Siri ya vuja posho bunge la katiba,Mwigulu azuia hazina kutoa posho z ya laki 7,fao la jumla ml 5

Siri ya vuja posho bunge la katiba,Mwigulu azuia hazina kutoa posho z ya laki 7,fao la jumla ml 5

Tema Mate

Senior Member
Joined
Dec 19, 2013
Posts
107
Reaction score
193
1901173_215680451967524_1211509833_n.jpg

Wakati sakata la Posho za Bunge la Katiba zikiwa kwenye sintofahamu baada ya Wajumbe kadhaa kuanza kudai Posho kuwa hii inayotolewa ya Laki 3 haitoshi eti Maisha ya Dodoma ni Magumu pia Kazi wanayoifanya pale Bungeni ni Kubwa kuliko ile iliyofanywa na Tume ya Warioba.

Wakati hayo yakiendelea kufukuta,Chanzo cha Karibu Kabisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kinasema,Awali Posho za Wabunge zilikuwa laki saba 700,000/ kwa kila Mjumbe Kwa Siku.Pia mbali na laki saba hiyo,Ofisi ya Bunge wakishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu iliadhimia kumlipa kila Mjumbe wa Bunge Maalum Fao la Kuhitimisha Bunge Maalumu Tsh.Milioni 5.

Katika Kikao Kilichofanyika Tar.13.02.2014 Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dsm kikihusisha Katibu wa Bunge,Naibu Waziri wa Fedha(sera) Mh.Mwigulu pamoja na Ujumbe kutoka Ofisi ya Rais.Kwenye Kikao hicho.Mezani kulikuwa na agenda ya kuruhusu Malipo ya Posho kwa wajumbe wa Bunge Maalumu yawe tsh.700000/=

Msimamo Mkubwa Kutoka Hazina ulikuwa hazina haina fedha za Kulipa Wajumbe wa Bunge la Katiba kwa Kiwango hicho cha laki saba,Mwigulu akiwa ndiye muwakilishi kutoka hazina alisimamia kuwa "Wakati huu Nchi ikiwa na Madeni kwa Walimu,Huduma za Afya hazijaboreshwa,Miradi ya maendeleo kama barabara na Umeme bado sehemu zingine imesimama,Leo hii tutawambia nini Watanzania kwa kuwalipa watu wanaokwenda kukaa Bungeni kwa siku walipwe Laki Saba.

Hoja hiyo ya Mwigulu inadaiwa iliungwa Mkono na Ujumbe kutoka kwa Rais na hatimaye kushawishi kikao kikubaliane na malipo ya Laki tatu.
Kinachofanyika hivi sasa na tume iliyoundwa Bungeni kwaajili ya Kutafuta ufafanuzi wa ama kuongeza posho kimya kimya au kusimama na posho ya laki saba,Wajumbe wa tume wanapo mbioni kukutana na Hazina(mwigulu) kwaajili ya kuangalia uwezekano wa kuongeza Posho hizo,Japo Mwigulu kwenye kikao cha awali kwa waziri Mkuu aliapa kuto ruhusu fedha ya Wananchi kulipwa kwa watu wanaokaa tu Bungeni.

MY TAKE:Mwigulu Simamia hapo hapo,Walizani Hazina ni Uchochoro wa kukwapua Fedha za Umma.Rais atangaze wazi,Wajumbe wasiotaka Posho ya laki Tatu wajiorodheshe waondoke Bungeni,Afanye Uteuzi mwingine.
 
mwigulu tutakupoteza dakika japo kuwa unasimamia upande wa haki, KUMBE NDIO MAANA MWIGULU ALIKIMBIA BUNGENI AKAENDA KUFANYA MKUTANO WAKATI WENZIE WANAANGAIKA NA POSHO,
 
Kama ni kweli basi atakuwa amenusuru taifa kwa ufujaji wa pesa za umma
 
Katika kamati iliyoundwa CDM inawakilishwa na Mhs Mbowe. Msimamo wa chama hakuna kuongeza posho. Zikiongezwa tunajua waliokubali ni chama tawala na CCM B and C. Ieleweke!
 
Mkuu, Mwigulu Nchemba unamuogopa bure, hana uwezo kuchota pesa hazina.
 
Biva Nchemba piga kazi hao wahafidhina wanaokuchukulia poa wakukubali japo sie tunajua kazi yako ni nzuri sana
 
hawa jamaa waangalie maslai ya taifa kwanza, nafkirii raisi angewaambia ambao hawataki laki 3 waondoke tu
 

Attention seeker.
Publicity stunt za ajabu kweli kweli hizi.



Mkuu Tumaini Makene acha unafiki,ulitaka akubaki ndio uamini ama umuone anafaa?!

Au siku zote ninyi mnayaka tu kuona anakosea?!

Hayo malumbani yenu ya kisiasa pelekeni huko huko,ameharibu tutamwambia,amefanya vyema tutamsifia!!
 
Last edited by a moderator:
Siyo mwigulu aliyezuia ongezeko la poho yeye kama mwakilishi wa hazina alitakiwa aeleze hali halisi ya kipesa ikoje angekuwa mtu wa ajabu kusema kuna uwezo wa kulipa wakati pesa hamna kumbuka mpaka sasa serikali inakopa pesa nyingi toka kwenye mabenki ya kibiashara kwanini tusiseme waziri wa fedha amezuia posho kuongezwa
 
Mwigulu ni nani huko hazina ? Huyu ni naibu waziri hana sauti hana maamuzi , hana mamlaka , hana haki ya kusema bila kupewa kibali na waziri wa fedha .....huyu kazi yake ni Kujibu maswali na kutumwa kumwakilisha waziri...
 
Mwigulu anapambana na kamati ya Kina Mbowe inayolazimisha Posho iongezeke. Mungu akubariki Mh. Mwigulu.
 
Post nyingine huwa ni vituko vitupu.

mkuu, siyo vituko mwigulu ni mzalendo sana wa nchi, amegoma kabisa wajumbe bunge la katiba kuongezewa posho, kamati ya akina mbowe walikuwa wanashinikiza posho ziongezwe mwigulu akakataa, hongera sana mwigulu taifa linakutegemea
 
Back
Top Bottom