Siri ya Malkia Elizabeth wa Usikochi (UK), Kanisa Katoliki, Nyerere na Uhuru wa Tanganyika

Siri ya Malkia Elizabeth wa Usikochi (UK), Kanisa Katoliki, Nyerere na Uhuru wa Tanganyika

Ili tufanye mnakasha wenye manufaa kwa wanaotusoma ni vizuri ukawa na adabu na heshima kijana wangu,

Kwenu hakuna wakubwa?

Wakubwa Kihehe maana yake nini?
Au kihehe mkubwa ni TAPELI maskini kama wewe!.
We mtoto shukuru sana JF! tena Sana.
Umeweza kutapeli wajinga Kupitia humuhumu na bahati mbaya Hao victims hawakwenda Shule km wewe.

We si unajiita MTUNZI?
Sasa ili watu wanaokuona we ni mpuuzi usie na Elimu km mimi nimeomba Utuwekee Qualifications zako hapa ili Siku ingine ukiandika Kitu tufahamu kuwa Msomi kaandika.

Umeshindwa Kufanya hivyo kwa sababu HUNA ELIMU YYT wewe.
Ni mwizi tu km hio mijizi mingine iliotapakaa hapa mjini.
Unajikweza mara Una Makampuni, mara Unaingiza vitu kutoka nje, mara mtoto wa Mwalimu nyerere! Leo unajibandika Cheo cha UANDISHI.
Very soon utasema We rubani au Mkuu wa chuo!

Teh teh teh teh!

Thats what we call foolishness.

Yericko let me tell you this Foolishness is more than being stupid, that deadly combination of arrogance and ignorance.
 
Last edited by a moderator:
Sasa ndio uamini, wewe pamoja na ghubu zako zote kama bimdogo, mimi hao wazee wakiislamu wananiamini kama kijana wao.

Teh teh teh!

Tazama Unavyojichanganya Sasa.!
Unasema Waislamu MAGAIDI,

Mara Ghafla Waislamu Hao hao Wanakutambua wewe kuwa ni KIJANA wao.

Ndio andiko likasema.

MITHALI 18 :7

"Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake, Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake."

Tazama Unavyojiabisha sasa.
 
Wakubwa Kihehe maana yake nini?
Au kihehe mkubwa ni TAPELI maskini kama wewe!.
We mtoto shukuru sana JF! tena Sana.
Umeweza kutapeli wajinga Kupitia humuhumu na bahati mbaya Hao victims hawakwenda Shule km wewe.

We si unajiita MTUNZI?
Sasa ili watu wanaokuona we ni mpuuzi usie na Elimu km mimi nimeomba Utuwekee Qualifications zako hapa ili Siku ingine ukiandika Kitu tufahamu kuwa Msomi kaandika.

Umeshindwa Kufanya hivyo kwa sababu HUNA ELIMU YYT wewe.
Ni mwizi tu km hio mijizi mingine iliotapakaa hapa mjini.
Unajikweza mara Una Makampuni, mara Unaingiza vitu kutoka nje, mara mtoto wa Mwalimu nyerere! Leo unajibandika Cheo cha UANDISHI.
Very soon utasema We rubani au Mkuu wa chuo!

Teh teh teh teh!

Thats what we call foolishness.

Yericko let me tell you this Foolishness is more than being stupid, that deadly combination of arrogance and ignorance.

Billy, mbona unafanya fujo?! We unamshambulia mtoa mada tu... kwanini usikae chini, ujifunze zaidi?!
 
Last edited by a moderator:
Tabia za Watoto watokao ktk michepuo hupendelea Kurusha maneno ya mipasho kila Wanaposhindwa na Hoja.

Msomi au mwenye Utambuzi wa mambo hata siku moja haandiki "...sijui bla bla bla". Wala Harushi lawama kwa mtu bila Kudadavua Kile anachotaka Kuonyesha Umma Kuwa sio sawa.

