LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] haya sasa tumerudi, kwa hali ninayoiona, RUSSIA hana cha kupoteza as amekaa na mabomu bila sababu. Katika kujilinda kwake afu atokee Mtu azuie? Nimefuatilia kwenye vyanzo mbalimbali, URUSI hayuko peke yake, na nakuhakikishieni huu ndio mwisho wa UTAWALA wa USA na NATO as a SUPER POWER na EASTERN BLOCK (CHINA & RUSSIA) Wanakuja kucontrol dunia. Kwa nilichoona (mimi binafsi) Russia anaanzisha hii vita, kisha anakuja IRAN na NORTH KOREA wakati USA anaingia full hapo ndipo CHINA anaingia FULL and tunarudi kwenye historia kurekebisha mambo.
I BET RUSSIA to WIN
 
Kwa jinsi watu na mataifa mengi kupiga kelele kuhusu uonevu wa Russia , naona kamavile ile kauli kanafanya kazi ." SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU"

Mungu amesikia ndio maana Putin haamini kinachotokea.
Na bado mfungo wa kuiombea Ukraine ulioitishwa na Papa Francis kwa Wakatoliki wote haujafanyika. Ukifanyika hiyo tarehe 2 Machi, Urusi atapata tabu sana!

Nasema atapata tabu sana, people are not going to pray for nothing.
 
Babu,mbona unakuwa na kichwa boga kama mashabiki wa CCM tafuta hotuba za putin-amelielezea hilo swala vizuri.kwa hiyo we we unaona ni sawa USA awekw base Ukraine na Ukraine ilimiko nuclear kwa mgongo wa USA??
Sawa mm kichwa boga.

Ila swali ni hili naomba nijibu.

Suala la uhusiano wa nchi na nchi ni kwanini ni sawa China kuwa na ukaribu na Russia kujilinda na NATO ila si sawa kwa Ukraine kuwa na ukaribu na USA kujilinda na Russia? Usiseme mambo ya ukaribu wa mipaka.

Zile ni nchi mbili tofauti kila nchi inalinda mipaka yake na kuheshimu mipaka ya mwingine.
 
Putin mbwa hutu anataka Kutumia Nyukliaa mamaee zakeee fala kabiss yani mbwa huyuu adhibitiweee
 
Nightmare
 
Story za kujifariji hizo 👇

 
Weka hayo maelezo ya Biden eti kamchorea mstari mwekundu mbona hajapeleka pua yake wakati rais wa Ukraine analia lia
Sio kila vita unaingilia tu wenzako wana maono ya miaka elfu mbele hapo wamemchokoza Putin maksudi ili aingie kichwa kichwa vitani wamnyuke vikwazo ili kuuporomosha uchumi vizuri.

Ndo maana Putin amegundua hilo ameanza kuomba poo ya mazungumzo.

Gharama ya vita kwa siku inakadiriwa kufikia dollar billion 15 sawa na takribani trilioni 43 za Kitanzania.

Putin amewekewa vikwazo na karibu kila nchi hata ndege zake haziruhusiwi kukatiza anga la EU.
 
Babu,mbona unakuwa na kichwa boga kama mashabiki wa CCM tafuta hotuba za putin-amelielezea hilo swala vizuri.kwa hiyo we we unaona ni sawa USA awekw base Ukraine na Ukraine ilimiko nuclear kwa mgongo wa USA??
Ko unaamin kabisa hotuba ya Putin ipo sahihi haipo biased?
 
Babu,mbona unakuwa na kichwa boga kama mashabiki wa CCM tafuta hotuba za putin-amelielezea hilo swala vizuri.kwa hiyo we we unaona ni sawa USA awekw base Ukraine na Ukraine ilimiko nuclear kwa mgongo wa USA??
Kuna shida gani? Kwani yeye kakatazwa kuweka base Cuba?

Mbona kapeleka wanajeshi Venezuela nani kamkatalia?

