VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,137
- 17,908
Sina haja ya kusubiri kampeni zianze ili nishawishike. Sina haja ya kuuficha ukweli huu. Mwaka 2015, nilimsambaratisha Lowassa na kumpigia kura mgombea wa CCM yangu Dr.John P. Magufuli. Baada ya miaka yake mitano madarakani, nimekata shauri kuwa SITAMPIGIA KURA. Kupiga au kutopiga kura kwa mgombea, kwa kila mtanzania, kuna sababu yake. Kwangu mimi kinachonivutia ni kuongoza kikatiba, kisheria, kikanuni na kistaha.
Mimi Mzee Tupatupa, kada mwandamizi wa CCM, SITAMPIGIA KURA Dr. Magufuli pamoja na kuwa ni mgombea wa chama changu. Kitendo chake na kauli zake za KUHODHI FEDHA za Serikali kimenifanya nitafakari na kuamua nilivyoamua. Dr. Magufuli amejipambanua kama 'mmiliki pekee' wa fedha za nchi hii zilizopaswa kusimamiwa na Bunge. Kila apitapo, husema kuwa 'ninawapa/ninawaletea' kiasi fulani za fedha kana kwamba fedha hizo ni zake binafsi.
Kitendo cha kuhodhi hivyo kimezalisha watanzania wanafiki na watu wa kujipendekeza. Utawasikia: 'Rais ametuletea shilingi....... kwa ujenzi wa madarasa; Rais amekubali kutuletea shilingi....kwa ajili ya barabara' na kadhalika. tena utawasikia: 'Rais ametujengea…...', 'Rais amejenga…..'.Hapo Rais anachorwa kama aliyehodhi mfuko wa Hazina na fedha zote za Serikali . Hili si jambo la kuliunga mkono wala la kumpa kura mgombea wa aina hii.
Fedha za nchi zina utaratibu wake wa kukusanywa, kutumika na kukaguliwa. Kuhodhiwa na mtu mmoja si jambo jema wala la kuungwa mkono. Kuwa kiongozi wa Serikali hakutoshi kumfamya mhusika kuhodhi fedha zote za umma. Kwa hilo tu, SITAMPIGIA KURA. Haya ni maamuzi yangu binafsi.
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa jijini Dodoma)
Mimi Mzee Tupatupa, kada mwandamizi wa CCM, SITAMPIGIA KURA Dr. Magufuli pamoja na kuwa ni mgombea wa chama changu. Kitendo chake na kauli zake za KUHODHI FEDHA za Serikali kimenifanya nitafakari na kuamua nilivyoamua. Dr. Magufuli amejipambanua kama 'mmiliki pekee' wa fedha za nchi hii zilizopaswa kusimamiwa na Bunge. Kila apitapo, husema kuwa 'ninawapa/ninawaletea' kiasi fulani za fedha kana kwamba fedha hizo ni zake binafsi.
Kitendo cha kuhodhi hivyo kimezalisha watanzania wanafiki na watu wa kujipendekeza. Utawasikia: 'Rais ametuletea shilingi....... kwa ujenzi wa madarasa; Rais amekubali kutuletea shilingi....kwa ajili ya barabara' na kadhalika. tena utawasikia: 'Rais ametujengea…...', 'Rais amejenga…..'.Hapo Rais anachorwa kama aliyehodhi mfuko wa Hazina na fedha zote za Serikali . Hili si jambo la kuliunga mkono wala la kumpa kura mgombea wa aina hii.
Fedha za nchi zina utaratibu wake wa kukusanywa, kutumika na kukaguliwa. Kuhodhiwa na mtu mmoja si jambo jema wala la kuungwa mkono. Kuwa kiongozi wa Serikali hakutoshi kumfamya mhusika kuhodhi fedha zote za umma. Kwa hilo tu, SITAMPIGIA KURA. Haya ni maamuzi yangu binafsi.
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa jijini Dodoma)