Soka la Tanzania limekua au soka la Afrika limeshuka?


We jamaa Upo wapi Taifa stars inayumba wakati ipo afcon mzee
 
Taifa star ina qualified caf sio mafanikio au unatak mafanikio aende kombe la dunia
 
Soka la bongo limekua sana kwa kiasi kikubwa na hili linatokana na uwekezaji mkubwa wa miundombinu, rasilimali watu na sera za nchi.

Leo hii mchezaji anasajiliwa kwa dau la zaidi ya milioni 400 na inakua sio stori ukilinganisha na miaka ya nyuma.

Miaka 8 nyuma zaidi tulikuwa tunafanya sajili za kukomoana na wala sio za mikakati na zisizo na tija kwa timu ilihali sasa hivi tunafanya sajili za kimkakati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi za west Africa Kama Ghana, Nigeria, Ivory coast, Zambia, Mali, Congo DRC, Algeria, Uganda, Zimbabwe kwa uchache wachezaji wao wengi wazuri wamekuwa walikimbilia ligi za ulaya au Africa Kusini. Wakati nchi za Uganda, Kenya, Zambia, Nigeria, Ghana, Mali, Congo DRC na Zimbabwe wachezaji wanaokosa nafasi ulaya wamekuwa walikimbilia Tanzania kutokana na uwekezaji uliopo hivyo washindani wetu wakubwa ni kutoka nchi za Afrika Kusini na nchi za kiarabu.
 
Kuna mchango wa Azam Media pia, bila kusahau watu kama Manara. Tunaelekea level zao kiushindani, kuanzia uwekezaji mpaka mafanikio.

Soon tutaanza kulipa mishahara ya milioni 50-100 kwa wachezaji, na italipa.
Manara amewekeza nini? Si kafungiwa na kwa Mara ya kwanza Yanga kafika fainali, Simba na Yanga zote zinaingia group stage?
Mnatukuza sana haya madomo kaya
 
Kuliko ligi ya DRC?
 
Kuliko ligi ya DRC?
thamani na ubora wa ligi yetu huwezi fananisha na DRC kwa sasa,top players wao wanaenda arabuni au Tanzania,.bingwa wao TP MAZEMBE kafungwa home and away na yanga,pia simba ya TZ kwa karibu miaka mitatu kacheza robo final,mazembe na vita hawajacheza..yanga kacheza final mazembe na vita sikumbuki mara ya mwisho wamecheza nusu
 
Ni muda mfupi tu lakini,
 
Manara amewekeza nini? Si kafungiwa na kwa Mara ya kwanza Yanga kafika fainali, Simba na Yanga zote zinaingia group stage?
Mnatukuza sana haya madomo kaya
Propaganda zipo kila sehemu, na zinatengeneza brand. Namna yake ya ushabiki tangu akiwa Simba na Sasa Yanga imeongeza hamasa katika soka.

Kama kuna anachovuna Manara katika soka, basi tambua kuna alichowekeza.
 
Propaganda zipo kila sehemu, na zinatengeneza brand. Namna yake ya ushabiki tangu akiwa Simba na Sasa Yanga imeongeza hamasa katika soka.

Kama kuna anachovuna Manara katika soka, basi tambua kuna alichowekeza.
Hivi Brand ya Simba na Yanga imekuzwa na Manara kweli?🤣🤣🤣

Simba na Yanga zipo miaka na zina mashabiki wengi toka enzi, Manara kaja juzi ndio unasema kakuza brand?

Manara ndio kadandia umaarufu wa Simba na Yanga kujikuza, sio kuwa amezikuza...
 
Brand haikuzwi na MTU mmoja.
Tunaposemea mchango wa watu waliokuza mpira bongo, hatuwezi kuwaacha kina manara, wachambuzi, media, wawekezaji, TFF, serikali, nk... Hao wote kwa pamoja wamesaidia kunyanyunyua soka letu mpaka vilabu vyetu.
Usichoelewa nini?
 
Na makocha wa kigeni wanatuletea kitu, wameondoa/punguza uswahili na ufaza kwenye timu zetu.
 
Radios karibu masaa 5 kwa siku ni habari za michezo
 
Sio nisichoelewa, usichoelewa wewe ni kuwa watanzania wanapenda mpira tangia zamani, hawahitaji hamasa kuipenda Simba, au Yanga,
ni Simba ikifanya vizuri kutokana na uwekezaji wake, na uwekezaji wa kampuni kama Azam, na mashabiki wanahamasika zaidi, hata Taifa Stars ni hivyo hivyo, haihitaji hamasa uchwara bali uwekezaji mzuri na uwanja wa Taifa unakua unajaa,

Hao wachambuzi uchwara na wapiga domo , mpira hauhitaji domodomo, ni hela na management nzuri....Dunia nzima, mpira ni uwekezaji na management nzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…