Siri iliyofichwa kuhusu BIBLIA

Siri iliyofichwa kuhusu BIBLIA

Habari za jioni wana JF mada ya leo pia ni sensitive kidogo maana inagusa imani za watu ila kutokana na kuwepo hitaji la kuweka rekodi sawa nimeona nilete uzi huu ili tujifunze zaidi. Na sababu kubwa ya kuleta uzi huu ni kutokana na mada nazoleta humu nyingi zinatumia pia vitabu nje ya biblia kama source ya taarifa na kumekuwa na wengi wanaokuja na hoja kwamba chochote kilicho nje ya biblia sio kweli yaani quran,midrash,tanakh/torah,zohar,apocrypha,Pseudipigrapha zote ni batili sasa ni kutokana na hoja hiyo imenipelekea kuandaa uzi huu hivyo tuusome kwa makini na tuujadili kwa ustaarabu tu yote kwa yote kujifunza. Nitaugawa uzi huu kwa sehemu mbili ili iwe rahisi kuusoma na ningependa kabla ya kuchangia uusome wote na kuuelewa. Karibuni
View attachment 830330

UTANGULIZI
1. Biblia ni mjumuiko wa vitabu vya manabii walivyoandika kuhifadhi matukio katika historia ya imani yao kwa Mungu na ilikusanywa katika karne ya 3 baada ya Yesu baada ya kuonekana vitabu vya kiimani viko vingi vinakinzana hivyo wakaamua wawe na kitabu kimoja cha kutumika na wote na ilikuwa katika kigiriki na kiebrania. Baada ya karne zaidi ya 10 kupita biblia ya mapema kabisa kutafsiriwa kuingia kwenye kilatin iliyokuwa lugha ya Roma, ilikuwa ''vulgate'' iliyotoholewa kutoka kiebrania na kigiriki kwenda kilatin na padre Jerome karne ya 14 ila tafsiri ya kiingereza ilikuwa king james version karne ya 15 ambayo hata biblia za kiswahili na lugha zingine maelfu zimetoholewa hapo na ambacho wengi hatujui ni kwamba vitabu ambavyo leo tunaviita apocrypha vilikuwepo kwenye KJV ya kwanza ila mataifa mengi yalipotafsiri hayakuvijumuisha hivyo vitabu 14!!! Na leo hii ukivitumia humu JF kujenga hoja utaambiwa ni vya kishetani wakati biblia ya kwanza ya english iliviweka??

Miaka mingi ikapita ndipo yakaja matoleo mengine tofauti ila kwa karne hii biblia inayotambulika kutumika dunia nzima ni NIV yaani New International Version ya 1973, ambayo ilikuja kufanya utafiti na kutumia vyanzo mbalimbali vya nyuma zaidi na kutengeneza tafsiri yake na muhimu hapa tufahamu NIV iligundua makosa kwenye KJV na ikafuta mistari hiyo kwa kigezo kwamba mistari hiyo haikuwepo kwenye vyanzo vya mwanzo ikimaanisha viliongezwa baadae sana. Baadhi ya mistari ilioongezwa na ambayo NIV imeifuta ama kutoitambua Ni Marko 11:26, 15:28,9:44,9:46 Mathayo 23:14,18:11,17:21, Luka 17:36 Yohana 5:3-4, Matendo 8:37 n.k kwa uchache wake ila mingi zaidi iligundulika haikuepo kwenye vyanzo vya mwanzoni kabisa na kwamba vimeongezwa kinyemela.

Simply ikimaanisha biblia ya kiswahili tunayotumia hii ya chama cha biblia iliyotokana na KJV tumepotoshwa?? Je wakristo tumeambiwa haya kanisani?

Je nani mkweli kati ya KJV na NIV??
View attachment 830331
VITABU VILIVYOPUNGUZWA
Baada ya biblia ya nwanzoni kabisa ya kilatin kuwa na vitabu zaidi ya 76 na version zingine hadi 84 kuna vitabu vilitolewa na kina Jerome kwa sababu mbalimbali ikiwemo kughushiwa majina, kutovuviwa na Roho mtakatifu, kukinzana na vitabu vingine vya Biblia,kuandikwa na manabii wa uongo,utata wa maandiko n.k na vitabu hivyo ni kama 4 Maccabees, Assumption of Moses, Ethiopic Book of Enoch (1 Enoch), Slavonic Second Book of Enoch,Book of Jubilees,3 Baruch, Letter of Aristeas,Life of Adam and Eve, Ascension of Isaiah, Psalms of Solomon, Sibylline Oracles, 2 Baruch,Testaments of the Twelve Patriarchs na vinginevyo na hii ndio kitovu cha uzi huu embu basi tuchambue kwa pamoja.
View attachment 830333

TATIZO LA UANDISHI
Kuna hoja zilitolewa kwamba hivi vitabu vilivyoachwa kwenye biblia yaani Pseudipigrapha na Apocrypha mfano book of enoch, Book of Adam & Eve n.k kwamba vilitolewa kwenye biblia sababu kuna utata juu ya waandishi na kwamba kurasa zingine ziliongezwa baadae.... Ila leo hii wanatheolojia wote duniani wanakubali kuwa biblia bado ina pseudipigraphi nyingi mfano Isaya iliandikwa karne 8 kabla ya kristo yaani sura 1-39, ila kipande kuanzia sura 40-55 iliandikwa na mtu ambaye hajatambuliwa mpaka leo huko babeli na sura 56 mpaka 66 imegundulika na wanatheolojia dunia nzima kuwa ziliongezwa baadae yaani miaka mia kadhaa tokea isaya akiandike!!! Hata jeremia kuanzia sura ya 26 iliongezwa miaka mamia baadae!! Hivyo swali la kujiuliza kwanini basi vitabu vingine vilitolewa kwa hoja hii ilihali biblia bado ina vitabu vyenye kasoro zilezile?? Mfano mingine ni waebrania, Wimbo ulio bora vyote vina utata wa uandishi na mikono zaidi ya miwili imehusika kwa gap la miaka zaidi ya 100!! Je sababu ya kupunguza vitabu vingine kwa kisingizio hiki ni halali au kuna mengine tunafichwa???

Hakuna kitu kilichofichwa. Ukisoma nyaraka za Paulo, Petro na Yohana utaona kuwa tangu Kanisa la karne ya kwanza, kuliibuka imani potofu za manabii wa uongo, wakitumia maneno 'roho ya mpinga Kristo'. Hivyo wakati wa kuandika biblia moja, au kukusanya vitabu hasa vile vya Agano la Kale, umakini ulifanyika kuona ni vitabu gani ambavyo havikua na utata wa kiimani. Kwa hiyo walikua sahihi, kwa kuwa baadhi ya vitabu vililenga maisha ya watu wa nyakati zile, na pia tangu Agano la Kale imani potofu ilikuwepo.

