Siri ya Furaha ya ndoa ni kuishi wanandoa kama marafiki (washkaji) wawili

Siri ya Furaha ya ndoa ni kuishi wanandoa kama marafiki (washkaji) wawili

safuher

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
11,837
Reaction score
17,412
Umeshawahi kujiuliza kwa nini kuna jamaa mke wake unamuona wa kawaida sana lakini wanaishi kwa amani kabisa na wanapendana?

Ni kwa sababu wamekuwa marafiki ndani ya ndoa, siri ya rafiki hata awe mbaya kiasi gani hauwezi kuchagua sura yake akiwa mshkaji ndio mshkaji huyo.

Kuna watu wana marafiki ambao hawataki wenza wao wawe kama marafiki zao. Mtu ana rafiki mlemavu lakini hataki mwenza wake awe mlemavu, Mtu ana rafiki kipofu lakini hataki awe na mwenza kipofu, mtu ana rafiki mzee saana lakini hataki mwenza wake awe mzee.

Hii ni kwa sababu urafiki una nguvu ya kuwaunganisha watu kwa muda mrefu kuliko ngono yenyewe. Lakini pia jiulize kwamba mbona suala la urafiki inawezekana kuwa watu wa jinsia moja wakawa marafiki?

Kuonesha namna ambavyo urafiki una nguvu kubwa ya kuwaunganisha watu na kuwafanya waendelee kuwa wamoja. Mwanandoa mwenzio anapokuwa rafiki yako kuna uwezekano mkubwa sana wa nyinyi kuishi kwa muda mrefu katika ndoa yenu kwa sababu ndoa yenu imeunganishwa na jambo la urafiki ndani yake.

Urafiki una nguvu kuliko ngono ndio maana kuna talaka kwa wanandoa na wala hakuna talaka kwa marafiki. Kwa sababu marafiki hawatengani kwa sababu ya ugomvi bali wanatengana kwa sababu ya umbali ndio maana una washkaji zako wa shule hamjawahi kugombana ila kwa sababu ya umbali una washkaji wengine.

Lakini kwenye ndoa watu hawatengani hivi hivi tu lazima wakorofishane wengi wao ndipo waachane. Ngono unaweza kupata kwa siku moja lakini urafiki hauwezi kupata kwa siku moja. Hivyo mwanandoa usijisahau sana ukahisi kwamba ngono ndio ishu kubwa katika ndoa, bali urafiki hasa ndio jambo kubwa.

Wanandoa msiconcetrate kwenye ngono kwa sababu ngono sio ishu tenconcetrate katika mahusiano mazuri ya urafiki na mkeo. Kinachowatenganisha wanandoa ni mahusiano ya kingono na wala sio mahusiano ya kirafiki. Ngono katika ndoa ni dharura endapo utakuwa na hamu ndipo unamaliza haja zako,ila kuna mambo mengi ya kufanya na kujadili na rafiki yako wa ndoa ukiacha ngono.

Mahusiano yanayotegemea ngono hudumu kwa muda mfupi na kuishia kwenye michepuko,mahusiano yanayounganishwa na urafiki hudumu muda mrefu sana.

Mke/mume wako ndiye rafiki yako.

1642487652447.png

 
Umeshawahi kujiuliza kwa nini kuna jamaa mke wake unamuona wa kawaida sana lakini wanaishi kwa amani kabisa na wanapendana ?

Ni kwa sababu wamekuwa marafiki ndani ya ndoa,siri ya rafiki hata awe mbaya kiasi gani hauwezi kuchagua sura yake akiwa mshkaji ndio mshkaji huyo.
Ndoa ikiunganishwa na ngono kuna vipindi vya mmoja kuugua magonjwa makubwa yanayofanya ngono isifanyike,au ifanyike chini ya kiwango, hapo ndoa inaingia shakani kwa mmoja kuchepuka au kuwa na mahusiano nje.

Ikiunganishwa na fedha kuna kufilisika na kuunguliwa moto biashara kama soko la karume,ndoa inakuwa shakani.

Ila ikiunganishwa na upendo na urafiki inadumu sana kwakuwa mnakuwa huru, urafiki ndoani unapunguza sana chuki na usaliti kwakuwa asilimia kubwa mnakuwa wawazi.

Sio unakuwa na mwenza mkilala kitandani unaogopa hata kujamba.
 
Ndoa ikiunganishwa na ngono kuna vipindi vya mmoja kuugua magonjwa makubwa yanayofanya ngono isifanyike,au ifanyike chini ya kiwango ,hapo ndoa inaingia shakani kwa mmoja kuchepuka au kuwa na mahusiano nje.
Ikiunganishwa na fedha kuna kufilisika na kuunguliwa moto biashara kama soko la karume,ndoa inakuwa shakani.

Ila ikiunganishwa na upendo na urafiki inadumu sana kwakuwa mnakuwa huru,urafiki ndoani unapunguza sana chuki na usaliti kwakuwa asilimia kubwa mnakuwa wawazi.

Sio unakuwa na mwenza mkilala kitandani unaogopa hata kujamba.
Bonge moja la Point
 
Ndoa ikiunganishwa na ngono kuna vipindi vya mmoja kuugua magonjwa makubwa yanayofanya ngono isifanyike,au ifanyike chini ya kiwango ,hapo ndoa inaingia shakani kwa mmoja kuchepuka au kuwa na mahusiano nje.
Ikiunganishwa na fedha kuna kufilisika na kuunguliwa moto biashara kama soko la karume,ndoa inakuwa shakani.

