SOMO LA BURE: Namna ya kuagiza bidhaa kutoka CHINA kwa ajili ya biashara (jumla) Kupitia Mtandao alibaba kwa kutumia simu yako

SOMO LA BURE: Namna ya kuagiza bidhaa kutoka CHINA kwa ajili ya biashara (jumla) Kupitia Mtandao alibaba kwa kutumia simu yako

Sorry naongelea Alibaba

The displayed price differ from the real product price
hili ni somo ambalo unapaswa kukaa chini kufahamishwaa... huelew ni namna alibaba wanaonesha bei zao.....

halafu usiwe unaangalia bei kwa tzs hapo ndio itakuvuruga kabisaa
 
hili ni somo ambalo unapaswa kukaa chini kufahamishwaa... huelew ni namna alibaba wanaonesha bei zao.....

halafu usiwe unaangalia bei kwa tzs hapo ndio itakuvuruga kabisaa
Hapo sawa hebu nifahamishe mkuu maana huwa siwaelewi

Wamedisplay product price tsh 1,700 kwenda inbox wanasema $8 nimechoka
 
Ndomaana kaweka contact Ili ufunzwe.Watu kama nyie huwa hamkosi,maelezo ya kina hivyo,hujaelewa?
Bora umpigie akueleweshe uelewe mazima,uepukane na kupigwapigwa na wajasiriamali.
Kuanzia hapo kwenye supplier na security ya Alibaba ndo.mtihani unaanza
 
Kuanzia hapo kwenye supplier na security ya Alibaba ndo.mtihani unaanza
Huu mwongozo nilioutoa kuna watu wameufuata kwa utaratibu na kuweza kuagiza bidhaa zao wenyewe na kurudi kuleta shuhuda na pongezi pia.
IMG_20241222_191824.jpg

Kama unajiona hujiamini katika mwongizo nilioutoa nitafute kwa mawasiliano niliyoweka mwisho wa uzi hapo.

Nitakushika mkono kukusaidia hatua kwa hatua mpaka unafanikiwa kuagiza mzigo wako mwenyewe.

Whatsapp +255 677 818283
 
Ningependa kutoa somo la bure kwa wale ambao wanawaza jinsi gani wanaweza kuanza kuagiza bidhaa kutoka china.
Bidhaa hizi ni za jumla kwa ajili ya biashara.
Utaagiza moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji.

Kupitia uzi huu utaweza kuona bei halisi za bidhaa pamoja na kujua ni jinsi gani utasafirisha mpaka mzigo unakufikia ulipo.

Pia utafahamu ni kwa namna gani utamtambua mzalishaji gani wa bidhaa utaweza kumtumia na yupi sio salama kumtumia.kuokoa pesa zako zisipotee.
Haya yote utaweza kuyafanya kupitia simu yako ya mkononi.

Niamini mimi haya mambo yanawezekana huhitaji mtu wa kukushika mkono zaidi ya huu mwongozo.

Watu wanapiga pesa kwa kuagiza bidhaa kupitia mtandaoni tu bila hata ya kukanyaga china.
Bidhaa utakayouziwa bongo 80,000 - 100,000.Jua mfanyabiashara huyo kainunua china 20,000 - 30,000.
View attachment 2945112
Bei ya china
View attachment 2945113
Bei ya Kuuzia Tanzania

Ijapokuwa kuna gharama za usafiri ila haiwezi zidi 15,000 mpaka 20,000 kwa kila blender.. hapo utaona gharama mpaka inamfikia mkononi mfanyabiashara ni 35,000 mpaka 40,000.

Ingia alibaba fanya utafiti wa bidhaa mbalimbali naamini huwezi kosa idea ya nini utaweza kuagiza na kuanza kuuza kwa faida nzuri.

Hata kama huhitaji kwa sasa embu download hii application, ufanye japo research ya kujua bei za bidhaa zipo vipi huko viwandani na huku masokoni wanauzaje.

Chunguza bidhaa zinazouzika mtandoni au madukani kisha jaribu kuja kuangalia viwandani china wanauzaje..kisha ujionee ni kwa jinsi gani watu wanapiga faida ndefu.

Tena kwa mikoani ndio usiseme.Kama mtu akinunua mzigo kariakoo anapata faida jee akiagiza kutoka china moja kwa moja itakuwaje?

