Sitasahau tanuru la moto nililopitishwa na Hayati Magufuli mimi kama mtumishi wa Serikali

Sitasahau tanuru la moto nililopitishwa na Hayati Magufuli mimi kama mtumishi wa Serikali

Kumbe sukuma gang ni wengi kiasi hiki?

Maana huku mtaani ni balaa! Muulize hata mumeo atakwambia Magu ni chuma,

Basi nae kumbe ni sukuma gang
Umeanza upuuzi sasa
 
Ma
Habari,

Niende kwenye mada, kama kichwa cha habari hapo juu, Ninaweza kusema kwamba waliotunga sheria mbalimbali za utumishi wa umma watakuwa wajinga na walikuwa na njia njema kabisa.

Miongoni mwa Vitu muhimu kabisa ni nyongeza ya mishahara, increments na kupanda madaraja kila baada ya miaka kadhaa ili kuendana na kupenda kwa gharama za maisha kila mwaka.HIVYO mtumishi aliweza kuyamudu maisha yake japo kwa kudanadana.

Utawala wa JPM yeye hakuona umuhimu wa jambo hili na kuwasugua watumishi kwa miaka sita bila kuwapatia hiyo haki yao ya msingi, aliwafanya watumishi wengi kushindwa kuendana na gharama za maisha na kuwa na hali mbaya sana kiuchumi.

Hivyo kitendo hichi kilififisha ufikiwaji na upelekaji wa maendeleo kiurahisi kwa wananchi japo wananchi wajinga walikuwa wa kwanza kupiga makofi wakifurahia hayo Mateso ya watumishi wa serikali yao.

Watumishi walifanya kazi quantity na si quality kama maroboti, ufanisi ulishuka sana na nidhamu ya uoga kuwa asilimia 100, nia na hamu ya kufanya kazi za serikali ilipungua kabisa na hata maendeleo yaliyoyowafikia wananchi yalikuwa hafifu japo yalikuwa jina kubwa sana na wale waimba mapambio kama mtakumbuka.

Watumishi wa serikali ni DARAJA la kupitisha maendeleo kutoka kwa serikali kwenda kwa wananchi wakiwa na hali mbaya kiuchumi, kiafya na kijamii basi hata maendeleo tarajiwa yatawafikia wananchi kwa namna hali yao ilivyo na wakiheshimiwa, kupewa stahiki zao kwa wakati basi hata utoaji wa huduma na maendeleo kwa jamii huongezeka maradufu.

Binafsi ninamuona MAMA samia kufanikisha zaidi katika mambo yake hata kwa kulijali hili kundi muhimu katika jamii, na 23% imewaongezea watumishi nguvu sana kabla hata ya kuipata, tunakuomba MAMA samia watumishi utushike mkono na sisi hatutakuangusha kuyatafsiri mawazo yako ya kimaendeleo kuwa uhalisia kwa wananchi wetu tunaowahudumia.

Mungu ibaraki Tanzania, Mungu ibaraki ccm na raisi wetu MAMA SAMIA
Mama anaupiga mwingi
 
An old ways of thinking by Mwenzake Chawa
Ungesema tu ule uwanja ulikuuma haya mengine yote ni ngojera.
ww unalalamika kutokupandishwa mshahara, kuna watu private sector walipunguziwa mishahara 25-40% for 1yr during covid na wengine walipoteza kazi kabisa ww unalia lia kutoongezewa salary while uliendelea kupata mshahara na you kept your job during covid.
Kweli shukrani ya punda ni mateke.
 
Sio kweli. Wewe sio mfanyakazi ndio maana huoni tofauti, kaa kimya usiwakumbushe watu machungu.
Wewe uliyekuwa na ajira unasema usikumbushwe machungu na je ambao hawakuwa na ajira je?ukikaa kutegemea mshaara utakuwa na ulemavu wa akili siku zote mshaara haujawahi kutosha...
Walimu mnatuchosha sana
 
We pimbi, kwani pamoja na Magufuli kutoongeza mishahara inflation haikutokea? kwani wakati anaingia madarakani alikuta sukari inauzwa sh.ngapi na akiwa madarakani ikawa inauzwa sh.ngapi? aliyependekeza kodi ya nyumba kupitia luku hakuwa Jiwe? Shenzy type.
Acha uzwazwa dogo!

Sukari alikuta inauzwa 1800 ikapanda hadi 2800..


Haya twambie nini kingine kilipanda maradufu?

Bajeti ya kodi ya nyumba imeanza kipindi cha Mwigulu mteule wa Samia huyo hakuwa Magu acha utahira.
 
Japo Magufuli hakuongeza mishahara lakini pia hapakuwepo na huu mfumuko wa bei uliopo sasa, kwa kifupi Magufuli na Samia hawana tofauti kwenye hili la kuinua hali ya wafanyakazi.
Unamtetea Magufuli mpaka yeye mwenyewe anashngaa huko aliko. Eti Magufuli na Samia hawana tofàuti!! Kweli?

