Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
- Thread starter
- #21
Inatoka bandiko #16
UNDANI WA SHERIA NAMBA 18 YA MWAKA 1964.
Awali tulijadili moja ya nyaraka za Muungano ziliyowasilishwa Dodoma – yani Sheria Namba 22, ya April 25, mwaka 1964. Tuliona kwamba, licha ya nyaraka iliyowasilishwa kuchakachuliwa saini za Nyerere na Msekwa, bado nyaraka hii sio Msingi wa Muungano bali Mkataba/Hati Ya Muungano (1964) ambayo hadi sasa kinachoendelea juu ya upatikanaji wake ni mazingaombwe. Rasimu Ya katiba (2014) imeweka wazi katika sura yake ya kwanza kwamba msingi wa Muungano uliopo ni Hati ya Makubaliano (1964). Rasimu Ya Katiba hii haijataja Sheria Za Muungano zilizofuatia baada ya HATI YA MUUNGANO, kutiwa Saini. Sababu za Rasimu kutofanya hivyo ni za wazi, hivyo hatuna haja ya kujidaili kwa sasa.
Katika sehemu inayofuata tutaitizama nyaraka nyingine iliyowasilishwa Dodoma – yani Sheria Namba 18, ya Machi 24, Mwaka 1965, kisha tutajadili kwanini, kama ilivyoile nyaraka nyingine (sheria namba 18, 1965), Nyaraka hii (Sheria namba 22, 1965), pia ni batili kwa matumizi ya Muungano .
UMUHIMU WA sheria namba 18 ulikuwa ni kuichakachua ibara ya ibara ya (7) ya Mkataba wa Muungano ambayo ilielekeza Rais Wa Muungano na Makamu wake (Rais wa Zanzibar) katika kipindi cha mpito (Mwaka Mmoja), waunde TUME YA KATIBA na BARAZA LA KUTUNGA KATIBA. Ibara hii ya (7) ya Mkataba wa Muungano inasema hivi:
Lakini kilichotokea MWEZI MMOJA tu kabla ya kipindi cha mpito (mwaka mmoja) kuisha muda wake, Bunge la Muungano likapitisha sheria tajwa hapo juu (Sheria Namba 18 ya Mwaka 1965). Lengo la Sheria ilikuwa ni kuhairisha masharti ya ibara ya ibara hii (7) ya Mkataba wa Muungano kwa muda usiojulikana, hivyo kwenda kinyume na maelekezo ya Mkataba wa Muungano (1964).
Sheria Namba 18 ya Mwaka 1965 ilieleza yafuatayo:
Kufuatia sheria hii, Muungano ukakosa fursa muhimu ya kupata katiba yake ya kudumu kwa mujibu wa matakwa ya ibara ya (7) ya mkataba wa muungano (1964), na badala yake muungano ukaingizwa chini ya Katiba ya muda kwa muda usiojulikana. Huu ulikuwa ni mwanzo wa tatizo kubwa mbeleni kama Shivji (1990, 2005 &2008) anavyolijadili.
Sambamba na Sheria hii namba 22 ya Mwaka 1965, MIEZI MINNE baadae, Bunge la Muungano pia likapitisha sheria nyingine – tarehe 11, Julai 1965, sheria iliyojulikana kama "KATIBA YA MUDA YA TANZANIA (Sheria no. 43) ambayo ilitengeneza madaraka kwa serikali ya jamhuri ya muungano na pia kwa serikali za nchi washiriki wa muungano.
Inaendelea bandiko linalofuatia…
UNDANI WA SHERIA NAMBA 18 YA MWAKA 1964.
Awali tulijadili moja ya nyaraka za Muungano ziliyowasilishwa Dodoma – yani Sheria Namba 22, ya April 25, mwaka 1964. Tuliona kwamba, licha ya nyaraka iliyowasilishwa kuchakachuliwa saini za Nyerere na Msekwa, bado nyaraka hii sio Msingi wa Muungano bali Mkataba/Hati Ya Muungano (1964) ambayo hadi sasa kinachoendelea juu ya upatikanaji wake ni mazingaombwe. Rasimu Ya katiba (2014) imeweka wazi katika sura yake ya kwanza kwamba msingi wa Muungano uliopo ni Hati ya Makubaliano (1964). Rasimu Ya Katiba hii haijataja Sheria Za Muungano zilizofuatia baada ya HATI YA MUUNGANO, kutiwa Saini. Sababu za Rasimu kutofanya hivyo ni za wazi, hivyo hatuna haja ya kujidaili kwa sasa.
Katika sehemu inayofuata tutaitizama nyaraka nyingine iliyowasilishwa Dodoma – yani Sheria Namba 18, ya Machi 24, Mwaka 1965, kisha tutajadili kwanini, kama ilivyoile nyaraka nyingine (sheria namba 18, 1965), Nyaraka hii (Sheria namba 22, 1965), pia ni batili kwa matumizi ya Muungano .
