Sisikii hamu ya kula na siumwi chochote, tiba ni nini?

Sisikii hamu ya kula na siumwi chochote, tiba ni nini?

KweliKwanza

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2016
Posts
3,520
Reaction score
2,816
Habari zenu wakuu,

Nina imani kila moja anaendelea na maisha yake vizuri.

Nina tatizo la kutosikia hamu ya kula na kukinai vyakula mapema. Sometimes naweza hata kuvukisha siku bila kula na njaa nisisikie.

Mwenye kujua hili tatizo either limemtokea yeye au mtu wake wa karbu naomba anieleze njia sahihi ya kuliovercome. Maana inafika wakati ukiwa unakula unajiuliza ndo hivi maishani kwangu kote itakuwa?

Sina vidonda vya tumbo na nahofia kuvipata..
 
hama nina hilo tatizo waka wa 5 huu nipo nalo tuu sijui tiba ni nn
 
Unaupungufu wa vitamin C. Kula matunda yenye uchachu kama machungwa, mananasi n.k
Pia unaweza kunywa dawa ya Vitamin B complex...
Hivi vyote vitakusaidia kuongeza appetite ya chakula...
Vitamin B nilikuwa nakunywa ila wap
Myb vitamin c mana silagi sana matunda
 
Habari zenu wakuu
Naimani kila moja anaendelea na maisha yake vzri
Nina tatizo la kutosikia ham ya kula na kukinai vyakula mapema. Somtyms naweza ata vukisha siku bila kula na njaa nisisikie. Mwenye kujua hili tatizo either limemtokea yeye au mtu wake wa karbu naomba anieleze njia sahihi ya kuliovercome. Maana inafika wakati ukiwa unakula unajiuliza ndo hivi maishan kwangu kote itakuwa

Sina vidonda vya tumbo na nahofia kuvipata
unaumwa kutokujisikia ham ya kula
 
Muda gani mpaka sasa huna hamu ya kula
Miaka mingi2 sahv naona nazidi2
Ila mwaka 2014 nilipoenda jeshin nilikuwa nakula sana kule nahisi kwa sababu ya kazi nyinginyingi
 
Oooh chukua Hiyo multiple vitamins then ufanye afya check up
 
Piga multivitamin,piga albendzole kidogo

Fanya mazoezi ya kutosha na weka timetable ya msos

Bila kusahau juis ya ukwaju mara 2 kwa siku

Nipe mrejesho ndani ya wki moja
 
Kwa kuanzia,kama hutajali unaweza kutupatia data zako binafsi za kiafya kama: umri,jinsia, urefu,uzito,kiuno na ulaji wako?
Mara nyingi huwa tunakula na kunywa kwa wingi zaidi ya miili yetu inavyohitaji ndio maana tunakuwa na vitambi, mahips na makalio makubwa. Hio sio afya nzuri hata kidogo ni ugonjwa.
 
Back
Top Bottom