HATUA YA KWANZA
1.Download application ya alibaba kupitia playstore au appstore.
Hiki ni zoezi rahisi tu.Ingia play store kwa wale wa android na appstore kwa wale wa iphone.

Application inaitwa alibaba
View attachment 2945124

Kisha idownload hakikisha unajisajili kupitia email ambyo ipo active kwenye simu yako na pia utakapohitajika kuweka namba ya simu weka namba ambayo ipo active kwenye simu yako.
ili watakapohitaji kufanya verification email na simu yako ziwe active kwa zoezi hilo.

Hatua hii ni fupi sana. Achana na taarifa za biashara wewe weka tu taarifa zako binafsi kisha anza kuperuzi..

Baada ya kujisajili unaweza kuamua kubadili fedha itakayoonekana kweny bidhaa ili uweze kupata picha ya bei kwa pesa yetu ya Tanzania.

Chini kulia kuna neno alibaba bonyezahl hapo kisha juu kulia utaona USD sasa ibonyeze kisha tafuta pesa ya tanzania TZS ili bidhaa zote zionekane kwa bei ya tzs
View attachment 2945131
Baada ya hapo unaweza sasa kuanza kutafuta bidhaa.

Kuna aina kuu mbili za utafutaji ningekushauri uanze nazo
.Kutafuta bidhaa (product)
.Kutafuta mzalishaji wa hiyo bidhaa (Supplier/manufacturer)

View attachment 2945132

Hapo juu utaona nimeandika hand bags halafu juu yake kuna maneno mawili products na manufacturers

Hapo juu nimechagua products ndii maana unaziona bidhaw mbalimbali na bei zake.

Ukichagua products wanakuletea bidhaa tu na ukichagua manufacturers wanakuletea viwanda/wauzaji wa hizo bidhaa tu.

Ili kama utataka kuona wauzaji uweze kuangalia bidhaa zao mbalimbali zinazohusiana na bidhaa uliyochagua.

Hapa chini nimechagua manufacturers/supplier utaona wananiletea majina ya viwanda au wauzaji wa aina hizo za bidhaa
View attachment 2945137

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA KUMCHAGUA SUPPLIER MZURI

1.Hakikisha ana alama ya verified (angalia picha hapo juu)

2.Mbele ya neno verified kuna miaka ambayo yupo katika mtandao wa alibaba.Kuanzia miaka 2 na kuendelea si mbaya ila angalia sifa ya 3 kujiridhisha zaidi

3.Angalia review (wanunuzi wanamzungumziaje huyu muuzaji)
hili ni muhimu pia.

View attachment 2945145

View attachment 2945146

Review itakusaidia kupata picha ya jinsi mzalishaji huyo au msambazaji anavyohudumia wateja wengine au ubora wa bidhaa yake..

Kitu kingine ni Trade Assuarance. Hii ni huduma ya alibaba ambayo pesa yako inakuwa haiend moja kwa moja kwa muuzaji mpaka alibaba watakapo kuridhisha kuwa hauna malalamiko yoyote juu ya muuzaji huyo.

View attachment 2945148

Unaweza muuliza huyo muuza kupitia chat now hapo kama ana support trade Assuarance.

Kitu unachotakiwa kufanya utakapo jiridhisha na bidhaa husika ni kubonyeza hiyo chat now ili uweze kuchat na muuzaji kabla hamjakubaliana kufanya malipo.

Unaweza muuliza wanaweza kuuuzia bidhaa ngapi kama MOQ (minimum order quantity) yaan idadi ndogo wanazoruhusu mtu kununua kutoka kwao.

Wapo wafanyabiashara wanaruhusu bidhaa kuanzia 10 wengine kuanzi 100 wengine 5 au hata 1.

Sasa ipo hivi ikiwa unataka ujihakikishie ubora wa bidhaa yaan uipate kwanza 1 ujiridhishe zaidi ongea na huyo suppier akutumie sample 1 ya bidhaa yao kwa njia ya ndege ili ukiipata hiyo bidhaa utajiri dhisha na kuamua kununua bidhaa nyingi zaidi kwa ajili ya biashara.

Hii itakusaidia kujiondoa katika riski ya kuagiza mzigo mkubwa ambao ukifika utajutia kwa kuwa haukidhi vigezo vyako.