Marekani na Ulaya ambao wengi wamekua wapagani, hawawezi kutupotosha kwa elimu zao za Theolojia kuwa kwenye Injili kuna mistari iliyopachikwa kinyemela. Bali katika kutafsiri kutoka lugha za asili, ndipo mapungufu kidogo yalijitokeza, ambayo hayana madhara kwa imani.

Hivyo ndugu yangu, Wikipedia isikupotoshe.
 
Hakuna kitu kilichofichwa. Ukisoma nyaraka za Paulo, Petro na Yohana utaona kuwa tangu Kanisa la karne ya kwanza, kuliibuka imani potofu za manabii wa uongo, wakitumia maneno 'roho ya mpinga Kristo'. Hivyo wakati wa kuandika biblia moja, au kukusanya vitabu hasa vile vya Agano la Kale, umakini ulifanyika kuona ni vitabu gani ambavyo havikua na utata wa kiimani. Kwa hiyo walikua sahihi, kwa kuwa baadhi ya vitabu vililenga maisha ya watu wa nyakati zile, na pia tangu Agano la Kale imani potofu ilikuwepo.

Marekani na Ulaya ambao wengi wamekua wapagani, hawawezi kutupotosha kwa elimu zao za Theolojia kuwa kwenye Injili kuna mistari iliyopachikwa kinyemela. Bali katika kutafsiri kutoka lugha za asili, ndipo mapungufu kidogo yalijitokeza, ambayo hayana madhara kwa imani.

Hivyo ndugu yangu, Wikipedia isikupotoshe.
Mkuu wikipedia inaingiaje hapa. Tunavyoongea tayari kuna biblia versions 9 na mzee zaidi ni KJV maana ndio ilikuwa ya mwanzoni na mpya zaidi ni NIV (2011) na ndio inadai chanzo cha watafsiri wa KJV ni text receptus waliokuwa nayo 1600 lakini hawa wa NIV waliikuta text receptus ya zamani zaidi kutoka dead sea scrolls ambayo haikuwa na hayo maneno 64,000 na hiyo mistari niliyoorodhesha sasa basi wakasema KJV ilichakachuliwa na ndio leo hii NIV ndio inayotumika zaidi duniani yaani kwenye kila biblia 100 zaidi ya 50 ni NIV ila bible ya kiswahili ilitoholewa kutoka KJV ndio nauliza sasa nani mkweli kati ya KJV na NIV?

Na kama NIV ni mkweli (wanatheolojia 80% wanakiri) je nini hatma ya uhalali wa Biblia kama imewahi kuchakachuliwa

ujibu kwanza hili ambalo halihitaji wikipedia bali uwe na biblia mbili tu ya KJV na NIV ili ujengee hoja
 
Mimi sijasema hivyo ila Biblia iliyopitishwa na wanatheolojia wakubwa duniani yaani NIV ndio imeorodhesha hizo kasoro kutoka KJV ambayo ndio biblia ya kiprotestant imetokea huko..... Ndio nauliza basi kama kweli KJV ina makosa ina maana kwa miaka zaidi ya 2000 protestant tunatumia biblia iliochezewa??? Embu tuwekane sawa hapo
Udaku naomaanisha mimi ni kwamba kuna vitabu viliondolewa kwenye biblia kwa sababu havikuwa na usahihi. Mfano hivi leo likitokea tukio kubwa kila mwandishi ataandika anavyoona na pia wengine wataandika kishabiki au kiudaku. Kwahiyo kwenye biblia kuna matukio mengi yalitokea ya kushangaza ambayo yali stajabisha watu kumbuka pia wapenda umbea walikwepo! Embu fikiri bikira anazaa bila kuingiliwa na mwanaume!

Unaweza kuona hiyo siyo habari ndogo kila mtu alielezea. Mfano mzuri humu JF huwezi kuweka kila habari au uongozi wa JF wakiona habari flani haileweki wanaifuta.. Kama JF inakuwa makini na habari zake! Biblia itakuwaje?
 
Kwahiyo unataka kukaa kwenye nafasi ya kumtetea Mungu au!? Mwache Mungu ajitwalie utukufu mwenyewe...
sina na wala sifikirii huo mpango wa kuchukua nafasi yake ila natetea imani kama mitume walivyo tetea.
 
Embu iweke hiyo mistari isije ikawa ni debe tupu..!
Marko 11:26, 15:28,9:44,9:46 Mathayo23:14,18:11,17:21Luka 17:36 Yohana 5:3-4, Matendo 8:37 n.k

Na pia wakadai kuna mistari iliongezewa mfano marko 16 inaishia mstari wa 8 ila 9 hadi 20 ni FEKI???

Pia yohana 7:52 hadi 8:12 wanadai 7:53 hadi 8:11 ilichomekwa hii muhimu sana kaisome utaona kuna ukweli hapo maana mtitiriko wa 7:52 umeendelezwa 8:12

Soma alafu urudi mkuu
 
kama biblia imetungwa na mtu basi huyo mtu atakuwa sio mtu wa kawaida
ni kitabu kilichojaa hekima nguvu uponyaji
hakuna kitabu maarufu dunia zaid ya biblia
mimi huwa nasoma kila siku na kupata vitu vipya

tatizo imani ndio shida usipokuwa na iman utaona kama gazet tu
Uwe unaelewa kidogo mada kabla hujacomments chochote ndugu hakuna mtu aliyekwambia biblia imetungwa mana biblia n mkusanyiko wa vtabu..kinachoongelewa na kujadiliwa kwmb wapo watu ambao wamekaa wanaijua nje ndan biblia na kwsabb zao muhimu wakaamua kutoa baadh y vtabu km vlvyoorodheshwa na vlvyobaki wakaamua kuvipunguza baadh y mistar na kuingiza mistar y kwao na hlo lnawezkana san mana waliyofany hii kaz n watu ambao wanauelewa na wanachokifanya..cku zote kuengeza maandish n rahs zaid kulko kutunga..
 
