Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,984
- 19,288
Shusha nondo mkuu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tarehe 4 mwezi wa pili 2020 nikiwa katika msongo wa mzito wa mawazo yaliyotokana na ugumu wa maisha nilijikuta nafanya maamuzi magumu bila kutarajia. Nilikuwa nakaa gheto maeneo ya buguruni sheli japo gheto lilikuwa na mshikaji wangu ambae tulisoma nae primary mawenzi shule ya msingi iliyopo moshi mjini mwaka 2006 ndotulimaliza darasa la saba hapo.
Nikiwa nimelala saa sita usiku naona napigwa mgongoni kwa nguvu kuamka namuona rafiki angu tunaelala chumba kimoja pia ndommiliki wa gheto mm kaniweka tu kishkaji, nikasema kulikoni jamaa akajibu kiunyenyekevu akisema "oya demu wangu kafukuzwa na Dada ake alipokuwa anakaa kwahiyo hana pakwenda nasaizi ni saa saba usiku amekuja yupo hapo kibarazani anataka tulale humu kwahiyo please wewe ni mwanaume ebu tafuta ustaraabu wa kuondoka saizi ukija asubuhi tutaweka mambo Sawa ".
Nikamwambia sasa mda huu mm niende wapi ndugu na Sina hata sehemu yakujiegesha!? Akajibu nitajua mwenyewe, ikabidi nivae niende kimboka night club kupoteza mda nikawa naangalia movie kwenye mabanda ya pale kimboka maana majamaa huwa hawalali. Ilipofika asubuhi nikatia timu bahati nzuri nikakuta wote wameamka ila wapo kitandani nikamsalimia shemeji pamoja na jamaa angu japo hawakuonesha uso wa tabasamu walikuwa serious kiasi ambacho nilishindwa kuwaongelesha.
Nilipotazama juu kwenye enga zakuwekea nguo zangu ghafla sikuona nguo yoyote, nilipouliza jamaa akasema nimekuwekea kwenye begi ili ukija usisumbuke kuzipanga maana shemeji ako kasema yeye hatoki atakaa hapahapa sasa hatuwezi kulala watatu. Ilikuwa ni kipindi kigumu sana Kwangu zaidi ya Alpha konde alipotolewa madarakani. Nikatazama juu chini nikawaza nikasema haina shida.
Nikabeba begi langu nikawaaga wakasema kila raheli. Nilikuwa na simu Aina ya tecno F1 na mfukoni nikawa na 20000 nikasema Poteleapote nitaenda popote pale kutafuta rudhiki.
Kwa pesa niliyokuwa nayo kukaa Dar Es Salaam hapakunifaa tena, hiki ndokipindi ambacho mikoani unapaona nafuu kuliko jiji la Dar Es Salaam. Nikiwa na begi langu Zito la nguo mpaka mida ya saa kumi jioni nilikuwa sijajua niende wapi na nitalala wapi. Nilipoona mda unakwenda ilibidi nimfate jamaa mmoja ivi yeye anauza nguo za jinsi buguruni sokoni kama unaenda shell nilipofika alinichangamkia akijua ni mteja kumbe ni mtu mwenye dhiki aliehitaji msaada. Sikupoteza mda ilibidi nimwambie ukweli yote yaliyotokea ila msaada wangu mkubwa ilikuwa anitafutie mteja wa kununua simu yangu.
Akasema nauzaje nikamwambia simu nauza 90000 tu jamaa akasema ngumu kupata mteja leoleo Sema ngoja nimpigie simu Dada mmoja anauza chakula Ana shida sana na simu kubwa. Yule dada akaja alivyoiona na alivyokuwa na pupa ya kumiliki smart phone nikajua tu huyu ni mteja. Jamaa akasema niongee nae ilibidi nimwambie nauza laki moja maana ngozi nyeusi ukitaja bei harisi ushahalibu. Yule Dada akasema ana 80000 nikajifanya nakataa akaongeza 5000 nikamwambia toa pesa akanipa nikampa simu akaagana na jamaa akaondoka. Sasa kimbembe kikaanza Kati ya mm na huyu Dalali.
Jamaa nikampa 5000 akasema niache utani inabidi nimpe 20000 nikacheka kidogo huku mdomo ukiwa umekauka maana mpaka jua lilizama sijapata chochote cha kuchezesha kinywa changu.
Nikamwambia 20000 hapana kutokana na shida niliyonayo jamaa akasema vinginevyo anamwambia yule dada hii simu ya uwizi arudishe. Nikaona isiwe tabu nikampa 10000 nikasema hutaki naondoka na pesa sirudishi maana ilibidi nikunje sura vinginevyo nitakwama. Jamaa akapokea.
Alipopokea Ile pesa nikapotea mda huohuo. Sasa kimbembe nipakulala maana ikawa ni usiku huku nikiwa nimechoka sana. Nikaingia bar moja ivi inaitwa sewa. Nikaongea na muhudumu akasema Vyumba kwanzia saa saba usiku mdaa huu ni short time. Kwa kuwa nilikuwa na shida nikavumilia Ilipofika saa saba nikawa hoi kweli kweli nikiwa nimekaa kwenye kiti huku bar ikiwa imefungwa yule muhudumu akaja akasema kaka pole nenda kalale chumba hicho apo. Akasema nimpe 4000 tu maana naonekana sipo sawa. Nikampa pesa yake Nikaingia kulala japo madadapoa walikuwa wanagonga sana mlango niwafungulie lakini sikujali.