Lkn bahati mbaya Hizi tabia Za Watoto wa michepuo Hakuna Jamii ikaweza Kuziepuka.
Ndio tukawa tunahimiza sana kwa Wazazi kuwa Ni Bora Kubaki Njia Kuu. Mchepuo sio Dili.
Watoto wakikua Bila malezi ya BABA jamii hupata tabu nyingi tu.

Na nyie ni Mifano Hai ya matatizo hayo.
Na Bahati yenu Mmemkuta Mzee Mohamed Said Ni mzee mwenye Subra.

Virukanjia km nyie Hamstahiki kabisa Kujadiliana na Mzee mwenye Elimu Na Heshima ktkJamii km Huyu.
Huruma zake Na Uungwana Wake Wakati mwingine Unapita Kiasi mpaka Anavunjiwa Heshima na vikojozi wasio na Elimu Hapa Jukwaani.
Remember you two that The truth is hard to swallow when you're choking on your pride...

Bill Cosby,
Mtume SAW anasema halitiwi jambo upole ila litapendeza.
Maalim wangu Sheikh Haruna akituasa kuhusu kujibu matusi na upuuzi.

Alikuwa anasema mtu akikutukana au kukukebehi wewe jiweke pembeni.
Mimi sina sababu ya kutukanana na hawa watu.

Nakuwekea hapa picha niliyopiga katika maziko ya Hassan Upeka nyumbani
kwake Mwananyamala mwaka wa 2010.

SAM_1033.JPG


Ni nani huyu Hassan Upeka?
Soma hapo chini umjue Hassan Upeka.

[TABLE="width: 601"]
[TR]
[TD]"When Abdulwahid died the Ministry of Information issued a press release announcing that the President had attended the funeral of Abdulwahid Sykes.[1] Surprisingly the press release gave few details of his government service, completely eclipsing his checkered political career. It was an Englishman, Brendon Grimshaw, the editor of Tanganyika Standard, who published a fitting obituary to Abdulwahid describing him as: ''one of the architects of the independence movement and one of the men who helped launch President Nyerere on his political carrier...''[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]The obituary also paid glowing tribute to the family on its contribution to the political development of Tanganyika by mentioning that ''much of the desire among Africans for a powerful political party in Tanzania came from the drive of the Sykes family.'' [2] It is said that this recognition of Abdulwahid as one of the founding fathers of the nation became a focus of attack from certain members of the TANU leadership. They were overheard grumbling in the corridors of the TANU headquarters in Dar es Salaam that Ally and Abbas Sykes were trying to glorify their elder brother. At the time of Abdulwahid's death, Abbas Sykes was Counselor at the Tanzania High Commission in Canada and Ally Sykes had resigned from politics and government service and was a private businessman. Ally Sykes had unceremoniously been made to resign from government service for failing to abide by the leadership code which required senior government officials not to own property or be engaged in business.[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]This position was to assert itself years later when the Party was researching its history. A research assistant by the name of Hassan Upeka, who happened to be one of earliest recruits of TANU, having joined the party directly from school in 1956, presented to the research panel, notes of an interview he had with Abdulwahid many years back. The research assistant was bluntly told that the intended book had nothing to do with Abdulwahid.[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


[1]See Press Release A/2746/68 IT/1.322 of 13 th October, 1968. East Africana, University
of Dar es Salaam.

[2] Sunday News, 20 th October, 1968.



Bill Cosby,
Nimemfahamu Hassan Upeka toka udogo wangu na alikuwa akiogopwa sana na watu wengi.
Kisa cha kuogopwa ni kuwa alikuwa katika TANU Intelligence.

Siku hizo watu waliokuwa katika kazi hizo wakitisha.
Alipostaafu kila nikikutananae alikuwa anaonyesha hamu ya kujisogeza kwangu kwa mazungumzo.

Siku moja akanikaribisha nende ofisini kwake Mtaa wa Mvita, Karikaoo.

Toka siku hiyo tukawa marafiki wakubwa na yeye alipojua kuwa naandika kitabu cha Abdul Sykes
Upeka alinifungulia moyo wake na akanishauri niende Maktaba ya CCM Dodoma nikafanye utafiti
wangu pale.

