Wacha porojo
Mbona ulaya hawajapeleka jeshi?
Wanamjoke Putin, jamaa ni kama kaja kuwazawadia majamaa dhana za kivita, inawezekanaje una run out of fuel means huna calculations, au wanajeshi wake wanamhujumu, kapigika sana hususani jana.Kifaru kinavutwa na trekta khe
Formula ni ile ile booby trap....wanaingia kwenye target wanavuja damu.Unafatilia vizuri hii vita?.maana kila baada ya muda kuna mabadiliko.warusi wanasonga mbele kila upande
Mbona Hammas wanafanya hivyo hivyo lakini Israel akishambulia mnasema anaua Raia?Sasa haya ni mawazo yako!
Wachambuzi wanasema Russia bado wanawahitaji raia wa Ukraine, ile nchi bado ipo na ni jirani yao na itabakia kuwa hivyo. Hakutakuwa na sababu ya kufanya uvamizi mkubwa kama alivyofanya Syria. Akifanya uvamizi wa namna hiyo atatengeneza adui mwengine mkubwa wa kizazi na kizazi ambaye ni jirani na ni mazingira hatari kwa usalama wa nchi ya Russia.
Kimkakati inambidi adili na wanajeshi tu baada ya amiri jeshi mkuu wa nchi ya Ukraine kukataa makubaliano waliyoyapendekeza. Na ndiyo maana akaanza na kupunguza nguvu ya jeshi la Ukraine kwa kushambulia base za kijeshi na maghala ya kuhifadhia silaha pamoja na viwanda vinavyojihusisha na utengenezaji wa silaha. Lengo no kupunguza nguvu za jeshi la Ukraine.
Operation inayofuata ndiyo hiyo ambayo anayoifanya sasa hivi na ni operation ngumu ambayo ni urban warfare. Ikiwa ni kuiondoa serikali ambayo kwake anaiona ni hatarishi. Kwa kuzuia uharibifu mkubwa wachambuzi wanasema ameingia na silaha za nyuma si za kisasa.
Urban warfare ni ngumu na ugumu wa hapa si kwamba Russia hana uzoefu. Ugumu wa hapa ni mnapambana kwenye makazi ya watu ambao ni raia, ambao sheria za kivita zinawalinda. Shambulio lolote dhidi yao ni uhalifu wa kivita kwa sababu umeshambulia wasiyostahiki. Na huu ni mtego kwa Russia, majeshi ya Ukraine yanajificha kwenye makazi/majengo ya makazi ya raia.
Kuna suala hapa umelisahau. Russia lengo la hii vita ni kulinda usalama wa nchi yake. Sote tunafahamu NATO ikiwa mlangoni kwake ni hatari. Ukraine pia inakuwa kijeshi ikiwa NATO na ikijijengea na uwezo wa kutengeneza mabomu ya nyuklia hatoweza kumdhibiti. NATO wanalijua hili na wanajua kuwa Ukraine ni kete muhimu dhidi ya Russia.
Naam; Ukraine ni nchi huru ina wajibu wa kufanya maamuzi yake lakini ni hatari kufanya maamuzi yatakayo hatarisha usalama wa nchi jirani yako. Russia anachofanya ni kumdhibiti Ukraine mapema. Ikiwa Russia mkakati huu utafeli wachambuzi wanasema itamlazimu alazimishe mazingira. Nayo ni kutunisha msuli wake. Akifanya hivyo maangamivu ya Syria miji kuwa gofu yatahamia Ukraine. Na Ukraine itaumia.
Russia inacheza mahesabu hapa! ni mahesabu yanayohitaji umakini wa hali ya juu. Atakayeumia zaidi ni Ukraine ikiwa akikaza msuli.
Unajua maana ya Warmonger? Tuanzie hapo kwanzani kweli, hata mimi siungi mkono vita, hapa ninacheka vile baunsa kakalishwa na kimbau mbau.