Japo bei ya bidhaa ya sample 1 huwa kubwa kidogo ila ni bora zaidi kwa kuwa unajiridhisha kwa mara ya kwanza kujua ubora wa bidhaa.View attachment 2945152

Ukisha fanya resarch yako ya kutosha na ukaona umejiridhisha na bidhaa na bei na idadi ya bidhaa unazohitaji.

Mambo ya muhimu ya kuzingatia maana hapo ni bei ya bidhaa huko china.

unatakiwa ujue huu mzigo kuusafirisha mpaka unakufikia gharama yake ni kiasi gani na utatumia muda gani mpaka kukufikia?

Kuna mizigo unaweza safirisha kwa ndege hiu unawahi kufika inaweza chukua siku 7 tu kulingana na ratiba za ndege.
mizigo hii hupimwa kwa uzito kgs.
Ukishajua uzito wa bidhaa zako unawasiliana na agent wa kukusafirishia mzigo na kumueleza uzito na aina ya mzigo wako ili akupe bei kwa kilogram 1 ni kiasi gani.

Kuna mzigo inabidi uusafirishe kwa meli hii mizigo hupimwa mwa ujazo wa mita CBM (Cubic Metres) yaani urefu * upana * kimo vyotr katika metres.
Hapo unaweza muuliza muuzaji wako huu mzigo una CBM ngapi ukiufunga pamoja.

Muuzaji akikupa CBM nenda kwa agent wako wa kusafirsha mzigo akupe gharama kulingana CBM ya mzigo wako.

Baada ya kuona gharama za mzigo pamoja gharama za usafirishaji unazimudu.

Ndio unaweza kumwambia akuandalie payment link.

Hii ni link maalum ambayo ukiibonyeza inakuletea gharama za kulipia oda yako.

View attachment 2945166
Utaona hapo baada ya kukubaliana na supplier gharama akanipa hiyo link ya kulipia.
Ambayo inahitaji nilipe initial deposit 50% kisha wakimaliza kuandaa mzigo wangu nawamalizia 50% kisha wanatuma.

Hiyo link ukiibonyeza inakupeleka kwenye aina za malipo uchague

Mimi nachaguaga paypal kwakuwa nimeiunga na bank account yangu.
yaan haina longolongo zaidi ya verification ya simu yangu tu.

paypal itanionesha kiasi nacholipia katika usd na kiasi kinachokatwa katika account yangu ya TZS.

View attachment 2945170

Ukibonyeza agree & pay now hakikisha kiasi hicho kipo kwenye account yako.

Hapo malipo yataenda alibaba na supplier atapata taarifa na kuanza kushughulikia oda yako kulingana na makubaliano.

Hakikisha umempa supplier wako address ya agent ambaye atakusafirishia mzigo.

Supplier atapeleka mzigo kwa agent na baada ya hapo ni kazi ya agent kukuletea mzigo wako hapa Tanzania.

Maagent wapo wengi kuna silent ocean, mapembelo cargo, tosh cargo kuna shamwaa n.k.

watafute maagent hawa kisha wakupe address zao za huko china ili supplier apelek mzigo wako kwao.

View attachment 2945177

Hizo ndio hatua utakazohitajika kufuata ili kuweza kuagiza mzigo wako kutoka kwa wazalishaji china mpaka kukufikia Tanzania.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi wa namna ya kuagiza bidhaa kutoka china.

Napatikana whatsapp tu +255677818283
I
Ningependa kutoa somo la bure kwa wale ambao wanawaza jinsi gani wanaweza kuanza kuagiza bidhaa kutoka china.
Bidhaa hizi ni za jumla kwa ajili ya biashara.
Utaagiza moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji.

Kupitia uzi huu utaweza kuona bei halisi za bidhaa pamoja na kujua ni jinsi gani utasafirisha mpaka mzigo unakufikia ulipo.

Pia utafahamu ni kwa namna gani utamtambua mzalishaji gani wa bidhaa utaweza kumtumia na yupi sio salama kumtumia.kuokoa pesa zako zisipotee.
Haya yote utaweza kuyafanya kupitia simu yako ya mkononi.

