LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Sawa mm kichwa boga.

Ila swali ni hili naomba nijibu.

Suala la uhusiano wa nchi na nchi ni kwanini ni sawa China kuwa na ukaribu na Russia kujilinda na NATO ila si sawa kwa Ukraine kuwa na ukaribu na USA kujilinda na Russia? Usiseme mambo ya ukaribu wa mipaka.

Zile ni nchi mbili tofauti kila nchi inalinda mipaka yake na kuheshimu mipaka ya mwingine.
Mkuu nimekueleza kuwa Putin amelitolea ufafanuzi mzuri hilo swala,ambapo kuna sababu nyingi ikiwemo za kihistoria.Kwani we we ujiulizi kwa nini Miaka na Miaka USA+NATO wanataka ukaribu zaidi na Ukraine na sio Nchi nyingine yoyote iliyopo karibu na Urusi-sababu hizo ndio hizo hizo zinazoifanya Urusi nayo ipinge kwa nguvu zote.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Mambo gani sasa haya kila mtu Ulaya anatuma silaha. Hawa Denmark wako serious kweli? Anti tank weapons 2,700 zote hizo kwa ajili ya invading forces. Ukraine walipofikia sasa hivi hata wanajeshi wa Russia wakienda na gari zisizo na armour kama Nissan au BMW watapigwa ATGM badala ya kurushiwa risasi.

Viktor Orban wa Hungary alikuwa amekubali kupeleka silaha ila ameghairi baadae sasa wanamshutumu. Haiwezekani sasa kila mtu atume silaha badala watafute suluhisho. Naanza kuona dalili hata Donetsk na Luhansk watalazimisha zirudi kwa Ukraine kwenye mazungumzo baadae. I bet zitatumika kwenye kuiondoa Russia kwenye vikwazo vya SWIFT. Ila Crimea ibaki Urusi, kwanza ni ya kwao na ni muhimu wawe nayo
Screenshot_2022-02-27-21-25-57-850_com.android.chrome.jpg
 
Duu!!! ni stress au ndio ule unyani aliousema mtikila..
Huo uraia wangu umeujulia wapi?
Mbona unajistukia, kwani wewe ndiye Victor Njogu au Abdirahim Hange? Ambao wamesema Putin aendelee kufanya anachofanya Ukraine kwa sababu wa Ukraine wamezuiz waafrika wasitoke nchini humo?
 
Wakati ule Urusi (USSR) yailiyokuwa SOVIET ilipopeleka Mabomu ya kinyuklia kule CUBA kwa Fidel Castro, Marekani ikapeleka manowari, za kivita na nyambizi kutishia kuivamia CUBA kijeshi kama Urusi (SOVIET) haitatoa mabomu yake ya kiatomic pale Cuba kwani Cuba haikuwa nchi huru "sovereignty" kama Ukraine?!

Wakati Marekani na vibarake wake wanaivamia Iraq tena bila idhini ya umoja wa mataifa , kwa kuidanganya dunia kuwa Saddam Hussein anamiliki silaha za maangamizi ya halaiki, kwani Iraq haikuwa nchi huru "sovereignty"?!
Vipi kuhusu marekani na washirika wake kuivamia Libya na Syria?! Kwani hazikuwa nchi huru?! Nani aliwawekea vikwazo vya kiuchumi?!

Usiwe bias...!!
Marekani na washirika wake hawakuwa sahihi kwenye suala la CUBA. Walitumia ubabe.
Pia hawakuwa sahihi kuivamia Libya. Tena ni tukio la kishenzi sana la Mmarekani alilowahi kufanya. Hawakuwekewa vikwazo kwa sababu hapakuwa na nchi yenye huo ubavu wa kufanya hivyo. Dunia yote ilinyamaza ikamuacha afanye yake.

Tunarudi kwenye tukio la wiki hii. Russia hakuiwekea vikwazo USA lakini leo inawekewa na dunia yote inampigia kelele.

