Uchaguzi 2020 Sitaki kuwa mnafiki. WanaCCM awamu hii tunaburuzwa na Mwenyekiti

Uchaguzi 2020 Sitaki kuwa mnafiki. WanaCCM awamu hii tunaburuzwa na Mwenyekiti

Kumbuka juzi alivyo mjibu yule mjumbe toka songwe kwamba hao machotara kupewa vyeo ni matakwa yake binafsi.

Kwa sababu hao machotara toka upinzani walitakiwa wapite kwenye mchujo wa kawaida na kura zipigwe kama kawaida ila anancho kifanya maoni yote ya wana ccm anayapuuzi na kuweka yake.
Yaah. Hili limeanzia huko mkuu, tunamuliwa mambo badala ya waccm we nyewe kuamua. WanaCCM hatujaipenda hii.
 
Anachokitaka ndicho huwa. Na anafanya mambo kwa manufaa yake ya kisiasa. Kwanini nasema haya??

1. Angalia namna mchakato wa uchukuaji fomu za kugombea urais wa JMT ulivyokuwa na figisu. Eti wanaCCM wengine hawaruhusiwi kuchukua fomu. Ni yeye tu.
2. Angalia chaguzi za marudio ktk majimbo ambayo wabunge wapinzani "waliunga mkono juhudi". WanaCCM tulinyimwa kushindana nao. Na hata ktk uchaguzi huu tumepigwa marufuku kushindana nao.

3. Angalia upigaji kura ktk mkutano mkuu, ukusanyaji wa kura ulikuwa wa kimikoa (hii mbinu imewekwa ili iwe rahisi kutufuatilia wale ambao tungepiga kura ya hapana).

4. Kwa kinywa chake mwenyewe amesema kura za maoni za watia nia wa ubunge hazina maaana. Yeye amesema anaweza kumchukuwa hata mtu wa mwisho. Yaani badala ya wagombea kutafuta ridhaa ya wananchi, Sasa wanasubiri maamuzi hinafsi ya mwenyekiti.

Demokrasia imezikwa rasmi ndani ya ccm. WanaCCM tunapelekwa pelekwa tu.

Sio kwamba wanaccm hawaujui ukweli huu, ila wanakaa kimya maana wanajua pia bila madaraka ya huyo mwenyekiti, hata wao kutangazwa washindi itakuwa ngumu. Uzuri hata mwenyekiti mwenyewe wa ccm anajua fika bila kutumia madaraka yake vibaya, ccm hawawezi kutangazwa washindi. Ndio maana hakuna mwanaccm anataka kusikia kitu kiitwacho tume huru ya uchaguzi.

Hapo walipo wanaccm wanaomba usiku na mchana wapinzani wasusie uchaguzi. Wanajua fika iwapo wapinzani watakaza kushiriki huu uchaguzi, watatumia nguvu kubwa kujitangaza washindi, hali itakayoliacha taifa hili na mgawanyiko mkubwa, na sifa mbaya ya utawala wa mabavu.
 
Hakuna ccm hapo, ccm ndio imekufa hivo.
Wajumbe wanalia dodoma, wazanzibar jana wamelia machozi wengine wanaume.

Ccm iliyo baki ni Chama Cha Magufuli (CCM) na siyo Chama Cha Mapinduzi.
Tuliwaonya huyu ni dikteta, mkafikiri udikteta utaishia kubagua wapinzani.

Nyerere alisema dhambi ya ubaguzi ni kama kula nyama ya mtu, ukianza huachi.

Magufuli kasema bila aibu kwamba atamkata mtia nia yeyote, si kwa katiba, si kwa miongozo, si kwa taratibu, si kwa utamaduni,bali kwa jinsi takavyojisikia alivyoamka siku hiyo.

Yani kasema wazi yeye ni dikteta.

Kuna vikao ya kumfukuza Membe, anasema hajapeleka mjadala kwenye kikao aliogopa mjadala wa kikao, kamaliza habari mwenyewe katangaza tu. Haoni hata aibu.

Huyu dikteta ataiharibu sana hii nchi.
 
Anachokitaka ndicho huwa. Na anafanya mambo kwa manufaa yake ya kisiasa. Kwanini nasema haya??

1. Angalia namna mchakato wa uchukuaji fomu za kugombea urais wa JMT ulivyokuwa na figisu. Eti wanaCCM wengine hawaruhusiwi kuchukua fomu. Ni yeye tu.
2. Angalia chaguzi za marudio ktk majimbo ambayo wabunge wapinzani "waliunga mkono juhudi". WanaCCM tulinyimwa kushindana nao. Na hata ktk uchaguzi huu tumepigwa marufuku kushindana nao.

3. Angalia upigaji kura ktk mkutano mkuu, ukusanyaji wa kura ulikuwa wa kimikoa (hii mbinu imewekwa ili iwe rahisi kutufuatilia wale ambao tungepiga kura ya hapana).

