figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,724
- 55,906
- Thread starter
- #11,321
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sio hulka yaoUrusi yeye hawezi Editing!?
Na vita ni editingHata US President Joe Biden bila shaka ni editing imefanyika hakwenda Ukraine yuko zake Washington ametulia tunalishwa upepo tu hapa, au siyo mwamba [emoji848][emoji849][emoji849]
Okay Kwa akili yakoUkisikia akili yenye ugirigiri iliyochanganyikana na tope ndo hii.
Basi sawa ngoja tuendelee kufuatilia editing tuone mwisho wake utakuwaje.Na vita ni editing
Barabara za supply. Hapo pekundu pako chini ya Urusi, sio rahisi barabara ikawa chi ya Ukraine. Barabara zilizopo chini ya Ukraine ni maeneo ambayo Ukraine imeyakomboa. Kumbuka haya maeneo ya Donetsk yapo chini ya Urusi tangu 2014. UKRAINE inafanya kutarudisha. Kuna sehemu walipiga kura ya kujiunga na Urusi lakini Ukriane imeyachukua. Donetsk na Luhansk Urusi ilishaweka Mizizi. Jeshini kuretreat ni jambo zuri kuliko kuzungukwa mkawekwa watu kati. Kumbuka Ukraine ina Rasilimali watu ndogo ukilinganisha na Urusi. Hadi sasa mji wa Severodonetsk ndo Ukraine walireteat tangu juni,yaani waliuachilia. Sehemu nyingine mapambano yanaendelea. Bado tunaamini kwa silaha mpya Ukraine imepata, itasonga mbele. Tujipe muda
View attachment 2527006View attachment 2527007View attachment 2527008View attachment 2527009View attachment 2527011
Your too low to urgue with me about this. Let those who knows and they make efforts to get inner informations urgue.Weka chanzo cha taarifa ndugu yangu wala, usiongee kama vile hujui kuwa na sisi tinafatilia hii viat!!
Kiukweli, Wagner hawaliwezi jeshi la Ukraine. Nadhani re-inforcements zilikuwa zimechelewa kuwafikia wapiganaji wa Ukraine ndiyo maana wagner wakaadvance. Kuna uzembe jeshi la Ukraine lilifanya kuhusiana na Bakhmut, nadhani ndiyo maana majuzi Zelensky alimtumbua waziri mmoja anayedeal na mambo ya ulinziWanajeshi wa Ukrane Bakhmut wamepelekewa magari na chopa ya kuongeza nguvu
View attachment 2526753
You nailed the point. That is the reality.Kiukweli, Wagner hawaliwezi jeshi la Ukraine. Nadhani re-inforcements zilikuwa zimechelewa kuwafikia wapiganaji wa Ukraine ndiyo maana wagner wakaadvance. Kuna uzembe jeshi la Ukraine lilifanya kuhusiana na Bakhmut, nadhani ndiyo maana majuzi Zelensky alimtumbua waziri mmoja anayedeal na mambo ya ulinzi
Ila kama re-inforcements zile nzitonzito zimeanza kupelekwa basi tutegemee Wagner kuishiwa upepo.
Sasa hivi Wagner hawana means za kusustain operation zao huko Bakhmut, kuna in-fightings kati yao na majenerali wakuu wa jeshi rasmi. Hiyo inawadhoofosha sana Wagner na kuwakatisha tamaa.
The other thing ni kwamba, pindi zile offensive weapons ambazo west amesema kumpa Ukraine zitaanza kufika, basi Ukraine itakuwa ktk position nzuri ya kukomboa maeneo
Hilo nalikubali ni point. 1. Kiongozi wa Wagner atakuwa ametathmini kile anachopata i.e. malipo ya kazi hiyo kwa mujibu wa Mkataba dhidi ya kile anachopoteza i.e. askari/wapiganaji wanaouawa au kujeruhiwa akaona "inakula kwake".1. Huenda kiongozi wa Wagner kachoka na Vita ndiyo maana kaonyesha picha hizi kwa makusudi ili wananchi wa Russia wajue na wampigie kelele Putin asitishe vita. Hii siyo bahati mbaya.
2. Huenda pia imemgusa sana kwa kuwa ni wanajeshi wa Wagner group. Muda utaongea tu.
napenda kusikia hiviAngalia Ukraine ilivyo angamiza Kutuo cha mfumo wa EW cha Urusi. (ground-based, electronic warfare (EW) system.
View attachment 2523680
Mzigo ukifika wote lazima amsaliti Putin. Dalili zote zinaanza kuonekana. Anapingana na Majenerali wa Russia wakati yeye ni kibarua tu. Wanakoelekea watamuua kiongozi wa Wagner. Wanaweza kutoa siri alipo kwa kutoa cordinates kwa Ukraine ili HIMARS afanye yake.Hilo nalikubali ni point. 1. Kiongozi wa Wagner atakuwa ametathmini kile anachopata i.e. malipo ya kazi hiyo kwa mujibu wa Mkataba dhidi ya kile anachopoteza i.e. askari/wapiganaji wanaouawa au kujeruhiwa akaona "inakula kwake".
