babumapunda
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 4,643
- 3,301
namba 2 ulbam ilikuwa inaitwa ugali na ilizinduliwa diamond jubilee
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
plus sitaki demuNachokumbuka ni Msitu wa vina A.K.A Sir Nature alivokua anamahusiano na Queen wa Bongo Movie enzi izo Sinta, bifu lao mpaka songii la Inaniuma sana daah Old is Gold
alikuaga na ngoma yake moja hivi maarufu imenitoka....alikua anaimba bila haraka. aliitoleaga na video enzi hizo channel 5 ilikua inakamata chatimi namkumbuka snoopy lee tu na yale ma`afro yake!
silent Inn ilikua bado.....?DAR YA KIPINDI KILE MKUU ILIKUWA NI DAR KWELI KWELI
MIMI NILIANZA KUPANGA CHUMBA KODI NALIPA ELFU 2,
ASUBUHI CHAI ILIKUWA INAUZWA SH.50 NA VITUMBUA SH.10.
2.MCHANA UBWABWA MAHARAGE BEI 500 UKITAKA CHIPS YAI 700 NA SODA 200._
3.USIKU HIVO HIVO KAA MCHANA
4.SIKU ZA WEEKEND CLUB ILIKUWA BILICANAS , MAMBO CLUB, FM CLUB HII ILIKUWA KINONDONI KIINGILIO ILIKUWA 500 NA UKIINGIA BIA ILIKUWA 500 TENA ILIKUWA NI SAFALI LAKINI KULIKUWA NA BIA KAMA BIGWA, THE KICK BEI MPAKA 300.
HAYA NDO MAISHA DAR MIAKA YA TISINI KUJA ELFU MBILI
hapo ongezea na kama unataka demu wa jay mo zilikua zinaenda sambamba hizoMimi na madem dam dam ya mwana FA , pembeni ilikuepo nyimbo ya kamanda ya daz nundaz, baadae umbo namba nane ya daz baba
one of the best bongo fleva album...nakumbuka nilikuaga natoka likizo miaka hiyo mambo ya boarding school...kufika shy town mtu mzima mmoja akiwa na prado akaamua kutusogeza rock city sasa njia nzima kaweka hiyo cassette ya aka Mimi inaisha inajirudia...akasema naona siku hizi vijana mnaimba nyimbo za akili na ujumbe kumbe hizo rap rap zenu ukisiklza vizuri ni nzuri....Album Kali ya The late Albert Mangwair iliyojulikana kwa jina la a.k.a Mimi chini ya producer mkali P funk majani.
kosa la marehemu.....waliitwa mabaga fresh wazee wa soko matora mbeya townHivi wale walioimba [HASHTAG]#HAKUVAA[/HASHTAG] KONDOM ni akina nani
Uswahilini Matola na Mabaga Fresh walikua walewale amaUswahilini Matola..
ila kibongo bongo hata mrahaba hakupata. dah!Wakati bushoke ametoa album yake ya kwanza barua. Cover lake kuna shati alikuwa amevaa basi likawa fassion kkoo yakawa yanauzwa kama njugu.
na lile Goma lake la mgambo wanaruka na kukanyaga.....enzi hizo team hakuna sijui [HASHTAG]#teamkiba[/HASHTAG] [HASHTAG]#teamdai[/HASHTAG].....hapo ilikuaga East Cost vs Temeke hakuna kurembaSir Kibla Nature Kassim Kiroboto alishinda tuzo ya channel O
O Ten na nichekii....ilivuma ikasanda.Bifu ya Afande Sele na O Ten
Sio kweli waliitwa uswahilini matola na sio mabaga fresh ambao hawa walikuwa walemavu na moja ya nyimbo yao ni tunataabika;kosa la marehemu.....waliitwa mabaga fresh wazee wa soko matora mbeya town
kaka kama una hii ngoma plz nisaidie nimesha itafuta sanaGonjwa hili limezua kizazaa, mzozoo.. gumzo..gumzooo kwa mabronzo, masista du, machizi, wazazi, walimu na wanafunzi..
Mzee wa kidhaa dhaa...
Unakumbuka na suruali kubwa walizokuwa wanafavaa,ingekuwa sasaiv sidhani Kama wangekubaliKing Crazy GK kuna kikofia cha matobomatobo alikuwa anapendelea kukivaa basi nakumbuka wakati huo nipo sekondari ikageuka kuwa fasheni kwa vijana, 'kikofia cha GK'. Na pia kundi la ECT liliwashika sana vijana miaka kama ya 2002-2004, ikatokea vijana sehemu mbalimbali hasa mashuleni wakiunda vikundi na kujiita East Coast, huku wakitumia majina ya members maarufu kama GK, AY na Mwanafalsafa. Mfano ni shule yetu, kulikuwa na kikundi cha namna hiyo, East Coast baadae walikuja kufunikwa na TMK Wanaume baada ya ujio wao wa ngoma kama NYUMBANI NI NYUMBANI wakitumia style ya kucheza iliyobamba sana miaka ya 2004-2005 (Mapanga Shaaa), huku ikiwa na members maarufu kama Juma Nature, Temba, Chege, KR Mullar, Dollo, Luteni Kalama, YP & Y'DASH, Mabaga Fresh, etc. Hiyo style ya mapanga ilishika ile mbaya kwenye clubs/madisco, ikipigwa ngoma ya NYUMBANI ni NYUMBANI mademu wanakaa pembeni, tunabaki washkaji tumejipanga line tunapiga mapanga huku tukichombezwa na slogan ya (WANAUMEE.....EEEHHH).
Na kutokana na kukubalika sana kwa kundi hili ilipelekea kutumika sana kwenye kampeni za uchaguzi wa mwaka 2005 huku wakizunguka sehemu mbalimbali za nchi na mgombea wa wakati huo wa CCM Jakaya Kikwete.