Asubuhi kukapambazuka nikasema leo inyeshe mvua liwake jua sikai Dar. Mm nimemaliza kidato cha sita ila sikubahatika kuingia chuo kikuu lakini najua sana kufundisha. Nikasema hapa ngoja nikatafute kibarua cha kufundisha mikoani ila tu isiwe dodoma. Nikawaza sana nikasema hapa safari ni kwenda lindi. Nikachukua daladala mpaka mbagala, ilikuwa saa sita mchana, kufika pale wakasema mda huu Gari za lindi mpaka temeke hapa mbagala ipo gari ya kwenda kilwa mda huu inaitwa MASHALAH.
Kwasababu kichwa changu mda huo hakikuwa sawa nikasema nikate tiketi tu hata ya kwenda kilwa nitajua mbele ya safari. Wakasema nauli Dar mpaka kivinje ni 11000 halafu Dar mpaka kilwa ni 13000.
Saa sita na nusu tukawa tumeondoka Dar Es Salaam kuelekea kilwa nikiwa Sina ndugu wala yoyote anaenijua lakini nikiwa na Amani ya moyo kwakuwa kilwa sio sudani wala Uganda ni Tanzania pia.
Inaendelea...
Safari ya kuelekea Kilwa ikaanza. Nililipa nauli ya Dar Es Salaam to Kilwa shilling 13000 mfukoni mpaka na panda bus nikawa nimebakiwa na 70000 tu kutokana na pesa nyingine Jana usiku Nililipa gest 4000 asubuhi kabla ya kwenda kukata ticket nilienda saloon kunyoa kwa 2000 baadhi ya pesa nilikula mihogo na maji ya kunywa njiani. Ubovu nikuwa kwenye siti nilikuwa nimekaa na mtoto mdogo wa kike ambae alipakiwa na mzazi wake ila yeye huyo mzazi hakuwa anasafiri sasa akaniambia kuwa nimsaidie kumwangalia lakini pia konda alikuwa amepewa taarifa kimsingi ni mtoto ambae huenda ni miaka 11 au 12 huyu dogo yeye alikuwa anashukia somanga. Kwahiyo nikakosa hata msaada wa kuanzia nikifika kilwa itakuwaje maana nilikuwa nategemea labda mtu nitakae kaa nae atanipa mawazo namna ya mji ulivyo na jinsi ya kuhendo swala langu. Tukiwa safarini ilibidi nimuulize huyu dogo endapo anaijua kilwa ili tu nipate pakuanzia dogo akasema yeye hajawahi fika anaishiaga tu somanga maana ndo kwao. Nikapiga moyo konde nikajisemea moyoni kuwa liwalo na liwe itajulikana.
Tukiwa safarini niliona kibao kimeandikwa IKWIRIRI gari likasimama kwa dakika chache nikajiuliza kulikoni tena kumbe Kuna wa mama walisimamisha wakapanda lakini cha ajabu walikuwa wananuka shombo ya samaki na mabeseni yao. Kuna mmoja alikuja kusimama karibu yangu nikamuuliza kama Ana samaki akasema Sina mwanangu samaki zimeisha. Nikakausha huku mawazo ya kwenda nisipopajua yanakuja nakunikosesha raha kabisa. Mungu yumwema baada ya dakika chache nilipata usingizi mzito sana hii nikutokana na siku ya jana kutokupata usingizi wa kutosha namm kulala Kwangu nikupumzisha mawazo. Nilikuja kushtuka kutokana na makerere mengi yawafanyabiashara wadogo wadogo hususani wanaouza biskuti, korosho, mahindi ya kuchoma na kadharika, kuangalia pembeni dogo simuoni niliyeambiwa nimwangalie nikasema kulikoni tena nikaamka chapu kwenye siti nikaenda kumuuliza konda dogo niliekaa nae yuko wapi??. Konda akasema nina mambo mengi kaka huyo dogo ni yupi? Nikamwambia nilikuwa nimekaa nae siti moja mm nikalala lakini cha ajabu simuoni konda akasema keshashuka. Nikamuuliza kwani somanga tumepita maana mm ni mgeni konda akasema nipande kwenye bus hapo tulipo ndosomanga yenyewe na dogo kashapokelewa na wazazi wake tayari.
Nikapanda kwenye gari. Bus likaiacha somanga na safari ya kwenda kilwa ikawa imewaka moto, niliona bus limejaza wa mama ambao walikuwa wanauza samaki kwenye bus. Kwa kuwa nilikuwa na njaa sana nikasema hapa samaki ni bei sana nilifanya mistake kutokununua muhindi wa jero somanga anyway nitauliza kama ana samaki hata wa buku mbili hata kambale nitatafuna usabato nauweka pembeni.
