Sitasahau nilivyonusurika kuchukuliwa mateka na majambazi mkoani Kagera

Sitasahau nilivyonusurika kuchukuliwa mateka na majambazi mkoani Kagera

Inaendelea............

.....ili nitoe pullover nivae kwa ajili ya kujikinga na kibaridi kilichokuwa kinachoma mwilini mpaka tumboni. Nilikaa pale kwa muda wa saa hivi kisha nikabeba mabegi yangu kuelekea kuitafuta breakfast maana tokea nilipokuwa nimekula jana saa moja usiku nyumbani kabla ya safari sikuwa nimekula tena hivyo nilikuwa nina njaa sana na hivyo nilichukua mabegi yangu nikaanza kupiga hatua za harakaharaka kuitafuta cafeteria moja ambayo haikuwa mara yangu ya kwanza kwenda kupata chochote pale, ilikuwa inaitwa Kishusi sijui Kama bado ipo maana kipindi kile ilikuwa inajitahidi sn kupika na kuuza vyakula vizuri sana vya kishua mjini Bk.
Nilikuwa na wasiwasi maana nilihofia kuwa huwenda wangekuwa hawajafungua lakini nilipofika nilikuta tofauti, nilisukuma mlango wa kioo kisha nikaingia. Niliagiza chai ya maziwa na kababu tano, nikazifuta zote mpk vile visalia vya vipande vidogovidogo vya nyama vilivyokuwa vinabaki kwa sahani nilifuta kabisa. Muhudumu alipokuja kunitajia bill nilijivuta nikasukuma kiti nyuma, ili nipate nafasi ya kumpatia pesa yake. Nikiwa nimekaa niliinama nikaelekeza mikono yangu mguu wa kulia kwenye raba yangu ya Nike nikafungua kamba zake kisha nikashusha soksi chini nikapenyeza mkono kwenye unyayo Kisha nikachomoa pesa noti za rangi ya bluu, miaka hiyo 10k note ndo ilikuwa mekuwa introduced na BOT, nilichomoa moja nikamkabidhi yule dada, muda wote huo alikuwa amepigwaa na butwaa alivyokuwa anashuhudia kile kitendo cha kuchomoa pesa kwenye viatu. Sikumbuki kwakweli nilitumia kiasi gani na chenji ilibaki kiasi gani Ila baada ya kunirejeshea chenji ilibidi nitumie dakika chache sn kutenga nauli na pesa ya kutumia ninapokuwa njiani ili nikishafunga buti (kiatu)nisianze kufungufungua kila mara.Niliwaza kujiondolea usumbufu. Ikumbukwe kuweka hela chini ya nyayo ndani ya soksi nilikuwa na sababu na nilishazoea kufanya hivyo siku zote za safari yangu ya kuelekea shule. Mguu wa kushoto niliweka ada ya shule na sikuwa nimegusa eneo hilo tokea nilipoiweka nikiwa home baada ya kupewa na mzee, na kulia nilihifadhi pesa ya matumizi.

Wakati huo ilishafika saa mbili kasoro, nikapiga hatua chapchap kurudi standi,kipindi kile magari ya abiria yalikuwa ya kuokotaokota Sana kuelekea huko wilayani hivyo Mimi nilishazoea kupanda kwa kuunga unga na siku hiyo nilipofika eneo hilo nilikuta usafiri unaoelekea Mutukula mpakani kabisa mwa Tanzania na Uganda. Nilipanda lile gari na tulipofika Kyaka kabla ya daraja walinishuka pale ili nisubirie usafiri wa kuunga angalau unifikishe Karagwe wilayani, kisha nikifika pale nilale ili nianze tena safari ya kuunga unga mpaka nifike mwisho wa safari yangu.

