Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

mzee visasi ameanza yake...mpaka 2020 atakuwa amebaki yeye mwenyewe kwenye chama. ukiona mtu hataki kukosolewa au mawazo mbadala ujue kuna udhaifu fulani anajaribu kuuficha.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
teh teh teh teh ila nyie aliwakomesha sana.. Pesa za majanga tutoe sie matumizi apange yeye..

Ametukomeshaaa, ametukomeshaaa sana.
Hahahahaha jehuri yote ya nshomile kwishaaaa.
Sijui pesa zile kapeleka wapi aiseee.
 
Ccm ina haki kumwondoa au kumkubali mwanachama kupitia vikao n.k. lakini tuzingatie sana watanzania wote bila upinzani changamoto itakufa. Hata ktk biashara unahitaji upinzani ili uboreke uwe na nidhamu pia. Kwa nchi yetu kwa sasa upinzani upo dhaifu sana unachangiwa na mambo mengi. Illa ni muhimu na ni jambo zuri kwa Ccm kwa na Taifa kwa ujumla wake kuwepo na upinzani wenye nguvu ili Taifa lisonge mbele kwakutambua ufisadi ubadhirifu n.k. na pia ujue kipimo cha utawala wako. Lakini kwa upinzani huu sio jambo zuri kabisa kwa mustakbali wa nchi hii kisiasa na kiuchumi. Bado tu wachanga ktk demokrasia tunahitaji kupiga hatua. Hata kama Ccm inatawala uwepo upinzani wenye nguvu kiuchumi na katika sifa za viongozi wao pia sio kwa hali hii ya sasa ya upinzani wapo dhaifu. Ni maoni yangu tu.
Upinzani upo dhaifu kivip ndugu yangu
 
Hivi nyie chadema si ndio mliomfukuza Zitto kwa tuhuma za kuwa 'msaliti?'

Kwa nini inawauma wenzenu wanapowafukuza watu kwa tuhuma ile ile ya 'usaliti?'

Kama wanaona wameonewa wataenda mahakamani kama alivyofanya Zito na hukumu ikitoka aliyeahinda ameahinda.

Jengeni chama chenu kwa kuitisha uchaguzi wa mwenyekiti maana naona amekuwa dikteta mwenyekiti wa kudumu yupo tu miaka nenda rudi.
 
Ikiwa chama kimeamua kukufukuza na unataka kuendelea kuwa ndani ya chama huku ukishikilia nafasi yako\zako, mfate msajiri wa vyama ili akurudishe kwenye chama na undelee kushika nafasi zako kama alivofanya kwa Lipumba.

Sofia Simba usipaniki, fata huo utaratibu, ni rahisi sana.

Chadema andaeni press conference kuwapokea wote waliogukuzwa. Msisahau DW
 
Ikiwa chama kimeamua kukufukuza na unataka kuendelea kuwa ndani ya chama huku ukishikilia nafasi yako\zako, mfate msajiri wa vyama ili akurudishe kwenye chama na undelee kushika nafasi zako kama alivofanya kwa Lipumba.

Sofia Simba usipaniki, fata huo utaratibu, ni rahisi sana.

Chadema andaeni press conference kuwapokea wote waliogukuzwa. Msisahau DW
 
Sio CHADEMA wala Sio CCM, tena afadhali huku CCM kwa sasa wanafagia fagia hakuna anaeona vizuri hasa watu wa chini wapo tu tunakoenda ndio huko huko, utamshangaa mtu wa CHADEMA pove linamtoka utadhani kwake hakuna udikteta, tena huyo Tundu Lizu nani wa kupinga wazo lake, semeni ukweli? Na Mbowe nani wa kumkosoa kwa sasa? Si umeona waliojaribu yaliyowakuta, na najua hamna uchaguzi wa Mwenyekiti tena dah...

Siasa za Tanzania ni bora wale wasio na vyama lakini hawa mashabiki uchwara ambao hata katiba za vyama vyao hawazijui ni shida... wako kusubiri nani wa kumtukana na kuongea USHILAWADU badala ya kujadili hoja za msingi kwa maendeleo ya taifa hili..

CCM acha ifagie, wakimaliza tunasubiri kama CHADEMA na nyinyi mtafagia au hayo makombo waliotupa chini CCM ndio mtaokota kama kawaida yenu?

Maana hamtaki kujibidiisha na nyinyi mkae mezani mle chakula fresh sijaona hata program za kuelemisha vijana wenu kuhusu maono ya CHADEMA kila siku viongozi wenu kwenye makorido kulinda nafasi zao kwa kutafuta kashfa ya mahakamani au ya kuuchafua utawala, huku mkipata washabiki badala ya wanachama watakao kijenga chama.
umenena vyema.
 
Kesi ya Sophia Simba sawa na ya Zito Kabwe wote wametimuliwa kwenye vyama vyao hawajajiuzulu kama Lipumba.
Kesi ya Lipumba inakuwa sawa na Lowassa akitaka rudi CCM wamkatae labda!..
Msajili anaingiaje hapa kwani Zito Msajili alimsaidiaje alipotimuliwa?..Tupunguze mihemko!..

Lipumba alipoleta vurugu kwenye kikao cha mkutano mkuu alifukuzwa na kuvuliwa uanachama
 
Mkuu kwa akili ya kawaida mtu aliyejiuzulu mwenyewe kwa matakwa yake na ambaye amefukuzwa ni nani mwenye haki angalau kidogo
Kujibu swali ni kwamba aliyefukuzwa ana haki!..swali langu Msajili amsaidiaje SS wakati kwa ZZK mlishabikia aondoke tuu alipotimuliwa!..
Yaliyomtokea Sophia Simba reference yake ni Zitto Kabwe maana na yeye kesi yake usaliti ilikua!...
 