MAANDIKO YENYE UTATA
Kuna mistari mingine ambayo ni halali kibiblia ila imebadilishwa maeneo husika ipo mistari zaidi ya 50 kwenye agano jipya mfano Yohanna 7:53-8:11 kuhusu Yesu kuwepo hekaluni ila ghafla kipande kati ya 7:52 na 8:11 vimechomeka story ya mwanamke kahaba alietaka kupigwa mawe na ghafla mstari wa 12 unaendelea Yesu akiwa hekaluni hii inakubaliwa na wanatheolojia wote kuwa kilichomekwa na hakikuwepo kwenye maandiko orijino kama una biblia hapo kasome hiki kipande alafu utaelewa nachosema. Kanisa likaamua kuita vitabu vyenye maandiko na uandishi wa utata kuwa ni disputed books ilihali zina sifa zile zile za kuitwa pseudepigraphi na kutakiwa kufutwa kwenye biblia. Mfano Marko 16 inaishia mstari wa 8 ila 9-20 haikuwepo bali iliongezwa miaka mingi mbele na mtu asiyetambulika ila bado kipo kwenye biblia lakini kitabu cha Enoch au Yuda iskariot vimetolewa kwa hoja hiyo hiyo?? Kuna ajenda gani hapa wakuu?? Kipi tunafichwa?? Anyway disputed books kulingana na mwanatheolojia E. P. Sanders ni waefeso,wakolosai,2 wathesalonike, 1 & 2, Tito na vingine vingi.... Je kama vina kasoro kwanini vimeachwa??

VILIANDIKWA NA MUNGU?
Kuna hoja inasema vitabu vya Biblia viliandikwa kwa uweza wa Roho mtakatifu hivyo vile vilivyoachwa havikuandikwa na Roho mtakatifu sasa tujiulize GT kama kuna mistari ya Biblia imeongezwa na wanadamu mfano isaya,wimbo ulio bora,Tito,Yeremia,marko je bado hoja hii ina mashiko ilihali wanatheolojia wanakiri biblia ilichezewa kwa mifano niliyotoa hapo juu na kama si kweli viliandikwa kwa uweza wa Roho bali fahamu za wanadamu je kwanini basi ilitumika kuzuia vitabu kama Injili ya Yuda ama Thomaso?? Je hakuna agenda ya siri kwanini vilizuiwa alafu sisi tukaaminishwa tu kuwa havikuwa na uvuvio wa Roho mtakatifu??
View attachment 830349
PSEUDEPIGRAPHI ZINAKINZANA NA BIBLE
kuna hoja ilitolewa kwamba vitabu vya biblia vinakinzana na Pseudipigrapha ndio maana vikatolewa kwenye bible ila cha kujiuliza GT mbona kuna taarifa zinakinzana ndani ya biblia lakini havijatolewa??

MIFANO
Mathayo 4:1-11 inasema mara tu baada ya ubatizo Yesu alienda kufunga siku 40 ila Yohana 2:1 anasema siku tatu baada ya kubatizwa Yesu alikua kwenye harusi ya Cana!!

Au mathayo 27:44 wale wezi wawili walimtukana Yesu ila luka 23:39 inasema mmoja alitukana mwingine alimtetea.

Mathayo 28:9 inasema Yesu baada ya kufufuka aliruhusu Mary amshike ila Yohana 20:17 Inaonyesha baada ya kufufuka na kuonana na mary, Yesu akamzuia kumgusa sababu alikua bado hajarudi kwa Baba!!

Hyo ni mifano tu ila kuna mistari zaidi ya mamia inayopishana taarifa ila vimeachwa kwenye bible lakini pseudipigraphi zikipishana hta neno moja ndio wanajengea hoja kwamba ndio sababu havipo kwenye bible je sababu hii ilisababisha vitolewe ama kuna mengi tunafichwa??

HITIMISHO
Kwa kuhitimisha labda niseme tu kumekuwa na maswali mengi juu ya chanzo hasa cha vitabu vingine kutolewa kwenye biblia na vingine kuachwa wakato vina kasoro zile zile..... Na hata mkuu Pendael24 alishawahi kuhoji kwamba kama tunafikiri biblia imechezewa je Mungu haoni hadi aruhusu hilo?? Na akahoji mbona Biblia inatenda ina maana kazi ya forgery inaweza kuwa na nguvu za Mungu na akanihoji je wachungaji wote hawa wakubwa hawalijui hili kiasi Mungu awaache watumie bibloa iliyochakachuliwa?? Kiukweli nilikosa majibu ila nategemea leo humu majibu yote yatapatikana

NB: Mimi nimechokoza mada tu ili kupata maarifa ya GT ila sio msimamo wangu kuwa bible ni batili au Qur'an ndio sahihi hivyo tunapojadili hoja humu tuhakikishe tunazingatia hilo pia udini na kejeli na matusi sio uwanja wake humu, nataka tujadili kwa kujifunza sio kupambana.

Karibuni kwa mjadala
Ndugu yangu nimesoma luka na Yohana nimegundua yafuatayo kwanza kwenye Yohana 2:1 haijasema siku 3 "baada ya ubatizo" kwamba Yesu alikua huko kana imesema tu siku ya 3,nimesoma Luka sura ya 4 yote inasimulia vile Yesu alibatizwa na kwenda nyikani na mstari wa 14 unasema baada ya hayo alienda galilaya alipofika huko ndo kisa cha kugeuza maji kuwa divai linatokea (maana kana ilikua galilaya.

Ni mji ulio mlimani kaskazini mwa nazareti) nilichojifunza ni nini? Kwamba biblia hapo haijipingi Yohana alikua anaelezea siku ya 3 ya Yesu kuwepo garilaya na si siku ya 3 ya Yesu tokea abatizwe
 
Mimi, ninavyojua Lengo la Maandiko Matakatifu ni kufikisha ujumbe uliotarajiwa wa Mungu kwetu sisi binadamu. Kupitia mafunuo au matendo ya wazi au maneno ya kusikia au hadithi na mifano, Mungu anahitaji kutufikishia amri zake flani ili tuzifuate. Hapa hoja ya Msingi ni Mungu kutufikishia ujumbe wake kama alivyotarajia. Nikitolea mfano wa Agano Jipya, Yesu alikuja duniani na akatuletea maagizo kutoka Mbinguni.

Yale maagizo yaliambatana na Matendo yake alipokuwa hapa duniani.
Waandishi wake akina Matayo, Marko, Luka na Yohana waliandika mafundisho ya Bwana Yesu. Hapo kila mmoja aliandika kwa mda wake kama alivyoshuhudia kwa macho yake mwenyewe. Kila mwandishi aliweza kuweka au kuondoa matukio fulani ambayo yalitendeka na Yesu wakati akifundisha kutegemea alivyo ona inafaa.

Kama akina Marko na Luka wangeandika sawa sawa, mstari hadi mstari, nukta kwa nukta, ushahidi wao ungetia mashaka na ingeonekana kama walikaririshwa kwa pamoja wakati mmoja. Ushahidi mzuri ni ule ambao kila mtu anautoa kwa maelezo yake yanayo pishana ki matukio na shahidi mwingine, lakini ujumbe wa kushuhudia kama mtuhumiwa alitenda kosa unadhibitishwa.