Niamini mimi haya mambo yanawezekana huhitaji mtu wa kukushika mkono zaidi ya huu mwongozo.

Watu wanapiga pesa kwa kuagiza bidhaa kupitia mtandaoni tu bila hata ya kukanyaga china.
Bidhaa utakayouziwa bongo 80,000 - 100,000.Jua mfanyabiashara huyo kainunua china 20,000 - 30,000.
View attachment 2945112
Bei ya china
View attachment 2945113
Bei ya Kuuzia Tanzania

Ijapokuwa kuna gharama za usafiri ila haiwezi zidi 15,000 mpaka 20,000 kwa kila blender.. hapo utaona gharama mpaka inamfikia mkononi mfanyabiashara ni 35,000 mpaka 40,000.

Ingia alibaba fanya utafiti wa bidhaa mbalimbali naamini huwezi kosa idea ya nini utaweza kuagiza na kuanza kuuza kwa faida nzuri.

Hata kama huhitaji kwa sasa embu download hii application, ufanye japo research ya kujua bei za bidhaa zipo vipi huko viwandani na huku masokoni wanauzaje.

Chunguza bidhaa zinazouzika mtandoni au madukani kisha jaribu kuja kuangalia viwandani china wanauzaje..kisha ujionee ni kwa jinsi gani watu wanapiga faida ndefu.

Tena kwa mikoani ndio usiseme.Kama mtu akinunua mzigo kariakoo anapata faida jee akiagiza kutoka china moja kwa moja itakuwaje?

HATUA YA KWANZA
1.Download application ya alibaba kupitia playstore au appstore.
Hiki ni zoezi rahisi tu.Ingia play store kwa wale wa android na appstore kwa wale wa iphone.

Application inaitwa alibaba
View attachment 2945124

Kisha idownload hakikisha unajisajili kupitia email ambyo ipo active kwenye simu yako na pia utakapohitajika kuweka namba ya simu weka namba ambayo ipo active kwenye simu yako.
ili watakapohitaji kufanya verification email na simu yako ziwe active kwa zoezi hilo.

Hatua hii ni fupi sana. Achana na taarifa za biashara wewe weka tu taarifa zako binafsi kisha anza kuperuzi..

Baada ya kujisajili unaweza kuamua kubadili fedha itakayoonekana kweny bidhaa ili uweze kupata picha ya bei kwa pesa yetu ya Tanzania.

Chini kulia kuna neno alibaba bonyezahl hapo kisha juu kulia utaona USD sasa ibonyeze kisha tafuta pesa ya tanzania TZS ili bidhaa zote zionekane kwa bei ya tzs
View attachment 2945131
Baada ya hapo unaweza sasa kuanza kutafuta bidhaa.

Kuna aina kuu mbili za utafutaji ningekushauri uanze nazo
.Kutafuta bidhaa (product)
.Kutafuta mzalishaji wa hiyo bidhaa (Supplier/manufacturer)

View attachment 2945132

Hapo juu utaona nimeandika hand bags halafu juu yake kuna maneno mawili products na manufacturers

Hapo juu nimechagua products ndii maana unaziona bidhaw mbalimbali na bei zake.

Ukichagua products wanakuletea bidhaa tu na ukichagua manufacturers wanakuletea viwanda/wauzaji wa hizo bidhaa tu.

Ili kama utataka kuona wauzaji uweze kuangalia bidhaa zao mbalimbali zinazohusiana na bidhaa uliyochagua.

Hapa chini nimechagua manufacturers/supplier utaona wananiletea majina ya viwanda au wauzaji wa aina hizo za bidhaa
View attachment 2945137

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA KUMCHAGUA SUPPLIER MZURI

1.Hakikisha ana alama ya verified (angalia picha hapo juu)

2.Mbele ya neno verified kuna miaka ambayo yupo katika mtandao wa alibaba.Kuanzia miaka 2 na kuendelea si mbaya ila angalia sifa ya 3 kujiridhisha zaidi

3.Angalia review (wanunuzi wanamzungumziaje huyu muuzaji)
hili ni muhimu pia.

View attachment 2945145

View attachment 2945146

Review itakusaidia kupata picha ya jinsi mzalishaji huyo au msambazaji anavyohudumia wateja wengine au ubora wa bidhaa yake..

