LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Unataka Russia aanze kuua raia!? Tayari rais ya Ukraine ameanza kufuata maelekezo ya Russia. Sasa hivi lazima aende Belarus. Na sharti alilopewa namba moja ni askari wake wajisalimishe.

Hakuna mjadala hapo. Kama hataki basi Russia atatoa mkong'oto wa kweli.
Usizidishe chumvi mzee
Mwisho wa siku ni Russia ataondoka ukrain kwa aibu
 
We unaongea nini kuna nchi yenye technologia na inteligencia kama Russia?

Teknolojia na Intelejensia kweli anavyo lakini sio kwa kiwango cha kushindana na wakubwa wenzie kama USA, UK , Israeli nk..

toka kuanguka kwa USSR, nguvu ya KGB ilipungua, uwezo wa kiteknolojia ulipungua kutokana na matatizo ya kiuchumi na mabadiriko ya siasa za kidunia... USSR enzi za kudai uhuru kwa mataifa ya Africa alikuwa na ushawishi sana Africa, Uarabuni na America ya kusini... maana mataifa mengi yaliamini kwenye ujamaa....Akili ya kibepari ilivyoingia kila mahala duniani Mrusi alipoteza ushawishi na baadala yake USA na allies wake wakakaa kila mahala..

Nguvu ya intelejensia ya Russia imebaki ndani ya mipaka ya Russia, wakati nguvu ya kiintelejensi ya USA ipo mpaka kwenye mdomo wa Russia..
 
Naacho omba ni Uncle Sam aingilie kati
Hawezi!

Kwa sababu kila mtu anajua consequences zitakazotokea. Njia pekee ambayo ni salama ni Ukraine akubaliane na masharti ya Mrusi, awe neutral.
 
Hao NATO wamepleka misaada ya kijeshi ikiwemo ndege za kivita,vifaru nakadhalika kuisaidia Ukraine amewafanya nini?

Marekani naye kapeleka misaada kibao na Biden amemwambia Putin kwmba ameshamchorea mstari mwekundu asithubutu kuuvuka.

Ndo maana mzee Putin kabaki kutishia sijui nuclear utadhani anazo peke yake dunia nzima wakati hata hapo Ukraine tu wanazo achilia mbali NATO na Marekani.
Hivi alimaanisha nini kwenye mstari mwekundu
 
Katika vita yoyote majeruhi wa kwanza ni ukweli. Kutakuwa na propaganda nyingi na uzushi mwingi sana wakati huu. Na watu watayasambaza bila kupata ushahidi wake. Mwisho wa siku ni kueneza uzushi kwa faida ya pande husika. Hii vita bado mbichi, ngoja tuone!
 
VICHWA MAJI HUMU NI ASILIMIA 99%
Unashindwa kujua kuwa Russia Hatakiwi kutumia Full force, Wanajeshi haswa kwa sababu wakati wa vita unaweza kupata strong resistance kutoka kwa support anayopewa adui yako.

Pili kumbuka utazalisha maadui wapya, Nyumbani unakuachaje? Pia kwenye vita kuna vitu tunaita chambo, lazima utangulize watu wakusogeza Gurudumu kabla ya kutuma Strong one.

Hakupanga kuichakaza Ukraine kwa roho mbaya, Angeua watu wasio na hatia, Watu kutoka nchi mbalimbali wapo bado kule.

So Ukraine anatumia hiyo advantage ku promote kwamba amempiga M Russia in fact m Russia ni kama hajapigana tu

Wengi mliojaa humu kwa mfano mdogo tu, Mkienda sehemu za starehe mnatumia mpaka reserve kuwafurahisha marafiki na watu utakaokua nao siku hiyo, ukisahau kwamba kesho Familia itahitaji hizo pesa iweze kusonga.

The same Russia hajatumia Nguvu ya Vita Ya First Degree wakati Ukraine katumia First Degree na kachanganya na citizens na msaada juu.​

#BUNCH OF BOZOS
Huna lolote unalojua , aheri ukojoe ulale
 
Akili za kijamaa shida sana, Putin bado anawaza kijamaa sana...miguvu miingi akili kidogo, wenzie wamewekeza kwenye teknolojia na intelenjia...Kaanchi kama Ukraine ambako unaborder nako mpaka ukavamia na mivifaru na midege?..

Angekuwa na akili za kibeberu aka kibepari hiyo Ulaya mashariki yooote ingekuwa na umoja wao na yeye ndiye angekuwa baba lao with full power angekuwepo mpaka kule Yugoslavia, Bosnia, Albania, Moldova, Uzbeg, Tajigi kwa wanangu, nk sasa amebaki mwenyewe na ubabe mavi anatumia miguvu...
Kuna mdau mmoja kasema PUTIN ana ule usela wa 80's 😂
 
Haya mambo hayajitaji mahaba au utimu bali yanahitaji wachambuzi wa masuala ya kimataifa na jana nilibahatika kuwasikiliza na miongoni mwa waliyoyazungumza ni haya: Hakuna ambaye anayekataa kuwa Russia ni nchi yenye nguvu kijeshi. Kwenye hii vita ameingia na zana za kawaida za silaha.