Ila ikiunganishwa na upendo na urafiki inadumu sana kwakuwa mnakuwa huru,urafiki ndoani unapunguza sana chuki na usaliti kwakuwa asilimia kubwa mnakuwa wawazi.

Sio unakuwa na mwenza mkilala kitandani unaogopa hata kujamba.
Point sana kaka.
 
Kila mmoja akifanya majukumu yake kwa uaminifu ndio kutakua na urafiki wenye umejaa upendo na utii
Majukumu ni neno pana sana.

Muhimu wanandoa wakubaliane wataishi vipi wasiishi kwa misingi ya watu wengine hata kama hawaifurahii.

Mimi sipendi nikawekewe maji na mke wangu chooni kwa sababu rafiki yangu hawezi kunifanyia hivyo japokuwa kuna watu wanaona kama hili ni jukumu la mke.

Mimi sipendi mke wangu afanye kazi zote za ndani lazima nimsaidie kwa sababu hata rafiki yangu huwa namsaidia baadhi ya kazi japokuwa watu wataona nafanya majukumu ya mke.

Hivyo kutimiza majukumu ni suala la kukubaliana tu, inawezekana mmoja hayatimizi majukumu yake kisawasawa na ndoa ikawa na amani tu.
 
Majukumu ni neno pana sana.

Muhimu wanandoa wakubaliane wataishi vipi wasiishi kwa misingi ya watu wengine hata kama hawaifurahii.

Mimi sipendi nikawekewe maji na mke wangu chooni kwa sababu rafiki yangu hawezi kunifanyia hivyo japokuwa kuna watu wanaona kama hili ni jukumu la mke.

Mimi sipendi mke wangu afanye kazi zote za ndani lazima nimsaidie kwa sababu hata rafiki yangu huwa namsaidia baadhi ya kazi japokuwa watu wataona nafanya majukumu ya mke.

Hivyo kutimiza majukumu ni suala la kukubaliana tu,inawezekana mmoja hayatimizi majukumu yake kisawasawa na ndoa ikawa na amani tu.

Majukumu neno pana sana lakini majukumu ya ndoa ni neno dogo kama kutakua na upendo na utii.

Makubaliano bila kutimiza majukumu kati ya wanandoa kwa upendo ni utumwa kama sio utapeli

Kuwekewa maji bafuni katika upendo ni furaha kwa muwekaji mwenyewe japo muwekewaji asiye na upendo anaweza geuza ikawa utumwa

Wanandoa wanaweza kutimiza makubaliano iwapo kuna uwajibikaji wa majukumu kwa upendo
 
ETI HII NI KWELI mama D 🙂

Sijui anaongelea pesa kwa misingi ipi ila mwanaume anapoamua kuingia kwenye jukumu la familia anatakiwa kujua kwamba ili familia yake iweze kuishi lazima iweze kupata mahitaji ya kijamii. Na hayo majukumu yanaweza kuwa yanahitaji pesa au mali ili yatekelezeke.

Mwanaume kichwa cha familia akiwa na pesa akapata na mke aliye msaidizi sahihi maisha ni mazuri sanaà
 
Umeshawahi kujiuliza kwa nini kuna jamaa mke wake unamuona wa kawaida sana lakini wanaishi kwa amani kabisa na wanapendana ?

Ni kwa sababu wamekuwa marafiki ndani ya ndoa,siri ya rafiki hata awe mbaya kiasi gani hauwezi kuchagua sura yake akiwa mshkaji ndio mshkaji huyo.
Urafiki unajengwa kwa

1. Muda
2. Isionekane mmoja yuko kwenye ndoa kwa sababu
3. Upendo

Mwanamke akiwa desperate ataolewa na mtu ambae huenda asimpende ial atataka tu heshima ya ndoa na watoto, bas hapo hesabu maumivu na hata sku1 urafik huwez upata hapa

Nmeongelea mwanamke sabab mara nying mwanaume ndio anaependa na ndomana anamfata mwanamke kumtongoza..mwanamke yeye ni mpokeaj..anapenda mbeleni huko

So ukizingatia haya juu..kuna uwezekano ukawa na urafik na mwenza wako.
 
Sijui anaongelea pesa kwa misingi ipi ila mwanaume anapoamua kuingia kwenye jukumu la familia anatakiwa kujua kwamba ili familia yake iweze lazima iweze kupata mahitaji ya kijamii. Na hayo majukumu yanaweza kuwa yanahitaji pesa au mali ili yatekelezeke.

Mwanaume kichwa cha familia akiwa na pesa akapata na mke aliye msaidizi sahihi maisha ni mazuri sanaà
So, PESA inatosha kusolve kila kitu kwenye mahusiano? I mean ukiwa na pesa basi umesha-win mahusiano bora yenye afya?

Pls mama D tena, before uende kwenye majukumu muhimu 🙂
 
So, PESA inatosha kusolve kila kitu kwenye mahusiano? I mean ukiwa na pesa basi umesha-win mahusiano bora yenye afya?

Pls mama D tena, before uende kwenye majukumu muhimu 🙂

Pesa sio kila kitu kwenye mahusiano. Kimsingi wanawake wengi hatuhitaji pesa ila tunahitaji kuwa maintained tuendelee kung'aa kama mlivyotukuta hata na zaidi.

Maana wanaume mnatupendaga mkitukuta makwetu tunang'ara mnapambana hadi mnatuoa huku mnajua kabisa tunahudumiwa, halafu miezi6 mnatuchakaza tunachakaa vibayaaa. Mtuhudumie tusianze kukumbuka makwetu na kurudi kuomba matumizi kwa wazazi
 
Back
Top Bottom