Soma unaweza jifunza kitu: Jinsi graduate nilivyopoteza 1.8M niliyoitafuta kwa jasho

Soma unaweza jifunza kitu: Jinsi graduate nilivyopoteza 1.8M niliyoitafuta kwa jasho

Unajua nimeingia huu uzi baada ya kusoma sana juu ya kilimo ndiyo nimekumbuka kwamba nilipanda nyanya, zikasombwa, kwa hasira nikapanda viazi vitamu halafu vilivyochipua sijavirudia tena? Huu unaenda mwaka aisee 🤔
 
Pole sanaa ndugu amini usiamini anaekuibaia anakuongezea utajiri, ngoja nikupe short yangu kidogo nipo kwa taasisi ya umma flani basi kuna kazi ikatokea ya kutengeneza madirisha ya ofisi ikatoka kama 2 mil kwaajili ya kazi hiyo. Sasa pale mtaani kuna mwana nilimzoea ana kijiwe chake ni fundi fundi mara nyingi alikuwa ananilalamikia kuhusu kazi basi nikaona nimuunganishe kama kawaida.

Ofisi yetu huwa ina tabia ya kukuamini mtumishi, unapewa hela yote kajingaike nayo nikamkumbuka jamaa nikamuunganisha jamaa akaomba hela robo tatu afuate material nikampa akafuata akarudi na material chache kazi ikaanza. Ebwanaee sujui alipatwa na nini jamaa kanikimbia bwanaee na madirisha sikupata msala ukawa wangu boss wangu haeliwi anataka pesa au madirisha mwaka sasa nimetoka kukopa kwa taasisi moja kwa riba chafu nimelipa madirisha yote jamaa mwaka hajaonekana na wala sijui yuko wapi ila process zote nilifuata mikataba na rb ninayo natembea nayo, Mungu si athumani ipo siku tutakutana kinachoniuma sio kuniibia bali kupotezewa credibility pale ofisini sipewi deal tena. Usikate tamaa hadi leo nalipa deni kwa hiyo taasisi. So usife moyo hatujakatwa mikono
Mkuu hapo ofisini kwenu tushtuane tenda nyingne zikitokea ....... hasa za ufundii
 
Unajua nimeingia huu uzi baada ya kusoma sana juu ya kilimo ndiyo nimekumbuka kwamba nilipanda nyanya, zikasombwa, kwa hasira nikapanda viazi vitamu halafu vilivyochipua sijavirudia tena? Huu unaenda mwaka aisee 🤔
Hahaa,pole mkuu
 
Mie sinaga hamu kbs...watu walipata laki 2 na wakati huo mbegu ya kiroba ilikua 60 elfu ..bado vibarua...na wakawa wanachagua mihogo mizr ile midg wanakuambia hatuchuki...unahangaika 9mths unakuja ambulia 200000!!
Maisha haya bn ni safari ndefu sn..alafu mtu akiona umefanikiwa anachukulia powa,alafu Unamwangalia unasema hiiiiiiii...
 
Mkuu vip hizo tracker huwa wanazichomoa kumbe wanafanyaje....??

Woiii, tracker kwenye boda ina faida kwa asilimia chache sana, kwa udogo wa boda lazima mtu akiitafuta aipate, na hizi za kwetu kibongo bongo haiwezi kufanya kazi miezi miwili bila kuzingua, inafika muda unachoka kuiservice mpaka majanga yanatokea.
 
Wapendwa wanajf habari za usiku,

Leo akili imetulia nimeona nitoe simulizi fupi ya jinsi nilivyoweza kupoteza tsh 1.8M.

Mara baada ya kugraduate pale SUA na (BSC GM) na kushindwa kupata tempo nilijichanga katika kazi mbalimbali kama nyuzi zangu baadhi za nyuma zilivyoelezea mishemishe zangu ikiwemo shughuli za mchanga, tofali na tuition centre.

Kwa mwaka 2020 nilifanikiwa kukusanya kiasi cha shil milion 2 na laki 4 na niliamua hii pesa isikae benk tu kwavile bado naendelea kufight na mambo mengine basi niliamua kufanya biashara ya bodaboda.

Nilinunua bodaboda iliyokaribia kuisha kwa mkataba kwa tsh. 1.8M na kumkabidh mtu aendeshe kwa makubaliano tuliyoafikiana. Nilikuwa namfahamu lakini nilikua simjui sana kiundani na ndugu zake sana nilikuwa siwafahamu sana.

Nadiriki kusema nimeweza kupewa mrejesho wa siku 10 pekee na muda huu navyoongea zimepita takribani wiki 3 sijaweza kuonana wala kuwasiliana na dereva wangu, polisi nimeripoti kwa kufata taratibu lakini sioni matumaini ya kupata chombo changu, sijui mwenzangu ni mzima au ameaga dunia, nimejarbu kufatilia watu wake imeonyesha ni mhamiaji katika maeneo ya mkoa niliopo.

Nawaza sana, nimeweza kupoteza pesa niliyoitafuta kwa jasho sana ndani ya mwaka mmoja, nikiri sikuweza kulala kwa siku 2 mfululizo, Nimeamini hii dunia haina huruma.

Kuna muda nawaza ile hela bora ningeweka tu, kuna muda nawaza sana nikiona mtu anaongelea pesa tu nawaza zile pesa zangu, nimebaki na kiasi cha laki 5 kwenye akaunti yangu nawaza lini nitafika tena kwenye milioni mbili na laki 4.

Kuna muda huwa nawaza sana nikifikiria njia ngumu nilizoweza kupata hii pesa na njia rahisi ilivyoweza kupotea hii pesa, kuna muda niliona haya maisha hayana maana na kupitia huu mkasa i was so harsh, niliweza hadi kuseparate na mtu wangu, Ok ni hayo tu nimeona nishare nanyi wakubwa.

Muwe na usiku mwema.
Nenda kwa mganga wa kienyeji
 
Naomba kuuliza swali kutokana na maelezo yako. Kwa nini uliachana na mwenza wako? Hii ni topiki tosha
 
Hizi ni pesa zinatafutwa mkuu. Afya njema ndio mtaji namba moja. Sahau hayo songa mbele,kama hakujatokea kitu
 
Kwenye harakati za utafutaji kupoteza ni sehemu ya maisha.

Jambo la msingi ni kupambana kupunguza risk za kupoteza.

Mimi nilifanya kazi za usiku, nikakusanya zaidi ya 1M nikaenda kulima mihogo huku Kibiti. Haikurudi hata 100.

So, ni kawaida tu.
Vip mkuu nguruwe walikula mihogo?
 
Mkuu, mazingira na muda haukuruhusu basi tu hata nikielezea ilivyokuwa ni kama maajabu yalipangwa kufanyika Siku hiyo.
Nairejesha taratibu lakini bado ni swala limefanya akili yangu isiwe sawa.
Uliibiwa au uliporwa?
 
Pole sana mkuu ila next time tujitahidi kupunguza risks 6M unapanda daladala? Si bora hata uchukue bajaji ama Uber tusilaumu sana ilikua siku yako tu yakufundishwa na ulimwengu. Pole
Sasa Jamaa alikuwa mchumi Sana bas angekodi daladala peke yake
 
Mie niliibiwa kwenye daladala 6.4 M mwezi uliopita tena ya Ofisi, nikitembea nahisi moyo unachomoka nikikaa nahisi hivyo hivyo ni mateso ambayo sijawi kuyapitia toka kuzaliwa kwangu.
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] noma sana
 
Back
Top Bottom