SMZ: Kuna ongezeko la uhamiaji holela wa watoto kutoka Tanzania Bara kuja Zanzibar

ANGALIZO:
Moderator naomba usibadilishe kichwa cha Uzi maana mnatabia ya kubadilisha uwelekewa uzito wajambo.

Kuna mda kuficha ukweli kwenye platform mlizoziweka wenyewe mjengi kitu sababu mnafanya watu kubaki na madukuduku yao.

Mada moja iliwekwa kuwa kuna wahamiaji wengi wakiingia visiwani toka tanzania je ili jambo baada ya kuona watu kuwa wakali mkabadilisha mada baada ya muhusika mwenye kutoka huko kuandika alivyo uona muungano kwake kama sisi wahamiaji kwenda huko.

Bado kuna mambo mengi ambayo muungano unamapungufu na tukiyaficha yanweza yasifichike tena huko mbeleni kwa watanganyika.

UZI USIFUTWE
 
Sasa hamtaki watu kuingia mbona nyie huku bara mmejaa kila kona ya nchi na husikii milio kama yenu. Acheni ubinafsi, ndo maana halisi ya neno muungano hiyo!
 
Akili zao ni maji taka sana

Hakuna wanachokijua zaidi ya ufuasi wa imani.
Hapa ndio mnapojichanganya, kitu kidogo tayari mnatia udini, Zanzibar ni inchi inakaliwa kwa mabavu na Tanganyika, ni eidha tuendelee kuvumilia hivi vimaneno au tuwape inchi yao tuishi kwa amani.
Kwanini tunawang'ang'ania?
 
tukisema icho kiwilaya kiondoke kwenye nchi yetu kijitegemee, wanagoma, inakuwaje wanawafanya watoto wa bara kama vile ni wageni toka nchi za nje? yaani watoto wa kitanzania ni wahamiaji ndani ya tanzania?
Sio kweli bwashee, wazenji wanataka hata sasa hivi muungano ufe na wawe na inchi yao, ni sisi ndio tunawan'gang'ania
Kwanini tuungane? Tuwaache tu tuone nani ataetaabika?
Viazi vyenyewe, nyanya, kabichi, matunda na kila mimea inatokea Tanganyika,
Kwanini tunawan'gang'ania?
 
Uhamiaji ni suala la Muungano tangu zamani.
Katika mazingira ya kutatanisha, Zanzibar wameondoa si la Muungano kwa mujibu wa Makamu wa kwanza wa Rais Othman Masoud Othman . Tuna ushahidi hapa JF

Hivi mtoto anaweza kuhamia Dar es Saaam kutoka Mbeya akaitwa mhamiaji haramu?

Wazanzibar walioko Tanganyika ni wengi kuliko waliobaki Zanzibar. Wakija huku wanasema 'ni Watanzania'
Wakitaka kuingiza bidhaa hafifu wanasema wasitozwe kodi na TRA kwasababu sisi ni nchi Moja
''Nchi hiyo moja haitambui watoto wa nchi moja''.

Lakini pia Watanganyika mnashangaa nini? Wazanzibar walisimama Bungeni Dodoma na kusema si Watanzania! Hakuna aliyekemea JMT au SMZ kwa maana viongozi waliridhia ''ukweli'' huo

Mnaaza kutuelewa tunaposema kuna tatizo !

JokaKuu
 
Hapa ndio mnapojichanganya, kitu kidogo tayari mnatia udini, Zanzibar ni inchi inakaliwa kwa mabavu na Tanganyika, ni eidha tuendelee kuvumilia hivi vimaneno au tuwape inchi yao tuishi kwa amani.
Kwanini tunawang'ang'ania?


Tuwang'ang'anie kwa manufaa gan toka kwao?

Kwamba huelewi kinachotufanya tubakie kwa huu muungano au ndio kujitoa lock tu kwa ubongo?

N.B Kuna kijimstari chembamba sana kilichotofautisha UDINI na ZANZIBAR.
 
eti Tanzania bara kuja Zanzibar na sio Tanzania visiwani tena😁
 
Ubaguzi huu
 
Ukweli ni kwamba Zanzibar (Unguja) kuna idadi kubwa ya waMasai, watoto na wadada waliokwama kwenye "modern slavery".
Hivyo hizo takwimu za watoto 66 au 19 ni kupunguza ukubwa wa tatizo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…