Hivyo basi, pamoja na akina Mathayo kutofautiana ki matukio mahali fulani fulani lakini wote wanaeleza kwa usahihi kabisa ujumbe wa Agano Jipya, kwa mfano.
1. Amri mpya mbili za kumpenda Mungu na Jirani.
2. Mateso, Kifo na Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo.
3. Mungu kukutana nasi kwa kupitia nafsi na mwili wa Yesu Kristo.
4. Ubatizo wa Maji na Roho (umuhimu wa kuzaliwa upya kwa mara ya pili)
5. Yesu kuja siku ya mwisho kutufufua wafuasi wake na kwenda kuishi naye Mbinguni milele. NK
Hapa nimetoa mifano michache ili nisiwachoshe wasomaji.
Hivyo basi wandugu wapendwa
Mchakato wa Mungu kuwasiliana na binadamu unapitia matukio mengi sana, kinachotakiwa, ni kufikisha kwa watu ujumbe ukiokusudiwa kwa usahihi.
Kwahiyo Biblia Imeandikwa na watu tena Wakati mwingine Wataalamu mbalimbali waliobobea katika fani mtambuka, hukutana na kujadiri nini kiandikwe na nini kiondolewe ili kuhakikisha UJUMBE ULIOKUSUDIWA NA MUNGU UNAWAFIKIA WALENGWA NA KWA KIASI CHA KUTO KUWACHOSHA.

Hivyo ikisoma Injiri hizo Nne za mwanzo unaona kabisa kutofautiana ki matukia mahali flani flani, na pia aya au sentensi flani kutoonekana kwa mwandishi flani, na kuonekana kwa mwandishi mwingine. Hali kadhalika Biblia kwa ujumla wake Waroma wanatumia vitabu 72 wakivijumuisha na vile vya DEUTROKANONI,

Wanamatengenezo wanatumia vitabu 66 na wameviondoa vile vya Deutrokanoni.
Lakini ukivisoma vyote maudhui yake ni yale yale.
Yanasisitiza Kumpenda Mungu na Kumpenda Jirani.

Hivyo basi Biblia imeandikwa na binadamu na sio Mungu.
Soma Kutoka 34 : 27 - 28. Mungu anamwagiza Musa kuandika kile anachokisikia toka kwake.
Yesu pia alimwagiza Yohana aandike anachokisikia katika mafunuo katika Kisiwa Cha Patmo. Kwenye Ufunuo wa Yohana.
" Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika "
2 : 1

Katika Kufasili toka Lugha moja hadi nyingine, waandishi wanapishana Kimazingila, Lugha, Kitamaduni na Kijamii jambo linalopelekea kuathiri Fasili kutoka tamaduni moja kwenda nyingine.
Mfano,
Ukisoma Biblia ya Kinyakyuswa au ya Kihaya, utagundua kuna tofauti ya kisarufi na Biblia ya Kiswahili lakini Maana ipo palepale.
Zinaeleza kwa usahihi kabisa Mpango wa Mungu wa kumuokoa Binadamu.
Cha msingi hapa sio kuangalia hizo tofauti za Kimuundo, na Kisarufi bali Muunganiko wa Kisemantiki (kimaana) ili kujenga dhamira iliyokusudiwa na Mungu kwa wanadamu.
Leo hii tunaona Injiri inahubiriwa, mapepo yanakimbia, wagonjwa wanaponywa, Watu wanaokolewa nk, kwa maombi ya watumishi wa Mungu kupitia mafundisho ya Biblia hiyohiyo inayotofautiana kisarufi mahali flani flani.

Hapa inathibitishwa wazi kuwa NENO la Mungu Limetufikia kwa Usahihi licha ya hizo Minor Errors za kibinadamu (ubinadamu) zinazojitokeza.
Na Hilo Ndilo Lengo Kuu la Neno La Mungu.

Mimi ndivyo nilivyo elewa.
Masahihisho yanakubaliwa

Za Masiku tele, Mheshimia
zitto jr.
 
Tafsiri Mpya ya Ulimwengu inafafanuliwa na shirika la wazazi wa Mashahidi wa Yehova (Shirika la Mnara wa Doria) kama "tafsiri ya Maandiko Matakatifu yaliyotoka moja kwa moja kutoka kwa Kiebrania, Aramaic na Kigiriki katika Kiingereza cha kisasa na kamati ya mashahidi waliotiwa mafuta wa Yehova." Tafsiri Mpya ya Ulimwengu ni kazi isiyojulikana ya "Kamati ya Tafsiri ya Biblia Mpya ya Ulimwengu." Tafsiri Mpya ya Ulimwengu ni ya kipekee kwa kitu kimoja — ni jitihada za kwanza za utaratibu wa kuzalisha tafsiri kamili ya Biblia iliyohaririwa na kurekebishwa kwa madhumuni maalum ya kukubaliana na mafundisho ya kikundi. Mashahidi wa Yehova na Shirika la Mnara wa Doria waligundua kwamba imani zao zilikuwa kinyume na Maandiko. Kwa hivyo, badala ya kufuata imani zao kwa Maandiko, walibadilisha Maandiko kukubaliana na imani zao. "Kamati ya Tafsiri Mpya ya Biblia ya Ulimwengu" ilibadilisha Andiko lolote ambalo halikubaliana na Teolojia ya Mashahidi wa Yehova. Hii inaonyeshwa wazi kwa ukweli kwamba kama matoleo mapya ya Tafsiri Mpya ya Ulimwengu yalichapishwa, mabadiliko zaidi yalifanywa kwenye maandiko ya kibiblia. Kama Wakristo wa kibiblia waliendelea kuelezea Maandiko ambayo yanaelezea waziwazi uungu wa Kristo (kwa mfano), Shirika la Mnara wa Dori lingechapisha toleo jipya la Tafsiri Mpya ya Ulimwengu na Maandiko hayo yamebadilishwa. Ifuatayo ni baadhi ya mifano maarufu zaidi ya marekebisho ya kimataifa:



