Songea mbona haibadiliki? Kuna tatizo gani na mmekuwa na Mawaziri toka miaka ya 1960?

Mkoa huu uko exaggerated mdomoni mwa watu yaani ujanja na umaarufu wa Kabila la Wangoni mjini huku haulingani na maendeleo ya mkoa wao, nilipata bahati ya kufika hapo June nikashangaa kukuta kamji kadogo kalikotenganishwa na barabara ya Lami kati na the only standard facility niliyoiona ni Ruhuwiko hotel /hunt club. In short Mtwara ndio leading place kwa hii mikoa ya kusini Ruvuma, Lindi na Mtwara ingawa hapavumi!
 
Bora umenena,wengine huko mikoani kwao kubovu hatari,na hakuna chochote cha maana
 
Hakuna totozi huku

Kama unataka totozi, Songea kuna uhaba na ukame sana

Sijaona mizigo wala watoto weupe huku

Wengi ni weusi sana kama Mbeya tu na wafupi wafupi sana

Jamani [emoji23][emoji23][emoji23] ndio unawapondea wifi zangu hivyo
 
Miji yote bongo ni full stress na umaskini uliokithiri, miji mingi ilikuwa mizuri miaka 70 iliyopita wakati wa mkoloni, CCM ni disaster na miaka 70 ijayo mambo yatakuwa worse kuliko sasa
 
Unaamuaje sasa?

Kwani tumekula chenu??

Mbona mnapenda kutufuatilia??


Mshafika mkoa wa mara??
Ninaamua kuja kuoa Namtumbo, ndio hata sasa niko Mara hapa Mugumu,karibu tule kichuri
 
Jamani [emoji23][emoji23][emoji23] ndio unawapondea wifi zangu hivyo
Ohooo WiFi tena, Kaka yako si atakatika kiuno sana

Mwambie awe makini na watu wa Songea na Mtwara, kiuno wanazungusha watu wa huko kama feni nasikia

Kiuno hakina spea Madukani awe makini
 
Haja kosea tatizo huna exposure

Mtwara kule wanasema Ntwara......
 
Mkuu wewe ndio Umekosea sasa
Watu wa Mtwara hakuna M huko bali kuna N

Mtu wanasema ntu

Mwanamke wanasema Mwananke

Jamaa ni mzoefu anawafahamu
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Nimecheka, yeye hana exposure alafu anakosoa
 
Lamory la chazl na yapenda mtini kula Sana Bata...karib Lindi Paris ama biashara kesho nichek
 
Lamory la chazl na yapenda mtini kula Sana Bata...karib Lindi Paris ama biashara kesho nichek
Yapenda Mtini naona ndio symbol ya Bar pale mjini maeneo ya deluxe

Jamaa naona amesimamia show kitambo kama muhindi hivi na Biashara zao, Kuna miaka walitaka kupabomoa hapo watu wa manispaa

Yule Jamaa kiziwi mtoto wa mmliki bado ndio anaiendesha?
 
Kagera na ruvuma Bora ruvuma mkuu. Kagera Ni masikini miaka yote pamoja na kuwa na wasomi wengi lakini washamba Sana wameshindwa kuendelea kwao.
Ni mpango wa CCM Kagera ikanyagiwe chini isiendelee. Tangu uhuru mpaka leo ni kahawa ya Kagera tu inayoitwa magendo pale mkulima anapouza kwa wafanyabiashara wa Uganda wenye bei nzuri. Sehemu nyingine magendo ni bidhaa zinazoingizwa nchini kinyemela.
Tetemeko likapiga, wahisani wakatoa mamilioni kufidia wahanga CCM ikawachinjia baharini. Mambo ni mengi ila kila mtu sasa hivi anafurahi kusikia Kagera ni masikini.
 
Kagera na ruvuma Bora ruvuma mkuu. Kagera Ni masikini miaka yote pamoja na kuwa na wasomi wengi lakini washamba Sana wameshindwa kuendelea kwao.
Sasa ushasema wasomi..halafu wasomi hao washamba[emoji23]
Mbona unajichanganya mwenyew...

Mtu aliyesoma si atakuwa anajua vitu vingi kuliko hasiye...sasa atakuwaje mshamba..

Una chuki zako wala huna hoja
 
Utajiri wa mikoa kwa calculation za NBS unatokana na idadi ya watu.

Mfano: Kama Darasa Lina wanafunzi 100 lakini 20 wakapata maksi za just na 15 wakapata sifuri. Na Darasa jingine lenyewe wanafunzi 10 na wote wakapata maksi za wastani bila sifuri.

Hili lenye wanafunzi wachache litakuwa JUU zaidi na litaonekana ni Bora.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…