Nikiwa nasubiri afike Kwangu yule mama muuza samaki nikawaza wale wa mama wa mwanzo waliopandia IKWIRIRI kwani ni tofauti na hawa? Mbona siwaoni? Pembeni Kuna mzee mmoja alipandia somanga kwahiyo tukawa siti moja nikamuuliza akasema wale kwao ni somanga IKWIRIRI huwa wanaenda kuuza samaki wakiisha wanarudi somanga, nikasema hapo Sawa
Mama muuza samaki akawa amefika Kwangu nikamwambia sogeza beseni nichague mwenyewe mama akasogeza beseni la samaki nijichagulie.
Kucheki kwenye beseni niliona samaki wakubwa tupu Aina ya kibua na Changu. Nikajisemea moyoni hapa nimetoka patupu hawa samaki bei yake siiwezi lakini acha tu nimuulize ni bei gani akitaja nimlushe aendelee kuwauzia wengine. Yule Dada akasema samaki ni buku buku. Nikasema ebu rudia tena? Akasema kaka bei haipungui samaki mmoja ni elfu moja. Jamani sikuweza kuamini samaki mkubwa ambae Dar Es Salaam ni 7000 somanga anauzwa buku. Nikasema hapa ndopenyewe nikamwambia anifungie samaki wa buku mbili. Nikachagua samaki wangu huku nikiwa na tabasamu la kusahau shida kwa dakika chache nitakazotumia kumnyanvua samaki na minofu yake. Mama akachukua samaki akawafunga kwenye gazeti na kumimina chumvi kiasi. Kwa kua biashara ni cash to cash basi ikabidi nitoe wallet nimpe pesa yake. Ningaingiza mkono mfuko wa nyuma sikuona wallet nikasema ivi kumbe nimeweka mfuko wa mbele kuangalia mfuko wa mbele wallet hakuna, nikasema nini tena nikaangalia mifuko yote Hola jasho jembamba likianzaga tu kunitoka ujue kweli. Yule mama akasema napitia nikamwambia Sawa aendelee tu kuwauzia abiria wa nyuma akianza kurudi atapitia...
Ikabidi niangalie chini ya seat huenda imedondoka yani Sasa mpaka mwili ukawa unatetema kichwa hakipo sawa na wale samaki nikawadondosha chini kwenye abiria huwa wanapita tukiwa tumekaa.
Nikasema hapana sio kweli wallet imeenda wapi?? Ilibidi nipaniki nikamnyanyua yule mzee tukiokuwa tumepanda nae mzee alivyoniona tu kuwa sipo Sawa nikaona akasimama nikawa naangalia kila Engle ya seat lakini sikupata wallet yangu yenye pesa zangu. Abiria wa pembeni yangu wakaniuliza kulikoni nikawaambia kilichotokea wakaishia tu kunipa pole. Nikajisemea labda nikiweka kwenye begi? Lakini sio kweli maana mpaka begi linawekwa kwenye boot la bus nilichomoa pesa yangu nikiwa ndani ya bus nikanunua maji tukiwa mbagala rangi tatu. Nikiwa nimechanganyikiwa nikasikia konda anatangaza kijiji flani jina nimesahau Kuna jamaa yupo nyuma akasema kwa sauti "shusha" konda akamwambia asogee mbele maana washafika ikumbukwe kuwa Ile misamaki kipindi nasechi wallet yangu nilidondosha chini ya tule tunjia twakupita abiria, jamaa aliekuwa anashuka akapiga akazikandamiza na American buti zake samaki zote zikawa chapati tena zikagandamana na kapeti la bus. Ile nasema we jamaa umekanyaga samaki zangu akajibu kwa hasira hapo ndobakuli ilipo samaki unazibwaga njiani, ikabidi ninyamaze Sasa nikawa sipo Sawa kabisa maana wallet siioni samaki sijalipia na mama ndohuyo anakuja kutoka nyuma kudai pesa ya samaki shilling 2000 na samaki zimekanyagwa hazitamaniki kiasi ambacho hata paka hawezi kula.
Post kama hii ilinitia kifungoni kwa kama siku sitaTumejaa kupata burdan na simuliziView attachment 2225342
Kwa kuwa safari bado inaendelea ataviona tu hapo mbele.Aah!! Afadhali ya ghetto. Mimi nshalala stendi juu ya zege katika kile kikalio kile na usingizi unakuja vizuri mixer unaota kabisa ndoto upo ughaibuni. Sembuse ghetto!!? Kuna vitu bado hujaona ndugu.