Tafsiri Mpya ya Ulimwengu inatafsiri neno la Kigiriki neno staurós ("msalaba") kama "kigingi cha mateso" kwa sababu Mashahidi wa Yehova hawaamini kwamba Yesu alisulubiwa msalabani. Tafsiri Mpya ya Ulimwengu haitafsiri neno la Kiebrania sheol au maneno ya Kigiriki hades, gehenna, na tartarus kama "jahannamu" kwa sababu Mashahidi wa Yehova hawaamini kuzimu. Tafsiri Mpya ya Ulimwengu inatoa tafsiri "uwepo" badala ya "kuja" kwa neno la Kigiriki parousia kwa sababu JW anaamini kwamba Kristo amekwisha rudi mapema miaka ya 1900. Katika Wakolosai 1:16, Tafsiri Mpya ya Ulimwengu inaweka neno "ingine" licha ya kuwa halipo kabisa kutoka kwa maandishi ya Kigiriki ya awali.Inafanya hivyo kutoa maoni kuwa "vitu vingine vyote" viliumbwa na Kristo, badala ya kile ambacho maandiko inasema," vitu vyote viliumbwa na Kristo." Hili ni kukubaliana na imani yao kwamba Kristo ni mtu aliyeumbwa, ambayo wanaamini kwa sababu wanakana Utatu. Tafsiri Mpya ya Ulimwengu haitafsiri maneno sawa ya Kigiriki mahali pengine katika Injili ya Yohana kwa njia sawa. Ni wazi kabla ya kuona tu, kukataa uasi wa uungu wa Kristo ambao unalazimisha Shirika la Mnara wa Doria kutafsiri kikizani maandishi ya Kiyunani, hivyo kuruhusu kosa lao kupata mfano halali kwa wale wasiojua ukweli. Ni waza kabla ya kuona tu ya Mnara wa Doria, imani ya uasi ambayo iko nyuma ya tafsiri isiyo na uaminifu na kizani ambayo ni Tafsiri Mpya ya Ulimwengu. Tafsiri Mpya ya Ulimwengu kwa hakika sio toleo sahihi ya Neno la Mungu. Kuna tofauti ndogo kati ya tafsiri zote kuu za Kiingereza za Biblia. Hakuna tafsiri ya Kiingereza iliyo kamili. Hata hivyo, watafsiri wengine wa Biblia hufanya makosa madogo katika kutafsiri maandiko ya Kiebrania na Kigiriki kwa Kiingereza; Tafsiri Mpya ya Ulimwengu kimakusudi hubadilisha tafsiri ya maandiko ili kuendana na teolojia ya Mashahidi wa Yehova. Tafsiri Mpya ya Ulimwengu ni upotovu, sio toleo la Biblia.
Tafsiri hizi za watu kubadilishabadilisha Biblia zimekuwepo kwa maelfu ya miaka na mambo mengi wanayoamini atu sasa kwamba ni neno la Mungu kutoka kwenye Biblia, ni tafsiri za watu tu zilizopandiana kwa maelfu ya miaka.

Hayo si maneno yangu mimi mja nisiyejua mengi, ni mawazo ya msomi wa Biblia, Myahudi anayeujua utamaduni wao vilivyo, ambaye kazi yake ni kusoma Biblia na ana Ph.D ya mambo ya Biblia, ambaye kashafundisha mpaka Harvard anaitwa James L Kugel.

Kaandika kitabu kizuri kinaitwa "How To Read The Bible: A Guide To Scriptures, Then Aand Now"

Narudia.

Biblia ni maneno ya watu tu walioandika kuhusu maisha yao.

Si maneno ya Mungu.

Mungu aliyeandikwa katika Biblia hayupo.
 
Marko 11:26, 15:28,9:44,9:46 Mathayo23:14,18:11,17:21Luka 17:36 Yohana 5:3-4, Matendo 8:37 n.k

Na pia wakadai kuna mistari iliongezewa mfano marko 16 inaishia mstari wa 8 ila 9 hadi 20 ni FEKI???

Pia yohana 7:52 hadi 8:12 wanadai 7:53 hadi 8:11 ilichomekwa hii muhimu sana kaisome utaona kuna ukweli hapo maana mtitiriko wa 7:52 umeendelezwa 8:12

Soma alafu urudi mkuu
Hao wanao sema ni watu gani? Ungeweka nahiyo ambayo unasema ipo sahihi ili tufanye ulinganisho.
 
MAANDIKO YENYE UTATA
Kuna mistari mingine ambayo ni halali kibiblia ila imebadilishwa maeneo husika ipo mistari zaidi ya 50 kwenye agano jipya mfano Yohanna 7:53-8:11 kuhusu Yesu kuwepo hekaluni ila ghafla kipande kati ya 7:52 na 8:11 vimechomeka story ya mwanamke kahaba alietaka kupigwa mawe na ghafla mstari wa 12 unaendelea Yesu akiwa hekaluni hii inakubaliwa na wanatheolojia wote kuwa kilichomekwa na hakikuwepo kwenye maandiko orijino kama una biblia hapo kasome hiki kipande alafu utaelewa nachosema. Kanisa likaamua kuita vitabu vyenye maandiko na uandishi wa utata kuwa ni disputed books ilihali zina sifa zile zile za kuitwa pseudepigraphi na kutakiwa kufutwa kwenye biblia. Mfano Marko 16 inaishia mstari wa 8 ila 9-20 haikuwepo bali iliongezwa miaka mingi mbele na mtu asiyetambulika ila bado kipo kwenye biblia lakini kitabu cha Enoch au Yuda iskariot vimetolewa kwa hoja hiyo hiyo?? Kuna ajenda gani hapa wakuu?? Kipi tunafichwa?? Anyway disputed books kulingana na mwanatheolojia E. P. Sanders ni waefeso,wakolosai,2 wathesalonike, 1 & 2, Tito na vingine vingi.... Je kama vina kasoro kwanini vimeachwa??

VILIANDIKWA NA MUNGU?
Kuna hoja inasema vitabu vya Biblia viliandikwa kwa uweza wa Roho mtakatifu hivyo vile vilivyoachwa havikuandikwa na Roho mtakatifu sasa tujiulize GT kama kuna mistari ya Biblia imeongezwa na wanadamu mfano isaya,wimbo ulio bora,Tito,Yeremia,marko je bado hoja hii ina mashiko ilihali wanatheolojia wanakiri biblia ilichezewa kwa mifano niliyotoa hapo juu na kama si kweli viliandikwa kwa uweza wa Roho bali fahamu za wanadamu je kwanini basi ilitumika kuzuia vitabu kama Injili ya Yuda ama Thomaso?? Je hakuna agenda ya siri kwanini vilizuiwa alafu sisi tukaaminishwa tu kuwa havikuwa na uvuvio wa Roho mtakatifu??
View attachment 830349
PSEUDEPIGRAPHI ZINAKINZANA NA BIBLE
kuna hoja ilitolewa kwamba vitabu vya biblia vinakinzana na Pseudipigrapha ndio maana vikatolewa kwenye bible ila cha kujiuliza GT mbona kuna taarifa zinakinzana ndani ya biblia lakini havijatolewa??

MIFANO
Mathayo 4:1-11 inasema mara tu baada ya ubatizo Yesu alienda kufunga siku 40 ila Yohana 2:1 anasema siku tatu baada ya kubatizwa Yesu alikua kwenye harusi ya Cana!!

Au mathayo 27:44 wale wezi wawili walimtukana Yesu ila luka 23:39 inasema mmoja alitukana mwingine alimtetea.