Putin ni warmonger wakati umemvua nguo yeye na jeshi lake wamapata aibu kuu zile porojo za kutajiwa majina ya silaha anazomiliki zitapungua hapa Jf. [emoji4][emoji4]
Kwani wewe uko Kuzimu? Msalimie Shetani,mwambie mpaka Sasa Yesu hajarudi.Tunaomba mtujulishe yanaondelea huko duniani jaman
Nchi imezungukwa, airport zote,anga lote zimepigwa Pini na warusi.Nchi takribani 28 zimeahidi hivi karibuni kupeleka silaha Ukraine. Mpaka sasa sidhani hata robo ya nchi hizo zimesema zitakachopeleka hasa.
mbona poland, Deutschland, Netherlands, turkey, wametoa msaada ya fedha na silaha kwa kyiv hawajafanywa chochote mpaka muda huu
Maelezo mazuri unaeleweka.Wakati wa dola ya Ottoman ya Kiislamu na dola nyengine kubwa ya Kikristo ilifika pahala pakuwa na mtafaruku mkubwa baina ya pande hizi mbili. Kuna jamii moja ya wazungu inaitwa Khazarian. Mfalme wao alichagua kama Taifa wawe na dini ipi itakayowaongoza katika Taifa. Dini iliyochaguliwa baada ya kukaa na baraza lake la Mawaziri ni dini ya kiyahudi.
Sababu ni kuwa ni kuepukana na athari ya aina yoyote kutoka kwa dola kubwa mbili, ya Ottoman ya waislamu na dola ya kikristu. Hivyo ana gain kotekote. Na athari itakayotokea baina ya dola hizo 2 hazitoweza kuathiri Taifa moja kwa moja.
Ukraine ilibidi iwe neutral ambapo kwake ni mahali salama. Mahusiano yake na west angeyaimarisha kwenye uchumi zaidi kuliko mahusiano ya kijeshi. Wakati mwengine hata kama ukiona ni sahihi ila ukiacha ndiyo njia salama itakayokuepusha na maafa basi ni vizuri kuicha hususani ikiwa unadhamana ya mustakabali kwa wengi.
Nasikia eti Wanafunzi na Waafrika wasio Wanafunzi wanazuiliwa kuingia Poland ambako awali ilikuwa waende Ili kuwa salama kiufupi wanabaguliwa
Tuwaombee tu watu wa ukraine ila kwa ninavyowajua warusi, si watu wa kukubali kushindwa kabisa wapo tayari wafe hata milioni ila lengo lao litimie.Formula ni ile ile booby trap....wanaingia kwenye target wanavuja damu.
Ngoja nikusaidie tu.Sasa kwa mfano Putin akawahi akatupia hilo Bomu katika Makao Makuu ya jeshi lako huo muda wa wewe kuanza kuji organize utautoa wapi?
Nani alikutuma uende huko bongo vyuo vipo vingi udom, udsm, st.john, Tumaini nk.
Ukifikiria kama hivi basi utaingia kwenye matatizo kama yaliyomkuta Ukraine. Russia haitaji uwe mshirika wake. Anachohitaji ni usalama wa nchi yake; lielewe dhumuni na mantiki ya Russia. Na hakuna anayepinga kama Russia naye kijeshi ni mkubwa kama huyu mkubwa aliye na ushawishi.Usalama wa nchi jirani isiyo na ushawishi kwa majirani zake una maana gani? Russia nae anatakiwa ajiunge tu NATO. Hana ushawishi zaidi ya kuwa na hayo mabomu ya nuclear anayotishia tishia nayo. Leo USA akiamua kuivamia nchi ndogo humuoni akitoka akasema nazima SWiFT ila ona yeye anavyotandikwa vikwazo. Sasa ana tofauti gani na Zimbabwe alivyolimwa vikwazo? Amwache Ukraine akawe na ushirika anapotaka.
Una maanisha nn mkuu sija kuelewa.Kama kuna mpango wa kufanya siege warfare, maana yake kuna uwezekano mkubwa sana wa kuongezeka kwa vifo vya raia endapo wataamua ku-react hapo baadaye. Hata hivyo, bado hakuna taarifa rasmi kuthibitisha suala hilo.