Upeka alinifahamisha kuwa yeye na Ditopile Mzuzuri ndiyo walikuwa waanzilishi wa maktaba ile pale
Makao Makuu ya CCM.

Nilkwenda Dodoma na nilifaidika na mengi na mengine nikaja kujaziwa na Upeka Dar es Salaam pale
ofisini kwake Mtaa wa Mvita.

Wengi hawafahamu lakini Upeka ndiyo mtumishi wa kwanza wa TANU akitoka Tabora School 1956
na jalada lake la kuajiriwa na TANU pale New Street ni no. 1.

Nina mengi ninayoyajua katika mengi aliyonisomesha kaka yangu Hassan Upeka.
Nina list niiyoandika kwa mkono ya wajumbe wa Mkutano wa Tabora wa 1958.

Abdul Sykes hakuwa mjumbe wa mkutano ule wala hapakuwa na agenda yoyote ya uchaguzi.
Nawaweka wajumbe kutoka Eastern Province hapa chini Wanamajlis mjionee:

Sheikh Suleiman Takadir, Julius Nyerere, Bibi Titi Mohamed, John Rupia, Elias Kissenge,
Dossa Aziz, Julius Mwasanyangi, Michael Lugazia, Ramadhani Chaurembo, Hussein Mbaruk,
Clement Mtamila, Idd Tulio, Mzee Salum, Idd Faiz Mafongo, Idd Tosiri, Haidari Mwinyimvua,
Rajab Diwani
na Juma Selemani (aka Juma Mlevi).

Wanamajlis,
Haya ni machache tu katika historia ya TANU na historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Billy, mbona unafanya fujo?! We unamshambulia mtoa mada tu... kwanini usikae chini, ujifunze zaidi?!

Lipi la kujifunza kutoka kwa huyu mtoto?

Anamwaga Uharo Jukwaani Akiulizwa maswali Analeta Ngonjera na majigambo ya kizamaani km mlevi wa chibuku.

Unaweza kujifunza kwa Mtu asie na ELIMU?
Hebu Muulize Ana Qualifications gani za Kujiita Yeye MTUNZI WA VITABU?
Manake mimi nimemuuliza mara nyingi lkn ananiletea Nyimbo za Mipasho na Taarabu km bi kidude.
 
Katika kitabu chake akimwelezea Abdul Sykis, bwana mohamedi said ametoa shutuma nyingi sana kwa Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikiwemo ya eti Mwalimu katika hotuba yake ya kuaga taifa alitamka wazi kuwa hamjui ABDUL SYKES, Inashangaza sana kwani Mohamed Said anajua wazi ameudanganya umma na kudhihaki wanaukombozi wetu.

Ilikujiridhisha ndugu zangu wadau pitieni sehemu ya Hotuba ya Mwalimu Nyerere ya kuaga taifa tarehe 5 Novemba, 1985 kabla hajastaafu urais aliyoitoa mbele ya wazee wa Dar es Salaam,




‘"Mimi nimeanza siasa na wazee wa Dar es Salaam; na wazee wa Tanzania. Nimeanza nao mapema sana; mapema kweli. Nilirudi kutoka masomoni, Uingereza Oktoba 1952 – miaka 33 nyuma. Wakati huo nikiwa kijana mdogo wa miaka thelathini na kidogo hivi.

Niliporudi nikakubaliana na wamisionari hapo Pugu (sekondari), nifundishe shuleni kwao. Lakini nikiwa shuleni – Chuo Kikuu – nilijua. Niliishaamua kwamba maisha yangu yatakuwa ya siasa. Niliamua hivyo: Nitafundisha kwa muda wa miaka mitatu, nione hali inavyokwenda na kuzoeana na wenzangu kabla ya kuanza maisha ya siasa.

Niliporejea nchini hapo Oktoba, nikaenda Butiama. Januari nikarudi Dar es Salaam. Nikaanza kazi. Nikataka kujua habari za African Association. Mzee Mwangosi anakumbuka. Yeye ndiye aliniambia habari za African Association. Aliisha niambia habari hizo tangu nikiwa Makerere – Chuo Kikuu – nikiwa mwanafunzi.

