Sirari: MwanaCCM aliyehamia CHADEMA kwenye mkutano wa John Heche akamatwa na Polisi

Sirari: MwanaCCM aliyehamia CHADEMA kwenye mkutano wa John Heche akamatwa na Polisi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Subpost 1 - Mpaka sasa polisi Sirari wanawashikilia watu wanane waliowakamata ba ( 800 X 640 ).jpg
Subpost 2 - Mpaka sasa polisi Sirari wanawashikilia watu wanane waliowakamata ba ( 800 X 640 ).jpg


Maagizo ya Bashiru Ally yanaendelea kutekelezwa kwa kishindo na dola.

Pamoja na huyu wako viongozi wengine 8 waliokamatwa na kunyimwa dhamana kwa sababu zisizoeleweka.

Uonevu wa kishamba kama huu utakuja kuleta machafuko yasiyo ya lazima.
 
Erythrocyte,
Chini ya Kamanda Mbowe hakuna mikakati ya kupeleka mbele mashambulizi yanayoendana na vita iliyopo na wakati na mahitaji ya makamanda wake badala yake makamanda uchwara wanabaki kulia lia kama Bundi !! Mshaambiwa kuwa siasa za CCM ni siasa za kijeshi chini ya dola CCM . Kwa maana kwamba Nchi hii ina wenye dola ;wanaolindwa na Dola na wengine hawalindwi wala dola haipo kwa ajili yao. Hawa ni kama wavamizi. Hawatambuliki na hawana Uhuru na haki sawa na wale wengine.

Dr. Bashirini Hali zenu ameamua kuliangamiza Taifa kwa sababu ya kulinda Neno CCM . Hajui hata hilo neno au Chama hata kikifa kesho watu ni wale wale na wataibukia kwingine na kuendelea na maisha na siasa tena za kistarabu zaidi. Huwezi kulinda jina la Chama kwa kutumia dhulma na kuumia nafsi na uhai wa wananchi ambao ndio walipa kodi.

Kama Dola CCM linategemea kodi za watanzania wote iweje litumie bunduki kunyamazisha haki na Uhuru wa wengine kwa kulinda watawala ambao kiuhalisia ndio wanaofaidika na kodi zetu kwa kiwango kikubwa na familia zao. Kwa nini wasiwaheshimu watu wote kwa kuwa wote wanatoa kodi zao kujenga nchi?

Dr . Bashirini hali zenu amepotoka kwa kuzungumzia kupotea kwa KANU kule Kenya kama vile ni Janga linaloiangamiza Kenya wakati KANU ndio ilikua adui wa wa Kenya namba Moja ;KANU alikua ni adui aliyeimarisha ukatili ,ubaguzi, ukabila ,udini na kila aina ya uovu lakini baada ya kufa hiyo chapa ya KANU Leo hii Kenya wanakua wamoja na wenye uhuru na haki zaidi. Na jambo jema zaidi Mtoto wa Mwasisi wa KANU yupo madarakani na hana Muda wa kuwaua wakenye ili kurejesha KANU iliyowatesa wakenya waliopigania Uhuru wakijua wanatafuta Uhuru kumbe wanataka kujenga Chama badala ya kujenga nchi.

Dr .Bashirini hali zenu nimempunguzia maksi nyingi sana kuanzaia kwenye imani yake na dini aliyoamua kuiasi na kujiona kuwa yeye ndiye mungu wa Tanzania anayeweza kupanga anachotaka mpaka akamfukuza Membe aliyeipigania amani na usalama wa nchi hii kwa uhai wake wote na nguvu zake zote na akili zake zote.

Kutumia mtutu wa Bunduki Kulinda Chama chenye wanachama ambao ni binadamu kama kilivyo kingine ni kumkosea Mungu Mwenye enzi na Muumbaji wa wote. Na siku Mungu akiingilia kati Mitutu ya bunduki haitaweza kuwashinda wasio na bunduki kwani wapo watu wema hata ndani ya CCM na dola lake ambao kwao haki ni agizo la Mwenyezi Mungu na katiba na sheria za nchi yetu.

Kwenye Biblia kuna mtu anaitwa mpinga Kristo mwenye namba 666 ambaye atasambaza misheni zake dunia nzima huku akipitia kwenye uchumi ,biashara na fedha.
Hakuna kununua wala kuuza kama mtu hatakua na chapa ya namba 666.

Huyu Mpinga Kristo alitumia mbinu ya kuweka mikakati ya kuhakikisha mtu hauzi wala kununua bila kuwa na chapa ya namba yake. Yesu aliwahi kusema wana wa Giza katika ulimwengu wao wanatumia Hekima kubwa kuliko wana wa Nuru.

Watanzania wanataka Demokrasia wasipoipata ,wasipoiona ndani ya nchi yao wataitafuta nje ya nchi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu erthrocyte watu washachoka haya malalamiko Mara ooh Yana mwisho Mara ooh ipo siku Mara ooh siku hazigandi uhalifu waliofanyiwa chadema unatisha na unatosha Sasa anzisheni jino kwa jino hu ushamba wa kusema Mungu yupo wakati mtu anakutia kidole cha tako ukome.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Superbug,
Ushauri wako sio wa makini kabisa. Ngoja nieleze kidogo kabla hujanilalamikia kwa kuandika hivyo.

