"Social Economic Empowerment Program" Madrassa Yabuni Mpango wa Kijamii wa Kuwezeshanana kiuchumi

"Social Economic Empowerment Program" Madrassa Yabuni Mpango wa Kijamii wa Kuwezeshanana kiuchumi

Hebu turudi nyuma, tusome hila na ghiriba zako. Je twaruhusiwa?
"ghiriba" ndio nini? Au ulitaka kuandika "ghilba"? Kasome kwanza uelewe kuandika vizuri Kiswahili, maana neno usilolielewa kuandika hata maana yake inaonesha huielewi, umejiandikia tu mradi na wewe uonekane waamo.

Au ndio kijiba cha roho?
 
Sujakuelewa hiyo "Je twaruhusiwa?"

Unakusudia nani kuruhusiwa au nani asieruhusiwa?
Hao ni kijiba tu cha roho, achana nao hao. Tuachie sisi tunaelewa hizo lugha zao za kiroho mbaya. Usongo tu umewashika.

Endeleza ubunifu Abdul, you have no match. Kule Shungubweni Beach mambo hayo ya Abaar Bricks nyumba kwa wote ya yanaanza lini?
 
Umeelewa lakini huamini.

Ndio, kwa Shillingi ,2500 (elfu mbili na mia tano) tu unaanza ujenzi wa nyumba yako tena, yenye ubora wa hali yajuu na ghorofa juu.
Weka namba tuanze kutuma hiyo 2,500 faster tujengewe nyumba
 
"ghiriba" ndio nini? Au ulitaka kuandika "ghilba"? Kasome kwanza uelewe kuandika vizuri Kiswahili, maana neno usilolielewa kuandika hata maana yake inaonesha huielewi, umejiandikia tu mradi na wewe uonekane waamo.

Au ndio kijiba cha roho?
Umefufuka ngariba wa JF
 
Weka namba tuanze kutuma hiyo 2,500 faster tujengewe nyumba
Kwanza napenda kukufahamisha kuwa hatupokeai pesa mpaka ufike kwetu tukubaliane namna ya kuwezeshana na tuwe na mkataba.

Jichunge sana kutuma pesa kwenye mtandao bila kuwa na mikataba. Utapeli wa mitandao ni mwingi siku hizi.

Karibu sana kwetu uje kujionea namna za uwezeshaji zilizopo.
 
Faiza naona katoka pangoni🤭😆😆😆 kimyaa kingi kina mshindo!
Mambo.mengi yamepita ukikuwa kimyaaaaa!
 
Hongera kwa kazi nzuri ndugu.

Ujue kuna utaratibu ambao hardware nyingi hutumia ambao mteja hununua vifaa vya ujenzi kidogokidogo ukifikia lengo unachukua mzigo na kupeleka site kwa ujenze.

Je, huu utaratibu wako wa 2,500/- ni kama huu yaani mtu anatoa pesa wee hadi itimie gharama ya matofali kadhaa ndio anafata ama inakuaje hasa..?

Hebu funguka juu ya hili maana haingii akilini mtu atoe 2,500/- tu hapohapo na muanze kumjengea.
 
Hongera kwa kazi nzuri ndugu.

Ujue kuna utaratibu ambao hardware nyingi hutumia ambao mteja hununua vifaa vya ujenzi kidogokidogo ukifikia lengo unachukua mzigo na kupeleka site kwa ujenze.

Je, huu utaratibu wako wa 2,500/- ni kama huu yaani mtu anatoa pesa wee hadi itimie gharama ya matofali kadhaa ndio anafata ama inakuaje hasa..?

Hebu funguka juu ya hili maana haMingii akilini mtu atoe 2,500/- tu hapohapo na muanze kumjengea.


Mpango wetu ni tofauti na hardware ingawa unaweza kulingana kidogo. Sisi hatungoji utimize pesa kadhaa ndio tuanze kukujengea. Sisi kima unachotoa kidogo unakuwa tayari umeshajinunulia kifaa cha ujenzi na tunappokuja kukujengea tunatazama urahisi na wepesi wa fundi kujenga na si nini ulichotoa.