Wachambuzi wanachohofia ni kuwa: kinachopiganwa sasa hivi ni urban warfare ambayo hii haiangalii nguvu za kijeshi wala teknolojia, ni vita ngumu mno. Ikiwa Urusi malengo yake ya kimkakati akiona hayatimii kwa muda aliyojiwekea itamlazimu atumie nguvu kubwa aliyokuwa nayo! ikiwa akifanya hivi itakuwa ni maafa kwa sababu itakuwa ni maafa kwa miundombinu, raia wa Ukraine na kwa wanajeshi pia na mji unageuzwa unakuwa gofu.

Tunachotakiwa ni kuomba malengo yake ya kimkakati yatimie Ukraine ijapokuwa kwa sasa sehemu kubwa ya miji ameshaiteka na amefanikiwa kuteketeza kambi na ghala za kuhifadhia silaha za Ukraine 200+ na hii imesaidia kuwapunguza Ukraine nguvu.
Ukraine naye asidharauliwe jamani, hajawashangaza tu? Russia akitumia silaha kubwa za kuifuta Ukraine isiwepo hawezi kuachwa salama pia. Raia wake watamsumbua, Dunia itamsumbua na ikiwezekana anaweza uwawa na wenzake huko huko ambao hatakubaliana nao. Hii vita dunia inamuhurumia Ukrain, na Warusi wanamuhurumia Ukraine. Ni vita vya Puttin kwa ajili ya manufaa kijeshi si kijamii.
 
Kwa jinsi watu na mataifa mengi kupiga kelele kuhusu uonevu wa Russia , naona kamavile ile kauli kanafanya kazi ." SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU"

Mungu amesikia ndio maana Putin haamini kinachotokea.
 
Mji Mkuu upi huo ambapo Russia yupo? Embu nitajie Mji Mkubwa wowote wa Ukraine ulio under Russia controls
Maletopol ulitekwa jana na Russia.

Huo mji unao sema ya kwamba umelejeshwa kwa Ukraine bado hakuna udhibitisho hata BBC wameripoti hivyo ya kwamba hakuna udhibitisho wowote unao unesha ya kwamba mji huo umerudi Miko noni mwa Ukraine.

Hivi mna tumia vigezo gani mpaka mnasema eti Urusi kashindwa na Ukraine.

Urusi huko Ukraine hapambani na vilema bali anapambana na watu wenye mafunzo na silaha kama yeye kwahiyo usitegemee mteremko.
Kwa hiyo nyinyi mlitaka Ukraine itekwe kwa siku mbili tu ? Unadhani vita ni kucheza ngoma?

Ukraine ni suala la muda tu itatekwa na Russia, anacho fanya Ukraine ana jitutumua tu kama Saddam alivyo jitutumua kwa miezi miwili na propaganda kibao lakini mwisho wa siku USA ikaiteka Iraq.
Mpaka sasa zaidi ya asilia 60 ya wanajeshi waliokuwa mpakani bado hawajaingia vitani wenda hii ni mbinu ya Russia kutuma hicho kikosi cha kwanza kama chambo ili kulipunguza nguvu jeshi la Ukraine alafu badae afanye ambushi ya nguvu kumbwa.

Usitegemee Urusi kutoa wanajeshi wake kabla ya lengo lake kutimia.

Aidha Ukraine ikubali kujiondoa kwenye mchato wa kutafuta uanacha kwenye NATO aidha itekwe.





Sent from my TECNO BB4 using JamiiForums mobile app
 
Kwa jinsi watu na mataifa mengi kupiga kelele kuhusu uonevu wa Russia , naona kamavile ile kauli kanafanya kazi ." SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU"

Mungu amesikia ndio maana Putin haamini kinachotokea.
UK imekiri kuwa imeisaidia Ukraine Silaha, Ujerumani imempatia Rockets lakini hawawezi kupeleka Troops zao kwasababu NATO wataingia na itasababisha vita kuu ya 3 ya dunia (WWIII)

Kwahiyo kwasasa Urusi haipigani na Ukraine peke yake.
 
