Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unamaanisha hukumu za hivi umezisikia Tanzania tu?Mahakama zetu ni za kipuuzi sana ,sasa mtu ana 40+ halafu unampiga miaka 200 , are they serious?
Sheria haiangalii miaka yako mkuu. Hata kama una miaka 100 unaweza kupigwa mvua 80 nyingine kulingana na kosa ulilotenda.
Na kuna wakati unaweza kusikia mtu kafungwa vifungo viwili au vitatu vya maisha. Ndiyo sheria hiyo na siyo upuuzi wa mahakama!
Unamaanisha hukumu za hivi umezisikia Tanzania tu?
Siku hizi ukitaka likes wewe iseme vibaya serikali kadri unavyotumia maneno mabovu ndivyo likes zinazidi.
Kila kosa na miaka yake lakini uhalisia atatumikia makosa yote kwa wakati mmoja.Sasa kuna binada anayefikisha miaka 200?.
si Bora angemwambia nakufunga kifungo cha maisha
Kila kosa na miaka yake lakini uhalisia atatumikia makosa yote kwa wakati mmoja.
Huyo kifungo chake ni miaka minne na ukitoa 1/4 inabaki mitatu.
Wanaotunga sheria ndiyo haohao wezi, hawawezi kutunga sheria za kujiumizaUkiangalia miaka hiyo inatisha. Ila ukiwaza kisheria kuwa inakwenda concurrently, haifiki hata kumi so to speak. Watu kama hawa ukitaka kuwakomesha tunga sheria isiyowataka kulipa faini hata shilingi au vifungo viende sambamba na faini. Vinginevyo wataendelea na michezo yao.
Parole ni1/3 mkuuHuyo kifungo chake ni miaka minne na ukitoa 1/4 inabaki mitatu.
Kesi imeisha kwa mtuhumiwa kukiri makosa, watuhumiwa/washtakiwa wengi huwa hawakiri makosa.Kesi imefinguliwa Leo tarehe 7/05/2021 na hukumu imetolewa leo leo. Mashauri yote mahakamani yakiendeshwa hivi malalamiko yatapungua Sana.
kwahyo home apasahau
May 7, 2021 by Global Publishers
![]()
Leo tarehe 07/05/2021 Mahakama ya wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe imemhukumu ndugu SEMENI GWEWA MSWIMA (Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mlowo) Kifungo cha miaka 200 au kulipa faini ya Tshs.52,000,000/= pamoja na kurejesha kiasi cha Tshs.30,850,000/= alichoiibia Halmashauri wilaya ya Mbozi.
Kesi hiyo ambayo ni Kesi ya uhujumu Uchumi Na.01/2021 ilifunguliwa leo na TAKUKURU Mkoa wa Songwe mbele ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Mbozi Mh.Vitalis Changwe ambapo Mshtakiwa alikuwa akikabiliwa na makosa sitini(60) ambapo ndani yake kuna makosa ya kutumia nyaraka za uwongo kinyume na vifungu vya 342 na 337 vya Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ya mwaka 2019 na makosa ya wizi kwa Mtumishi wa Umma kinyume na vifungu vya 258(1) na 270 vya Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 ya Mwaka 2019.Akisomewa Mashtaka hayo,
![]()
Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU Mkoa wa Songwe Bwn Emanuel Ndembeka akisaidiana na Bi.Simona Mapunda,alieleza mahakamani hapo kwamba Mshtakiwa kwa tarehe tofauti tofauti kati ya tarehe 04/07/2019 hadi tarehe 08/05/2020 kwa kutumia hati za malipo na hundi zilizoghushiwa aliweza kutoa na kuiba fedha jumla ya Tshs.30,850,000/= toka katika akaunti Na.61210014674 ambazo ni mali ya Halmshauri ya wilaya ya Mbozi.
![]()
Mshtakiwa alikiri makosa yote 60 yaliyokuwa yakimkabili.
Akitoa hukumu hiyo,Hakimu Changwe alimwamuru Mshtakiwa kulipa faini ya Tshs.800,000/= au kwenda jela miaka mitatu(3) kwa kila kosa la kuwasilisha nyaraka za uwongo,ambapo kulikuwa na jumla ya makosa arobaini(40).
![]()
Hakimu huyo pia alimwamuru Mshtakiwa alipe faini ya Tshs.1,000,000/= au kwend jela miaka minne(4) kwa kila kosa la wizi kwa Mtumishi wa Umma ,ambapo kulikuwa na jumla ya makosa ishirini(20).Pamoja na kulipa faini hizo,Mahakama ilimwamuru Mshtakiwa ajereshe katika halmashauri husika fedha alizoiba kiasi cha Tshs.30,850,000/=.Mshtakiwa alishindwa kulipa fedha.
Mi pia sijakupata mkuu....ebu fafanua kitaalamu...Parole ni1/3 mkuu
chawa Kama wote uyu mupe uyu muruke😂Ila naamini hakuwahi kupiga huo mshindo kwa mkupuo.....Ingawa si"support" uhalifu ila cha ajabu ukute hizo hela jamaa aliziteketezea zote Bar
Asante kwa elimu nzuriHuyo jamaa amefungwa miaka minne tu.
Ndio maana ameona isiwe tabu akae mahabusu miaka kibao Wakati hukumu ya juu hapo ni miaka 4.
Ikumbukwe kuwa vifungo vyote vinaenda Kwa pamoja hivyo lile kosa lenye miaka mingi ndio hukumu yake halisi.
Hata ukiambiwa Una makosa 200 na kila kosa ni miaka 5=miaka1000 kimsingi hapo naenda jela miaka chini ya mitano.
Mramba na Yona walikaa gerezani kwa muda; wamekuja kutolewa kuwekwa kifungo cha nje enzi ya Jiwe!!kina B Mramba walifungwa kifungo cha nje...
Ukiangalia miaka hiyo inatisha. Ila ukiwaza kisheria kuwa inakwenda concurrently, haifiki hata kumi so to speak. Watu kama hawa ukitaka kuwakomesha tunga sheria isiyowataka kulipa faini hata shilingi au vifungo viende sambamba na faini. Vinginevyo wataendelea na michezo yao.
Ni miaka saba mkuu