Somo kwa wahafidhina wa Laliga

Somo kwa wahafidhina wa Laliga

Je Timu ya Uengereza yaweza Kucheza Fainali ya UCL?

  • Ndiyo

  • Hapana


Results are only viewable after voting.
E.P.L ni ligi yenye ushindani maana ina timu nyingi zenye viwango vinavyokaribiana...

La liga ni ligi ya kibepari, kuna timu bora kabisa ambazo hata uzipeleke wapi lazima zitajipigia tuu watu na pia kuna timu zingine nzuri kama sevilla , atletico madrid na valencia ambazo timu za England zikikutana nazo huwa zinaijua shughuli yao
viwango vibovu sio vinavyo kalibiana.... hakuna ushindani ni kelele nyingi tu hamna kitu pale...
 
Wachache sana tulioiamini Madrid kama ingeweza win Uefa back to back last season....

By the way Madrid hana cha kupoteza hata wakishindwa,ukizingatia bado ana kikosi kile kile cha back to back, akishinda tena kuna haja ya yeye kashiriki kombe lisilo na ushindani na kikosi kimoja tu???
Acha porojo nimekwambia njoo tuandikishane huo mkataba
 
Kwa season 10 ilopita, kombe la UEFA limeenda spain mara 6, barca mara 2 na real mara 4.
Mara ya mwisho mchezaj bora kutoka epl ilkua lin??
 
Kwa season 10 ilopita, kombe la UEFA limeenda spain mara 6, barca mara 2 na real mara 4.
Mara ya mwisho mchezaj bora kutoka epl ilkua lin??

Wewe Unaweweseka Na Ndiyomana Hujui Hapa Watu Wanajadili nini..
 
Mara ya mwisho bingwa wa champions league kutoka England ni 2012..

Kwahiyo kwa misimu 5 champions league imechukuliwa na nchi nyingine..

Kati ya mara hizo 5 , mara 4 ubingwa umeenda la liga, na moja ujerumani...

Hapo usiulize katika mfululizo huo la liga wamekutana fainali wenyewe mara ngapi, nusu fainali mara ngapi wanakutana wao tuu wanapunguzana..

Uliza wafungaji bora wa uefa champions league wanatoka ligi gani kwa miaka 10 iliyopita???

Wachezaji bora wa hiyo Uefa, kuanzia mabeki , viungo hadi washambuliaji wanatoka ligi gani?

Ukishamaliza kujiuliza na kupata majibu utajua mwenyewe ligi bora ni ipi..

Tatizo England mafanikio kidogo mdomo mwingi, just imagine harry kane angekuwa ana goli 9 za kama Ronaldo sahizi au Manchester united wangekutana fainali champions league na liverpool mara mbili ndani ya miaka mitatu kama atletico na real madrid.. uone jinsi wangepiga makelele
Huu uzi ni matokeo ya furaha ya Liverpool kushinda 7-0. Otherwise kwa kuwa muhusika hataki kujadili yaliyopita isipokuwa yanayojiri msimu huu, well and good. Tukutane naye May tuone 5 EPL vs 3 La LIGA vs 2 (SERIE A) Vs 1 (other leagues)6.
 
Naomba huu uzi usiufute maana wanafiki kama nyie hamchelewi kubadilika badilika kama taxi bubu
 
EPL au EFL?

sevilla kachukua mara ngingi pia europa itabidi amuongeze ktk idadi ya timu zinazo compete pale laliga... bila kusahau wakina AT, AB, VL, VR nk...

celte ana mfunga sana barca huyo vipi.... nae...

Umeshindwa kusoma nilichoandika?
 
IWAPO TIMU ZISIZOPUNGUA 2 KATI YA TIMU 5 ZILIZOFUZU LAST 16 HAZITATINGA SEMI FINAL BASI NITAJIPIGA BAN YA KUTOZUNGUMZIA CHOCHOTE HAPA JF KUHUSU CL MPAKA MSIMU UISHE
 
Mimi Nina Uhakika na Ninajiamini Kuwa Ninatamka Wazi CL marahii inatua Uengereza! isipokuja basi Salary Yangu Ya Miezi 6 ya Kazini Naichoma Moto Hadharani..

Nani Yuko Tayari Tubeti?
 
Mashabik wa epl mnalazimisha sana mambo ila huwez kuwa na ligi bora kama huna wachezaji bora, ukweli ni kwamba laliga inaifunika epl
 
Tatizo Letu Hamujui Tofauti Ya LIGI BORA, na TIMU BORA...

Yawezekana LIGI IKAWA MBOVU kama LALIGA lakini Ndani Yake Mukawa na TIMU BORA kama Zilivyo REAL na BARCA kutokana na uwekezaji Wao...