Unadhani Ukraine itapigania kuwa na ushirika na nchi isiyoweza hata kutoa adhabu kwa bullies iende kwa nchi ambayo hata yeye anatunishiana nayo misuli? Nchi gani isiyotaka kuwa upande wa mwenye nguvu?
 
Si ilipigwa mkwara juzi na Russia,nadhani hii ni wake up kwa Sweden,Finland na Nordic countries zingine wakiwemo akina Kazakhstan,hazitakubali kupangiwa maisha tena na Russia.

Hii ni technical error Russia imefanya.
Kwasisi tusio fungamana na upande wowote, tunapenda kukwambia kua. Baada ya mazungumzo ya hao waheshimiwa wawili/wajumbe wao. Wasipo afikiana ni Ww3 ndicho kitu kinafuata. Maana ndio Vita rasmi itaanza Sasa.

NATO kusogeza vifaa, Russia kuvipiga alafu wanaingia na styre ya dog it another 🐕. North Korea anatuma wanajeshi 300,000 huku wengine laki 4 wakisogea mpakani na south. Ila south Korea anamuwahi mchinaamsihi kiduku wao hawafungamani na upande wowote. Kisha Iran inaanza kuzitarget base za NATO middle east. Israel anajiweka 100%military readiness. Hizbullah,Hamas nao wanakaa mguu nje mguu ndani Saudia anakataa kujiunga na Vita pamoja na Sunn country. Ila Egypt inaanza kumlia timing Uturuki Algeria inapewa jukumu la kuingia ulaya kutokea Mediterania akiwa na Tunisia na wanamgambo toka Libya, Mali, west Sahara na nchi za west africa wanaingia morroco mudahuo urusi yupo Berlin.
Finland, Switzerland,luxenburg,wao hawafungamani na yeyote hivyo watabakia Kama Tanzania tu. Wakati marekani inaamua kwenda kuisaidia ulaya China inaivamia Japan ikisaidiana na urusi na North korea. Marekani inakaribia kutia nanga inapewa Habari Saudia,Use,Qatar,Iraq, Afghanistan, Kuwait, Yemen, Lebanon na india, Jordan, Egypt, na Uturuki zimeigeuka na wanaipiga Israel kutokea kote kote, Israel inaona ngoja nife nao inaipiga mecca,tehlan na Cairo atomic bomb. Wakati huo huo manuali za North korea,China na Russia zinaichakaza america. Ndipo hapo unapitishwa uamuzi wa mwisho wa dunia awamu ya kwanza kwa kubofya vitufe vyekundu
Basi mchezo unaishia hapo dunia ikiwa imebaki na Super Powe south africa, Nigeria Tanzania alafu mpinzani Brazil.

Haya wakati yanatokea akina Thailand, south Korea na Australia mungu yupo pata jivujivu.
 
Lakini mm mkuu naona hatua ya Ujerumani kupeleka silaha Ukraine ni mbaya maana ninahofia wenda Urusi ika lazimika kuanza kutumia nguvu kubwa sana kitu ambacho kitasababisha maafa makubwa kwa Ukraine ikageuka Siyria ya Ulaya.
Maana nikikumbuka yale mashambulizi ya anga yaliyo fanywa na Urusi kule Allepo na pata hofu.

Sent from my TECNO BB4 using JamiiForums mobile app
Urusi ikitumia mbinu za kushambulia [ovyo] maeneo yoyote ambayo itaona yana msaada kwa majeshi ya Ukraine na nchi ya Ukraine kwa ujumla mfano, scorched earth policy, itaharibu kabisa mikakati yao yote iliyojiwekea hasa ya kisiasa hapo baadaye kuhusu Ukraine. Tangu mwanzo, Urusi imeonesha mpango wa kutaka kuung'oa utawala uliopo madarakani kwa njia ya kulisalimisha jeshi.