Nilikaa Kyaka takribani masaa matatu sikuwa nimepata usafiri, yakipita magari matatu ya abilia lakini yalikuwa yamejaa. Nakumbuka gari za abiria mara nyingi zilikuwa ni Land lover. Pia magari binafsi pamoja na ya Mashirika ya Umoja wa mataifa kama UNHCR, Calitas, UNICEF, Help Age niliyashuhudia yakipita nilikuwa nayasimamisha but hayakuwa yakisimama. Sikukata tamaa niliendelea kusubiri, lakini nikiwa pale niliona nijisogeze kwa mmoja wa vijana wengi waliokuwa wanauza ndizi za kuchomo kule zinaitwa gonja tamu sana i see, nilikula kadhaa huku nikisukumia na soda yangu bariiidi kabisa ndizi mbili tu nikatosheka zingine nikahifadhi kula huko mbele ya safari. Nilikaa Kyaka mpaka saa tisa hivi ndipo gari binafsi iliposimama kisha tukapanda na abilia wachache waliokuwepo pale nakumbuka ilikuwa double cabin, wote tulipanda nyuma

Tulianza safari bila ya kuchelewa,
kipindi hicho barabara zilikuwa mbaya, mbaya mbaya kabisa mashimo kwa kwenda mbele na ukichanganya na kipindi hicho mvua zilikuwa zinanyesha mkoani Kagera barabara zilikuwa hovyo kabisa. Kadiri tulivyokuwa tunaiacha misenyi ndivyo jua lilizidi kuelekea usoni kwetu kwa maana ilikuwa linaelekea magharibi.

Baada ya kuwa tumevuka vilima na mabonde na Safari yetu ikingali inaendelea magari yaliyokuwa yanatokea upande tunakwenda sisi yalikuwa hayaji tena, hatukuwa tukiyaona kupishana nayo kama ambavyo ilikuwa hawali ama kipindi kile bado niko Kyaka nasubiri usafiri.Kwa ujumla nilifikiria kuwa ni kwasababu ya muda kuwa umekwenda. Kitu kilichonishangaza ni yale magari ya abiria yaliyokuwa yamenipita pale Kyaka stand na yalishatembea muda mrefu lakini tuliyapia, Ila nilijiambia moyoni kuwa sababu ni mabovumabovu ndio maana tumeyacover na kuyapita.

Tuliendelea na Safari yetu lakini kilomita chache za mwendo tulikuta gari moja limekwama kwenye dimbwi la tope katikakati ya barabara na hivyo likasababisha tushindwe kuendelea na safari kwa kuwa liliziba njia. Tulikaa hapo kwa muda kama wa nusu saa na muda huo yalishafika magari mengi yaliyokuwa yanasubiri njia iwe wazi. Watu tuliokuwa eneo hilo tuliokuwa tumeshuka kabisa kwenye magari yetu tunalandalanda tu huko na huko wakati huo ni saa kumi na mbili jioni. Nikielekea kwenye bag langu nikafungua mfuko wa pembeni nikachukua kidevice changu Cha kuchezea cassette nikatia cassette moja ya 2pac Omary Shakur kisha nikachukua headfone zangu nikaziseti juu ya masikio barabara (Kama DJ vile) nikaanza kula hip hop kali za moto sana kipindi hicho nikikoshwa zaidi na kibao cha 'Dear Mama'

Ile naanza kuenjoy biti nilishtushwa na milio ya risasi .....papapu..papapaa..... zilipigwa mfurulizo Kama dk 5 hivi tena zilipigwa kutokea both sides yaani kule tulikotokea na huko tunakoelekea, sikujua zile headfone ziliacha kichwa muda gani zaidi nilipokuwa nazungusha macho huku na huko niliyaona mabandidu yanameshika siraha yanahamrisha watu tulale kifudifudi muda wa sekunde kadhaa eneo kulikuwa kimyaa.