Yawezekana LIGI IKAWA MBOVU kama ilivyo FRANCE lakini Mukawa na TIMU BORA kama ilivyo PSG kutokana na uwekezaji wake...

Yawezekana Ligi IKAWA MBOVU kama ilivyo Ujerumani lakini Ndani Yake Mukawa na TIMU BORA kama ilivyo Beryan kutokana na Uwekezaji wake
...

Kwahiyo Jifunzeni Kudadavua Mambo...

EPL NI BEST LEAGUE IN THE WORLD

Technical hakuna ubora kwenye ligi ya EPL.....
1.British Football Imperialism through Media Empirialism ndicho kilichowabeba EPL walikuwa wajanja kutoa ligi yao ionekane mataifa mengine kwa muda sahihi
2.EPL ilivutia mataifa mengi hasa baada ya kukaribisha wachezaji wa mataifa mbalimbali tena wakiwa hawana ubaguzi wa kiwango cha juu kama Italy,German na hata Wahispania wenyewe

Mataifa mengi Tanzania ikiwemo yalikuwa hayana option ya kuangalia mpira hivyo Uingereza walijipatia umaarufu.
Licha ya La Liga kuwa bora mataifa mengi hasa ya Africa mashariki hayakupata nafasi ya kuangalia mechi za La Liga kutokana na muda wa kick off lakini walitambua hili na ndio maana hata watanzania sasa tumeanza kufuatilia la liga.
Mbona unauliza maswali mepesi...

La liga kati ya miaka mitano 5 imechukua ubingwa mara 4, we unaleta mifano hata hailingani, eti fc porto mara inter, nambie ligi yao ndani miaka mitano ilichukua mara ngapi..

Wachezaji bora wote wa dunia wapo la liga, mataji yapo la liga, kigezo chako cha ubora ni kipi?
Wanashindwa kutofautisha kati ya UBora na Umaarufu.......EPL ni maarufu na kupitia hilo imeweza kuvutia wachezaji wengi baada ya matangazo ya TV kuwaingizia mabilioni ya fedha.
 
E.P.L ni ligi yenye ushindani maana ina timu nyingi zenye viwango vinavyokaribiana...

La liga ni ligi ya kibepari, kuna timu bora kabisa ambazo hata uzipeleke wapi lazima zitajipigia tuu watu na pia kuna timu zingine nzuri kama sevilla , atletico madrid na valencia ambazo timu za England zikikutana nazo huwa zinaijua shughuli yao
Ndugu yangu Valencia shughuli gani? Ni team ndio mwaka huu imeanza kurudi kwao ndani. Sevilla ni team za misimu tu zinakuja na zikipotea zinapotea vibaya kama deportivo. Athletico circle yao inaisha kama ile ya 1996. Ni team hazina muonekano kama wa Barca na Madrid. La liga ni team mbili tu hizo zingine kama mvua za msimu.
 
Hatuzungumzii timu au ligi zinazoshinda Uefa kwa ngekewa au mara moja moja tu

tunazungumzia sure team ambazo kila siku zipo tunazungumzia sure ligi ambazo zenyewe kila msimu kama sio mabingwa basi semi final inawahusu kaanzia Uefa mpk Europe wacha kuwaonea Porto na Inter Milan ambao tangu washinde Uefa miaka kibao mpk sasa bado wapo na hangover za ubingwa

Ukija kwa bayern mi tangu nianze kushabikia mpira 2002 nimeona bayern kashinda Uefa mara moja tu na ni mara 2 tu kuona timu za bundes kufika fainali kwahiyo usijifiche kwenye kichaka cha timu zilizokuwa na takwimu duni na ndo maana ligi zao hazijawahi kuwa bora...
Kwa hiyo kwa maneno yako wakati Real Madrid waliposubiri miaka 30 kushinda tena CL toka 66 mpaka 98 walikuwa wabovu? Real ni team kubwa hata miaka hiyo japo hawakuweza kuchukua ubingwa. Barca ina history team kubwa wameanza kuchukuwa CL 92 miaka yote zero. CL ni circle tu kila mtu anapita halafu anapotea. League bora ni league ya ushindani ila watu humu tuko katika CL. Ukifika knock out stage hata ukiwa mzuri unaweza ukapigwa na team ya kawaida.
 
Timu za la liga zimelichoka hilo kombe maana miaka mitatu mfululizo wanachukua,fainali mbili zikihusisha timu za la liga ndani ya miaka minne. Msimu huu ni upepo tu umeegemea upande wenu EPL na mtashangaa hatua zinazofuata mnaondolea wote.
 
Back
Top Bottom