4. Kwa kinywa chake mwenyewe amesema kura za maoni za watia nia wa ubunge hazina maaana. Yeye amesema anaweza kumchukuwa hata mtu wa mwisho. Yaani badala ya wagombea kutafuta ridhaa ya wananchi, Sasa wanasubiri maamuzi hinafsi ya mwenyekiti.

Demokrasia imezikwa rasmi ndani ya ccm. WanaCCM tunapelekwa pelekwa tu.
Haya hangaikeni na Mwenyekiti wenu ; tuliwaonya ila mkatuona waongo!! Haya sasa!!

Bila kuwa kwenye list yake ubunge utausikia tu kwa majirani.
 
Magufuli kasema bila aibu kwamba atamkata mtia nia yeyote, si kwa katiba, si kwa miongozo, si kwa taratibu, si kwa utamaduni,bali kwa jinsi takavyojisikia alivyoamka siku hiyo.
Hili ndiyo suala linalo nong'onwa Sana hapa Dodoma na wajumbe wa mkutano mkuu. Wengi wanaenda mbali na kusema "wagombea pendwa" tu ndiyo watapitishwa. Na Kuna majimbo wanapelekewa wagombea na kuitaka kamati ya siasa ya wilaya kuwapa ushirikiano. Hatari hii.
 
Nenda kapige kura, then watuoneshe kwa vitendo hiyo kauli yao, talking is always cheap.

Tangu mwaka 2000 nimekuwa mpiga kura mwaminifu. Ila kuanzia mwaka wa jana 2019, niliapa kutoshiriki chini ya utawala wa Magufuli, mtu asiyeheshimu demokrasia na matakwa ya wananchi walio wengi .

Akitoka madarakani, Inshallah! Nitarudi. Huu ni msimamo wangu binafsi.
 
Anachokitaka ndicho huwa. Na anafanya mambo kwa manufaa yake ya kisiasa. Kwanini nasema haya??

1. Angalia namna mchakato wa uchukuaji fomu za kugombea urais wa JMT ulivyokuwa na figisu. Eti wanaCCM wengine hawaruhusiwi kuchukua fomu. Ni yeye tu.

2. Angalia chaguzi za marudio ktk majimbo ambayo wabunge wapinzani "waliunga mkono juhudi". WanaCCM tulinyimwa kushindana nao. Na hata ktk uchaguzi huu tumepigwa marufuku kushindana nao.

3. Angalia upigaji kura ktk mkutano mkuu, ukusanyaji wa kura ulikuwa wa kimikoa (hii mbinu imewekwa ili iwe rahisi kutufuatilia wale ambao tungepiga kura ya hapana).

4. Kwa kinywa chake mwenyewe amesema kura za maoni za watia nia wa ubunge hazina maaana. Yeye amesema anaweza kumchukuwa hata mtu wa mwisho. Yaani badala ya wagombea kutafuta ridhaa ya wananchi, Sasa wanasubiri maamuzi binafsi ya mwenyekiti.

Demokrasia imezikwa rasmi ndani ya CCM. WanaCCM tunapelekwa pelekwa tu.
Lini umehama CHADEMA?
 
Anachokitaka ndicho huwa. Na anafanya mambo kwa manufaa yake ya kisiasa. Kwanini nasema haya??

1. Angalia namna mchakato wa uchukuaji fomu za kugombea urais wa JMT ulivyokuwa na figisu. Eti wanaCCM wengine hawaruhusiwi kuchukua fomu. Ni yeye tu.

2. Angalia chaguzi za marudio ktk majimbo ambayo wabunge wapinzani "waliunga mkono juhudi". WanaCCM tulinyimwa kushindana nao. Na hata ktk uchaguzi huu tumepigwa marufuku kushindana nao.

3. Angalia upigaji kura ktk mkutano mkuu, ukusanyaji wa kura ulikuwa wa kimikoa (hii mbinu imewekwa ili iwe rahisi kutufuatilia wale ambao tungepiga kura ya hapana).

4. Kwa kinywa chake mwenyewe amesema kura za maoni za watia nia wa ubunge hazina maaana. Yeye amesema anaweza kumchukuwa hata mtu wa mwisho. Yaani badala ya wagombea kutafuta ridhaa ya wananchi, Sasa wanasubiri maamuzi binafsi ya mwenyekiti.

Demokrasia imezikwa rasmi ndani ya CCM. WanaCCM tunapelekwa pelekwa tu.
wewe lazima utakuwa ndiye yule mjumbe wa NEC kutoka Songwe aliyemuuliza mwenyekiti wake swali gumu jana wewe.... si bure!!
 
Nenda kapige kura, then watuoneshe kwa vitendo hiyo kauli yao, talking is always cheap.

Ni vyema kama ni kushiriki kupiga kura watu wahimizwe kwenda na silaha za jadi. Ila kwenda kupiga kura kama wanaenda kwenye nyumba za ibada ni utani. Uchaguzi wa safari hii kama wapinzani wamekubali kushiriki chini ya tume hii, wajiandae kwa machafuko zaidi kuliko kinyume chake.
 
Back
Top Bottom