Mabandidu yakajichukulia utawala wa gafla Katika kale kaeneo tukiwa tumelazwa pale nilishtushwa na mtu akiniinua Kama sisimizi maana alishika ile kofia ya 'pullover' ilivyokuwa imelalia nyuma ya kisogo akanivuta kisha nikamtizama usoni jamaa lilikuwa limevalia siraha Ina mkanda kama wale waasi wa M23, I see jamaa lilinistua na banzi (kibao)moja heavy la usoni, nikaziona nyota na rangi za bluubluu ilochanganyika na rangi ya damu wakati huo akili yangu ikanituma kuwa sikutaka nimtizame usoni though alikuwa amejifunika uso. Kabla sijatafakari nisali Sala gani nikashangaa mtu ameleta gunia akanivika, nilistuka gunia linanivaa, nikajua nimekwenda na maji.

Ubongo wangu ukiwa umefeli kutafakkari niliishangaa wanaletwa watu wengine sikujua ni wangapi Ila nilikuwa nasikia vishindo kuja kwangu Kisha tukaambiwa kwa kiswahili kibovu 'Mutu hakuna kutembeya' Mimi kila kiungo kimoja kilikuwa hakina mawasiliano na kingine maana kwanza nilikuwa mdogo na ndiyo mara ya kwanza nasikia milio ya risasi. Nilikuwa natetemeka Kama generata bovu kuzidi yale majenerata ya mgao wa Umeme ya tanesco.

Kipindi chote hicho nilikuwa nimefunikwa gunia, Kuna Yale magunia ya enzi hizo yalikuwa yanatengenezwa na katani. so hewa ilikuwa inapita na muda wote ule tokea nimepigwa like Kofi nilikuwa nimefumba macho kwa uoga.Lakini nilikaza moyo baada ya kuhisi majamaa yamesogea hatua chache kutoa pale nilipo nikafumbua macho, kupitia kwenye gunia nikaona mabandidu kama wanasearch magari kwa haraka haraka kisha ndio nikaona pembeni yangu tuko kama watano hivi tuliosimama.Hapo hapo bandidu moja likasogea pàle tuliokuwa huku limetulenga na bunduki sikuwa na mawasiliano ya mwili Ila nilihisi mkojo unateremka kutokana na kuhisi maji ya Moto yakiteremka kutoka saizi ya kiuno Hadi chini kwenye viatu. Jamaa alipokaribia na sisi akapiga risasi (nahisi juu) Kisha Mimi miguu ikaishiwa nguvu nikahisi nimepigwa mimi, nikadondoka chini. Chakushangaza jamaa akaja akaniinua tena akanitoa lile gunia kisha akanambia "we mwana we ntakupiga 'rishashi' cha ajabu nikahisi nguvu zimenirejea maana nilidhani ile risasi amenifyatulia mimi na tayari nimeshakufa kumbe nilikuwa hai sina hata jeraha. Basi wale wenzangu nao walikuwa wanapita wameshika magunia yao nyuma yao kuna mabandidu yanasimamia zoezi kama ilivyokuwa kwangu. Mimi nilikuwa mdogo lakini nashangaa hata leo kwanini Yale majamaa yalining'ang'ania kunipa gunia?? Waga najiuliza Sana, kisha wakawa wanatupitisha kwa abiria pâle walipolazwa, ukifikiwa unaamrishwa utoe ulichonacho kila kitu uwe na pesa saa nzuri unatia kwenye gunia hakuna kupoteza muda.Zoezi hilo likiwa linaendelea wakati huo mateka unatekeleza zoezi kichwa ukiwa umeinamisha chini , mijamaa ikawa inasema ukiinua kichwa unakula 'rishashi' Nakumbuka hili jina rishashi mpaka Leo jinsi walivyokuwa wanatamka neno 'risasi'

Ikumbukwe kitendo kile kilichukua dk zisizozidi ishirini hv, na sehemu walipotutekea ilikuwa ni sehemu ya Kona maana waliokuwa wanatokea tunakokwenda walikuwa hawawezi kuona kuna nini kinaendelea na hata waliokuwa wanakuja wasingejua kutokana na ile kona ambayo pale Kati ndio hiyo ambushi ilipofanyika.