Putin hakujiandaa na hii vita, amekurupuka tu, sidhani kama wamefanya tathmini sahihi kwenye muda na kila stage ya vita.
Sasa haya ni mawazo yako!
Wachambuzi wanasema Russia bado wanawahitaji raia wa Ukraine, ile nchi bado ipo na ni jirani yao na itabakia kuwa hivyo. Hakutakuwa na sababu ya kufanya uvamizi mkubwa kama alivyofanya Syria. Akifanya uvamizi wa namna hiyo atatengeneza adui mwengine mkubwa wa kizazi na kizazi ambaye ni jirani na ni mazingira hatari kwa usalama wa nchi ya Russia.

Kimkakati inambidi adili na wanajeshi tu baada ya amiri jeshi mkuu wa nchi ya Ukraine kukataa makubaliano waliyoyapendekeza. Na ndiyo maana akaanza na kupunguza nguvu ya jeshi la Ukraine kwa kushambulia base za kijeshi na maghala ya kuhifadhia silaha pamoja na viwanda vinavyojihusisha na utengenezaji wa silaha. Lengo no kupunguza nguvu za jeshi la Ukraine.

Operation inayofuata ndiyo hiyo ambayo anayoifanya sasa hivi na ni operation ngumu ambayo ni urban warfare. Ikiwa ni kuiondoa serikali ambayo kwake anaiona ni hatarishi. Kwa kuzuia uharibifu mkubwa wachambuzi wanasema ameingia na silaha za nyuma si za kisasa.
Binafsi toka mwanzo wa vita nilijua kuna urban warfare inakuja kwenye mitaa ya miji ya ukraine huku Urusi akiwa hana uzoefu wa vita hizi... na hili urban warfare naamini ni ushauri wa Nato kwa Ukraine kumdhoofisha Urusi maana wanajua hatakuwa na budget hiyo, muda unavyodhidi kwenda na vikwazo walivyomuwekea lazima anyong'onyee na aishiwe nguvu kabisa..
Urban warfare ni ngumu na ugumu wa hapa si kwamba Russia hana uzoefu. Ugumu wa hapa ni mnapambana kwenye makazi ya watu ambao ni raia, ambao sheria za kivita zinawalinda. Shambulio lolote dhidi yao ni uhalifu wa kivita kwa sababu umeshambulia wasiyostahiki. Na huu ni mtego kwa Russia, majeshi ya Ukraine yanajificha kwenye makazi/majengo ya makazi ya raia.
Russia akiwa anaendelea na vita Ukraine ambayo itakuwa Urban kila mahala Ukraine, Huku nako NATO wakipandikiza masceneries na askali wao kuingia na kutoka Ukraine kwa ajili ya kutrain na kutoa backup na kupeleka supply.. Ndani ya Russia kutakuwa na njaa na raia watakuwa barabarani kulalamikia ugumu wa maisha wakichochewa na mamluki ndani ya Russia...
Kuna suala hapa umelisahau. Russia lengo la hii vita ni kulinda usalama wa nchi yake. Sote tunafahamu NATO ikiwa mlangoni kwake ni hatari. Ukraine pia inakuwa kijeshi ikiwa NATO na ikijijengea na uwezo wa kutengeneza mabomu ya nyuklia hatoweza kumdhibiti. NATO wanalijua hili na wanajua kuwa Ukraine ni kete muhimu dhidi ya Russia.

Naam; Ukraine ni nchi huru ina wajibu wa kufanya maamuzi yake lakini ni hatari kufanya maamuzi yatakayo hatarisha usalama wa nchi jirani yako. Russia anachofanya ni kumdhibiti Ukraine mapema. Ikiwa Russia mkakati huu utafeli wachambuzi wanasema itamlazimu alazimishe mazingira. Nayo ni kutunisha msuli wake. Akifanya hivyo maangamivu ya Syria miji kuwa gofu yatahamia Ukraine. Na Ukraine itaumia.

Russia inacheza mahesabu hapa! ni mahesabu yanayohitaji umakini wa hali ya juu. Atakayeumia zaidi ni Ukraine ikiwa akikaza msuli.
 
Vita hii urusi alikuwa anapigana na mamluki wa NATO nasio ukraine pekee,baada yakuona EU wanapeleka vifaa na silaha ukraine ameona wanamprovoke waziwazi akaona afanye kama alivyoahidi mwanzo wakati anatoa onyo kwa NATO, raisi waukraine kila move aliyokuwa anaifanya kuanzia kugomea negotiations amidst war yalikuwa ni maagizo ya NATO,baada ya putin kutaka kutumia silaha za nuclear naona sasa NATO ndio wamesurrender kwakumambia rais waukraine akubali negotiation....maoni yangu!
Kwani hao NATO na Marekani hawana Nuclear?
 
We unaongea nini kuna nchi yenye technologia na inteligencia kama Russia?
Kitu ambacho ni tishio kwa dunia na sikulifahamu ni kuwa Russia ndio nchi yenye stock kubwa zaidi ya Nuclear
Screenshot_20220225-193950~4.jpg
 
Back
Top Bottom