Sipendi ugali kabisa na ninaishi

Unazungumzia ugali wa nafaka gani ndio uliletwa na mabeberu na ni mwaka gani???
Ugali wa mahindi mswahili yeyote ukisema ugali anajua wa mahindi...ngano na mtama Nchi nyingi wanalima na kutumia hizo nafaka hata kichwani wapo sawa tofauti na wala ugali harafu wanauamini balaa huwezi kuwaambia kitu kwa sababu washadumazwa...
 
Nchi za Afrika Magharibi wana chakula chao mara nyingi hawatumii ugali utaona hata baadhi ya mambo Senegal,Nigeria na wengine huko akili hazijaganda kama wabongo kutwa na ugali wao harafu wanauamini balaa hamna kitu kabisa zaidi ya kudumaza Ubongo wa watu...kutwa kuulizana vitu vya hovyo hovyo kisa ma Ugali...
 
Ghanaians wana fufu na banku, japo ni mchanganyiko wa nafaka tofauti tofauti, binafsi sikuwahi kuupenda wakati nikiwa naishi close na hawa jamaa.

White wao wanakula corn kwa namna tofauti kidogo, niliipenda. Mahindi mabichi(njano) yanatengeneza salad(mixture na veggies nyingine), unapata vegetable salad moja matata sana, ila huwezi kuwaona wanasonga nguna nzito.

Tatizo letu lingine ni kula starch/carbohydrates debe, huku tukila veggies + others nutrients kwa kiwango kidogo. Lazima ubongo u-seize!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…