Pale, mimi na wanafunzi wenzangu tulikuwa tumeanzisha chama kinachoitwa Tanganyika African Welfare Association (TAWA) cha wanafunzi wa Tanganyika; mimi nikiwa katibu wao. Hapa tukaona mambo yanakwenda vizuri kidogo.

Tukaona kwanini TAWA iwe ya wanafunzi peke yao na siyo Tanganyika nzima. Kwa hiyo nikawaandikia baadhi ya watu Tanganyika. Nikasema, jamani ee, tumeanzisha chama, kwanini msianzishe huko matawi ya chama hicho?

Ndugu Mwangosi akapata barua hiyo. Alikuwa miongoni mwa waliopata barua hiyo. Akaniandikia – nikiwa Makerere – akasema: wewe kwanini unataka kuanzisha chama kipya? Kipo chama. Kipo chama cha TAA (Tanganyika African Association).

Kwa hiyo la maana siyo kuanzisha matawi, maana chama kipo na matawi yameenea; la maana ni kwamba hicho chama chenu mfute, na muanzishe tawi la Tanganyika African Association.

KUVUNJWA KWA TAWA

Hivyo ndivyo tulivyofanya. Kwa hiyo mimi nikawa katibu wa katawi ka TAA hapo Makerere. Niliporudi Tabora na kuanza kufundisha pale St. Marys (sasa inaitwa Sekondari ya Milambo), nikachaguliwa katibu wa TAA wa jimbo ambalo makao yake makuu yalikuwa Tabora. Ulipofanyika mkutano wa TAA mjini Dar es Salaam, nilihudhuria nikiwa mjumbe kutoka Tabora.

Kwa hiyo nilikuwa naijua Tanganyika African Association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda Ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za TAA. Sasa niliporudi, baada ya kukaa Pugu siku chache, nikaja mjini Dar es Salaam. Nikauliza nani wanaongoza TAA? Nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.

Nilipelekwa na Kasela Bantu - ambaye naye aliteleza-teleza na hatunaye hapa (kwenye mkutano). Kasela Bantu alikuwa mwalimu mwenzangu. Tulifundisha pamoja Milambo. Nilipokuja Dar es Salaam, nikakuta anafanya kazi Redio (Tanganyika Broadcasting Corporation). Ni Kasela Bantu aliyenipeleka kwa Sykes.

Wakati huo mambo yalikuwa yanasinzia kidogo. Kwa muda mfupi mwaka ule, tukafufua-fufua, hasa kutoka Januari. Kufika Aprili, TAA ikafufuka. Tukafanya mkutano hapo Anautouglou. Kwenye mkutano huu wakanichagua kuwa Rais wao – wa TAA.

Ninasema yote haya kwa shukrani kwa wazee. Jamaa hawa walikuwa watu wazima wa Dar es Salaam, na mimi kijana mdogo Mzanaki, na Kiswahili changu si kizuri sana – cha matatizo.

Nimekuja, natoka Ulaya, tena masomoni. Muda mfupi tu jamaa hawa wakaniamini haraka sana – katika muda wa miezi mitatu. Wakanichagua Rais wa TAA. Hapo ndipo nilianza shughuli mpya ya kuandika katiba ya TAA na kuipa madhumuni hasa ya shabaha ya kuleta uhuru.

Baada ya miezi 13, hapo 1954, tukaanzisha TANU. Jina hili lilipendekezwa na akina Abdul Sykes. Walikuwa wamelifikiria tangu zamani, walipokuwa askari vitani huko Burma (Vita vya Pili).

WAZEE NA MSIMAMO

Miezi minne baada ya kuanza kazi Pugu nikawa ninakuja Dar es Salaam, kwa mguu; kila Jumamosi. Baadaye wazee wakanipa baiskeli nikawa ninakuja mjini kukutana na wenzangu; kufanya mikutano.