2. Kiongozi wa vita anapofikia mahali analalamika kuhusu uwezeshwaji ki-silaha halafu pia anatoa siri ya vifo na kuweka idadi na picha kuthibitisha madai yake:-
(a) Anajenga hoja ya kuvunja Mkataba kwamba Mkataba hauheshimiki/hauzingatiwi na hauna maslahi tena kwake.
(b) Anawavunja moyo wapiganaji wake kuhusu vita hiyo na kutoa ushawishi kwao ili wamuunge mkono wasimjengee hoja atakapovunja Mkataba na kushindwa kuwapa malipo yao wanayostahili lakini wamkubalie kwamba atawapeleka kupigana maeneo mengine duniani ambako kuna maslahi zaidi.
(c) Anajenga hoja ya kumwangushia jumba bovu Putin mbele ya mataifa duniani ambapo Putin ambaye awali alionekana mbabe na mwenye kujiweza sana lakini kwa sasa hana mwelekeo unaoeleweka i.e.Majigambo mengi lakini wkati huo-huo huku anaomba-omba misaada.
(d) Ikumbukwe kwamba kundi la Wagner kutokana na walichokifanya dhidi ya raia na miundombinu ya kiraia nchini Ukraine kundi hilo sasa limepewa hadhi ya kundi la kigaidi. Kwa maana hiyo, kiongozi wake (Prigozhin) atakuwa ni mwenye kutafutwa akamatwe kama ilivyokuwa kwa Osama n.k. Hilo limemkuta baada ya yy kujihusisha na vita Ukraine i.e. Kujihusisha kwake na Vita Ukraine kumegeuka kuwa balaa kwake. Sasa anataka aachane na Vita hiyo, ajisafishe mbele ya Mataifa na aweze kuondolewa kwenye list ya "Wanted dead or alive"
Mkuu, naomba nikuhakikishie, njia kuu ya Izyum kwenda Bakhmut inashikiliwa na Ukraine. Hata Lysychans'k ikikamatwa na Urusi sio njia kuu. Angalia hapa Izyum, Lysychans'k na Bakhmut. Naomba nikuondos wasiwasi kwani Majeruhi wanapelekwa Izyum, vyakula na Silaha bado zinafaka Bakhmut. Hata juzi nilipost picha za Magari na ndege wakienda kuongeza nguvu Bakhmut1. Nakubaliana na wewe kwamba Russia kabla ya mwezi June 2022 wakati hatujapata HIMARS njia kuu ya kutoka Bakhmut kuelekea Lysychans'k ilikuwa under Russia control. Lakini Ukraine ikaikomboa sehemu kubwa wakati HIMARS anatamba na maeneo yafuatayo Ukraine ikafanikiwa kuyakomboa kuanzia July - September 2022 na hatimae njia kuu hiyo ikawa mikononi mwa Ukraine. Maeneo yaliyokombolewa na Ukraine upande wa kaskazini mashariki kuelekea kusini mashariki mwa Bakhmut ni yafuatayo; Verkhn'okam'yanka, Spirne, Berestove, Bilohorivka, Yakovlivka, Vasylivka, Soledar, Nova Kam'yanka, Bakhmuts'ke, Pokrovs'ke, Vesela Dolyna, Opytne, Ivanhrad, Klishchiivka, Odradivka, Mykolaivka Druha, Kurdyumivka na Ozarianivka. Sasa hivi maeneo yote hayo yamerudi tena kuwa chini ya Russia/Wagner ndiyo maana njia kuu hiyo iko under control ya Russia.
2. Umetuonyesha vizuri sana kwenye ramani njia kuu inayotoka Bakhmut kuelekea Izyum via Slovyansk. Sasa kama Wagner/Russia wameshaidhibiti kama ulivyoonyesha kwenye red kuanzia baadhi ya mitaa ya Bakhmut kuelekea pryvillya na Min'kivka utasemaje kuwa supply logistic route kuingia Bakhmut haijaathirika?. Utapelekaje vifaa frontline ya wanajeshi walio katikati ya mji.
Let us accept the reality even if it is painful to us. But something has to be done by Ukrainian troops to rescue the situation.