Mfano, kuja kukujengea tofari moja au mbili na tuna uwezo wa siku moja kwa gharama hizo hizo kukujengea tofari kumi basi tutakujengea tofari 10 hata kama katika kuanzia kwako hesabu zako ni za tofari moja au mbili. Inayobaki ni wewe ku topup tu akaunti yako mara kwa mara lkwa kadiri uwezavyo.


Tukifanyacho ni kukuwezesha kujenga na kutimiza ndoto zako.

Mfano, kwa teknolojia tunayotumia kwenye vifaa na ujenzi wetu, ni gharama nafuu kujenga nyumba ya uwezo wa kuwa na ghorofa zaidi ya moja, kwanini tukujengee ghorofa moja au ya chini pekee?


Mpango wetu na jinsi tunavyoutekeleza haijawahi kutokea duniani. Hatupo kujilimbikizia ma(kipato (mali). Tupo katika katika kujilimbikizia thawabu (kutumikia walimwengu wenzetu kadiri ya uwezo wetu> Sustainble human empowerment and development.


Hatukupi samaki, tunakupa nyavu za kuvulia samaki.
 
Of course vifaa vya ujenzi, iunatoa 2,500 unapata kifaa cha ujenzi. Kama hauna pa kukiweka tunakuwekea, vikitimia kumi tunakuja kuanza kukujengea. Unadunduliza kidogo kidogo.

Huu ni mpango wa kipekee, haujwahi kutokea. Si lazima uwe na mamilioni ndio uanze kujenga, unaanza kwa Shillingi 2,500 tu...
View attachment 1735662


Hivyo vifaa vya mtu anadunduliza.

Naomba kufahamu kuhusu hizo tofali Zenye mwanya katikati, 1. Je matumizi ya cement wa Kati wa ujenzi ukilinganksha na za kawaida. 2. Dhumuni la mwanya katikati ni kufanya bei ya Tofali ipungue ama ile nafasi inamatumizi maalum? Na nini maana ya Reinforcement concrete blocks?
 
Naomba kufahamu kuhusu hizo tofali Zenye mwanya katikati, 1. Je matumizi ya cement wa Kati wa ujenzi ukilinganksha na za kawaida. 2. Dhumuni la mwanya katikati ni kufanya bei ya Tofali ipungue ama ile nafasi inamatumizi maalum? Na nini maana ya Reinforcement concrete blocks?
Tofari zetu zenye mwnya kati zina kazi nyingi tofauti na zina faida nyingi tofauti na zipo za aina tofauti.

Kwanza naomba ufahamu kuwa tofari zetu zote ni za zege (cement, mchanga na kokoto) na zina kazi zaidi ya moja.

Zenye mwanya (hollow) kwa sasa zipo za aina tatu tofauti na zote zina kazi zaidi yamoja. Zipo za nchi 12 ambazo ni kazi yake ya kwanza ni kujengeaa nguzo (colums), zipo za nchi 8 kazi yake kuu ya kwanza ni kujengea chini ya ardhi (msingi) wa ukuta au basements. Za nchi nne kazi yake kuu ni kukatia kuta za juu ya ardhi (partitions) na hata kupandishia kuta za nje.

Kazi za ziada za tofari za nchi nane zemye "mwanya' ni kuwa unaweza pia kupandishia ukuta juu au zikawa ni floor slab hali kadhalika kwa zile za nchi 4.

Faida zake, kwanza ni ngumu sana, pili, hazipitishi na hazinywi maji maji kupandisha maji kwenye ukuta. Tatu, ule mwanya unasaidia kuifanya nyumba isipate joto la jua mchana na usiku inafanya usiipate baridi kwa haraka. Ule uwazi ni insulation.

Faida yake nyingine kuu ni unapozitumia kwenye msingi, unakuwa huna haja wala kuingia gharama za mbaoya mbao, misumari au fundi mbao. Na kwa misingi mingi ambayo haizidi kina cha meter moja kwenda chini na hakuna udongo wa kumomomnyoka basi hauhitaji nondo kwenye msingi wako.

1619476939157.png


Mfano hizo juu zinatumika kama tofari za msingi kabla hazijaongezewa zege kuuimarisha msingi. Na hapa chini zimeongezewa zege...

1619477164262.png
 
Tofari zetu zenye mwnya kati zina kazi nyingi tofauti na zina faida nyingi tofauti na zipo za aina tofauti.