Basi, baada ya like tukio kukamilika waliamrisha watu kulala kimya tena uso chini Kisha wakatwambia sisi wenye yale magunia kwa ukali kilammoja abebe furushi alilonalo tuanze kukimbia kufuata njia kuelekea kwenye msitu. Kiukweli hapo ndipo nilianza kuwaza sitawaona tena Baba, Mom, na ndg zangu, tena nilianza kuwaza ninapotea kwenye uso wa dunia bila kutambliwa nimefia wapi. Uso wote ulijaa machozi, tumaini likapotea tukabebeshwa yale maroba ya vitu na wao walikuwa wamebeba mamizigo kibao waliopora kwenye magari, safari ya maisha nisiyoyafahamu ikaanza, nikakata tamaa, nikakosa tumaini, mwili ukazidi kuvibrate, miguu ikawa inagongana gongana kama mtoto aliyeugua utapiamlo,akili yangu itaitengeneza taswira ya mama angu machozi yakajaa machoni hata kushindwa kuona vema, moyoni mwangu nikahisi kutamka jina langu Mara tatu....Derick....Derick......Derick (Code) why was I born??!!

Itaendea...

Muendelezo soma
Sitasahau nilivyonusurika kuchukuliwa mateka na majambazi mkoani Kagera
 
Ilipoishia......
....moyoni mwangu nikahisi kutamka jina langu mara tatu....Derick....Derick....Derick.... why was I born??!!

Inaendelea........
Kweli tukaiza safari, kichwa changu kikawa kinawaza jambo moja tu kuuwawa, wakati huo machozi yakazidi kububujika machoni, mpaka hali ile ikawa inanisababishia uono hafifu mwendo ulikuwa ni wa kukimbia kimchakamchaka. Nilikuwa nakimbia lakini nahisi miguu haina nguvu, ule mzigo niliokuwa nimeubeba haukuwa mzito maana vitu vilivyokuwemo vilikuwa vyepesi ingawa furushi lenyewe lilionekana kubwa.

Wenzangu walionekana kuwa na kasi kuliko mimi, na mwanzo tulishaonywa kuwa Kama utaonekana kuzembea au kutokutii amri zao wanakupiga risasi. Wale majambazi walikuwa wengi sikuweza kuwaza hata kuwahesabu kwa kuwa kichwani mwangu nilikuwa nawaza mambo mengine kabisa na hata hivyo walikuwa wakikimbia 'zigzag' maana wakati fulani wengine walikimbia wakiwa nyuma yetu, mara nyingine kadhaa wako mbele wengine nyuma so sikuweza wahesabu kabisa na kiukweli nilifocus na mbele ninakokwenda maana sikutaka kujichanganya kabisa.

Tukiwa tunazidi kutokomea mwituni, nafikiri ilikuwa imepita Kama robo saa hivi tukiwa tunasonga mbele, Mimi nilikuwa nimechoka wakati huo, nilikuwa niko nyuma ya wote ispokuwa jambazi mmoja aliyekuwa sambamba na mimi, niliona anazidi kunisogelea kwa karibu kabisa akanifokea kwa sauti kali 'chimbia' na mimi kwa mshtuko nikakurupuka kwa kuongeza spidi zaidi, na ndiyo huo muda sikuwa nimekiona kisiki kifupi mbele yangu ambapo nilijikwaa kisha nikaanguka chini.

Yule jambazi alikasirika sana na muda huo sikutumia hata sekunde tano kunyanyuka maana nilihisi angeniua palepale. Nikiwa ninainuka alinishika kwa kunikwida akavivuta kwa kasi uelekeo wake huku amenikunja akanitazama kwa hasira kwa sekunde chache sana akaongea neno moja "gweee" akanipokonya furushi kisha akanikanyaga teke moja heavy la tumbo na lile buti lake....sikutambua kilichoendelea tena.