Hivyo ndivyo tulivyofanya. Wazee wakaniamini upesi sana. Tukawa na uhusiano mkubwa sana. Wadogo wenzangu wengine walikuwa Abdul Sykes, Abass Sykes (mdogo wake), Dosa Aziz – waliokuwa wengi ni wazee.

Katika kuhutubia mikutano yangu, nilikuwa nikisema: Wazee na Ndugu zangu! Wazee hasa ndio walikuwa na mikutano ya awali ya TAA na TANU. Walikuwa na msimamo wa hali ya juu kabisa! Hawakuyumba hata kidogo! Vijana walikuwa na mashaka. Wengine walikuwa na vikazi vyao, waliogopa kuvipoteza.

Nalo jambo lenyewe ni la hatari – la kuzungumzia uhuru! Unaweza ukakosa kazi; na wapo waliopoteza kazi; wengine wakaacha kazi. Akina Rashid (Kawawa) waliona watoke kwenye shughuli hizo tuje tuungane katika chama.

Wazee wa Dar es Salaam, na baadaye wa nchi nzima, wakatuunga mkono, na kila nilipokwenda, watu wa kwanza walionielewa, walikuwa wazee.

Nilikwenda Songea mwaka 1955 mara baada ya kujiuzulu. Huko wazee walinipokea na kunielewa. Nilianza safari za kuitembelea Tanganyika nzima. Nilikwenda Mbeya. Mkutano wangu niliufanya na wazee; kikundi kidogo cha wazee, ndani ya nyumba ya mtu.

Kwa mkutano huu wa Mbeya, wazee wakauliza: Unatafuta nini? Nikawaambia natafuta uhuru. Wale wazee, kwa sababu ya vita vya Maji Maji, na wanakumbuka, kabisa, wakaona mimi ninatafuta jambo la hatari. Tulifanya mkutano wa makini kweli. Wakauliza: Wewe unawezaje kuleta uhuru? Wewe una njia gani kudai uhuru na usitiwe kitanzi na Waingereza?

WAINGEREZA WAONGO

Tulielezana. Nikawaambia ninyi wazee, Waingereza wanawadanganya, Waingereza wametumwa na ule Umoja wa Mataifa uliokufa (League of Nations), waje kuishika Tanganyika kwa muda tu; watusaidie, na wakati tutakapokuwa tayari, watuachie tukajitawale.

Waingereza wanafanya ujanja; hawasemi. Vita vimekwisha (vya Pili) na Umoja wa Mataifa mwingine – mpya (United Nations Organisation – UNO) umewakabidhi Tanganyika kwa shabaha ileile. Sisi siyo koloni lao. Wamepewa dhamana tu.


Kwa hiyo nikawaambia wazee, hakuna haja ya kumwaga damu. Tuwaseme tu! Tuwashitaki kwa waliowaleta hapa kwamba hawafanyi kazi yao; wamesahau kabisa!

Wazee wakauliza: Eh, inawezekana? Nikasema inawezekana. Kazi yetu ya kwanza ilikuwa kuwaambia watu kwamba uwezekano wa kujitawala upo. Hilo lilikuwa la kwanza. Wazee walijua maana ya kujitawala. Walitamani kujitawala, lakini hawakujua waanzie wapi.

Vijana hawakuwa na habari kwamba kujitawala kunawezekana. Kwa hiyo kwa wazee sikuwa na matatizo. Wao hawakuwa na kazi; hawakumwogopa Mwingereza. Hawakuogopa kufukuzwa kazi. Baadhi walikuwa wafanyabiashara.

Mzee John Rupia (marehemu) alikwua mfanyabiashara na kaidi kidogo. Aliwahi kutishwa na kunyang’anywa leseni yake ya biashara. Akaambiwa akiendelea kushirikiana na kijana mwenda wazimu (Julius Nyerere), atanyang’anywa leseni moja kwa moja. Rupia aliwajibu: Potelea mbali!

Nasema yote haya ikiwa njia ya kutoa shukrani kwa wazee na imani yao kwa vijana wakati huo.