Kwanza naomba ufahamu kuwa tofari zetu zote ni za zege (cement, mchanga na kokoto) na zina kazi zaidi ya moja.

Zenye mwanya (hollow) kwa sasa zipo za aina tatu tofauti na zote zina kazi zaidi yamoja. Zipo za nchi 12 ambazo ni kazi yake ya kwanza ni kujengeaa nguzo (colums), zipo za nchi 8 kazi yake kuu ya kwanza ni kujengea chini ya ardhi (msingi) wa ukuta au basements. Za nchi nne kazi yake kuu ni kukatia kuta za juu ya ardhi (partitions) na hata kupandishia kuta za nje.

Kazi za ziada za tofari za nchi nane zemye "mwanya' ni kuwa unaweza pia kupandishia ukuta juu au zikawa ni floor slab hali kadhalika kwa zile za nchi 4.

Faida zake, kwanza ni ngumu sana, pili, hazipitishi na hazinywi maji maji kupandisha maji kwenye ukuta. Tatu, ule mwanya unasaidia kuifanya nyumba isipate joto la jua mchana na usiku inafanya usiipate baridi kwa haraka. Ule uwazi ni insulation.

Faida yake nyingine kuu ni unapozitumia kwenye msingi, unakuwa huna haja wala kuingia gharama za mbaoya mbao, misumari au fundi mbao. Na kwa misingi mingi ambayo haizidi kina cha meter moja kwenda chini na hakuna udongo wa kumomomnyoka basi hauhitaji nondo kwenye msingi wako.

View attachment 1765246

Mfano hizo juu zinatumika kama tofari za msingi kabla hazijaongezewa zege kuuimarisha msingi. Na hapa chini zimeongezewa zege...

View attachment 1765248

Asante sana kwa ufafanuzi naamini ninaweza kuwa na mengi ya kujifunza ila nimeridhika kwa kiasi fulani je unaweza kuelekeza jinsi ya kufika ofisini kwenye maana sipajui misugusugu ni wapi labda na panda basi la wapi nashukia wapi?
 
Sisemi kufundishwa kujenga ni vibaya. Hata wamisionari walitufundisha elimu lakini haikutusaidia kitu ikilinganishwa na ukoloni waliouwezesha. Hizi dini zimeua mila na namna yetu ya kuishi na kutufanya mafala tunaotegemea pepo katika umaskini wa kutengenezwa nazo. Kwanini sisi tusiende kuwasaidia hao waarabu na wairani au wazungu wakati tumejaliwa raslimali nyingi kuliko wao? Blessed is the hand that giveth than the one that taketh mwanangu.
Tumezoea kuzoea mazoea, kuna wakati tunabidi tufikirie nje ya sanduku, kwanza tuache kuitana majina mabaya, kwani jina baya humuua mbwa, halafu tuwe na dhana njema kwa kila mmoja wetu, ikiwa unadhani kuna mtu anaweza kudhulumu au kudhulumiwa katika mradi huu basi jaribu kuelewana na muhusika ili upate kujihakikishia ukweli, utekelezaji na uhalisia wa mradi wenyewe huenda ukawa na fikra bora zaidi za kuboresha mradi huu kwani nia ya mradi ni mtu kupata makazi kwa gharama nafuu, kutoa elimu ya ujenzi bora na wa gharama nafuu na kutoa ajira, kwa kweli ikiwa tutaweza kuungana mkono bila shaka hatatokea mtanzania mwenye kukosa nyumba ya kuishi.

Tuwekeni imani zetu pembeni, kama Mzee Abdul Ghafur angetaka mradi huu uwe kwa watu wa imani moja tu basi angekuwa akitangazia katika sehemu zao za ibada, lakini kauleta hapa penye kila ya aina watu ili watu wapate nao kujua kuwa mtu anaweza anza kujenga hata kwa 2500/-, tumezoeshwa kujenga nyumba lazima uwe na pesa nyingi, kumbe hata ukiwa na pesa kidogo unaweza anza kujenga.
 
Asante sana kwa ufafanuzi naamini ninaweza kuwa na mengi ya kujifunza ila nimeridhika kwa kiasi fulani je unaweza kuelekeza jinsi ya kufika ofisini kwenye maana sipajui misugusugu ni wapi labda na panda basi la wapi nashukia wapi?
Ikiwa unatokea Dar mjini, unapanda basi la kuja Mbezi Mwisho, hapo utapata mabasi ya kwenda Mlandizi. Unapanda basi la kwenda Mlandizi, unashuka kituo kinaitwa Miyomboni shule au Misugusugu shule ya Msingi, usishuke Misugusugu check point.