Na, ikiamua kuongeza majeshi zaidi na rasilimali zaidi kuendelea na pace hiihii inayotumia sasa, bado itazidi kupata upinzani mkubwa sana kutoka kwa majeshi ya Ukraine ambayo tayari yameanza kupokea nyongeza za silaha kutoka katika mataifa mbalimbali. Hapo tunazungumzia mapigano ya muda mrefu sana.

Urusi imekuwa ikikumbana na mashambulizi mengi sana ya kushtukiza yanayofanywa na Ukraine, achilia mbali yale ya kutafutana mitaani (ukizingatia kwamba silaha zimegawiwa kwa wingi sana kwa raia). Mapambano ambayo bado wakati wake haujawasili ipasavyo.
 
Kwasisi tusio fungamana na upande wowote, tunapenda kukwambia kua. Baada ya mazungumzo ya hao waheshimiwa wawili/wajumbe wao. Wasipo afikiana ni Ww3 ndicho kitu kinafuata. Maana ndio Vita rasmi itaanza Sasa.

NATO kusogeza vifaa, Russia kuvipiga alafu wanaingia na styre ya dog it another 🐕. North Korea anatuma wanajeshi 300,000 huku wengine laki 4 wakisogea mpakani na south. Ila south Korea anamuwahi mchinaamsihi kiduku wao hawafungamani na upande wowote. Kisha Iran inaanza kuzitarget base za NATO middle east. Israel anajiweka 100%military readiness. Hizbullah,Hamas nao wanakaa mguu nje mguu ndani Saudia anakataa kujiunga na Vita pamoja na Sunn country. Ila Egypt inaanza kumlia timing Uturuki Algeria inapewa jukumu la kuingia ulaya kutokea Mediterania akiwa na Tunisia na wanamgambo toka Libya, Mali, west Sahara na nchi za west africa wanaingia morroco mudahuo urusi yupo Berlin.
Finland, Switzerland,luxenburg,wao hawafungamani na yeyote hivyo watabakia Kama Tanzania tu. Wakati marekani inaamua kwenda kuisaidia ulaya China inaivamia Japan ikisaidiana na urusi na North korea. Marekani inakaribia kutia nanga inapewa Habari Saudia,Use,Qatar,Iraq, Afghanistan, Kuwait, Yemen, Lebanon na india, Jordan, Egypt, na Uturuki zimeigeuka na wanaipiga Israel kutokea kote kote, Israel inaona ngoja nife nao inaipiga mecca,tehlan na Cairo atomic bomb. Wakati huo huo manuali za North korea,China na Russia zinaichakaza america. Ndipo hapo unapitishwa uamuzi wa mwisho wa dunia awamu ya kwanza kwa kubofya vitufe vyekundu
Basi mchezo unaishia hapo dunia ikiwa imebaki na Super Powe south africa, Nigeria Tanzania alafu mpinzani Brazil.

Haya wakati yanatokea akina Thailand, south Korea na Australia mungu yupo pata jivujivu.
Rubbish 🚮🚮
 
Pengine labda ukifahamu wanchofanya Moscow ni nini!

Kipindi ambacho USSR walipoweka base ya kijeshi Cuba na kuweka makombora ya nyuklia USA ilihangaika sana kwa sababu USSR ni hasimu wao hivyo ni mazingira hatari kwa usalama wa nchi. Walitumia njia tofauti tofauti kukabiliana na hilo. Waliwawekea vikwazo Cuba. Walianzisha vita kwa kuwafadhili wana Cuba wengine ili kufanya jaribio la mapinduzi ambalo lilifeli.

Na haya ndiyo mazingira yale yale kwa Urusi. NATO ni hasimu wake. Ukraine ni nchi huru. Ila uhuru wa kuhatarisha usalama wa jirani yako huo uhuru inabidi uangaliwe. Ikiwa Ukraine akijiunga na NATO ni hatari kwa Usalama wa Urusi. Ukraine alikuwa na mabomu ya nyuklia. Vipi akirudi kwenye mpango wa kuyazalisha ukijumlisha akiwa kwenye umoja wa NATO itakuwa ni hatari zaidi kwa usalama wa Urusi.

