Hammaz
JF-Expert Member
- May 16, 2018
- 6,607
- 14,076
Unajua muda mwengine Mtanzania anaweza akang'ang'ania kitu sana hata kwenye nchi yake anaona kama ni uzalendo. Au akang'ang'ania kitu sana hata asichokijua akaona yupo sahihi kumbe suala ni elimu ndogo.Huwezi kujifunga kwenye minyororo ya historia,huyo Russia angetaka hicho anachodai asingeruhusu Nchi zilizokuwa sehemu ya federations ziwe Republics.
Kwa kuruhusu tuu hilo hana haki tena na anachodai.Ndio maana sasa ameamua kupandikiza watu kwenye majingo yanayojitenga,anatumia njia ile ile walioyotumia west so vita ya nini sasa.
Kingine hatuna utaratibu wa kuwa wasikilizaji wa mambo tusiyoyajua ili tufahamu kwa mapana. Sisi kila kitu tunazungumza tu.
Tunashindwa kutofautisha kati ya mawazo ya mtu na ukweli uliyosemwa na mtu juu ya suala fulani. Mawazo ni haki ya mtu na yataheshimiwa ila kuyarasimisha mawazo ndiyo yawe ukweli ni kuukosea ukweli ukweli.
Nakushauri tusome Mzee.