Unamdanganya nani kuwa bidhaa hazikupanda bei kipindi chake? Sukari ilikuwa Tsh 1,800 wakati anaingia mwaka 2015 akaivuruga hadi Tsh 3,000- 5,000 na mpaka anakufa haijawahi kurudi pale pa awali.
 
Mleta mada anawaza tumbo tu.

Hujali kabisa namna tunavyopigwa mnada kwa kasi ya umeme.

Yaani wewe ukipata uhakika wa kula hata ukiuzwa hutajali.
 
Kaongezewa laki mbili anaporwa laki nne bado anachekelea tu, hakuna mradi wowote wa kimkakati kama taifa unaoendelezwa, Mradi mkuu umekua mradi wa Kusafiri
Magufuli alianzisha mega projects 3 kwa wakati mmoja; SGR, Stiglers Gorge na Dodoma City. Mbali ya projects zingine kama Busisi, hospitals na barabara. Na mpaka anakufa yeye mwenyewe alishindwa kumaliza sababu ya kukosa uwezo wa ku PLAN

Hizo projects zinahitaji fedha za kujengea na zingine tumeanza kulipa riba wakati hatujaanza kuzalisha. Mama Samia amefanya restructuring tu ili maisha mengine yaendelee Wakati miradi inajengwa
 
Ukiwakuta maofisi wanavyozurura, wasivyofanya kazi kwa uadilifu na wanavyokusubirisha; ila wanavyolalamikia nyongeza sasa.
 
Enzi za Magufuli nilikuwa napokea mshahara 300,000 ilitosha kununua 240Kg za mchele ,mshahara umeongezeka napokea 369,900 inatosha kununua 185Kg za mchele,nisaidieni hesabu hesabu hapo mshahara umepanda au umeshuka?
Mshahara umepanda ila tatizo ni mfumuko wa bei.
 
Mwacheni Magu aitwe Magufuli na Mama Samia aitwe Samia kila Zama na kitabu chakeMagufuli alitenda kwa kiwango chake na alitufumbua macho watanzania wengi anastahili sifa zake na mama anaandika chake tumpe muda
 
Tulitaka kuwa na raisi Magufuli kwa miaka kama 20 hivi inchi iendelee

USSR
Magufuli angekuwa Raisi miaka 20 watumishi wa serikali akili zingewakaa sawa na wananchi pia tungeanza kuwa na akili za kujitengemea bila kuwaza Ajira za serikali ambazo zinafanya tuendelee kuwa masikini uku wageni wakijiajiri sisi watanzania akili zetu zikiitaji kazi za ualimu na Upolisi na kwenda jkt kupoteza muda basi.
 
watu aina ya mletamada ni hasara kubwa kwa taifa.
 
Maweee!! nani ampe?? yule ni kuruta kule anaponda kokoto kila uchao!! na kutumwa barabarani ili kusababisha ajali!!...anatamani arudi atubu lkn wapi!!!....... ..imekwisha pitishwa........

Anatamani angekuwa anaongoza km Rais wetu mpya Mama Samia...lkn ndo basi tena!!.......amemnunia shetani kule kuzimu eti alimdanganya!! na shetani kwa kumkomoa huyo Jiwe, ameamua kumpa kazi ngumu!
sawa mke wa shetani😁😁😁

hizi ndio info anakupa akiwa faragha nawewe.
 
Mkuu bado upo kwenye ajira? Labda tuanzie hapo kwanza, and Jee increment ulopewa imeleta impact kiasi gani kwenue maisha yako.
Mkuu wewe ni mbinafsi sana voz unasngalia upandishiwe mshahara wako ila kumbuka asilomia kibwa ya watanzania ni maskini wasio na kazi hao nao maisha yao wanasaidiwa na nani.
Utawala wa mwendazake ulijikita katika kuweka mazingira mazuri kwanza kwa kila mtanzania aweze kujiingizia kipato chake kirahisi lakibi atimize pia wajibu wake kulipa kodi.
Mtazamo wa mwenda zake ulikuwa ndo mtazamo walioanza nao china, angalia china walipo sasa. China walifsnya kazi kwa nguvu na hadi kufikia masaa zaidi ya 10 na wengi walifia kwenye mashine sababu ya kuchoka
Leo dunia nzima inafurahia kila aina ya bidhaa kutoka china sababu walijengewa utamaduni wa kufanya kazi bila kuchoka.
Ndugu yangu mm nimeanza kazi enzi ya kikwete nlikuwa kijana mdogo tu 20+ na sasa nimekuwa mbaba . Hakuna kipindi nlifanya kazi kwa bidii na kwa umahiri wangu wote na kwa uzalendo kama kipindi cha JPM sababu alikuja na mtazamo niliokuwa naota kabla hajawa rais. Kwangu mimi magufuli atakuwa rais wa maisha yangu yote sababu bado naishi kwenye ndoto zake hadi sasa. Na nitaendelea kuwa hivo mpaka nife.
Wewe ni mzalendo wa kweli, mawazo yako yanawakilisha Watanzania wengi! Hao wanaoshinda hapa kumkashifu Magufuli wengi wao hata kazini kwao ni wavivu na Mizigo kwa mwajiri.
 
Back
Top Bottom