Kitu kingine ni Trade Assuarance. Hii ni huduma ya alibaba ambayo pesa yako inakuwa haiend moja kwa moja kwa muuzaji mpaka alibaba watakapo kuridhisha kuwa hauna malalamiko yoyote juu ya muuzaji huyo.

View attachment 2945148

Unaweza muuliza huyo muuza kupitia chat now hapo kama ana support trade Assuarance.

Kitu unachotakiwa kufanya utakapo jiridhisha na bidhaa husika ni kubonyeza hiyo chat now ili uweze kuchat na muuzaji kabla hamjakubaliana kufanya malipo.

Unaweza muuliza wanaweza kuuuzia bidhaa ngapi kama MOQ (minimum order quantity) yaan idadi ndogo wanazoruhusu mtu kununua kutoka kwao.

Wapo wafanyabiashara wanaruhusu bidhaa kuanzia 10 wengine kuanzi 100 wengine 5 au hata 1.

Sasa ipo hivi ikiwa unataka ujihakikishie ubora wa bidhaa yaan uipate kwanza 1 ujiridhishe zaidi ongea na huyo suppier akutumie sample 1 ya bidhaa yao kwa njia ya ndege ili ukiipata hiyo bidhaa utajiri dhisha na kuamua kununua bidhaa nyingi zaidi kwa ajili ya biashara.

Hii itakusaidia kujiondoa katika riski ya kuagiza mzigo mkubwa ambao ukifika utajutia kwa kuwa haukidhi vigezo vyako.

Japo bei ya bidhaa ya sample 1 huwa kubwa kidogo ila ni bora zaidi kwa kuwa unajiridhisha kwa mara ya kwanza kujua ubora wa bidhaa.View attachment 2945152

Ukisha fanya resarch yako ya kutosha na ukaona umejiridhisha na bidhaa na bei na idadi ya bidhaa unazohitaji.

Mambo ya muhimu ya kuzingatia maana hapo ni bei ya bidhaa huko china.

unatakiwa ujue huu mzigo kuusafirisha mpaka unakufikia gharama yake ni kiasi gani na utatumia muda gani mpaka kukufikia?

Kuna mizigo unaweza safirisha kwa ndege hiu unawahi kufika inaweza chukua siku 7 tu kulingana na ratiba za ndege.
mizigo hii hupimwa kwa uzito kgs.
Ukishajua uzito wa bidhaa zako unawasiliana na agent wa kukusafirishia mzigo na kumueleza uzito na aina ya mzigo wako ili akupe bei kwa kilogram 1 ni kiasi gani.

Kuna mzigo inabidi uusafirishe kwa meli hii mizigo hupimwa mwa ujazo wa mita CBM (Cubic Metres) yaani urefu * upana * kimo vyotr katika metres.
Hapo unaweza muuliza muuzaji wako huu mzigo una CBM ngapi ukiufunga pamoja.

Muuzaji akikupa CBM nenda kwa agent wako wa kusafirsha mzigo akupe gharama kulingana CBM ya mzigo wako.

Baada ya kuona gharama za mzigo pamoja gharama za usafirishaji unazimudu.

Ndio unaweza kumwambia akuandalie payment link.

Hii ni link maalum ambayo ukiibonyeza inakuletea gharama za kulipia oda yako.

View attachment 2945166
Utaona hapo baada ya kukubaliana na supplier gharama akanipa hiyo link ya kulipia.
Ambayo inahitaji nilipe initial deposit 50% kisha wakimaliza kuandaa mzigo wangu nawamalizia 50% kisha wanatuma.

Hiyo link ukiibonyeza inakupeleka kwenye aina za malipo uchague

Mimi nachaguaga paypal kwakuwa nimeiunga na bank account yangu.
yaan haina longolongo zaidi ya verification ya simu yangu tu.

paypal itanionesha kiasi nacholipia katika usd na kiasi kinachokatwa katika account yangu ya TZS.

View attachment 2945170

Ukibonyeza agree & pay now hakikisha kiasi hicho kipo kwenye account yako.

Hapo malipo yataenda alibaba na supplier atapata taarifa na kuanza kushughulikia oda yako kulingana na makubaliano.

Hakikisha umempa supplier wako address ya agent ambaye atakusafirishia mzigo.