Hapo unachukua bodaboda, unamwambia bodaboda akulete Madrassatul Abraar au kwa Mzee Ghafur. Wanachukua 1,000 pakiwa pakavu. Wanaweza kuongeza kidogo siku pakiwa na matope na inabidi wazunguke kutafuta barabara nzuri.

Karibu sana.
 
Sisemi kufundishwa kujenga ni vibaya. Hata wamisionari walitufundisha elimu lakini haikutusaidia kitu ikilinganishwa na ukoloni waliouwezesha. Hizi dini zimeua mila na namna yetu ya kuishi na kutufanya mafala tunaotegemea pepo katika umaskini wa kutengenezwa nazo. Kwanini sisi tusiende kuwasaidia hao waarabu na wairani au wazungu wakati tumejaliwa raslimali nyingi kuliko wao? Blessed is the hand that giveth than the one that taketh mwanangu.
Unakaribishwa kuja kujioneaa huo unaouita "ugaidi" na tunakuomba baada ya kututembelea na kujionea yaliopo urudi hapa kutangaza ulichokikuta. Ruksa kuja na camera kupiga picha zetu, za tunachokifanya na au za chochote utachokikuta hapa. Kwa sharti tu urudi hapa kukiandika ulichokikuta.

Achana na fikra hasi, hazitakuendeleza wewe wala wanaokuzunguka.

Kwa kukujulisha zaidi; Kuna vija zaidi ya 25 waliofaidika na kumaliza mafunzo ya awali ya mwezi mmoja. Wengine wameamua kuendelea na mafunzo ya ziada (kupata uzoefu). Kuna mafundi waliojifundisha ufundi kivyao na waliokuwa wakifanya kazia zao za ufundi, kwa miaka mingi, waliojiandikisha mafunzo yetu, wameamua kubaki hapa hapa na kufundisha wanaokuja wapya.

Tunashukuru tumefanikiwa vizuri sana katika miezi yatu miwili ya mwanzo, kiasi sasa tuna wanafunzi wapya wanajiandikisha kwa uwiano wa mwanafunzi mmoja mpya kila siku. Mpaka inabidi wengine wasubiri na inabidi tuongeze madarasa na shifts za kufundisha ili kila mmoja afaidike kwa wakati.

Kumbuka, hapa kwetu ni mafunzo kwa vitendo, sio kwa porojo.
 
Unakaribishwa kuja kujioneaa huo unaouita "ugaidi" na tunakuomba baada ya kututembelea na kujionea yaliopo urudi hapa kutangaza ulichokikuta. Ruksa kuja na camera kupiga picha zetu, za tunachokifanya na au za chochote utachokikuta hapa. Kwa sharti tu urudi hapa kukiandika ulichokikuta.

Achana na fikra hasi, hazitakuendeleza wewe wala wanaokuzunguka.

Kwa kukujulisha zaidi; Kuna vija zaidi ya 25 waliofaidika na kumaliza mafunzo ya awali ya mwezi mmoja. Wengine wameamua kuendelea na mafunzo ya ziada (kupata uzoefu). Kuna mafundi waliojifundisha ufundi kivyao na waliokuwa wakifanya kazia zao za ufundi, kwa miaka mingi, waliojiandikisha mafunzo yetu, wameamua kubaki hapa hapa na kufundisha wanaokuja wapya.

Tunashukuru tumefanikiwa vizuri sana katika miezi yatu miwili ya mwanzo, kiasi sasa tuna wanafunzi wapya wanajiandikisha kwa uwiano wa mwanafunzi mmoja mpya kila siku. Mpaka inabidi wengine wasubiri na inabidi tuongeze madarasa na shifts za kufundisha ili kila mmoja afaidike kwa wakati.

Kumbuka, hapa kwetu ni mafunzo kwa vitendo, sio kwa porojo.
Samahaniii hiyo nauli- kutoka kibaha Hadi hapo madrasa ni 10000 kwa pikipiki au umekosea kuandika ulimaanisha 1000
 
Back
Top Bottom