Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

Alisaliti kivipi? Usaliti ni nini? Kuwa na maoni tofauti ni usaliti. Kupenda mtu asiyependwa na wenye madaraka ni usaliti? Mtu aliyetoka hadharani kulikosoa chama chake kwa kukiuka kanuni za uchaguzi, je ni msaliti? Yupi bora, msaliti au mnafiki?
Tungeuliza sababu za kuwafukuza kama umefatilia ni kwamba walichunguza mienendo yao inawezekana hao waliotolewa walikua taxi bubu mchana CCM usiku kwengine!.
Usaliti upo kwa kila chama unabisha na hilo?
 
Safi sana. Wale waliokuwa wanamtetea Nchimbi waje hapa
1469823731619-jpg.373162
 
Bora CCM wameamua kuvua unafiki ....wapinzani wanaibeza CCM inayojitengeneza ...watatutawala hadi labda wajukuu zetu wajielewe lakini si upinzani huu uliojaa ujanja ujanja ....
hivi upinzani uki lost ni nani anaye umia ni mbowe au??? Shida sio upinzani shida ni watanzania wengi bado ni wajinga
 
Mbowe kama namuona vile akipiga jalamba kwa ajili ya usajili wa ghafla wa dirisha dogo.
Kwani Mtanzania akifukuzwa CCM kwa kuipenda Chadema akienda huko ni makapi kwa Chadema? The same kama akifukuzwa Chadema kwa mapenzi na ccm huko ccm ni makapi?
Tujiulize kina Juliana Shonza na Mtela waliofukuzwa Chadema mbona huko ccm mumewapa Ubunge na u DAS? Jee kwenu ni makapi? Kwanza mmezoea kumuita Lowassa eti ni makapi ya ccm wakati aliondoka mwenyewe huku NEC wakiwa wanaimba "tunaimani na Lowassa"?
Ngoja Sofia aje na kina mama kibao ambao walikosa wa kumtanguliza mbele safari ya kuitosa ccm isiyo wajali
 
aje chadema...awe kamanda bila kozi
Kama uchafu huo umekaa nao miaka arobaini huoni ulisha haribu kila kitu hata leo ukiutoa vileunadhani ni visafi navyo vimabakia vinanuka uvundo. Sasa bhasi kabla haujaingia sehemu safi huku utachujwa kwanza kisha usnaingia ukiwa safi.
 
Nilidhani wataka kuleta u "call me jay" maana huyu mtu file lake nalifahamu kinaga ubaga hasa ukikaribia maeneo ya pale karibia na IFM .

Ila ulivyosalimu amri ikabifi Yale madude yangu ya Intercontinental Ballistic Missile (IBM ) niliyarudishe kama nungu nungu afanyavyo.

Huyu mama sidhani kama atayumba sana, tatizo ni kwa Sophia Simba na mzee Kimbisa.

Si unafahamu masuala ya pensheni kama hukujiweka sawa basi itakula kwao.

Inasikitisha sana.
 
Siasa za visasi hivi.. Iringa bwana yule alinyimwa wadhamini..
 
Tungeuliza sababu za kuwafukuza kama umefatilia ni kwamba walichunguza mienendo yao inawezekana hao waliotolewa walikua taxi bubu mchana CCM usiku kwengine!.
Usaliti upo kwa kila chama unabisha na hilo?

Huwezi kuniambia myu aliyepinga maamuzi ya chama mbele ya vyombo vya habari kama Sofia Simba ni msaliti nikakuamini! Tayari najua sisi nchi hizi kupingana na viongozi ni dhambi kubwa.
 
Sio CHADEMA wala Sio CCM, tena afadhali huku CCM kwa sasa wanafagia fagia hakuna anaeona vizuri hasa watu wa chini wapo tu tunakoenda ndio huko huko, utamshangaa mtu wa CHADEMA pove linamtoka utadhani kwake hakuna udikteta, tena huyo Tundu Lizu nani wa kupinga wazo lake, semeni ukweli? Na Mbowe nani wa kumkosoa kwa sasa? Si umeona waliojaribu yaliyowakuta, na najua hamna uchaguzi wa Mwenyekiti tena dah...

Siasa za Tanzania ni bora wale wasio na vyama lakini hawa mashabiki uchwara ambao hata katiba za vyama vyao hawazijui ni shida... wako kusubiri nani wa kumtukana na kuongea USHILAWADU badala ya kujadili hoja za msingi kwa maendeleo ya taifa hili..

CCM acha ifagie, wakimaliza tunasubiri kama CHADEMA na nyinyi mtafagia au hayo makombo waliotupa chini CCM ndio mtaokota kama kawaida yenu?

Maana hamtaki kujibidiisha na nyinyi mkae mezani mle chakula fresh sijaona hata program za kuelemisha vijana wenu kuhusu maono ya CHADEMA kila siku viongozi wenu kwenye makorido kulinda nafasi zao kwa kutafuta kashfa ya mahakamani au ya kuuchafua utawala, huku mkipata washabiki badala ya wanachama watakao kijenga chama.
Chadema walisha fanya haya zamaaaaani,sasa hivi chama kusafi ni kupiga kazi ya kukiimarisha kwa kushika dola.
Huyo lowasa mnae mnanga kilasiku,mmeshondwa kumshtaki,kwa maana ingine ni msafi.
 
Ndani ya ccm kama ni uchafu basi hautaisha maana wote walioko huko bado mfumo ni uleule leo hii hata ukisema aje malaika ndani ya ccm utajikuta hawezi tena kufanya kazi inavyopaswa maana atafinywa kila kona na asipate majibu.
 
Back
Top Bottom