1. Narudia tena na tena kuwa the only route to Izyum from Bakhmut is via Kostyantynivka, Kramatorsk and Slovyansk.Mkuu, naomba nikuhakikishie, njia kuu ya Izyum kwenda Bakhmut inashikiliwa na Ukraine. Hata Lysychans'k ikikamatwa na Urusi sio njia kuu. Angalia hapa Izyum, Lysychans'k na Bakhmut. Naomba nikuondos wasiwasi kwani Majeruhi wanapelekwa Izyum, vyakula na Silaha bado zinafaka Bakhmut. Hata juzi nilipost picha za Magari na ndege wakienda kuongeza nguvu Bakhmut
View attachment 2527757
Mamluki siku zote hupigana kwa ajili ya maslahi tu hawana adui wa muda wote. Sasa usishangae wakapigana upande wa Ukraine watakapogundua Putin anaelekea kushindwa vita, hawalipwi vizuri, hawana silaha za kutosha.Hilo nalikubali ni point. 1. Kiongozi wa Wagner atakuwa ametathmini kile anachopata i.e. malipo ya kazi hiyo kwa mujibu wa Mkataba dhidi ya kile anachopoteza i.e. askari/wapiganaji wanaouawa au kujeruhiwa akaona "inakula kwake".
2. Kiongozi wa vita anapofikia mahali analalamika kuhusu uwezeshwaji ki-silaha halafu pia anatoa siri ya vifo na kuweka idadi na picha kuthibitisha madai yake:-
(a) Anajenga hoja ya kuvunja Mkataba kwamba Mkataba hauheshimiki/hauzingatiwi na hauna maslahi tena kwake.
(b) Anawavunja moyo wapiganaji wake kuhusu vita hiyo na kutoa ushawishi kwao ili wamuunge mkono wasimjengee hoja atakapovunja Mkataba na kushindwa kuwapa malipo yao wanayostahili lakini wamkubalie kwamba atawapeleka kupigana maeneo mengine duniani ambako kuna maslahi zaidi.
(c) Anajenga hoja ya kumwangushia jumba bovu Putin mbele ya mataifa duniani ambapo Putin ambaye awali alionekana mbabe na mwenye kujiweza sana lakini kwa sasa hana mwelekeo unaoeleweka i.e.Majigambo mengi lakini wkati huo-huo huku anaomba-omba misaada.
(d) Ikumbukwe kwamba kundi la Wagner kutokana na walichokifanya dhidi ya raia na miundombinu ya kiraia nchini Ukraine kundi hilo sasa limepewa hadhi ya kundi la kigaidi. Kwa maana hiyo, kiongozi wake (Prigozhin) atakuwa ni mwenye kutafutwa akamatwe kama ilivyokuwa kwa Osama n.k. Hilo limemkuta baada ya yy kujihusisha na vita Ukraine i.e. Kujihusisha kwake na Vita Ukraine kumegeuka kuwa balaa kwake. Sasa anataka aachane na Vita hiyo, ajisafishe mbele ya Mataifa na aweze kuondolewa kwenye list ya "Wanted dead or alive"
Sawa, ila soma na hapa. Ili usije sema ni maneno yangu au mimi nimepotosha1. Narudia tena na tena kuwa the only route to Izyum from Bakhmut is via Kostyantynivka, Kramatorsk and Slovyansk.
2. Hakuna sehemu niliyosema kuwa njia kuu ya kwenda Izyum iko under control ya Russia. Nilichosema ni kuwa kipande cha njia kuu kutoka Bakhmut kuelekea Slovyansk kiko chini ya Wagner/Russia. Nikaongeza kwa kusema kutoka Bakhmut hadi Pryvillya na Min'kivka kipande hicho ndo kiko chini ya Wagner/Russia.
3. Nikaongeza kuwa njia kuu iliyo salama ni kutoka Bakhmut kwenda Kramatorsk via Kostyantynivka. Kutoka Kramatorsk kwenda Slovyansk hadi Izyum njia iko salama. Hiyo ndo safe route kuingia Bakhmut.
4. Tension kubwa sasa hivi kwa Bakhmut ni kuzungukwa na majeshi wa Russia. Hata msemaji wa jeshi la Ukraine alisema jana kuwa the situation at Bakhmut is difficult as Russian troops are trying to encircle Bakhmut. Akaongeza kwa kusema Russian Artillery, MLRS, Mortars, Tanks are concentrated at Bakhmut. Kwenye hili endeleeni kubisha lakini huo ndo ukweli.
5. Tatizo letu uzalendo umetuzidi tunataka kuwaaminisha watu kuwa Russia/Wagner hawaipigi Ukraine ila Russia ndo wanapigwa kitu ambacho siyo sahihi hata kidogo. Isingekuwa hivyo wangewezaje kusonga mbele all the way kutoka Nova Kam'yanka, Soledar hadi sasa wanakaribia Pryvillya. Kama hilo ndo sahihi si tungekuwa tumeshawafurusha Donetsk yote na Luhansk.
Let us accept the reality. Russia nao wanapiga siyo kwamba wanapigwa wao tu.