Mathayo 28:9 inasema Yesu baada ya kufufuka aliruhusu Mary amshike ila Yohana 20:17 Inaonyesha baada ya kufufuka na kuonana na mary, Yesu akamzuia kumgusa sababu alikua bado hajarudi kwa Baba!!

Hyo ni mifano tu ila kuna mistari zaidi ya mamia inayopishana taarifa ila vimeachwa kwenye bible lakini pseudipigraphi zikipishana hta neno moja ndio wanajengea hoja kwamba ndio sababu havipo kwenye bible je sababu hii ilisababisha vitolewe ama kuna mengi tunafichwa??

HITIMISHO
Kwa kuhitimisha labda niseme tu kumekuwa na maswali mengi juu ya chanzo hasa cha vitabu vingine kutolewa kwenye biblia na vingine kuachwa wakato vina kasoro zile zile..... Na hata mkuu Pendael24 alishawahi kuhoji kwamba kama tunafikiri biblia imechezewa je Mungu haoni hadi aruhusu hilo?? Na akahoji mbona Biblia inatenda ina maana kazi ya forgery inaweza kuwa na nguvu za Mungu na akanihoji je wachungaji wote hawa wakubwa hawalijui hili kiasi Mungu awaache watumie bibloa iliyochakachuliwa?? Kiukweli nilikosa majibu ila nategemea leo humu majibu yote yatapatikana

NB: Mimi nimechokoza mada tu ili kupata maarifa ya GT ila sio msimamo wangu kuwa bible ni batili au Qur'an ndio sahihi hivyo tunapojadili hoja humu tuhakikishe tunazingatia hilo pia udini na kejeli na matusi sio uwanja wake humu, nataka tujadili kwa kujifunza sio kupambana.

Karibuni kwa mjadala
Mzee ni tafsiri gani ya biblia unayotumia? Maana mm nina UV hiyo mathayo 27:44 imesema tu wale wezi haijasema idadi yao ila Luka ndio inasema kuhusu huyo mwizi 1 aliemtukana Yesu contradiction iko wapi hapo sasa?
 
Tafsiri hizi za watu kubadilishabadilisha Biblia zimekuwepo kwa maelfu ya miaka na mambo mengi wanayoamini atu sasa kwamba ni neno la Mungu kutoka kwenye Biblia, ni tafsiri za watu tu zilizopandiana kwa maelfu ya miaka.

Hayo si maneno yangu mimi mja nisiyejua mengi, ni mawazo ya msomi wa Biblia, Myahudi anayeujua utamaduni wao vilivyo, ambaye kazi yake ni kusoma Biblia na ana Ph.D ya mambo ya Biblia, ambaye kashafundisha mpaka Harvard anaitwa James L Kugel.

Kaandika kitabu kizuri kinaitwa "How To Read The Bible: A Guide To Scriptures, Then Aand Now"

Narudia.

Biblia ni maneno ya watu tu walioandika kuhusu maisha yao.

Si maneno ya Mungu.

Mungu aliyeandikwa katika Biblia hayupo.
Mkuu nadhani unatamani sana kumjua Mungu lakini hujua pakuanzia! Nami sipendi kukuvunja moyo endelea kuwa nasi pengine mambo ya kakwendea vyema,coz hakuna aliye zaliwa akiwa anajua yote.
 
swali dogo tu wakristo mnijibu
unaweza kunipa historia ya marko,mathayo,luka ,petro na yohana

Can you handle the truth?

No "hidden code", no "secret bloodline", no "arcane wisdom", no "holy grail", in fact, no mystery at all – just the unembellished truth about the greatest fraud in history. Jesus Never Existed reveals a disturbing truth: that the triumph of Christianity was a disaster for humanity – made chillingly ironic by the bogus nature of its central character, superstar and "saviour". Jesus Never Existed is an uncompromising exposure of the counterfeit origins of Christianity and of the evil it has brought to the world. Not a book for those who wish to keep their faith in the cosy bliss of historical ignorance.
 
Mkuu nadhani unatamani sana kumjua Mungu lakini hujua pakuanzia! Nami sipendi kukuvunja moyo endelea kuwa nasi pengine mambo ya kakwendea vyema,coz hakuna aliye zaliwa akiwa anajua yote.
Natamani sana kujua chochote ambacho kina ushawishi. Na kwa nini kina ushawishi.

Imani ya Mungu ina ushawishi sana.

Ushawishi unaotokana na historia ya kihadithi kuliko ukweli.

Ndiyo maana mpaka sasa huwezi kuthibitisha Mungu yupo.

Unaishia kufupisha mjadala kwa kuniambia niendelee kuwa nanyi.

Hiyo habari ya kwamba hakuna aliye zaliwa akiwa anajua yote, inaweza pia kuwa inamaanisha habari ulizojua za kwamba kuna Mungu, ni habari za uongo ambazo hukuzifahamu vizuri, na hapa una nafasi ya kujifunza zaidi.
 
Mkuu usichanganye New International Version na New World Translation ni vitu viwili tofauti kabisa, NIV inatumika na protestants ila NWT ndio inatumika na Jehovah witness.

So bado swali linasimama je NIV na KJV ipi ni sahihi??? Na kama NIV imekubalika kuwa sahihi nini hatma ya waliotumia biblia iliyochakachuliwa kwa miaka zaidi ya 2000?? Na credibility ya biblia haipo mashakani kama tumeshajua kuna uwezekano wa kuwepo mistari iliyoongezwa?? Kumbuka pia maneno zaidi ya 64,000 yamefutwa na mistari zaidi ya 100 imefutwa sasa basi hatma ni ipi kwa uhalali wa biblia kama kitabu muhimu kwa rejea za wakristo
Tafsiri ya Biblia ya “halisi kimsingi” dhidi ya “ulinganifu mtambuka”

Kwa vile ujumbe ni msingi wa kutafuta maana, toleo la Biblia tunayotumia (ikiwa tunatumia toleo

lililotafsiriwa) ni muhimu sana. Kuna nadharia mbili za msingi katika kutafsiri biblia: (1) “halisi kimsingi” kama vile NASB, ESV, NKJV na RSV; na (2) “ulinganifu mtambuka” kama vile NIV, Good News Bible, New Living Traslation, na Contemporary English Version