UMUHIMU WA sheria namba 18 ulikuwa ni kuichakachua ibara ya ibara ya (7) ya Mkataba wa Muungano ambayo ilielekeza Rais Wa Muungano na Makamu wake (Rais wa Zanzibar) katika kipindi cha mpito (Mwaka Mmoja), waunde TUME YA KATIBA na BARAZA LA KUTUNGA KATIBA. Ibara hii ya (7) ya Mkataba wa Muungano inasema hivi:
(vii) Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kukubaliana na Makamo wa Rais ambaye ni kiongozi wa serikali ya Zanzibar
a) Atateua tume kwa ajili ya kutoa mapendekezo kwa ajili ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.
b) Ataitisha Baraza la kutunga katiba ikiwa na wawakilishi kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa likutane katika kipindi cha mwaka mmoja tokea kuanza kwa muungano kwa madhumuni ya kutafakarimapendekezo ya tume iliyotajwa juu na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Lakini kilichotokea MWEZI MMOJA tu kabla ya kipindi cha mpito (mwaka mmoja) kuisha muda wake, Bunge la Muungano likapitisha sheria tajwa hapo juu (Sheria Namba 18 ya Mwaka 1965). Lengo la Sheria ilikuwa ni kuhairisha masharti ya ibara ya ibara hii (7) ya Mkataba wa Muungano kwa muda usiojulikana, hivyo kwenda kinyume na maelekezo ya Mkataba wa Muungano (1964).
Sheria Namba 18 ya Mwaka 1965 ilieleza yafuatayo:
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Sheria Namba 18 ya 1965
NAKUBALI
J.K NYERERE
Rais
MACHI 24, 1965
Sheria ya Kuongeza Muda Wa Kuitisha Baraza La Kutunga Katiba
Jina Fupi na Tafsiri Sheria Na. 22 1964 GN. Na 243 1964
IMETUNGWA na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1. Sheria hii inaweza ikaitwa Sheria ya Baraza la Kutunga Katiba ya 1965 na itasomwa kama sheria moja na Sheria za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Kuongeza muda wa kuteua Tume ya Kuitisha Baraza la Kutunga Katiba
2. Bila ya kuathiri masharti ya Sheria za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar au yale ya Mkataba wa Muungano baina ya jamhuri ya zamani ya Tanganyika na Jamhuri ya zamani ya watu wa Zanzibar, Rais wa Jamhuri ya Muungano hatalazimika kuteua Tume ya kutoa mapendekezo ya katiba kwa ajili ya Jamhuri ya Muungano, au kuitisha kikao cha Baraza la Kutunga Katiba kwa ajili ya kuyatafakari mapendekezo hayo na kupitisha Katiba, katika kipindi cha mwaka mmoja toka kuanza kwa Muungano isipokuwa Rais kwa kukubaliana na makamu wa Rais ambae ndiye Mkuu wa Serikali ya Zanzibar atateua Tume hiyo na kuitisha kikao cha Baraza la Kutunga Katiba wakati atakaoona unafaa.
3. Bila ya kuathiri masharti ya Sheria za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar marejeo ya Sheria hizo kuhusu Baraza la kutunga Katiba lililoitishwa kwa mujibu wa kifungu cha (2) cha sheria hii lakini kuyafanya yawe yametolewa na Mkataba wa Muungano na kipindi cha mpito kiichoelezwa humi kitaongezwa muda itakavyokuwa.
Nathibitisha kuwa Muswada kuwa Sheria hii ulipitishwa na Bunge kwa mujibu wa masharti ya ibaraya 35 ya Katiba.
Dar-es-salaam
A.S MKWAWA
MACHI 24, 1965
Spika
Umepitishwa na Bunge siku ya Kumi na Nane Ya Mwezi wa Machi, 1965.
P. MSEKWA
Karani wa Bunge
Source: [Source: Jumbe, A (1995): The Partner-ship – Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Miaka 30 Dhoruba.
Kufuatia sheria hii, Muungano ukakosa fursa muhimu ya kupata katiba yake ya kudumu kwa mujibu wa matakwa ya ibara ya (7) ya mkataba wa muungano (1964), na badala yake muungano ukaingizwa chini ya Katiba ya muda kwa muda usiojulikana. Huu ulikuwa ni mwanzo wa tatizo kubwa mbeleni kama Shivji (1990, 2005 &2008) anavyolijadili.
Sambamba na Sheria hii namba 22 ya Mwaka 1965, MIEZI MINNE baadae, Bunge la Muungano pia likapitisha sheria nyingine – tarehe 11, Julai 1965, sheria iliyojulikana kama "KATIBA YA MUDA YA TANZANIA (Sheria no. 43) ambayo ilitengeneza madaraka kwa serikali ya jamhuri ya muungano na pia kwa serikali za nchi washiriki wa muungano.
- Je, Katiba Ya Muda (1965) ilitambua uwepo wa TANGANYIKA?
Inaendelea bandiko linalofuatia…