1d6bb09df98228f1e8166e9fcc51ab57.jpg




Nimeiona kwny JF twitter:

=========
UPDATES:

Waliofukuzwa Uanachama wa CCM kuanzia leo:
1. Sophia Simba
2. Ramadhan Madabida
3. Mwenyekiti wa Mkoa wa Iringa
4. Mwenyekiti wa Mkoa wa Mara na
5. Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga



View attachment 479745
View attachment 479746
View attachment 479747
View attachment 479748
View attachment 479749

=====
KWA UFUPI:

Machi 11, 2017 - Dodoma

Habari kutoka Makao Makuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Dodoma ambapo Mkutano Mkuu unaendelea ni kwamba, baadhi ya wananchama wa CCM wamevuliwa uanachama huku wengine wakipewa onyo kali kwa sababu mbalimbali, kubwa ikiwa ni usaliti katika uchaguzi mkuu mwaka 2015.

Miongoni wa waliofukuzwa uanachama ni pamoja na mwanachama mkongwe na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Sophia Simba huku Adam Kimbisa akisamehewa na Emmanuel Nchimbi akipewa onyo kali. Onyo kali alilopewa Nchimbi ina maana kuwa hatoruhusiwa kugombea nafasi yoyote kwa miaka minne.

Kufuatia maamuzi hayo, Sophia Simba amepoteza rasmi nafasi yake ya Ubunge wa Viti maalumu na Uenyekiti wa UWT kwani nafasi hizo zinahitaji mtu ambaye ni mwanachama wa chama aweze kuzishika. Hivyo, CCM italazimika kupeleka jina jingine Tume ya Uchaguzi kuteua mbunge wa kuziba nafasi ya Sophia, huku nafasi yake ya Uenyekiti UWT ikisubiri uchaguzi baadae mwaka huu.

Wengine waliovuliwa uanachama ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni Madenge, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala, Assa Simba, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Christopher Sanya, Mwenyekiti Mkoa wa Shinyanga Ernest Kwirasa, Mwenyekiti wa Mkoa wa Iringa, Nesta Msabatavangu, Mjumbe wa Halamshauri Kuu (NEC) ya CCM, Ali Sumaye, Mjumbe wa NEC Arumeru, Mathias Manga.

Pia, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Longido, Leizer amefukuzwa uanachama pamoja na Mwenyekiti wa CCM Arusha Mjini, Saileli Mollel, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo, Omary Awadhi, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Muleba, Mwenyekiti wa CCM Babati, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Bunda, Mjumbe wa NEC Gureta.

Waliopewa onyo kali kwa makosa mbalimbali ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini, Ahmed Kiponza ambaye amepewa onyo kali na kuondolewa madarakani, Mjumbe wa NEC Mkoa wa Singida, Hassa Mzaha, Mwenyekiti wa UWT Gezabulu, Mjumbe wa NEC Kilwa, Ali Mchumo na Mjumbe wa NEC Tunduru, Cheif Kalolo ambaye amevuliwa ujumbe huo na kupewa onyo kali.

View attachment 479785
View attachment 479786
View attachment 479783
View attachment 479784

Ni vizuri.Tunataka CCM mpya yenye nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi.CCM ambayo uwezo wa mtu kiuongozi ndicho kitakachokuwa kigezo kikubwa, sio fedha. Mageuzi CCM ni lazima,vinginevyo wananchi hawatatuelewa.
 
mzee visasi ameanza yake...mpaka 2020 atakuwa amebaki yeye mwenyewe kwenye chama. ukiona mtu hataki kukosolewa au mawazo mbadala ujue kuna udhaifu fulani anajaribu kuuficha.
Ebu mkosoe muuza ngada, kama hujaitwa msaliti na kufukuzwa kwenye chama
 
Lipumba alipoleta vurugu kwenye kikao cha mkutano mkuu alifukuzwa na kuvuliwa uanachama
CUF wamegawanyika kwenye kesi ya Lipumba kuna wanaomkubali na wanaomkataa, je Zito kuna aliejitokeza pinga maamuzi yalipotolewa?
Narudia kesi ya Sophia Simba sio sawa na ya Lipumba ipo sawa na ya Zito Kabwe!..Msajili hana maamuzi labda mahakama waende!..
 
Ikiwa chama kimeamua kukufukuza na unataka kuendelea kuwa ndani ya chama huku ukishikilia nafasi yako\zako, mfate msajiri wa vyama ili akurudishe kwenye chama na undelee kushika nafasi zako kama alivofanya kwa Lipumba.

Sofia Simba usipaniki, fata huo utaratibu, ni rahisi sana.
Hii weka mbali na ccm. special menu for opposition side only
 
Kujibu swali ni kwamba aliyefukuzwa ana haki!..swali langu Msajili amsaidiaje SS wakati kwa ZZK mlishabikia aondoke tuu alipotimuliwa!..
Yaliyomtokea Sophia Simba reference yake ni Zitto Kabwe maana na yeye kesi yake usaliti ilikua!...
Ninachojua mimi ukisha fukuzwa na chama ama kujiuzulu katika chama hamna mwenye mamlaka tena ya kukurudisha tofauti na chama
 
Ebu mkosoe muuza ngada, kama hujaitwa msaliti na kufukuzwa kwenye chama
mimi itabidi tu nikae kimya...kama wanachama wenzangu wanafukuzwa ovyo hivi mimi nitaponea wapi? tatizo mwenyekiti wetu hashauriki na wala hapingiki. kuwafukuza wanachama wenye nguvu kama sofia simba kutakipasua chama chetu.
 
Back
Top Bottom