Amemtushia na Sweden na Finland eti watakumbana na hatua za kijeshi wakijiunga NATO matokeo yake kwa sasa ni haya hapa sasa. 👇

 
Mkuu unajishushia heshima kwa kutoelewa vitu vidogo. Sijui una elimu gani, ila angalia miaka 1980-90s URUSI alipeleka BASE yake ya kijeshi NCHINI CUBA, ulitokea mzozo kama huu wa leo. Hii ina maana kwamba, UKRINE hana adui katika ukanda huu, ila URUSI ana maadui ukanda huu ambao ni NATO. hivyo walikubaliana na NATO kuwa kuwe na ukomo wa nchi fulani kuwa NATO, ambapo hizi majirani na RUSSIA zisiwe NATO, leo hii UKRAINE anataka kuungwa NATO huoni ni UGOMVI?? Nchi kama, FINLAND mbona wametulia na hawataki kuwa NATO??
Kwenye huu mzozo URUSI yuko sahihi na wapenda haki watasimama na URUSI.
 
Ukraine ni nchi huru nayo ina haki ya kujilinda na Russia kama anaiona ni tishio kwake.

Yaani ihalalishwe Russia kuivamia Ukraine sababu Russia inajilinda na NATO kwa kuingilia uhuru wa taifa ambalo lenyewe pia linajilinda na Russia?

Wakati ule Urusi (USSR) yailiyokuwa SOVIET ilipopeleka Mabomu ya kinyuklia kule CUBA kwa Fidel Castro, Marekani ikapeleka manowari, za kivita na nyambizi kutishia kuivamia CUBA kijeshi kama Urusi (SOVIET) haitatoa mabomu yake ya kiatomic pale Cuba kwani Cuba haikuwa nchi huru "sovereignty" kama Ukraine?!

Wakati Marekani na vibarake wake wanaivamia Iraq tena bila idhini ya umoja wa mataifa , kwa kuidanganya dunia kuwa Saddam Hussein anamiliki silaha za maangamizi ya halaiki, kwani Iraq haikuwa nchi huru "sovereignty"?!
Vipi kuhusu marekani na washirika wake kuivamia Libya na Syria?! Kwani hazikuwa nchi huru?! Nani aliwawekea vikwazo vya kiuchumi?!

Usiwe bias...!!
 
Misaada ipi wametoa!? Hebu tupatie na reference.
Ujerumani pekee amepeleka vifaru zaidi ya 40,ndege za kivita nakadhalika achilia nchi nyinginezo.

Marekani kapeleka msaada wa vifaa vya kijeshi wa zaidi ya Tsh trilioni 1 za Kitanzania na Ukraine imethibitisha kuvipokea.

Nato wamepitisha azimio la dharura kupeleka wanajeshi kadhaa kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wanajeshi wa Ukraine.

Kuwa updated mkuu mbona kila kitu kipo uchi dunia ya leo usisubiri kutafuniwa.
 
Kuna na hawa ndugu hapa kwa kweli wamechoka kweli kweli:

View attachment 2133244

Hiiiiii bagosha!
Russia kabeba conscripts wenye miaka 19-22 around hapo ndio troops. From poor family zisizo na sauti na uwezo wa kuhonga ili watoto wao kukwepa mandatory exercises, walikuwa kwenye training wakabadilishiwa wavamie, hawajaaga nyumbani, hawana justification ya kuvamia wanayoijua. Lengo la Kremlin ni kutishia Waukraine wajisalimishe, hawakuwaza kupambana sana. Walijua yaleyale ya Crimea wakati kipindi kile nchi ilikuwa na political turmoil. Sera za Urusi ni zile "show of force" ndio maana magwaride kila mwaka ila NATO hakuna nchi ina gwaride hata moja.