Giza nene, baridi na upepo mkali ulioambatana na mvua nyepesi vilikuwa vinapiga vyote kwa pamoja, nilijikuta nimelala chali nimelowa na mvua iliyokuwa inanyesha eneo hilo. Nilianza kutazama pembeni yangu huku na huko ili nijue niko na nani eneo like lakini ilikuwa ni giza tupu.Muda mfupi miale ya radi ilianza kumulika na huku radi zikiunguruma kwa sauti za kutisha. Niliogopa sana, kila sekunde chache nilikuwa nahisi nywere kuninyonyoka, na nilikuwa nahisi shoti za Umeme kukatiza kwenye mishipa ya ubongo kila wakati. Nilikuwa natetemeka sana, meno yalikuwa yanagongana kinywani na yalifanya sauti kusikika Kama cherehani ya singa.

Muda ule mvua ilizidi kuongezeka kutoka kuwa nyepesi ikawa mvua nzito, nilikuwa tayari nimeinuka na kukaa palepale nilipokuwa nimelala, radi ziliendelea kufyatuka nikawa nimedata kabisa.Sikujua nifanye nini Ila ilibidi niwe mpole,nilikuwa nalia kimyakimya. Muda ule nikayakumbuka yale majambazi nikajikuta nimejikunyata tena pale pale. Nilihisi labda yako maeneo yale aidha, niliwaza labda yamejikinga na mvua. Nilikaa pale kwa muda nilinyeshewa mvua nikawa 'ronyaronya' . Baada ya kukaa pale kwa muda na kuamini niko peke yangu wazo la kwenda kupanda juu ya mti ili nisiendelee kukaa pale chini nikaliwa na wanyama wakali lilinijia.

Kwa kuwa ilikuwa giza Sana niliamua kungoja mwanga wa radi unimulikie ili nione ni mti gani nikakwee. Muda mfupi tu nilishapata wapi nielekee lakini wakati nataka kunyanyuka viungo vya mwili vilikaza kwa ujumla nilishindwa kunyanyuka pale, mwili wote ulikuwa wa baridi kabisa. Ilibidi niachane na ule mpango wa kwenda kwenye mti nikaamua nijisogeze kwenye kichaka kilichokuwa karibu yangu ili nikajibanze pale. Nilijisogeza kwa kutambaa chini kwa chini hadi nikajichomeka kwenye matawi ya kile kichaka nikakaa pale nikiwa nimechuchumaa kwa kujikunyata. Muda ule nilikuwa naombea kupambazuke lakini wapi. Nilikumbuka wakati huo kuwa nilikuwa na saa mkononi, nikasogeza juu mkono wa 'pullover' kweli saa ilikuwepo mkononi lakini nilihisi hata hivyo haiwezi kuwa inafanya kazi kwasababu nilikuwa nimenyeshewa sana.

Wakati huo mvua ilikuwa imepungua sana na sauti za vyura zilianza kusikika Katika anga lote lile, sikutaka kufunua macho hovyo hovyo maana nilikuwa naogopa kupita kiwango,nilibaki nimejikunyata pale huku kichwa nimekiinamisha usawa wa magoti yangu. Mvua zilikuwa zimekata kabisa n'a ardhi yote ikawa tulivu, Mara moja moja nilisikia sauti ambazo sikuelewa ni za wanyama ama watu. Nilichukua kofia ya pullover nikaitia kichwani ili nizibe masikio nisisikie chochote. Dakika chache tu kupita nilianza kuhisi kama kuna kiumbe anakuja.... taratiiiibu nikatoa masikio nje ili nijirizishe, kweli kiumbe alikuwa anakuja uelekeo ule niliyokuwepo...nikahisi kutetemeka zaidi na zaidi..nikahisi nywere zimeninyonyoka kichwani gafla shaaaaaaa.....