1. Nadharia iliyopo nyuma ya Tafsiri za Biblia

a. “Halisi kimsingi” hujielekeza katika ngazi ya muundo wa kifungu. Kimsingi wanafanya tafsiri ya lugha (i.e., maamuzi hufanyika kwa kuzingatia maneno [Kiingereza] mazuri zaidi kuelezea maneno ya Kiebrania na ya Kigiriki ya kifungu cha Biblia cha asili)

b. Tafsiri ya “ulinganifu mtambuka” pia hushughulika na muundo lakini hujielekeza katika “wazo” au ngazi ya maana. Huhusika na tafsiri ya maudhui ya kifungu (i.e, tafsiri ya maana ya kitheolojia ya maana ya kifungu cha asili). Hilo husababisha mpangilio na matumizi ya maneno na muundo ambao haufanani na maneno ya asili ya kiebrania na kigiriki, ingawa hakuna awezaye kueleza mabadiliko yamefanywa wapi. Katika kutekeleza, wahariri wa tafsiri ya ulinganifu mtambuka wamefanya tafsiri ya Biblia kwa ajili ya msomaji, ingawa msomaji hawezi kujua wapi lilitokea. NIV na NRSV hazibadiliki kabisa (i.e, inakaribia tafsiri ya maana halisi ya lugha ya asili) kuliko tafsiri za Jerusalem Bible au Good News Bible.

c. .Vifupisho. Kwa upande mwingine wa Tafsiri ya ulinganifu mtambuka (i.e, ikiachana sana na uhalisia) ni vifupisho kama vile Living Biblia. Vifupisho vinatafsiriwa kwa kufuata “ulinganifu mtambuka lakini wakati mwingine huenda mbali kwa kuweka daraja kati ya baadhi ya tofauti za kitamaduni na za kihistoria kati yetu na nyakati za biblia”. Hivyo, “msomaji hupokea tafsiri kiasi Fulani cha theologia ya mtafsiri (na inapaswa ijulikane hivyo)” (Ibid.) Hayo matoleo ni mazuri kwa ajili kutupatia maana halisi na ya msingi katika kupata tafsiri ya kifungu cha Biblia, tahadhari ni lazima ichukuliwe na ni muhimu kulinganishwa na tafsiri za maneno halisi toka lugha ya asili ikiwa zinapatikana.

2. Mapungufu yaliyomo kwenye matumizi ya tafsiri ya ulinganifu mtambuka. Tafsiri zote za ulinganifu mtambuka husumbua “usomaji” wa tafsiri kwa msomaji wa siku za leo akilinganisha na kifungu halisi alichoandika mwandishi. Kibaya zaidi hubadili kabisa kifungu cha asili kwa namna ambayo haiwezi kuvumilika kama ingelifanyika kwa riwaya au tamthiliya. Huwa zinaondoa maneno mengi ya kitheolojia yaliyotumiwa na mwandishi wa asili. Hivyo tafsiri sahihi hufanywa kuwa ngumu zaidi— hususan katika kuelewa tofauti ndogo vichwa vidogo vya kifungu, ukizingatia kwamba maudhui huwa yanapatikana katika baadhi ya maneno, nukuu na dhana, na kulinganisha vifungu vya maneno tofauti tofauti—wakati mtu anapotumia tafsiri ya ulinganifu mtambuka badala ya tafsiri halisi zaidi.

Tafsiri sahihi ya biblia hatimaye ni ile inayotokana na yale aliyosema mwandishi wa asili na si vinginevyo (i.e., “maana ya lugha”), badala ya kile anachowaza mhariri wa siku za leo kuwa ndicho alichomaanisha mwandishi wa asili (i.e., “ maana ya kimaudhi”)
 
Habari za jioni wana JF mada ya leo pia ni sensitive kidogo maana inagusa imani za watu ila kutokana na kuwepo hitaji la kuweka rekodi sawa nimeona nilete uzi huu ili tujifunze zaidi. Na sababu kubwa ya kuleta uzi huu ni kutokana na mada nazoleta humu nyingi zinatumia pia vitabu nje ya biblia kama source ya taarifa na kumekuwa na wengi wanaokuja na hoja kwamba chochote kilicho nje ya biblia sio kweli yaani quran,midrash,tanakh/torah,zohar,apocrypha,Pseudipigrapha zote ni batili sasa ni kutokana na hoja hiyo imenipelekea kuandaa uzi huu hivyo tuusome kwa makini na tuujadili kwa ustaarabu tu yote kwa yote kujifunza. Nitaugawa uzi huu kwa sehemu mbili ili iwe rahisi kuusoma na ningependa kabla ya kuchangia uusome wote na kuuelewa. Karibuni
View attachment 830330

UTANGULIZI
1. Biblia ni mjumuiko wa vitabu vya manabii walivyoandika kuhifadhi matukio katika historia ya imani yao kwa Mungu na ilikusanywa katika karne ya 3 baada ya Yesu baada ya kuonekana vitabu vya kiimani viko vingi vinakinzana hivyo wakaamua wawe na kitabu kimoja cha kutumika na wote na ilikuwa katika kigiriki na kiebrania. Baada ya karne zaidi ya 10 kupita biblia ya mapema kabisa kutafsiriwa kuingia kwenye kilatin iliyokuwa lugha ya Roma, ilikuwa ''vulgate'' iliyotoholewa kutoka kiebrania na kigiriki kwenda kilatin na padre Jerome karne ya 14 ila tafsiri ya kiingereza ilikuwa king james version karne ya 15 ambayo hata biblia za kiswahili na lugha zingine maelfu zimetoholewa hapo na ambacho wengi hatujui ni kwamba vitabu ambavyo leo tunaviita apocrypha vilikuwepo kwenye KJV ya kwanza ila mataifa mengi yalipotafsiri hayakuvijumuisha hivyo vitabu 14!!! Na leo hii ukivitumia humu JF kujenga hoja utaambiwa ni vya kishetani wakati biblia ya kwanza ya english iliviweka??

Miaka mingi ikapita ndipo yakaja matoleo mengine tofauti ila kwa karne hii biblia inayotambulika kutumika dunia nzima ni NIV yaani New International Version ya 1973, ambayo ilikuja kufanya utafiti na kutumia vyanzo mbalimbali vya nyuma zaidi na kutengeneza tafsiri yake na muhimu hapa tufahamu NIV iligundua makosa kwenye KJV na ikafuta mistari hiyo kwa kigezo kwamba mistari hiyo haikuwepo kwenye vyanzo vya mwanzo ikimaanisha viliongezwa baadae sana. Baadhi ya mistari ilioongezwa na ambayo NIV imeifuta ama kutoitambua Ni Marko 11:26, 15:28,9:44,9:46 Mathayo 23:14,18:11,17:21, Luka 17:36 Yohana 5:3-4, Matendo 8:37 n.k kwa uchache wake ila mingi zaidi iligundulika haikuepo kwenye vyanzo vya mwanzoni kabisa na kwamba vimeongezwa kinyemela.

Simply ikimaanisha biblia ya kiswahili tunayotumia hii ya chama cha biblia iliyotokana na KJV tumepotoshwa?? Je wakristo tumeambiwa haya kanisani?