Imani hujenga imani. Na mambo haya makubwa ya nchi, kama hayana baraka za wazee hayaendi. Magumu sana. Wanasema ngoma ya watoto haikeshi! Mimi nilipata baraka za wazee tangu zamani. Tangu awali kabisa.

TWAININGI AMEKWISHA

Siku moja, Dosa akanifuata Magomeni (Dar es Salaam). Akasema: Leo wazee wanakutaka. Wapi? Kwa Mzee Jumbe Tambaza. Wanakutaka usiku. Nikasema haya, nitakuja. Nikaenda. Nikakuta wazee wameshakaa; wameniita kijana wao kuniombea dua. Mimi Mkristo, wao Waislamu watupu. Wakaniombea dua za ubani. Tukamaliza.

Tulipomaliza wakasema kuna dua pia za wazee wao. Basi wakanitoa nje. Tukatoka. Zilipomalizika zilikuwa za Korani; sasa zikaja dua za wazee – za jadi.

Walikuwa na beberu la mbuzi. Wamechimba shimo. Wakaniambia simama. Nikasimama. Beberu akachinjwa, huku anaambiwa, “Twining (Twainingi) umekwisha!” (Edward Twining alikuwa Gavana wakati huo). Ndipo nikaambiwa: Tambuka! Nikavuka lile shimo. Hapo nikaambiwa na wazee: Basi nenda zako; tangu leo Twainingi amekwisha!

Sasa mimi Mkristo; hao Waislamu. Na mimi mkorofi-korofi katika mambo haya (ya kutambika). Lakini tulikuwa tunaelewana na wazee wangu hao. Kwa hiyo nilitambuka pale na kuambiwa: Nenda nyumbani salama. Twaining hawezi tena!

Wazee wangu wengine wanakumbuka tulikuwa tunakwenda Bagamoyo. Kwenye makaburi kule! Tunapiga dua huko kwenye makaburi na wazee wangu.

Baadhi yetu mtakumbuka safari moja jamaa wa Kenya, hawa akina Tom Mboya (marehemu) walishitakiwa. Tukasema tuwasaidie. Tuwasaidie vipi? Tukasema tufunge. Tukaomba nchi nzima kufunga siku hiyo. Tufunge! Tukafunga. Hakuna kula. Na siku ya kufunga tulikuwa na mkutano Bagamoyo. Tukaenda huko. Tukafanya mkutano hadi saa 12 jioni.

Baada ya mkutano tukaenda nyumbani kwa Mzee Mohamed Ramia (marehemu). Hapa ndipo tulikuwa tumefikia. Mimi nikamuuliza mzee: Sheikh, una Aspro? Akajibu: Kwa nini unataka Aspro? Nikajibu kuwa kichwa kinaniuma kwelikweli. Akasema subiri.

Tulisubiri hadi saa ya kufuturu. Tukafuturu vizuri. Mzee Ramia akaniuliza: bado unataka Aspro? Nikajibu kichwa sasa hakiumi. Kumbe ilikuwa njaa.

Nawaelezeni haya kwa sababu huko tulikotoka, tulishikamana sana. Tulishirikiana sana na wazee."’


Mohamed Said kuwa mkweli, waambie ukweli watanzania (waislamu) kuwa umetumia mgongo wa Uislamu na Hayati Abdul Sykes, kwakumkashifu na kumdhihaki Hayati Mwalimu Julius Nyerere na kuwasafisha wazee wako walioasi serikali mpya ya Mwalimu ambapo ndipo madhila hayo wakayapata.
 
Last edited by a moderator:
Wakubwa Kihehe maana yake nini?
Au kihehe mkubwa ni TAPELI maskini kama wewe!.
We mtoto shukuru sana JF! tena Sana.
Umeweza kutapeli wajinga Kupitia humuhumu na bahati mbaya Hao victims hawakwenda Shule km wewe.

We si unajiita MTUNZI?
Sasa ili watu wanaokuona we ni mpuuzi usie na Elimu km mimi nimeomba Utuwekee Qualifications zako hapa ili Siku ingine ukiandika Kitu tufahamu kuwa Msomi kaandika.

