Sirari-Tarime: Inadaiwa Askari wa Kenya Wamewashambulia Wafanyabiashara wa Mahindi, baadhi wamejeruhiwa kwa Risasi

Sirari-Tarime: Inadaiwa Askari wa Kenya Wamewashambulia Wafanyabiashara wa Mahindi, baadhi wamejeruhiwa kwa Risasi

nokwenumuya

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2019
Posts
820
Reaction score
2,896
Nimepata taarifa toka kwa rafiki yangu zinazo dai kuwa, kuna Watanzania wamepigwa risasi na Polisi wa Kenya mpakani Sirari eneo linaloitwa Kipimo.

Wengine pia wamevunjwa miguu na mikono na wamekimbizwa hospital.

Katika hali ya kushangaza baadhi ya Watanzania waliopigwa risasi wamechukuliwa na askari wa Kenya na kupelekwa eneo la Kehancha huko Kenya katika jitihada za askari wa Kenya kuficha tukio hilo.

CHANZO CHA MGOGORO

Inasemwa kuwa mgogoro ulianza baada ya maafisa wa Kenya kusema kuwa katika mahindi yaliyopimwa asilimia 55 ni mazima na asilimia 45 yana sumu kuvu hivyo wanaenda kuyachoma moto huko Kehancha.

Wafanyabiashara wa Tanzania wakatoa sharti kuwa hayo mahindi basi yachomwe moto huku wakiona jambo ambalo Wakenya walikataa na kuwaambia hawawezi kuwapangia namna ya kuchoma mahindi hayo.

Basi wakaanza kuyapakia kwenye malori kwa nguvu na Watanzania wakagoma ndipo askari wa Kenya wakawafyatulia risasi Watanzania kadhaa na kujeruhi kadhaa na kukimbiza baadhi ya majeruhi.
 
Tujue mamlaka husika zinasemaje na nini chanzo, otherwise kwanini hao polisi wa Kenya wachukue hayo mahindi wakayaharibie Kenya?

Hii story ingenoga kwa picha au video, hapakuwa na smartphone yenye chaji huko Tarime?
 
Hii ni hatari, uchunguzi ufanyaike na kama ni kweli hatua stahiki zichukuliwe ikiwa ni pamoja na hao polisi kuadhibiwa.

Inasikitusha sana tukio hilo lingeweza kushughulikiwa kidiplomasia bila kuumiza mtu yoyote.
 
Tujue mamlaka husika zinasemaje na nini chanzo, otherwise kwanini hao polisi wa Kenya wachukue hayo mahindi wakayaharibie Kenya?

Hii story ingenoga kwa picha au video, hapakuwa na smartphone yenye chaji huko Tarime?
Nilidhani wewe Chadema utafurahi, Hawa jamaa aliwaweza Magufuli Sasa huyu mh sijui Kama tutatoboa.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
"Taarifa kutoka kwa rafiki yangu".

Huyu rafiki yaki ambae ni source ya hii habari. Ana ushahidi wowote? Au na yeye kaambiwa?
 
Kama kweli tukio kubwa kama hilo linatokea balozi Mulamula na waziri wa mambo ya ndani wanakuwa vipi kimya mpaka muda huu.

Si hata wangetoka hadharani kuomba maelezo upande wa pili kuwapa pressure tu.

Hii serikali inataka kuwa ya kupandwa kichwani na kila mtu.
 
Kama kweli tukio kubwa kama hilo linatokea balozi Mulamula na waziri wa mambo ya ndani wanakuwa vipi kimya mpaka muda huu.

Si ata wangetoka hadharani kuomba maelezo upande wa pili kuwapa pressure tu.

Hii serikali inataka kuwa ya kupandwa kichwani na kila mtu.
Subiri: "Ukinizingua, Ntakuzingua"!
 
HAO ASKARI WA KENYA WAMEMVUNJIA HESHIMA RAIS WAO KWA KIASI KIKUBWA SANA NADHANI SOON WATAACHISHWA KAZI.
 
Back
Top Bottom