Serikali ya Ukraine imekataa makubaliano na Moscow ya kuwa wawe neutral. Njia ambayo Moscow inaiona itailinda nchi yake ni kuiondoa serikli ya Ukraine na kufanya hivi itakuwa ni tishio kwa Ukraine na kumfanya abadili sera yake.

Hivyo unavyosema ni vita ya Putin kwa manufaa ya kijeshi kuna angle haujaiangalia vizuri. Putin na wakubwa wengine wa Urusi wanalinda maslahi ya usalama wa muda mrefu wa Taifa lao. Ukraine ipo vizuri kijeshi lakini imezidiwa na Urusi. Njia pekee ambayo ni salama kwa Ukraine ni kufanya mazungumzo na Urusi na wakubaliane ili amani irudi tena Ukraine. Rais wao anataka aonekane shujaa lakini hili litamgharimu kwa sababu hatumii akili.

Na usihofia kuhusumaandamano nchini Urusi. Sehemu ya raia wanaoandamana ni ndogo tofauti na wanaokubaliana na maamuzi ya serikali. Ila yote juu ya yote vita si jambo zuri.
Boss ni sawa. Issue yangu ni kwamba katika mataifa mawili yenye nguvu mataifa madogo yanachagua kuwa na ushirika na mwenye nguvu zaidi. Russia hawezi kuweka vikwazo kwa NATO na USA wakifanya uvamizi. Kwanini Ukraine awe na ushirika na nchi isiyo na ushawishi iache nchi ambayo ikitaka kumchapa hakuna wa kuiwekea vikwazo?
 
jasiri huwa anatakiwa kutumia akili. hakuna faida yeyote kusifiwa kuwa ni jasiri wakati hautumii akili. na unasababisha collateral damage to your own country ambayo umeijenga kwa muda mrefu. hebu jaribu kufikiria mfano Tz tulivyoijenga kwa miaka mingi kwa kodi zetu hivi, halafu anatokea rais mmoja anataka kututia kwenye hasara ambayo ingeepukika ili asifiwe kwamba aliipigania nchi, ikisambaratishwa tuanze tena kuijenga upya. hiyo akili au matope? tena kwa maslahi ya wamagharibi sio ya watu wako.
Ndo maana Kuna watu wanamlaumu Sana nyerere kwenye Ile Vita ya kagera,

Hakukua na ulazima wa Vita na Uganda. Wazungu wangemalizana nae kwa vikwazo TU mpk akanyooka mwnyw.

Hata Trump pia kalaumiwa Sana mpk kupigwa chini kwny uchaguzi, kakurupuka kwa kuingia kwny Vita zisizo na faida kwa kutumia Kodi za wananchi wa us,
 
Ukraine ndiyo kiburi...

Ni sawa na Zanzibar imvimbie Tanzania... Ni makonzi tu..
 
Ikiwa kama uhuru huo ni wa kuhatarisha usalama wa taifa la jirani yako basi uhuru huo uangaliwe.
Usalama wa nchi jirani isiyo na ushawishi kwa majirani zake una maana gani? Russia nae anatakiwa ajiunge tu NATO. Hana ushawishi zaidi ya kuwa na hayo mabomu ya nuclear anayotishia tishia nayo. Leo USA akiamua kuivamia nchi ndogo humuoni akitoka akasema nazima SWiFT ila ona yeye anavyotandikwa vikwazo. Sasa ana tofauti gani na Zimbabwe alivyolimwa vikwazo? Amwache Ukraine akawe na ushirika anapotaka.
 