Umeshindwa Kufanya hivyo kwa sababu HUNA ELIMU YYT wewe.
Ni mwizi tu km hio mijizi mingine iliotapakaa hapa mjini.
Unajikweza mara Una Makampuni, mara Unaingiza vitu kutoka nje, mara mtoto wa Mwalimu nyerere! Leo unajibandika Cheo cha UANDISHI.
Very soon utasema We rubani au Mkuu wa chuo!

Teh teh teh teh!

Thats what we call foolishness.

Yericko let me tell you this Foolishness is more than being stupid, that deadly combination of arrogance and ignorance.

Wala hilo lisikuume sana kijana, mimi ninaumhimu mkubwa kwa taifa hili kuliko wewe,

Hilo utapinga, utalia, utatapika, lakini huo utabaki kuwa ndio ukweli.

Nani anakutambua wewe Bilikobla ikiwa hata jf tu unaiogopa kama ukoma?
 
Last edited by a moderator:
Cosby kila nikisoma andishi la Yeriko nazidi kupata mashaka na afya ya akili yake
 
Bill Cosby

Unataka kusomeshwa juu ya kitabu changu kiitwacho vita dhidi ya ugaidi ama unataka kuendelea kuropoka na maneno yako machafu kama upo eda?
 
Last edited by a moderator:
Lipi la kujifunza kutoka kwa huyu mtoto?

Anamwaga Uharo Jukwaani Akiulizwa maswali Analeta Ngonjera na majigambo ya kizamaani km mlevi wa chibuku.

Unaweza kujifunza kwa Mtu asie na ELIMU?
Hebu Muulize Ana Qualifications gani za Kujiita Yeye MTUNZI WA VITABU?
Manake mimi nimemuuliza mara nyingi lkn ananiletea Nyimbo za Mipasho na Taarabu km bi kidude.

Elimu ya uandishi, Kitabu unaandika tu, kwani wangapi wameweza kuandika?! Kwani kazi ya wahariri ni ipi?!
 
Watu hawafahamu kwanini idhaa nyingi za kiswahili zina watangazaji wenye mlengo mmoja, Hali hii ni kutokana na sekta ya habari kwa Afrika na hasa Afrika Mashariki kuwa ndio sekta kimbilio la waliofeli masomo yote, yaani sekta ya wajinga darasani. Utaona jamii fulani ya watangazaji wa idhaa za kiswahili duniani ndio inayohudumu kwa wingi, jamii hiyo hasa ya mwambao ndio ambayo huwa si rafiki wa elimu kwakisingizio kuwa wao husoma elimu ahera sio elimu dunia ya makafili/wazungu, Sasa hao ndio watangazaji wa bbc, dw, nk. Je unataraji wasiwe kipenzi cha mzee huyu muongo Mohamed Said?
Ni idhaa za hovyo sana, BBC wenyewe wanadhani kwamba wanajenga mahusiano.Ila hadi sasa wamekuja kundua kwamba multiculturism ni failure na tools za kuwapa viwango duni nafasi ya ku abuse resources kwa course mbaya.Haroub Othman alikuwa kainitia kichefuchefu sana haswa,alivyokuwa akipewa mic kwa sanaa km za huyu mzee asiye na soni wala haya.Kuchangia kuhusu sera za marekani, lazima aem israeli sijui na nani ktk issue zinazohusu ugaidi ktk mbingu za magaidi...afie kuzimu yule jamaa.
 
Last edited by a moderator:
Cosby kila nikisoma andishi la Yeriko nazidi kupata mashaka na afya ya akili yake

Teh teh teh!
Mkuu huyu mpuuzi watu wanashindwa kumdadavua hapa kwa kupenda hivi vichekesho vyake.
Watu wamemgeuza Km KINGWENDU.
Tatizo ni kwamba Akiachiwa muda mrefu Anatumia maandiko haya haya Kuibia Wajinga huko mitaani.