hadi sasa naendelea kupata maziwa fresh kwa kikombe, sijapata chai. naweka kambi hapa.-----SEHEMU YA TATU - - - -
Konda wa bus la MASHALAH alipotangaza kituo yule jamaa aliekanyaga samaki zangu akasogea mbele bus likasimama jamaa akashuka. Nikiwa nimeinama chini nikijikuta nadondosha chozi huku namkumbuka mama alikuwa akiniambia "Mwanangu mpwayungu village kabla hujafanya maamuzi fikiri kwanza". Maamuzi niliyokurupuka Kuanza safari ya kwenda kilwa ilihali mm sio mmakonde wala mmwera nasina ndugu wala kibarua cha kwenda kufanya maamuzi haya yaliniweka kwenye wakati mzito sana. Ghafla mama wa samaki akafika nikasikia sauti nikiwa nimeinama inasema "kaka samahani naomba 2000 nataka kushuka" lakini kwa kuwa nilikuwa kwenye msongo mkubwa wa mawazo wa kupotelewa pesa plus njaa sikuweza kumjibu zaidi ya kukaa kimya nikiwa nimeinamia siti, yule mama nikasikia analalama we mkaka nataka kushuka mbona hunijibu nataka pesa yangu aliongea kwa sauti ya radi yenye mrindimo nadhani alikuwa mndengereko wa rufiji huyu. Ilinibidi niamke kukumbana na fedheha nikamjibu kuwa mama sio tu 2000 hapa sina hata Mia pesa zangu zote sizioni maana zilikuwa kwenye pochi. Yule mama nikaona ameshika kola yangu nilikuwa nimevaa Shati jeupe akasema hunijui sikujui nilikupa samaki wakiwa wazuri naomba pesa yangu natafuta riziki sikuja kuimba injili.
Aliponishika Ile kola yule babu wa pembeni yangu nikaona anamuongelesha kilugha sikuelewa ni lugha gani baada ya maongezi mengi yenye kerere nikaona yule babu kaingia mfukoni akampa mama wa samaki shilingi 1000 nasio 2000 yule mama alipopokea nikaona kaachia Shati langu akachukua beseni kwa hasira akaenda kukaa mbele karibu na dreva pale chini yake huwa hakunaga kiti ila unaweza kaa pia hususani hawa wachuuzi wa kupanda na kushuka. Yule babu akiniambia kijana kuwa na Amani nimempa pesa yake nikasema asante sana halafu nikakaa kimya. Bus likiwa kwenye mwendo kasi huku upepo unapukuta kufungua dirisha niangalie nje nikaona kumbe usiku umeingia. Nikasema hapa nikikaa kimya sitapata msaada wowote ikabidi nimwambie mzee tuliekuwa tumekaa nae hali halisi, yule mzee akanipa pole Kisha nikamwambia mm huku niendako ni mgeni sina mtu yoyote ninae mjua nimekuja kutafuta maisha. Yule mzee akasema hata yeye anaenda kwa mtoto wake ameoa juzi Kati kwahiyo anaenda kuwasalimia na kule ni mgeni pia ila ingekuwa ni somanga angeongea mengine. Nikasema hapa nimebugi hii safari ni ngumu kuliko ya wana wa Israel kuitafuta kanani.
Saa mbili usiku tukaingia stend ndogo hivi niyavumbi nikasikia konda anasema haya jamani wa kilwa kivinje teremkeni. Yule mzee akaniaga akashuka nikabaki peke angu. Nikiwa Sina hata Mia mfukoni saa mbili na nusu usiku bus likaiacha kilwa kivinje safari ya kuelekea kilwa masoko ikaanza. Nikawa najiuliza ivi nikishafika pale stend halafu naelekea wapi usiku huu, Shati lenyewe yule mama alilikunjakunja kalipaka mishombo ya samaki limechafuka siwataniona kibaka?. Nikasema sawa wacha tufike itafahamika tu maadam niendako ni watanzania wenzangu. Saa tatu na nusu hivi tukaingia kilwa masoko nandomwisho wa safari. Pale Kuna bodaboda nyingi vijana wa pale hawalali wakajazana kwenye mlango wa bus kutafuta abiria mkono uende kinywani, nikashuka nikapewa begi langu kwenye buti nikalibeba, bodaboda kila baada ya dakika mbili wanakuja vipi bro boda nawajibu Sina haja ya usafiri lakini wanarudi tena kuniuliza mwishowe nikatoka kwa mguu pale stend nikajisogeza pembeni kidogo nikakuta Kuna prutable wanacheza hapo ikawa kama ni saa nne na nusu hivi.
Nikiwa na begi langu kama mkimbizi mida ya saa tano yule mwenye prutable akaja akasema jamani nafunga nendeni mkalale, nikasema hapa sasa kazi ipo, nikaona wale vijana wanapita Kwangu kuniuliza tena kama ni abiria nikawa na jitahidi kuwa jibu kistaarabu kwamba siendi kokote ila ingekuwa kwetu mpwayungu wangeshapokea matusi, mwishowe wote wakaondoka. Sasa tukabaki mimi na yule mwenye prutable japo niliona ana kibanda cha vinywaji pia maana alikuwa anafunga. Anataka kuondoka tu nikamuwahi akasema wewe nani nikajieleza matukio yote yaliyotokea yule kijana akasema hapana siwezi kukupa msaada wowote maana saizi binadamu tumegeuka nyoka. Ikabidi aniache tena akasema nitoke pale sehemu yake ya kazi kwa ajili ya usalama wa mali zake. Ikawa ni saa sita usiku giza tororo Sina PA kwenda Sina hata Mia njaa inanipukuta, usingizi nikawa Sina kabisa kutokana na mashambulizi ya misukosuko.