Ila tuwe makini, ikitokea Russia ikavamiwa hawatapigana namna hii. Uwezo wa kupigana wanao sana ila justification for war hawana. Nilikuwa namlaumu Biden na Olaf Scholz wa Ujerumani kwamba wameitelekeza Ukraine mapigano yalipoanza. Kumbe wazee wa siasa wazoefu walikuwa wanatafuta justification, yani sasa hivi dunia inajua Putin mchokozi. Walisubiri aggression ionekane waziwazi walete retaliation.

Nikisoma historia ya vita nyingi mara zote vita ikianza huwa makamanda wanaokuwepo wanakuwa wamedumaa kama hawakuwa na combat muda mrefu, sera zao hazibadiliki na mbinu za kijeshi huwa zinakuwa nyuma ya muda mara zote. Hii vita tech giants zimehusishwa kama Google, Meta na Apple. Mwaka juzi vita ya Azerbaijan na Armenia ilisababisha UK Defence Ministry wakaingie field kutafuta matumizi ya drones, US ikakazana zaidi kutafuta drone countermeasures, Russia ikaona drones ni tishio sio utani tena, terrorists wakapata kujua wakafanya shambulizi vituo vya mafuta Saudi Arabia. Mpaka nchi ije kujirudi inatumia muda, losses hazikwepeki. Ila sikutarajia performance ndogo hivi ya Urusi
 
Mpaka sasa hivi vita vimemletea Urusi hasara kubwa, huu ulioahidiwa na nchi za NATO ukifika vita vitakuwa vigumu kupita maelezo. Hata maeneo ambayo Urusi kayateka hajui afanye nayo nini na mbaya zaidi mashambulizi yanatokea hata kwa raia wa kawaida.
Urusi atafanikiwa kuharibu miundombinu wala si zaidi.Ukiona alivyoanza vita, alishambulia miundombinu ya kijeshi, akahamia kubomoa miundo mbinu, vita bado ngumu, akasema Ukraine imepewa sophisticated drones na US na sasa amehamia kwenye kikosi cha nyuklia, kwa mtiririko huu unaweza pata picha ni nini kinaendelea uwanja wa vita.
 
Urusi inazidi kusogea kijiografia nchini Ukraine, ila kwa kasi ambayo haukutarajiwa na wengi. Maana tuliambiwa kuwa ni "special operation" na wala si military campaign.

Wana-advance zaidi hasa katika maeneo ambayo hawapati resistance kubwa. Hata hivyo, wanaonesha kukumbana na changamoto zingine ambazo hazitokani na upinzani wa Ukraine, hasa logistically.

Wana uhitaji mkubwa wa supply ya nishati kwaajili ya zana zao, ammunition sambamba na huduma zingine kwaajili ya majeshi yao kadri ambavyo watahitaji kusonga mbele.

Kumekuwa na taarifa kwamba majeshi ya Urusi yamekuwa yakifanya uporaji (looting) katika maduka na masoko katika maeneo wanakopita. Nafuatilia usahihi wa taarifa hizi ingawa kuna videos zinazoonesha baadhi ya matukio hayo. Pia, kuna videos pamoja na picha za zana za kijeshi zilizotelekezwa kwa kukosa nishati.

Kuendana na hali ilivyo mpaka sasa, inaonesha kuwa Urusi haikuwa na mpango wa vita ya muda mrefu, ama military campaign, ila mazingira yanaonesha kuwa ni magumu kwake kufanya hivyo. Ndio maana limeibuka suala la kufanyika kwa mazungumzo hivi karibuni ambalo limeingilia kati.

All in all, bado ni mapema. Vita si jambo jema sana hasa kwa anayedhurika. Endapo majeshi ya Ukraine yataendelea kuonesha upinzani kama ambavyo tunaona kwa kiasi fulani, na kama Urusi itahitaji kurefusha hii vita kwa kubadili mpango (military campaign), kunaweza kutokea maafa makubwa zaidi hasa mbinu kama 'scorched earth' zitakapotumika. Swali ni je, Urusi ina maslahi na rasilimali za kutosha za kuirefusha hii vita?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…