Itaendelea


Muendelezo soma Sitasahau nilivyonusurika kuchukuliwa mateka na majambazi mkoani Kagera
 
Ilipoishia......
....kweli kiumbe alikuwa anakuja uelekeo ule niliyokuwepo...nikahisi kutetemeka zaidi na zaidi...nikahisi nywele zimeninyonyoka kichwani gafla shaaaaaaa.......

Inaendelea.........

nilipigwa bubuwazi, akili ikasiz gafla kishindo kikawa kinaashiria kukikaribia kichaka,akili ikanituma nipige kelele kwa upande mwingine nikasikia sauti ndani yangu ikiniambia Derick husipige kelele,nikaiheshimu ile ya pili. Wakati huo nilijikuta nimesimama lakini nikiwa nimepinda mgongo mithiri ya mtu anayepiga chabo kwenye vidirisha vya ushazi, nilikuwa nimeyatungua macho mithili ya fundi saa aliyedondosha visumari, nilianza kuona mauzauza nywele zikawa zinatikisika kila sekunde, mwili ukazidi kuvibrate nikahisi vile kichwa changu kimeacha kiwiliwili nikajishika usoni ili niprove nikahisi nimeshika kitu kigumu hivi yaani kama ubao, kichwa kilijam kwa uoga wa kupindukia .

Nikiwa nimetumbua macho kwa hofu nilishtushwa na upepo mkali sana ambao uliyatawanya hata yale matawi ya miti pale nilipokuwa nimejificha ikabidi nichuchumae, nikapiga magoti kabisa dakika chache sana nilianza kusikia sauti za watu wananong'ona nong'ona moyo wangu ukajibu haraka hao ni wachawi. Sikuwaona kwa macho ila nikawa nasikia vishindo na minog'ono yao mara nisikie vicheko kama milio ya mbuzi nikachanganikiwa kabisa, nikasikia kama wamekuja pale kichakani wakaanza kukizunguka kichaka though sauti zao nazisika mbali Kama watu walioko mbali na pale Ila nasikia vishindo vinazunguka zunguka pale nilipo nikajawa uoga, nikaanza kutoa sauti 'mmma..ma...mamaa..maa' lakini mdomo mzito sauti haikutoka, nikadata kabisa nikahisi nichomoke pale mbio lakini ndio kwanza miguu ilikuwa inacheza kwasakwasa (inatetemeka) pale pale nikahisi kuguswa mgongoni nikasikia mapigo ya moyo yapanda sikujua kilichoendelea. Nilizima!

Nilishtuka gafla ...... wadudu flani hivi wakubwa jamii ya sisimizi wanaitwa chungu nilikuta wananilandalanda kila sehemu ya mwili wangu, nikasimama nikaanza kujikung'uta, nikajitizama mavazi yangu yalikuwa yanaubichi sana sikujali, nikasikia furaha na moyo wa matumaini ulinifunika nikahisi nguvu mpya ya ajabu.

Ilikuwa tayari ni asubuhi kumepambazuka, nyasi za green zenye umande mwingi pamoja na vichaka na miti ndivyo vilionekana kupamba mandhali ya msitu huo. Nilitizama pande zote nne za dunia katika msitu huo ili kujihakikishia Kama Kuna uwepo wa mtu yeyote,palikuwa kimya.

Nilijisogeza tena kwenye majani ya kile kichaka nikafungua kamba za viatu nikavua viatu kisha nikatoa na soksi nikacheki pesa yangu ilikuwa salama kabisa nikatabasamu, nikachukua zile soksi nikazikamua vizuri kisha chapchap nikazivaa alafu nikapenyeza ule mkwanja kila fungu eneo lake kama ilivyokuwa hawali. Baada ya hapo nikazivua nguo moja baada ya nyingine nikazikamua maji zote Kisha nikazivaa tena.