Tazama hapo juu.
Anasema Yeye ni MUANDISHI HODARI Anafahamika SANA USA!
teh teh teh, sasa hizi km sio bangi mbichi Ni Nini?
Halafu anamalizia kuwa Yeye ni MUHIMU SANA Ktk Hili TAIFA.

Huyu Sio Amnesia tu inayo msumbua. Kuna Maradhi yanaitwa borderline personality disorder (BPD), na bahati mbaya Dawa Bado haijapatikana. Huyu mtoto yamemvaa vibaya mno.
 
Elimu ya uandishi, Kitabu unaandika tu, kwani wangapi wameweza kuandika?! Kwani kazi ya wahariri ni ipi?!

Msamehe huyu mgonjwa wa akili anafikiri uandishi wa vitabu/simulizi husomewa,

Amuulize Mohamed Said kasomea wapi na anangazi gani ya usomi wa uandishi wa vitabu?

Mohamed Said kwa fani ni kuli wa bandalini, utunzi/uandishi nikipaji tu,
 
Last edited by a moderator:
Elimu ya uandishi, Kitabu unaandika tu, kwani wangapi wameweza kuandika?! Kwani kazi ya wahariri ni ipi?!

Huyu hajasema Yeye ni Muhariri.
Huyu Anajiita MTUNZI!! lzm uone tofauti hapo.

Na uhariri pia Unataka Elimu. Unless uwe ni ule uhariri wa magazeti ya UDAKU. Ama Km ni Hivyo basi Aseme hapa Kuwa Yeye ni Muhariri wa UDAKU leo ili watu Wasiibiwe na Huyu mtoto.

Na Hapo Anapoandika kuwa Yeye ni MUANDISHI anaejulikana USA we Umemuelewa Anajulikana USA as United States of America?
Au USA pale Kwenye Kijiwe cha Wauza BANGE kigogo?

Hawa Matapeli wa Kujifunza Kuwakamata Ni dakika tu.
 
Ni idhaa za hovyo sana, BBC wenyewe wanadhani kwamba wanajenga mahusiano.Ila hadi sasa wamekuja kundua kwamba multiculturism ni failure na tools za kuwapa viwango duni nafasi ya ku abuse resources kwa course mbaya.Haroub Othman alikuwa kainitia kichefuchefu sana haswa,alivyokuwa akipewa mic kwa sanaa km za huyu mzee asiye na soni wala haya.Kuchangia kuhusu sera za marekani, lazima aem israeli sijui na nani ktk issue zinazohusu ugaidi ktk mbingu za magaidi...afie kuzimu yule jamaa.

Hayo ndio maajabu ya vyombo vyetu vya Afrika,
 
Cosby kila nikisoma andishi la Yeriko nazidi kupata mashaka na afya ya akili yake

Kivava,
Hapa chini ninafanya mahojiano na Al Jazeera.
Sijui kama hawa nao ni wajinga sawa na BBC...

Walikuja nyumbani kwangu mwaka wa 2007 na tukafanya kipindi cha saa nzima:

CIMG1164.JPG
 
Huyu hajasema Yeye ni Muhariri.
Huyu Anajiita MTUNZI!! lzm uone tofauti hapo.

Na uhariri pia Unataka Elimu. Unless uwe ni ule uhariri wa magazeti ya UDAKU. Ama Km ni Hivyo basi Aseme hapa Kuwa Yeye ni Muhariri wa UDAKU leo ili watu Wasiibiwe na Huyu mtoto.

Na Hapo Anapoandika kuwa Yeye ni MUANDISHI anaejulikana USA we Umemuelewa Anajulikana USA as United States of America?
Au USA pale Kwenye Kijiwe cha Wauza BANGE kigogo?

Hawa Matapeli wa Kujifunza Kuwakamata Ni dakika tu.

Kwani kitabu chake ulishakiona, umekisoma?! Sasa kama hujakisoma kwanini unatia shaka?!

Yericko huwa anaandika hadi kwenye magazeti sio yale ya udaku...
 
Back
Top Bottom