Nikaona kukaa maeneo yale hapafai Sasa naenda wapi?? Kwa mbali nikasikia mziki unaunguruma nikasema huko huko naenda nikafata Ile sauti Kuna barabara ya mchanga ikawa inaenda mpaka kwenye huko mziki kumbe Kuna disco na watoto wa kike mle japo siwezi Sema ni watoto wakali maana hata hamu ya kuangalia Kuna nini humo sikuwanayo kabisa. Ile nafika tu disco ikawa imezimwa nikaona lundo la watu wa naondoka na vidada poa ila kwa muonekano vile vidada poa vimekubuhu vimefanya sana umalaya kimboka vikichuja vinaenda huko pembeni ya mji kuwa kamata maboya. Kila mtu alikuwa ananishangaa jinsi nilivyo maana wanajiuliza huyu wa wapi usiku huu na mbegi nzito halafu Shati haitamaniki sura ngeni?. Saa saba kamili kwenye Ile disco hapa kuwa na mtu tena. Sasa tukabaki mm na wale wahudumu wa ule ukumbi wa disco nikawafata nikawaambia maswahibu yangu wakasema msaada peke watakaonipa nikunipeleka kituo cha polisi maana pale naweza Pata pakujistiri.
Nikasema kwani kituo cha polisi Kuna vitanda vya kulala wageni, wakacheka kidogo huku wakiendelea kupanga maspika yao na manyaya Kisha wakajibu kuwa polisi hawawezi kukosa pakukuweka maana ni binadamu kama mm, ila wao kunipokea ngumu kwa sababu juzi Kati Kuna tukio kubwa lilitokea la mtu kuuawa kwenye njumba yake kwahiyo polisi kila siku wanasisitiza tusipokee wageni ambao hatuwafahamu. Nikaona kwenda kuomba msaada polisi huo ni uongo ngoja niendelee kuwashawishi tu. Nikawaambia kama hawana Imani na mimi nitawakabidhi hata vyeti vyangu vya shule bado walikataa wakafunga wakaondoka nikabaki peke angu. Ikawa ni saa saba na nusu hivi. Giza likawa totoro sauti pekee nilizoziskia ni za chura kwenye madibwi na bodaboda za wahuni wasiolala usiku.
Kukaa pale niliogopa sana maana lile eneo limejitenga nikasema hapa nirudi stend nilipotoka, nikafika stend Ile kufika tu Kuna vijana watatu nikakuta wamekaa kwenye bench moja hivi pembeni ya barabara ya lami karibu na stend nikasema hapo powa ngoja niende tupige story mpaka asubuhi. Nilipo fika nikasalimia wakasema mbona upo na begi usiku nikasema kawaida tu ila asubuhi nataka niende Dar kwa hiyo nasafiri ~niliwadanganya maana sio kila mtu wa kumwambia unayoyapitia kwa mda huo utaonekana mwehu angalia na nature ya Eneo. Kuna kijamaa flani hivi ni cheupe kirefu kiasi afu chembamba kikaja pale kikasema oya huyu Nani mazee mbona sura ngeni wakamjibu lakini kile kijamaa nikishari sana nadhani kakajua huyu nimeokota Leo. Kuna jamaa mmoja umri umeenda kiasi akasema mwache unamuhoji wa nini kila mtu na maisha yake. Yule jamaa akavutwa pembeni na hiki kushkaji kigomvi akapewa nadhani ilikuwa bangi Ile jamaa nikasikia anasema shukurani mtu wangu ngoja nikalale. Kumbe aliambiwa chukua bangi huyu mtu tuachie kwa nilivyohisi.
Wakabaki watatu Sasa hawa wote nilikuja kugundua ni vibaka wanaosumbua mji baadae nitaeleza. Kile kijama kikaja kilikuwa na bodaboda mbaya zaidi haina plate number. Kakasema ebu nitoe buku ten nakurudishia. Nikajisemea moyoni kumbe huku pesa ni rahisi kiasi hiki? Yani hata simjui tayari nimpe pesa lakini kwa kuwa nimejua hawana Nia nzuri ngoja tuone. Nikasema Sina hata Mia jamaa wenzake wawili wakakaa nyuma yangu wakasema nyie ndo wezi mnakuja kilwa kuiba mnatoroka usiku huu saa saba Kuna bus gani la Dar ebu fungua Hilo beg. Nikafungua begi haraka maana sura zao hata maongezi yalibadilika ghafla, nilitamani mda huo hata Gari ya polisi ipite lakini Hola sikuskia hata sauti za pikipiki. Majamaa wakasachi begi walipoona hamna kitu wakaona vyeti vyangu vya form 4 na form six. Kile kijamaa kikawaambia oyaaaa chukua hivyo vyeti pesa atatoa. Niliposkia hivyo nikasema bora mniue cheti hakitoki Ile nashangaa nikaona kile kijamaa kimetoa kisu kikasema hiki kisu kina rangi gani nikajibu haraka nyekundu. Kikasema basi hatuogopi kukutoboa macho maana sisi hatuui sisi tunakupa ukilema tu. Jamani watu wa kilwa mtanisamehe ila mna roho mbaya Sana.
Ile nataka kuzuia begi langu kile kijama kikasogeza kisu kwenye jicho langu.
....... I naendelea........
Hii story imenikumbusha yako jamani.[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] siuache
Unabadikishaje nguo mwili ukiwa mchafu, si bado itakua chizi kavaa nguo mpya.Kwanini kipindi una minguo michafu na una muonekano wa chizi hukubadilisha nguo ili uitengeneze muonekano mzuri ili hata ukitaka kuongea na watu wakuone sio chizi ila ukaamua uje kubadilisha baadae ulipoenda kuoga? Huoni kwamba unaondoa hisia za waodhani hii ni stori ya kweli kwa huko kupanga kwako matukio?
Ungemalizia tujue safari ilitamatikaje..Tarehe 4 mwezi wa pili 2020 nikiwa katika msongo wa mzito wa mawazo yaliyotokana na ugumu wa maisha nilijikuta nafanya maamuzi magumu bila kutarajia. Nilikuwa nakaa gheto maeneo ya buguruni sheli japo gheto lilikuwa na mshikaji wangu ambae tulisoma nae primary mawenzi shule ya msingi iliyopo moshi mjini mwaka 2006 ndotulimaliza darasa la saba hapo.
Nikiwa nimelala saa sita usiku naona napigwa mgongoni kwa nguvu kuamka namuona rafiki angu tunaelala chumba kimoja pia ndommiliki wa gheto mm kaniweka tu kishkaji, nikasema kulikoni jamaa akajibu kiunyenyekevu akisema "oya demu wangu kafukuzwa na Dada ake alipokuwa anakaa kwahiyo hana pakwenda nasaizi ni saa saba usiku amekuja yupo hapo kibarazani anataka tulale humu kwahiyo please wewe ni mwanaume ebu tafuta ustaraabu wa kuondoka saizi ukija asubuhi tutaweka mambo Sawa ".
Nikamwambia sasa mda huu mm niende wapi ndugu na Sina hata sehemu yakujiegesha!? Akajibu nitajua mwenyewe, ikabidi nivae niende kimboka night club kupoteza mda nikawa naangalia movie kwenye mabanda ya pale kimboka maana majamaa huwa hawalali. Ilipofika asubuhi nikatia timu bahati nzuri nikakuta wote wameamka ila wapo kitandani nikamsalimia shemeji pamoja na jamaa angu japo hawakuonesha uso wa tabasamu walikuwa serious kiasi ambacho nilishindwa kuwaongelesha.
Nilipotazama juu kwenye enga zakuwekea nguo zangu ghafla sikuona nguo yoyote, nilipouliza jamaa akasema nimekuwekea kwenye begi ili ukija usisumbuke kuzipanga maana shemeji ako kasema yeye hatoki atakaa hapahapa sasa hatuwezi kulala watatu. Ilikuwa ni kipindi kigumu sana Kwangu zaidi ya Alpha konde alipotolewa madarakani. Nikatazama juu chini nikawaza nikasema haina shida.
Nikabeba begi langu nikawaaga wakasema kila raheli. Nilikuwa na simu Aina ya tecno F1 na mfukoni nikawa na 20000 nikasema Poteleapote nitaenda popote pale kutafuta rudhiki.
Kwa pesa niliyokuwa nayo kukaa Dar Es Salaam hapakunifaa tena, hiki ndokipindi ambacho mikoani unapaona nafuu kuliko jiji la Dar Es Salaam. Nikiwa na begi langu Zito la nguo mpaka mida ya saa kumi jioni nilikuwa sijajua niende wapi na nitalala wapi. Nilipoona mda unakwenda ilibidi nimfate jamaa mmoja ivi yeye anauza nguo za jinsi buguruni sokoni kama unaenda shell nilipofika alinichangamkia akijua ni mteja kumbe ni mtu mwenye dhiki aliehitaji msaada. Sikupoteza mda ilibidi nimwambie ukweli yote yaliyotokea ila msaada wangu mkubwa ilikuwa anitafutie mteja wa kununua simu yangu.
Akasema nauzaje nikamwambia simu nauza 90000 tu jamaa akasema ngumu kupata mteja leoleo Sema ngoja nimpigie simu Dada mmoja anauza chakula Ana shida sana na simu kubwa. Yule dada akaja alivyoiona na alivyokuwa na pupa ya kumiliki smart phone nikajua tu huyu ni mteja. Jamaa akasema niongee nae ilibidi nimwambie nauza laki moja maana ngozi nyeusi ukitaja bei harisi ushahalibu. Yule Dada akasema ana 80000 nikajifanya nakataa akaongeza 5000 nikamwambia toa pesa akanipa nikampa simu akaagana na jamaa akaondoka. Sasa kimbembe kikaanza Kati ya mm na huyu Dalali.
Jamaa nikampa 5000 akasema niache utani inabidi nimpe 20000 nikacheka kidogo huku mdomo ukiwa umekauka maana mpaka jua lilizama sijapata chochote cha kuchezesha kinywa changu.
Nikamwambia 20000 hapana kutokana na shida niliyonayo jamaa akasema vinginevyo anamwambia yule dada hii simu ya uwizi arudishe. Nikaona isiwe tabu nikampa 10000 nikasema hutaki naondoka na pesa sirudishi maana ilibidi nikunje sura vinginevyo nitakwama. Jamaa akapokea.
Alipopokea Ile pesa nikapotea mda huohuo. Sasa kimbembe nipakulala maana ikawa ni usiku huku nikiwa nimechoka sana. Nikaingia bar moja ivi inaitwa sewa. Nikaongea na muhudumu akasema Vyumba kwanzia saa saba usiku mdaa huu ni short time. Kwa kuwa nilikuwa na shida nikavumilia Ilipofika saa saba nikawa hoi kweli kweli nikiwa nimekaa kwenye kiti huku bar ikiwa imefungwa yule muhudumu akaja akasema kaka pole nenda kalale chumba hicho apo. Akasema nimpe 4000 tu maana naonekana sipo sawa. Nikampa pesa yake Nikaingia kulala japo madadapoa walikuwa wanagonga sana mlango niwafungulie lakini sikujali.
Asubuhi kukapambazuka nikasema leo inyeshe mvua liwake jua sikai Dar. Mm nimemaliza kidato cha sita ila sikubahatika kuingia chuo kikuu lakini najua sana kufundisha. Nikasema hapa ngoja nikatafute kibarua cha kufundisha mikoani ila tu isiwe dodoma. Nikawaza sana nikasema hapa safari ni kwenda lindi. Nikachukua daladala mpaka mbagala, ilikuwa saa sita mchana, kufika pale wakasema mda huu Gari za lindi mpaka temeke hapa mbagala ipo gari ya kwenda kilwa mda huu inaitwa MASHALAH.
Kwasababu kichwa changu mda huo hakikuwa sawa nikasema nikate tiketi tu hata ya kwenda kilwa nitajua mbele ya safari. Wakasema nauli Dar mpaka kivinje ni 11000 halafu Dar mpaka kilwa ni 13000.
Saa sita na nusu tukawa tumeondoka Dar Es Salaam kuelekea kilwa nikiwa Sina ndugu wala yoyote anaenijua lakini nikiwa na Amani ya moyo kwakuwa kilwa sio sudani wala Uganda ni Tanzania pia.
Inaendelea...
Safari ya kuelekea Kilwa ikaanza. Nililipa nauli ya Dar Es Salaam to Kilwa shilling 13000 mfukoni mpaka na panda bus nikawa nimebakiwa na 70000 tu kutokana na pesa nyingine Jana usiku Nililipa gest 4000 asubuhi kabla ya kwenda kukata ticket nilienda saloon kunyoa kwa 2000 baadhi ya pesa nilikula mihogo na maji ya kunywa njiani. Ubovu nikuwa kwenye siti nilikuwa nimekaa na mtoto mdogo wa kike ambae alipakiwa na mzazi wake ila yeye huyo mzazi hakuwa anasafiri sasa akaniambia kuwa nimsaidie kumwangalia lakini pia konda alikuwa amepewa taarifa kimsingi ni mtoto ambae huenda ni miaka 11 au 12 huyu dogo yeye alikuwa anashukia somanga. Kwahiyo nikakosa hata msaada wa kuanzia nikifika kilwa itakuwaje maana nilikuwa nategemea labda mtu nitakae kaa nae atanipa mawazo namna ya mji ulivyo na jinsi ya kuhendo swala langu. Tukiwa safarini ilibidi nimuulize huyu dogo endapo anaijua kilwa ili tu nipate pakuanzia dogo akasema yeye hajawahi fika anaishiaga tu somanga maana ndo kwao. Nikapiga moyo konde nikajisemea moyoni kuwa liwalo na liwe itajulikana.
Tukiwa safarini niliona kibao kimeandikwa IKWIRIRI gari likasimama kwa dakika chache nikajiuliza kulikoni tena kumbe Kuna wa mama walisimamisha wakapanda lakini cha ajabu walikuwa wananuka shombo ya samaki na mabeseni yao. Kuna mmoja alikuja kusimama karibu yangu nikamuuliza kama Ana samaki akasema Sina mwanangu samaki zimeisha. Nikakausha huku mawazo ya kwenda nisipopajua yanakuja nakunikosesha raha kabisa. Mungu yumwema baada ya dakika chache nilipata usingizi mzito sana hii nikutokana na siku ya jana kutokupata usingizi wa kutosha namm kulala Kwangu nikupumzisha mawazo. Nilikuja kushtuka kutokana na makerere mengi yawafanyabiashara wadogo wadogo hususani wanaouza biskuti, korosho, mahindi ya kuchoma na kadharika, kuangalia pembeni dogo simuoni niliyeambiwa nimwangalie nikasema kulikoni tena nikaamka chapu kwenye siti nikaenda kumuuliza konda dogo niliekaa nae yuko wapi??. Konda akasema nina mambo mengi kaka huyo dogo ni yupi? Nikamwambia nilikuwa nimekaa nae siti moja mm nikalala lakini cha ajabu simuoni konda akasema keshashuka. Nikamuuliza kwani somanga tumepita maana mm ni mgeni konda akasema nipande kwenye bus hapo tulipo ndosomanga yenyewe na dogo kashapokelewa na wazazi wake tayari.
Nikapanda kwenye gari. Bus likaiacha somanga na safari ya kwenda kilwa ikawa imewaka moto, niliona bus limejaza wa mama ambao walikuwa wanauza samaki kwenye bus. Kwa kuwa nilikuwa na njaa sana nikasema hapa samaki ni bei sana nilifanya mistake kutokununua muhindi wa jero somanga anyway nitauliza kama ana samaki hata wa buku mbili hata kambale nitatafuna usabato nauweka pembeni.
Nikiwa nasubiri afike Kwangu yule mama muuza samaki nikawaza wale wa mama wa mwanzo waliopandia IKWIRIRI kwani ni tofauti na hawa? Mbona siwaoni? Pembeni Kuna mzee mmoja alipandia somanga kwahiyo tukawa siti moja nikamuuliza akasema wale kwao ni somanga IKWIRIRI huwa wanaenda kuuza samaki wakiisha wanarudi somanga, nikasema hapo Sawa
Mama muuza samaki akawa amefika Kwangu nikamwambia sogeza beseni nichague mwenyewe mama akasogeza beseni la samaki nijichagulie.
Kucheki kwenye beseni niliona samaki wakubwa tupu Aina ya kibua na Changu. Nikajisemea moyoni hapa nimetoka patupu hawa samaki bei yake siiwezi lakini acha tu nimuulize ni bei gani akitaja nimlushe aendelee kuwauzia wengine. Yule Dada akasema samaki ni buku buku. Nikasema ebu rudia tena? Akasema kaka bei haipungui samaki mmoja ni elfu moja. Jamani sikuweza kuamini samaki mkubwa ambae Dar Es Salaam ni 7000 somanga anauzwa buku. Nikasema hapa ndopenyewe nikamwambia anifungie samaki wa buku mbili. Nikachagua samaki wangu huku nikiwa na tabasamu la kusahau shida kwa dakika chache nitakazotumia kumnyanvua samaki na minofu yake. Mama akachukua samaki akawafunga kwenye gazeti na kumimina chumvi kiasi. Kwa kua biashara ni cash to cash basi ikabidi nitoe wallet nimpe pesa yake. Ningaingiza mkono mfuko wa nyuma sikuona wallet nikasema ivi kumbe nimeweka mfuko wa mbele kuangalia mfuko wa mbele wallet hakuna, nikasema nini tena nikaangalia mifuko yote Hola jasho jembamba likianzaga tu kunitoka ujue kweli. Yule mama akasema napitia nikamwambia Sawa aendelee tu kuwauzia abiria wa nyuma akianza kurudi atapitia...
Ikabidi niangalie chini ya seat huenda imedondoka yani Sasa mpaka mwili ukawa unatetema kichwa hakipo sawa na wale samaki nikawadondosha chini kwenye abiria huwa wanapita tukiwa tumekaa.
Nikasema hapana sio kweli wallet imeenda wapi?? Ilibidi nipaniki nikamnyanyua yule mzee tukiokuwa tumepanda nae mzee alivyoniona tu kuwa sipo Sawa nikaona akasimama nikawa naangalia kila Engle ya seat lakini sikupata wallet yangu yenye pesa zangu. Abiria wa pembeni yangu wakaniuliza kulikoni nikawaambia kilichotokea wakaishia tu kunipa pole. Nikajisemea labda nikiweka kwenye begi? Lakini sio kweli maana mpaka begi linawekwa kwenye boot la bus nilichomoa pesa yangu nikiwa ndani ya bus nikanunua maji tukiwa mbagala rangi tatu. Nikiwa nimechanganyikiwa nikasikia konda anatangaza kijiji flani jina nimesahau Kuna jamaa yupo nyuma akasema kwa sauti "shusha" konda akamwambia asogee mbele maana washafika ikumbukwe kuwa Ile misamaki kipindi nasechi wallet yangu nilidondosha chini ya tule tunjia twakupita abiria, jamaa aliekuwa anashuka akapiga akazikandamiza na American buti zake samaki zote zikawa chapati tena zikagandamana na kapeti la bus. Ile nasema we jamaa umekanyaga samaki zangu akajibu kwa hasira hapo ndobakuli ilipo samaki unazibwaga njiani, ikabidi ninyamaze Sasa nikawa sipo Sawa kabisa maana wallet siioni samaki sijalipia na mama ndohuyo anakuja kutoka nyuma kudai pesa ya samaki shilling 2000 na samaki zimekanyagwa hazitamaniki kiasi ambacho hata paka hawezi kula.
Nyizi kama hizi zilipotea sana humu, [emoji22] nakumbuka stori kama hizi alikuwa nazo KITOABU, na jamaa mmoja nime msahau jina alisafiri kwenda South Africa [emoji1221] miaka hiyo aka kutana na pisi kali Tshepiso kama sija kosea [emoji38] yaani Jf kuna raha sana.
Hii chai, maeneo ya Stand, kibaka hawezi kuwa na ujasiri sijui wa kunificha chin ya gari kukungoja wewe usiye na hela, na vyeti vya nini.
Inawezekana ni kweli ila umeongeza uongo mwingi, sehemu hii ya Vibaka imeharibu uhalali wa andiko lako kwa 100
Inaonekana kwelikwa kutaja majina ya shule nimeanza amini hii stori