Hivi huoni CCM wanavyohangaika sasa hivi; unaona au huoni?

Juhudi zote walizofanya CHADEMA hadi kuwafikisha CCM kwenye hali hiyo unataka zote zifutike wakati ndio kwanza zinazaa matunda?

Unaelewa ninachoandika hapa ama...!

Kwa ushauri wako huo, usikasirike ukiambiwa wewe ni wakala wa CCM mkuu wangu Superbug.
Tuendelee kuomba Mungu sana
Mkuu Erythro,

Ukiwahi kukutana na 'Superbug, mpe ukweli huo. Naona hawatakii mema huyu jamaa.

Anahimiza "mlianzishe" ili iweje..., anajua kitakachotokea baada ya hapo?

CCM watatoka na tabasam la mwaka!
 
Chini ya Kamanda Mbowe hakuna mikakati ya kupeleka mbele mashambulizi yanayoendana na vita iliyopo na wakati na mahitaji ya makamanda wake badala yake makamanda uchwara wanabaki kulia lia kama Bundi !! Mshaambiwa kuwa siasa za CCM ni siasa za kijeshi chini ya dola CCM . Kwa maana kwamba Nchi hii ina wenye dola ;wanaolindwa na Dola na wengine hawalindwi wala dola haipo kwa ajili yao. Hawa ni kama wavamizi. Hawatambuliki na hawana Uhuru na haki sawa na wale wengine.
Erythro, mwingine huyo hapo, asiyejua kitu.

Anahimiza mkapambane na dola..., sikusoma bandiko lake hadi huko mwisho, sijui kama anayo mawazo tofauti na hayo machache aliyoweka hapo juu.

Hawa watu ni wakala wa CCM bila shaka!

Anasema CCM ina 'dola', na kwa hiyo anawahimiza mkapambane na dola?

Huenda hajui kazi mnayofanya kwa sababu wengi wetu tumekuwa tukiwahimiza muifanye, na kuwalalamikia kwa kutoona matokeo ya kazi yenu hiyo.
Kidogo tunaanza kuamini kwamba huenda ushauri tuliokuwa tukiimba kila siku, taratibu mmeanza kuukubali na kuufanyia kazi.

Hawa wasioelewa ni kwamba kwa vile CCM ina 'dola' njia pekee ya kuikabili ni kukabiliana na 'dola' moja kwa moja, jambo ambalo ni la kipuuzi.

Hawajui mwenye 'dola' ni nani, na leo akikohoa tu kidogo CCM itasambaratika hata wasijue 'dola' imepotelea wapi.
Tuendelee kuomba Mungu sana
Hawa watu wenye mawazo kama haya wanahitaji shule ya nguvu ili waelewe kuwa wanhachokililia mkifanye, hicho ndicho kitakachokuwa nafuu ya CCM.
 
Erythrocyte,
Imenibidi nirudi hapa na kukuita wewe mwenyewe mkuu kuhusu kichwa cha habari ya mada yako hii kinachosomeka ifuatavyo:

"...Mwanaccm aliyehamia CHADEMA kwenye mkutano wa John Heche akamatwa na polisi, anyimwa dhamana, anakabiliwa na kesi ya kuhamia CHADEMA."

Nimekaa kwa mda baada ya kusoma hiki kichwa cha habari, na kuangalia picha, nikajaribu kuweka kila 'scenario' ninayoweza kuibuni ili habari hii iweze kidogo kuleta mantiki..., Nikashindwa kabisa!

Unao uhakika wa usahihi wa taarifa hii mkuu?

Naelewa sana hapa jukwaani wewe na kundi lako mnao watani zenu, lakini sio kwenye taarifa za aina hii hata kidogo

Yaani kweli viongozi wa CCM na watendaji wao serikalini wamefikia kwenye hatua mbovu kiasi hiki?

Na kama ni kweli, hivi viongozi hao na watendaji wanadhani vitendo hivi ndio vitakavyoiokoa CCM?

Lema juzi kalazwa sero Singida, hata sijui kama kuna lolote lilotokea huko au la, kama kuna lilotokea, Lema kuwekwa mahabusu hakutasaidia kuondoa hilo lililotokea

Mbona wasiwasi umekuwa mwingi kiasi hiki wakati huu?..., ninayo nadharia juu yake. Lakini ni bora kuvuta subira!
 
Chadema Kuhamia Ccm Heri, lakini Ccm Kuhamia Chadema Shari.
 
View attachment 1381369

Maagizo ya Bashiru Ally yanaendelea kutekelezwa kwa kishindo na dola.

Pamoja na huyu wako viongozi wengine 8 waliokamatwa na kunyimwa dhamana kwa sababu zisizoeleweka.

Uonevu wa kishamba kama huu utakuja kuleta machafuko yasiyo ya lazima.
Huo ni uzushi wa kipumbavu haijawahi tokea unatudanganya unataka kuleta taharuki katijka jamii
 
Back
Top Bottom