Siridhishwi na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo

Siridhishwi na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo

gstar

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2011
Posts
790
Reaction score
1,373
Awali ya yote, nipongeze juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya kiongozi wake Raisi Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha kuwa anatekeleza miradi yote iliyoachwa na mtangulizi wake hayati Dk. John Pombe Magufuli, pia kuibua miradi mipya na kuitekeleza kukamilifu.

Hata hivyo, kuna hali ya kusuasua kwa utekelezaji wa miradi mingi hasa ya ujenzi wa barabara, kwamba inachukua muda mrefu kukamilika ama inakamilika ikiwa chini ya kiwango. Kuchelewa kukamilika kwa miradi kunatoa mwanya wa rushwa na kuongezeka kwa gharama za utekelezaji. Ujenzi wa barabara unapochukua muda mrefu unaweza kusababisha uharibifu ama kuchakaa kwa miundombinu hiyo kabla hata ya mradi kukabidhiwa kwa serikali matokeo yake mzabuni atapaswa kurudia ama kukarabati mradi kwa gharama nyingine zilizo nje ya gharama za wali. Tuliliona hili kwenye mradi wa Mwendokasi Mbagala.

Nataka nitolee mfano wa barabara ya mwendo kasi awamu ya tatu na nne. Awamu ya pili ni ujenzi ulio husisha barabara ya Kilwa (barabara ya Mbagala) licha ya mradi ule kusemwa kwamba umekamilika bado umeonekana una mapungufu mengi, sehemu nyingi za barabara zimeonekana nyufa baadhi ya vituo vya mwendo kasi kutokuwa na ubora stahiki, na sehemu ya kingo za barbara kubomoka kabla ya matumizi rasmi. Hata hivyo mpaka sasa mradi wa mwendokasi Mbagala haujaanza kutumika licha ya adha kubwa wanayoipata wakazi wa Mbagala kwenye swala la usafiri. Mpaka najiuliza hivi Hawa viongozi wetu wana uchungu na maisha yetu kweli?

Barabara ya Gongo la Mboto au Nyerere Road naona ujenzi wake unasuasua ni zaidi ya mwaka tangu ujenzi ulipoanza, lakini kumbuka kwamba barabara hii ndio kioo cha Tanzania, wageni wengi wanapofikia hapa nchini wakitua Airport lazima wapite katika barbara hii sasa kitendo cha kuijenga barabara hii kwa zaidi ya mwaka mmoja, licha ya kuendelea kuwapa adha ya usafiri wakazi wa Gongo la Mboto lakini pia kinaharibu taswira ya nchi yetu hasa kwa wageni wanaotutembelea mara kwa mara.

Lakini wakati barabara hiyo ikiwa bado haija kamika tayari awamu nyingine ya ujenzi imeanzishwa ni katika maeneo ya katikati ya mji yote hayo yamesha bomolewa na kazi ya ujenzi inaendelea. Ninajiuliza ikiwa kipande cha barabara ya Gongo la Mboto hakija kamilika iweje waanzishe ujenzi mpya? Nilidhani ingekuwa busara kukamilisha ujenzi wa hatua moja kabla ya kuhamia hatua nyingine na iwapo kampuni iliyopewa tenda ni moja, itakuwa ni vigumu kusimamia maeneo yote hayo yanayo endelea na ujenzi kwa wakati mmoja, inaweza kusababisha barabara hizi kujengwa chini ya kiwango kutokana na usimamizi duni na upungufu wa rasilimali za kutosha kutekelezwa mradi kwa pamoja.

Kwa ushauri wangu ningependekeza kwamba serikali kupitia kwa wizara ya ujenzi na kamati za bunge iweze kutazama ujenzi wa barabara hasa ya mradi wa mwendokasi wa Dar es Salaam ili waone ni namna gani bora inayopaswa kuchukuliwa kutekelezwa ujenzi huo bila kuathiri shughuli za kibinadamu zinazo endelea ndani ya Jiji. Pia kuangalia uwezekano wa kuharakisha ukamilishwaji wa miradi kwa wakati na kwa uharaka. Kama nchi ya China walijenga hospitali kubwa ya kutibu wagonjwa wa korona ndani ya masaa 72 iweje kipande cha barbara kisichozidi kilomita 100 kichukue muda mrefu kukamilika?

Natanguliza Shukrani zangu za dhadi.

CC. Prof. Makame Mbarawa, Kassim Majaliwa, Dr. Philip Mpango, Dr. Mwigulu Nchemba.
 
hamia burundi. So says Dr. Mwigulu.
 
PhD uchwara haziyaoni haya. Fundi Maiko huko kijijini ndanindani hawezi panga kujenga kama mwehu namna hii. Ujenzi wa mwendokasi hapo Nyerere road ulitakiwa uwe wa haraka, badala yake wakatifua mashimo mpaka Gongo la Mboto kisha wakagawa tenda za kumwagilia maji kila siku maana rami imeisha. Wageni wanaenda na kutoka airport wamelowa vumbi, biashara alongside ile barabara zimekufa mfano mwekezaji wa Blue Sapphire jengo lake linapigwa vumbi kali zaidi ya mwaka sasa najua anakosa wateja wengi.