Je nani mkweli kati ya KJV na NIV??
View attachment 830331
VITABU VILIVYOPUNGUZWA
Baada ya biblia ya nwanzoni kabisa ya kilatin kuwa na vitabu zaidi ya 76 na version zingine hadi 84 kuna vitabu vilitolewa na kina Jerome kwa sababu mbalimbali ikiwemo kughushiwa majina, kutovuviwa na Roho mtakatifu, kukinzana na vitabu vingine vya Biblia,kuandikwa na manabii wa uongo,utata wa maandiko n.k na vitabu hivyo ni kama 4 Maccabees, Assumption of Moses, Ethiopic Book of Enoch (1 Enoch), Slavonic Second Book of Enoch,Book of Jubilees,3 Baruch, Letter of Aristeas,Life of Adam and Eve, Ascension of Isaiah, Psalms of Solomon, Sibylline Oracles, 2 Baruch,Testaments of the Twelve Patriarchs na vinginevyo na hii ndio kitovu cha uzi huu embu basi tuchambue kwa pamoja.
View attachment 830333

TATIZO LA UANDISHI
Kuna hoja zilitolewa kwamba hivi vitabu vilivyoachwa kwenye biblia yaani Pseudipigrapha na Apocrypha mfano book of enoch, Book of Adam & Eve n.k kwamba vilitolewa kwenye biblia sababu kuna utata juu ya waandishi na kwamba kurasa zingine ziliongezwa baadae.... Ila leo hii wanatheolojia wote duniani wanakubali kuwa biblia bado ina pseudipigraphi nyingi mfano Isaya iliandikwa karne 8 kabla ya kristo yaani sura 1-39, ila kipande kuanzia sura 40-55 iliandikwa na mtu ambaye hajatambuliwa mpaka leo huko babeli na sura 56 mpaka 66 imegundulika na wanatheolojia dunia nzima kuwa ziliongezwa baadae yaani miaka mia kadhaa tokea isaya akiandike!!! Hata jeremia kuanzia sura ya 26 iliongezwa miaka mamia baadae!! Hivyo swali la kujiuliza kwanini basi vitabu vingine vilitolewa kwa hoja hii ilihali biblia bado ina vitabu vyenye kasoro zilezile?? Mfano mingine ni waebrania, Wimbo ulio bora vyote vina utata wa uandishi na mikono zaidi ya miwili imehusika kwa gap la miaka zaidi ya 100!! Je sababu ya kupunguza vitabu vingine kwa kisingizio hiki ni halali au kuna mengine tunafichwa???
Nimejaribu kusoma kile mleta mada anachosema ni siri sijaona kama kuna siri hapo. Kila kitu kipo sawa kabisa na kimenyooka tu. Nafikiri nia yake ni kupigania vitabu ambavyo havipo katika biblia viwepo, lakini sionia akieleza huko viliko vina msaada gani kwake usiokuwepo kwa wengine.

Ninavyofahamu biblia ina siri lakini sii hizi za mtoa posti. Siri zza biblia zipo ndani ya mistari yake na zinasomwa katikati ya hiyo hiyo mistari mfano katika vitabu vya ufunuo kuna mihuri ambayo lugha yake ya kuwakilisha ni ya fumbo kama mpanda farasi, wenye uhai, mnyama, namba 666, kahaba nk.

Hizi ndizo siri za mifano inayohitaji kufunguliwa na kuwa wazi.
Biblia ni kitabu ambacho kina kusudi moja kuu la ukombozi wa manadamu aliye anguka, nalo limeshikamana vilivyo bila kujikanganya licha ya waandishi kutofautiana kwa karibu ya miaka elifu tatu. Sasa mwandishi yeyote akijitokeza na utunzi wake usiovuviwa sii tu kwamba anatengwa bali amejitenga mwenyewe na lile kusudi kamilifu la Mungu.
 
Nimefurahishwa saana kwa huu ufafanuzi.....
Tatizo watu wa GT wanazani wamesoma kila kitu wamemaliza kumbe si kweli, wengi ni vi 'hoja' wanaokoteza kwa wafuasi wa mashetani na kuja kupotosha watu.

Mleta mada ameleta mada vikorishi kwa watu wasiojua maandiko wala imani.

Biblia ni kitabu kilicho vuviwa kila moja kwa wakati wako ila kwa dhumuni moja tuu kama kuna vilivyo acjwa maana dhumuni ni tofauti na hivi vingine ambavyo Mungu alikusudia vitufikie.

Kama zama hizo manabii haikua rahisi kuwaamini mpaka kujaribiwa wengine unadhani ni waongo wangapi waliibuka wakijifanya wanatoka kwa Mungu?? Na ndio maana Mtume s.w.a anawaambia waislamu Quran imekamilishwa na taorati, zaburi, injili pamoja na Quran yenyewe kwakua msingi wa Imani kwa Mungu wa kweli ni kutoka kwa wayahudi kama taifa teule.

Biblia kwangu ni kitabu kisicho na shaka bali ni kimbilio na majibu ya maswali yangu yoote maana hata hichi kuulizwa juu ya kweli kutiliwa shaka ilashanijulisha.

Wakristo tusome biblia, waislamu tusome biblia na Quran.
tatizo lako huna taarifa kuwa biblia yako na quran imecopy vitabu vya kale (hususani the book of the dead cha wamisri wa kale)
kama ungejua hilo usingesema biblia na quran havina shaka
kati ya vitabu vichekesho biblia na quran vinaongoza
 
Ndugu yangu nimesoma luka na Yohana nimegundua yafuatayo kwanza kwenye Yohana 2:1 haijasema siku 3 "baada ya ubatizo" kwamba Yesu alikua huko kana imesema tu siku ya 3,nimesoma Luka sura ya 4 yote inasimulia vile Yesu alibatizwa na kwenda nyikani na mstari wa 14 unasema baada ya hayo alienda galilaya alipofika huko ndo kisa cha kugeuza maji kuwa divai linatokea (maana kana ilikua galilaya. Ni mji ulio mlimani kaskazini mwa nazareti) nilichojifunza ni nini? Kwamba biblia hapo haijipingi Yohana alikua anaelezea siku ya 3 ya Yesu kuwepo garilaya na si siku ya 3 ya Yesu tokea abatizwe
Mkuu ni vizuri kama hujaona contradiction yeyote hapo basi ungenisaidia na hyo mistari mingine iliyobaki mfano hyo story ya wezi pale mslabani mathayo anasema wote walimtukana ila luka anasema mmoja tu ndio alimtukana Yesu ipi ni ipi mkuu

Karibu tuelimishane
 
Back
Top Bottom