Supplier atapeleka mzigo kwa agent na baada ya hapo ni kazi ya agent kukuletea mzigo wako hapa Tanzania.

Maagent wapo wengi kuna silent ocean, mapembelo cargo, tosh cargo kuna shamwaa n.k.

watafute maagent hawa kisha wakupe address zao za huko china ili supplier apelek mzigo wako kwao.

View attachment 2945177

Hizo ndio hatua utakazohitajika kufuata ili kuweza kuagiza mzigo wako kutoka kwa wazalishaji china mpaka kukufikia Tanzania.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi wa namna ya kuagiza bidhaa kutoka china.

Napatikana whatsapp tu +255677818283
Nimeuliza CBM nimepewa majibu hayo sijamuelewa
 

Attachments

  • Screenshot_20241223-145722.png
    Screenshot_20241223-145722.png
    136.6 KB · Views: 10
Kuanzia hapo kwenye supplier na security ya Alibaba ndo.mtihani unaanza
Wala hakuna mtihani hujapata elimu sahihi na hata ukifuata maelekezo yangu niliyotoa hapo unafanikiwa vizuri tu
 
Nimeanza kutafuta pesa tangu 1999 hakuna chochote nisichokijua kuhusu watu na pesa
Na mpka sasa bado unatafuta.Dunia ya kisasa imeshakuacha ndugu. Unaleta utafutaji wa pesa wa 1999 mwaka huu wa 2024.
 
Na mpka sasa bado unatafuta.Dunia ya kisasa imeshakuacha ndugu. Unaleta utafutaji wa pesa wa 1999 mwaka huu wa 2024.
Nikuambie kitu mambo ya pesa hayahitaji blahblah tena nikuambie kitu dunia ya sasa ndiyo yenye dhulma sana na ujanjaujanja mno
 
Nikuambie kitu mambo ya pesa hayahitaji blahblah tena nikuambie kitu dunia ya sasa ndiyo yenye dhulma sana na ujanjaujanja mno
Hakuja ujanja ujanja... ndio dunia ilipo.wewe sema tu dunia ya kisasa imekuacha na ujuzi wa kwenda nayo umekushinda.

Ndo nyie mtu akikwambia yupo bongk ila anafanya kazi za online na kulipwa mnasema utapeli kumbe ni dunia ya kisasa msiyoijua
 
Nikuambie kitu mambo ya pesa hayahitaji blahblah tena nikuambie kitu dunia ya sasa ndiyo yenye dhulma sana na ujanjaujanja mno
wewe unachokosa ni ujuzi ndio maana bado utatumia nguvu nyingi kuendes mambo yako katik dunia iliyorahisishwa
 
wewe unachokosa ni ujuzi ndio maana bado utatumia nguvu nyingi kuendes mambo yako katik dunia iliyorahisishwa
Ninachohitaji duniani ni pesa na sio blahblah shida yako ni moja unaamini mno nadharia....hayo yote nimeshawahi kuyafanya na nikayaona matokeo yake kiukweli utakuwa mjinga mno uagize bidhaa mathalani nguo online kwa mtaji ambao ukiamua kwenda china unaenda vizuri tu bila wasiwasi...mimi naitwa mnachihangu nipo na ofisi mtwara mjini na Tunduru ungekuwa huku ningekualika uje uone vitu nilivyopigwa kwa mfumo huo
 
Ninachohitaji duniani ni pesa na sio blahblah shida yako ni moja unaamini mno nadharia....hayo yote nimeshawahi kuyafanya na nikayaona matokeo yake kiukweli utakuwa mjinga mno uagize bidhaa mathalani nguo online kwa mtaji ambao ukiamua kwenda china unaenda vizuri tu bila wasiwasi...mimi naitwa mnachihangu nipo na ofisi mtwara mjini na Tunduru ungekuwa huku ningekualika uje uone vitu nilivyopigwa kwa mfumo huo
Miaka yangu yote ya biashara sijawahi kanyaga china na wala usa lakini biasharw ninaifanya bila kunyanyua mguu popote.

wew baki na unachoamini na sisi wa kisasa tubaki tunachoamini wala hakuna ugomvi wala mashindano..

Naamini ulipigwa kwa kukosa maarifa ya namna ya kufanya hii biashara
 
Back
Top Bottom