Aliomba mazungumzo ..Russia akasema yafanyikie Belarus... Ukraine amegoma kufanyia Belarus...anataka sehem nyingine.. deadline aliyoitoa Russia ndo imeexpire saa moja lililopita..maana yake Sasa Russia hahitaji mazungumzo tena Bali kuondoa madarakan utawala wa zelensky...
Upande wa Ukraine umependekeza mazungumzo yafanyike katika mji mmoja kati ya Warsaw, Poland; Bratislava, Slovakia; Istanbul, Uturuki; Baku, Azerbaijan ama Budapest, Hungary.
Hili jambo la kufanyia mazungumzo Belarus kama Urusi inavyotaka, linazua wasiwasi kwa Ukraine. Pia, linataka kufanana na tukio moja katika historia wakati wa mapinduzi ya Hungary ya mwaka 1956 dhidi ya USSR ama Umoja wa Kisovieti. USSR ilipeleka majeshi yake nchini Hungary kwenda kuzuia mapinduzi hayo yaliyokuwa yakiongozwa na mtu mmoja aliyefahamika kama Imre Nagy, Waziri Mkuu wa Hungary baada ya awamu ya kwanza ya mapinduzi.
Imre Nagy aliwahi kuhadaiwa kufanya mazungumzo na makubaliano ya amani na USSR jijini Moscow wakati majeshi ya USSR yalikuwa tayari yameshaweka kambi Hungary kuelekea Budapest ili kumng'oa madarakani.
Ujumbe/uwakilishi wa Hungary ulipofika Moscow kwaajili ya mazungumzo, uliwekwa kizuizini kisirisiri; wakati huohuo majeshi ya USSR yaliamriwa kuendeleza mashambulizi dhidi ya majeshi ya Hungary. Hatimaye Nagy alikimbilia ubalozi wa Yugoslavia nchini Hungary kuomba hifadhi baada ya jeshi la Hungary kuzidiwa nguvu. Hata hivyo, Imre Nagy alikamatwa baadaye na kupewa kesi ya uhaini na kisha kuuawa (execution).
Nafikiri, wasiwasi huu wa Ukraine unakuwepo kwa sababu Belarus ni mshirika wa karibu sana wa Urusi katika huu mgogoro, pia ni nchi iliyotumika kuhifadhi na kupitishia majeshi kwaajili ya kuivamia Ukraine ambapo mpaka sasa, majeshi hayo yapo.