Baada ya kuvaa, likaja swali ndani yangu Derick... now where to.... niliinua kichwa nikatazama juu nikaangalia angani hapakuwa na jua mawingu yalikuwa yametanda eneo lote nikageuka kulia kwangu na kushoto kisha mbele na nyuma nikawa natafuta direction ya jana tulitokea eneo upande gani. Sikuweza kutambua, nikaangalia juu tena kucheki labda ntaona jua, halikuonekana kabisa mawingu yalikuwa yametanda. Niliwaza kuwa angalau ningeliona jua ningeweza kuelewa haraka uelekeo wa Kayanga makao makuu ya Wilaya ya Karagwe kwa wakati huo sijui sasa hivi maana Kayanga ilikuwa inapatikana uelekeo wa North West kutokea pale tulipotekewa.

Baada ya sintofahamu ya mgongano wa mawazo ya mwenyewe kwa mwenyewe nilihisi nafsini mwangu sauti ikiniambia Derick acha ujinga anza kuondoka eneo hili haraka. Sikutaka kubishana nayo nilikaza mkanda wangu vema juu ya kiuno Cha suruali yangu na hapo niliyasikia yale maumivu ya lile teke nililopigwa na jambazi jana yake. Bado suruali ile naikumbuka hata leo maana nilikuwa nimepiga t-shirt yangu yenye chata ya Chicago bulls, na kodrai trouser ya rangi ya kijivu chini raba ya nyeusi aina ya Nike na pullover ilikuwa ya rangi bluu Ina chata ya Fila. Hata hivyo nilikuwa Bshow sana wakati huo.

Niliamua kubet upande upi niufuate, nilichukua Jani la mti ambalo halipepesuki na upepo kwa haraka na kwa kuwa palikuwa patulivu niliona hapa nitapata ninachohitaji. Nilichukua jani kisha nikaenda kukwea kwenye mti mfupi sana baada ya kuwa juu nikaliachia nikimaanisha kule litakapoelekea diko huko huko ntakapoenda. Kweli nilipokuwa pale juu ya mti nikaliachia taratiiiibu kabisa likapepea kuelekea upande ambao mimi niliupa jina kuwa hiyo ndiyo north direction na bila kupoteza muda nikajisemea Sisi tulitokea magharibi ndiko barabara ilipo.

Nikaanza kukatisha vichaka nikijipa tumaini kuwa narudi barabarani kule tulipotekewa hata kama sio eneo hilo Ilimradi tu nifike na niione barabara. Nilitembea , nikatembea sitoboi kabisa, nikaanza kushangaa mbona tulikimbia kama dk. 15 au ishirini tukafika pale waliponiacha? Lakini mbona nimetembea takribani saa nzima hv( nilihisi muda ) mbona sioni kufika barabarani? Nilijiuliza.

Niliendelea kwenda mbele kwa mbele,nilishajua ile direction haukuwa ya uelekeo nilioutaka, Ila nikijipa moyo nikasema kwakuwa no mchana na sio usiku acha niendelee labda naweza kupata msaada , labda kuna wakulima wenyeji naweza kukutana nao..labda kuna Kijiji kinaweza kuwa karibu...nikawa mtu wa labda...labda ingawa moyo wangu ulikuwa na amani wakati huo. Baada yakutembea sana nilifika sehemu nikakaa kupumzika maana hata njaa ilikuwa inaniuma. Nikiwa nimekaa pale nilikiona kijua kwa mbaali kabisa na ndipo hapo nikatambua ni Kati ya saa sita na Saba maana jua lilikuwa Kati ya utosi. Nikiwa pale nilianza kusikia kengele kwa mbaali, nikajiuliza mmh..kengele porini...wapi na wapi nikawa najisemea misitu nayo Ina mambo ya ajabu? Nikakaa kwa kutulia ili nisikilize vizuri, jinsi dk zinavyoenda ndivyo kengele nayo inaongezeka nikakimbia kupanda juu ya mti....
Itaendelea.

Muendelezo soma
Sitasahau nilivyonusurika kuchukuliwa mateka na majambazi mkoani Kagera
 
Back
Top Bottom