nitakutafuta na lazima utalipia kwa hili , nataka nijue nani yupo nyuma yako kwenye hili? " Romy alibwata kwa hasira machozi yakiwa usoni mwake.
Hakika ungemuona basi moyo wa huruma ungekuingia, Romy alijiweka kipembeni na kuinamisha uso wake kwenye mapaja yake akilia kwa hasira, alijuta kumfahamu Larah kwenye maisha yake, alijilaumu kwanini alimuamini kupitiliza . Hakua na habari ya mlango wa ofisi yake kugongwa mfululizo, mamaake aliita kila jina ila hakuna alichoambulia zaidi ya ukimya ambao ulimtia mashaka, uamuzi aliochukua ni kuwaita walinzi ambao walianza kuuvunja mlango.
Ule usemi wa uchungu wa mwana aujuae mzazi ulionekana kwa Madam Ziya, hakujali kabisa mazingira machafu ya ofisi ambayo alikumbana nayo , yeye alimsogelea kijana wake ambae bado alijikunyata huku mikono yake ikiwa imerowana damu, alimkumbatia na kunyanyua pale alipokaa huku akimtaka waondoke eneo lile kuepuka mapaparazi ambao walijaa kutafuta taarifa za undani wa tukio ambalo lilijitokeza .
******
"DEAL DONE" hayo yalikua ni maandishi mekundu makubwa yaliyoonekana kwenye ukuta mkubwa mweupe ambao ulipatikana ndani ya chumba ambacho kilikua na vijana wawili wa kiume. Maandishi hayo yalionekana kuchorwa muda mfupi uliopita maana rangi yake ilionekana kuchuruzika na kufanya michirizi.
"Nadhani mpango huu umekamilika, kinachofuata sasa ni kuendelea kuharibu imani zao kwa kuwaendesha vile ambavyo mimi nataka, nitahakikisha hakuna amani kati yao na jina la kampuni yao linakufa kama ambavyo alikufa baba yangu" maneno yenye hisia zito yalitolewa kinywani kwa sauti iliyojaa hasira huku akimgeukia mwenziwe.
Licha ya sura yake kuonyesha hasira lakini mavazi yake yalionekana wazi kabisa kuwa ni mtu aliyejiweza kiuchumi , muonekano wake kwa wakati ule ulionekana kubadilika kabisa! Naam huyu ndie Meddy 🙄 laiti mngemuona basi mngesema hakua yule Meddy wa Larah 😀 wala Meddy ambae alionekana na Wanageza akiranda ovyo mitaani ila ukweli hauwezi kujificha siku zote. Itawashangaza! ndio yeye kabisa .