Bado Mbagala yaleyale, sasa wameamia mjini kati uko Buguruni mpaka Karume yaleyale. Mji unatema vumbi.
 
Kwa wale wanaoifahamu TANROADS kwa miongo zaidi ya miwili au mitatu, wanasema wakala huyu wa barabara yuko hoi.
TANROADS bado ina miradi mingi lakini haina fedha za kujiendesha.
Tatizo kubwa inaonekaka kwa sasa TANROADS pamoja na wizara yake ya Ujenzi si kipenzi cha serikali..

Nimekutana na makandarasi zaidi ya wawili na ni kilio bin malamiko ya kutolipwa fedha kwa wakati au hakuna kabisa.
 
Kwa wale wanaoifahamu TANROADS kwa miongo zaidi ya miwili au mitatu, wanasema wakala huyu wa barabara yuko hoi.
TANROADS bado ina miradi mingi lakini haina fedha za kujiendesha.
Tatizo kubwa inaonekaka kwa sasa TANROADS pamoja na wizara yake ya Ujenzi si kipenzi cha serikali..

Nimekutana na makamdarasi zaidi ya wawili na ni kilio bin malamiko ya kutolipwa fedha kwa wakati au hakuna kabisa.
Ndio hasara ya kuanzisha miradi Kwa pupa bila mkakati ,madeni tuu inayodaiwa ni balaa Bado fidia ni matrilioni.

Huwezi kuwa na taasisi ambayo haiwezi fanya ujenzi wake Kimkakati badala yake wanafanya Kisiasa.

Unaanzishaje ujenzi Kila mahala wa km 1,2,5,10 wakati ungejenga Barabara chache na hizo hela kupelekeshwa huko kiasi kwamba Tija ingeonekana.
 
Kwa wale wanaoifahamu TANROADS kwa miongo zaidi ya miwili au mitatu, wanasema wakala huyu wa barabara yuko hoi.
TANROADS bado ina miradi mingi lakini haina fedha za kujiendesha.
Tatizo kubwa inaonekaka kwa sasa TANROADS pamoja na wizara yake ya Ujenzi si kipenzi cha serikali..

Nimekutana na makamdarasi zaidi ya wawili na ni kilio bin malamiko ya kutolipwa fedha kwa wakati au hakuna kabisa.
Tatizo kubwa walilonalo Tanroads ni kwamba Wamekosa Ubunifu na Maarifa mazuri. Bado Wana fikra mgando Kama za Watu wa enzi za Ujima au Watu wa zama za mawe za kale wakati wapo kwenye Karne ya 21.
Yaani ni aibu tupu nchi hii, tumeshindwa kila kitu. Hakuna hata kitu kimoja au jambo moja lililo zuri ambalo tumefanya.

Tumeshindwa kila kitu kabisa!
 
Ndio hasara ya kuanzisha miradi Kwa pupa bila mkakati ,madeni tuu inayodaiwa ni balaa Bado fidia ni matrilioni.

Huwezi kuwa na taasisi ambayo haiwezi fanya ujenzi wake Kimkakati badala yake wanafanya Kisiasa.

Unaanzishaje ujenzi Kila mahala wa km 1,2,5,10 wakati ungejenga Barabara chache na hizo hela kupelekeshwa huko kiasi kwamba Tija ingeonekana.
Nilipita week ilio pita Jiji lenu pendwa la Dar, Nikaone badala ya kufanya project za maana mnaziba viraka tu barabarani.

mnajenga barabara kama mlivo kua mnajenga shule za kata, Shule inaanza 2012 ila maabara kujengwa 2022.
 
TANROADS hawana hela mkuu.
Haiwezekani labda kama Kuna Hila,unachukua fuel yote kwa Lita itakayotumika kwa namna yote hapa Tanzania unazidisha kwa kile kiwango kinachokatwa toka Kila Lita ya fuel consumed mzigo huo unaupeleka Tan road.si mabilioni hayo kama si Matrilioni,Sasa watakosa je fedha kwa mfano!
 
Haiwezekani labda kama Kuna Hila,unachukua fuel yote kwa Lita itakayotumika kwa namna yote hapa Tanzania unazidisha kwa kile kiwango kinachokatwa toka Kila Lita ya fuel consumed mzigo huo unaupeleka Tan road.si mabilioni hayo kama si Matrilioni,Sasa watakosa je fedha kwa mfano!
Wadau tumefuatilia.
TANROADS hawapewi hiyo fedha kama inavyostahili.
Siasa zinaua huyu wakala wa maendeleo.
 
Back
Top Bottom