FF ndo yuleyule au,niliandaa uzi kukuulizia wewe na maralia sugu,nirudi kwa mada,vijana wetu wanachangamoto kubwa sana kabla ya mwaka 2005 simu hazikuwa nyingi na pia simu hazikuwa na teknolojia kubwa kama sasa,sasa sisi tuliosoma miaka hiyo tulikosa changamoto hizo,ila sasa wanafunzi wa baada ya 2005's kuna changamoto,ipad,simu nyingi plus intanet,tablet mitandao ya kijamii mingi,fm radio nyingi,matamasha ya mziki sasa mtoto kama ajitambui anazolewa na ulimwengu wa digitali
"VV"
Kila nikipata muda huwa natazama hiki kipindi kinachorushwa katika EATV na host wake akiwa ni Allan Laki. Sina shaka na upeo wa huyu kijana maana maswali yake ya papo kwa hapo kwa wanafunzi yanatoa changamoto ya kutosha. Hofu yangu ni uelewa finyu mno wa wanafunzi ambao huwa wanakutana na maswali ya huyu kijana.
Ni vijana walio kati ya umri wa miaka 14 hadi 22 hivi. Ukiwaona kabla ya maswali ni vijana waliochangamka sana na wenye kujiamini. Confidence zao huanza kupotea pale wanapotupiwa swali la kwanza tu, mathalan tofauti kati ya trekta na katapila. Mwanafunzi anaweweseka. Glacier erosion ni nini. Mwanafunzi anaweweseka wakati amesoma hayo.
Wanafunzi hao ni werevu sana kwenye burudani lakini taaluma zao wako hoi mno. Nini kifanyike? Hili ni suala letu kujadili wote hapa.
Isitoshe, watoto wa siku hizi tunawadekeza sana. Hatupo "strict" kama tulivyolelewa sisi.
Mi nazani kama wazazi na walezi tuwape elimu ya kujitambua watoto na ndugu zetu,pia kuwa wa kali juu ya swala la elimu kwa wale watoto wasiojitambua,kuna baadhi ya familia zamani kama utaki kusoma au unafukuzwa unaambiwa nenda kijijini unapewa na shamba,ukiona ugumu unarudi shule kwa nguvu,sema tuna katishwa tamaa na wabunge wetu,kuna mbunge mmoja aliwai sema kuferi si kuferi maisha sababu yeye alifeli na ni mbunge nilisikitika kwa kweli
CC Raiafulan,madame b,Faizafoxy
"VV"
sasa hapo ndipo ujue waalimu wake wanachoka kiasi gani.
Kuna siku niliwah kujiuliza mbona enzi zetu sisi akili tulikuwa nazo?? Mbona wakati ule kipindi cha mama na mwana kilikuwa na maswali lkn tulimudu kuyajibu?? Ama kipindi cha watoto wetu cha rtd??
Yumkini maisha halisi yamebadili wanetu, yumkini wazazi tumejisahau kabisa. Leo hii usishangae kwenye familia utakutana na magazeti ya udaku mwanzo mwisho kila siku lkn hukuti magazeti ya siasa, uchumi, habari na michezo.
Zile quiz kwenye magazeti zamani tulishindana kuzifaya iwe ni hesabu ama kiingereza ama sayansi ama somo lolote lile. Atlas tulitumis kujifunza dunia na mabara yake. Watoto tulijua mito mikubwa si tu tanzania bali ulimwenguni mwote. Nakumbuka mfereji mkubwa kuliko yote duniani nilijifunzia kwenye atlas (suez canal) lkn leo hii hata maziwa yaiyopo nchini mwanafunzi hajui.
Kongosho kumbuka kila mkoa tulijua ni maarufu kw akilimo cha zao gani la biahsara kwa la chakula. Tulijifunza makao makuu ya kila mkoa, pamoja na miji maarufu kila mkoa na makabila yake leo hii mwambaie mwanafunzi akutajie makabila yaliyopo kwenye mkoa wake uone kama atataja.
Lkn waulize mwanamziki gani anatoka na nani utamsikia weee bwana acha kabisa
Ni kweli mkuu, ila nawe naomba ukajinoe na imla kidogo.
Kuhusu imla nakumbuka mwanafunzi mmoja aliulizwa imla ni nini akasema ni wakati ule mwalimu anasoma na wanafunzi wanaandika. Akawa sahihi. Akaulizwa kama ameshawahi sikia kuhusu utawala wa kiimla akasema hapana. Akaulizwa kiongozi wa kiimla ni wa aina gani hakuelewa. Akaulizwa dictator ni kiongozi wa aina gani akajibu ni yule anayetawala kimabavu, akapata. Akaulizwa tena uongozi wa kidikteta kiswahili unaitwaje akasema hajui. Ilipaswa atumie akili kidogo kuoanisha hayo. ina maana udadisi hakuna.
mkuu kichwa cha habari na yaliyomo east and west
mkuu kwann unasema hivyo??
hivi unajua aina za uandish wa vichwa vya habari??
je huoni kwamba katumia tamathali za semi kufikisha ujumbe kwa hadhira yake?? kwanza kwa uandish huu ameonekana ni mtu anayejua vyema tasnia ya uandish na ambaye amebobea katika matumizi sahihi ya tamathali za semi.
unless na wewe ni wale wale
Hakyanani kwa kweli.. unashindwa hata uanzie wapi, wakati huohuo unaskia serikali inataja maasilimia makubwamakubwa ya ufaulu hujui hata wameyatoa wapi, kimsingi hali ni mbaya.
Kama Mwamedi?Huyo ndiye usiseme kabisa, badala ya watoto kulala na kutuliza bongo zao, saa 9 za usiku tukiamshwa kuwahi foleni ya unga. Usinikumbushe mateso aliyotupa nchi nzima.
Mzee yule, Mungu amlaze anapostahiki.
Kama wazazi na walezi tufanye nini maana changamoto ndo hizi
"VV"""
Kama Mwamedi?
Hujatulia wewe. Nadhani somo la gfsonwin limekukomboa.