Unataka Russia aanze kuua raia!? Tayari rais ya Ukraine ameanza kufuata maelekezo ya Russia. Sasa hivi lazima aende Belarus. Na sharti alilopewa namba moja ni askari wake wajisalimishe.

Hakuna mjadala hapo. Kama hataki basi Russia atatoa mkong'oto wa kweli.
kahawa hii sasa,tuletee na kashata kabisa
 
Ukianza nao taratibu hawaji tena,maana wanajua fika unakotaka kumpeleka hawezi chomoka,hawa ndiyo pro Russia sasa,wakati mwingine unaamua kwenda nao kwa style yao ya story za vijiweni tu
😀😀😀😀
Wanataka Ukraine aisikilize nchi ambayo haina ushawishi, haiwezi hata kuweka vikwazo.
 
Russia lengo lake ni kumfanya Ukraine asiingie NATO. Na wengine walioingia kinyume na makubaliano, siku zao zinahesabika.

NATO sasa hivi hawama pesa za kujiendesha.
Kahawa ya baridi sana hii Mkuu
 
Mkuu nimekueleza kuwa Putin amelitolea ufafanuzi mzuri hilo swala,ambapo kuna sababu nyingi ikiwemo za kihistoria.Kwani we we ujiulizi kwa nini Miaka na Miaka USA+NATO wanataka ukaribu zaidi na Ukraine na sio Nchi nyingine yoyote iliyopo karibu na Urusi-sababu hizo ndio hizo hizo zinazoifanya Urusi nayo ipinge kwa nguvu zote.
Ukraine kwanini hawatakaki ukaribu na Urusi wanawachagua NATO+USA?
 
Kwasisi tusio fungamana na upande wowote, tunapenda kukwambia kua. Baada ya mazungumzo ya hao waheshimiwa wawili/wajumbe wao. Wasipo afikiana ni Ww3 ndicho kitu kinafuata. Maana ndio Vita rasmi itaanza Sasa.

NATO kusogeza vifaa, Russia kuvipiga alafu wanaingia na styre ya dog it another 🐕. North Korea anatuma wanajeshi 300,000 huku wengine laki 4 wakisogea mpakani na south. Ila south Korea anamuwahi mchinaamsihi kiduku wao hawafungamani na upande wowote. Kisha Iran inaanza kuzitarget base za NATO middle east. Israel anajiweka 100%military readiness. Hizbullah,Hamas nao wanakaa mguu nje mguu ndani Saudia anakataa kujiunga na Vita pamoja na Sunn country. Ila Egypt inaanza kumlia timing Uturuki Algeria inapewa jukumu la kuingia ulaya kutokea Mediterania akiwa na Tunisia na wanamgambo toka Libya, Mali, west Sahara na nchi za west africa wanaingia morroco mudahuo urusi yupo Berlin.
Finland, Switzerland,luxenburg,wao hawafungamani na yeyote hivyo watabakia Kama Tanzania tu. Wakati marekani inaamua kwenda kuisaidia ulaya China inaivamia Japan ikisaidiana na urusi na North korea. Marekani inakaribia kutia nanga inapewa Habari Saudia,Use,Qatar,Iraq, Afghanistan, Kuwait, Yemen, Lebanon na india, Jordan, Egypt, na Uturuki zimeigeuka na wanaipiga Israel kutokea kote kote, Israel inaona ngoja nife nao inaipiga mecca,tehlan na Cairo atomic bomb. Wakati huo huo manuali za North korea,China na Russia zinaichakaza america. Ndipo hapo unapitishwa uamuzi wa mwisho wa dunia awamu ya kwanza kwa kubofya vitufe vyekundu
Basi mchezo unaishia hapo dunia ikiwa imebaki na Super Powe south africa, Nigeria Tanzania alafu mpinzani Brazil.

Haya wakati yanatokea akina Thailand, south Korea na Australia mungu yupo pata jivujivu.
ghahawa ya wapi hii uliokunywa maaalim 😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom