Siyo lazima kila alama ya mvuka kwa miguu (zebra) dereva wa gari asimame, Sheria ifumuliwe imepitwa na wakati

Siyo lazima kila alama ya mvuka kwa miguu (zebra) dereva wa gari asimame, Sheria ifumuliwe imepitwa na wakati

Sheria yetu ya usalama barabarani (Road Traffic Act, 1973) hailazilimishi dereva kusimama bila uwepo wa mvukaji. Sheria inamtaka dereva kusimama endapo kuna mwenda kwa miguu anataka kuvuka.
Hata hivyo kuna baadhi ya vivuko vya waenda kwa miguu vyenye alama au mchoro unaosomeka "STOP', hapa ni lazima kusimama hata kama hujaona mvukaji anataka kuvuka. Alama hizi zinawekwa sehemu yenye waenda kwa miguu wenye changamoto kama watoto au wenye ulemavu na kwenye mazingira yenye uoni hafifu.

Pia sheria haitamki gari kuzuiliwa endapo dereva kafanya kosa. Kinachofanyika ni kuzuia gari ili liwe kama dhamana, lakini sheria haitamki hivyo.

Makosa yanayofanywa na askari yasichukuliwe kama madhaifu kwa sheria. Hata hivyo kuna haja ya kuipitia upya RTA ili kurekebisha mambo yaliyopitwa na wakati.

Hata hivyo ili kuleta ufanisi kuna haja ya kufanya mabadilko kwa kikosi cha usalama barabani ili kiwe na askari wenye weledi wa sheria wanayosimamia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Angeongelea sheria zenye madhaifu lakini sio ishu ya zebra hiyo ni international infact sheria za barabarani zote ni international kama umeendesha nchi nyingine utanifahamu so sioni cha kurekebisha labda kuongeza tu
 
Siyo kweli, weka takwimu ! Ndiyo maana nikasema ziwepo zebrà nyekundu kuonesha ulazima, na nyingine ziwepo kuonesha tahadhali kwa wote dereva na mpita njia ambayo mtu anavuka tu kukiwa salama/ siyo lazima kusimama
Utakua umeondoa maana ya Zebra ukiweka nyekundu...
 
Nchi zilizoendelea unakuta watu wengi wanasubiri taa yao nao waukesha upo sahihi Hong Kong kwa zile bara bara pana bila Zebra tusingevuka...
Bila kusahau wenzetu hata kama ni saa9 usiku hakuna mvukaji mtu akifika kwenye taa kama imewaka red atasimama mpa green ukivuka utakutana na invoice mlangoni..watz wengi wana ulimbukeni utaki kuheshimu zebra unawahi wapi?
 
Bila kusahau wenzetu hata kama ni saa9 usiku hakuna mvukaji mtu akifika kwenye taa kama imewaka red atasimama mpa green ukivuka utakutana na invoice mlangoni..watz wengi wana ulimbukeni utaki kuheshimu zebra unawahi wapi?
Unakuta mtu yupo mishe za mjini tu hiyo speed anayokwenda utadhani ambulance ukimwambia tuitafute Mbeya/ Arusha anasinzia Road...
 
Wenye magari naona mnataka na barabarani tusivuke tupite angani sasa
 
Mbona rahisi tu dereva anaangalia kama kuna uhitaji wa kusimama anasimama ila kama hakuna anapita.
Hivyo hivyo mwenda wa miguu anangalia kama kuna sababu za kusubiri anasubiri sio unavuka tu madereva wengine wanawapapasa mapaja mademu zao huku wanaendesha hivyo unaweza akakuparamia 🤣🤣
 
Unakuta mtu yupo mishe za mjini tu hiyo speed anayokwenda utadhani ambulance ukimwambia tuitafute Mbeya/ Arusha anasinzia Road...
Sifa za kijinga kwelikweli...juzi tu hapa jamaa kauliwa kwa kipigo cha bodaboda kisa kagonga bajaji na kuua wote waliokuwamo kisa speed za kijingajinga jamaa wakamchomea kwenye kasubaru kake
 
Sifa za kijinga kwelikweli...juzi tu hapa jamaa kauliwa kwa kipigo cha bodaboda kisa kagonga bajaji na kuua wote waliokuwamo kisa speed za kijingajinga jamaa wakamchomea kwenye kasubaru kake
Daah wapi hiyo Mkuu aisee Bajaji nazo za kuchunga sana maana unakuta dereva kajaza harafu nae hayupo makini...
 
Nimekuuliza ni wapi huko traffic police anakupiga fine unapopita zebra wakati hakuna watembea kwa miguu, hutaki kusema! Hivyo wewe ni muongo!

Mimi siyo traffic ila mimi ni dereva na mtembea kwa miguu!
Kibaha maili Moja kwenye mzani wa zamani
 
Back
Top Bottom