LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
wanaandamana moscow huko

Huyo Putin ushawishi wake utazidi kupungua kadiri muda unavyokwenda, hao maoligarch na hizo wealth families ambazo washakula kibano cha vikwazo vya kiuchumi hawawezi kuendelea kuwa bega kwa bega na Putin kwa muda mrefu maana maslah yao yatakuwa yanazidi kupotea so ni suala la muda hao russians now wanachukiwa sehemu nyingi dunian hasahasa western na maisha kwa russians yatazidi kuwa magumu sana matokeo yake shinikizo likizidi atang'oka au kwa aibu itabidi anga'tuke kilinda heshima yake na kupisha kiongozi mwingine ambayo kwa ajili ya mashinikisho atajikuta anakaa na western meza moja. Western wanatumia akili zaidi na wamemtafuta Putin muda naye now kaingia cha kike na wanamsulubu kweli kweli bila huruma mpaka zee limesema;

Western countries are not only taking unfriendly actions against our country in the economic area. I'm speaking about the illegitimate sanctions that everyone is well aware of. However, the top officials of the leading NATO countries also make aggressive statements against our country as well,” Putin stated.
 
Kuna mtu leo aliongea kuhusu hili humuView attachment 2134478
Russia inafaidika na hiyo permanent membership sababu ni "continuing state" kutoka iliyokuwa USSR. Continuing state ni sehemu kubwa ya nchi iliyobaki baada ya sehemu ndogo kujitenga ama kuvunjika.

Hiyo ndiyo hoja iliyotumika kuirithisha Urusi (Russian Federation) hiyo nafasi katika UNSC. Urusi ya sasa imerithi vitu vingi sana kutoka USSR.
 
wanaandamana moscow huko

Binadamu wa kipindi hichi sio wale wazalendo wa zamani wa kutaka kuifia nchi kwa kuua na kutesa wengine kwa jina la kiongozi wao. Vijana waliozaliwa miaka ya 2000 ni wapenda uhuru, kusafiri, kuoa/kuolewa mataifa mengine, michezo, mapenzi, nyimbo ndo wanataka. Mambo ya kufa kwa ajili ya kiongozi wako hawataki.
 
Binadamu wa kipindi hichi sio wale wazalendo wa zamani wa kutaka kuifia nchi kwa kuua na kutesa wengine kwa jina la kiongozi wao. Vijana waliozaliwa miaka ya 2000 ni wapenda uhuru, kusafiri, kuoa/kuolewa mataifa mengine, michezo, mapenzi, nyimbo ndo wanataka. Mambo ya kufa kwa ajili ya kiongozi wako hawataki.
Umekula leo kweli!?
 
Umekula leo kweli!?
Nimesoma hoja zako ukiwajibu watu, naona unapambana kweli kutoa majibu yasiyo na staha na yanayokera kwa watu wenye mtazamo tofauti na imani yako kwa Putin wa Urusi. Putin unamuhusudu kweli kweli, Well ni sawa na naheshimu hilo ila ukumbuke ni imani tu, ukirudi kwenye uhalisia yule ni putin binadamu mwanaume kama wewe tu sasa angalia imani isikuzidi ukajikuta unafanya ibada.
 
Mimi nimejiuliza sana masuali mengi (sidhani kama wengi humu wamejiuliza suali hilo) kwamba, je hasira zote hizi za nchi za magharibi na NATO huenda wanahofia vifo kwa askari wengi wa nchi hizo ambao wamekuwepo ndani ya Ukraine na Putin alipogundua hilo akaona awashughulikie.

Vikosi vidogo vya majeshi ya Canada, USA, na nchi zingine zilikuwemo nchini Ukraine kwa muda mrefu wakitoa mafunzo kwa jeshi la Ukraine ambapo Putin alionya na ilikuwa ni suala la muda tu Ukraine iwe nchi ya Umoja wa Ulaya na hatimae NATO.

Ndio maana kwa sasa wanajitahidi kutaka kutoa misaada zaidi ya vifaa vya kijeshi (kupitia Poland) lakini inakuwa ngumu kwani tayari Ukraine imezingirwa vibaya.

Ni suali la msingi sana kujiuliza je, hasira za nchi za magharibi na NATO zinatokana na kuathiriwa na hali kwamba Russia inashambulia raia wake (wanajeshi) ingawa hii kitu hawawezi kukisema hadharani na kutuficha kwa kivuli cha vikwazo mbalimbali vya kiuchumi?
Braza umeongea kitu ambacho wengi hawakioni. Watu wamejaa ushabiki kuliko uhalisia. Kinachotokea Ukraine sio bahati mbaya, na jeshi la Ukraine peke yake wasingeweza kuzuia warusi. Wapo watu nyuma ya hili, muda utatuambia
 
Hakuna madikteta wowote duniani wanaompenda US . ukiifuata demokrasia huwez kukwaruzana naye hata Mara moja .
Acha uongo US...ililaaniwa na wise man kama NELSON MANDELA kuwa haina humanity!!!...sasa wewe unajua nin kumzid madiba katika medani za deplomacy na democracy???
 
Braza umeongea kitu ambacho wengi hawakioni. Watu wamejaa ushabiki kuliko uhalisia. Kinachotokea Ukraine sio bahati mbaya, na jeshi la Ukraine peke yake wasingeweza kuzuia warusi. Wapo watu nyuma ya hili, muda utatuambia
Ndo maana sasa hivi wanahangaika kutaka kutoa misaada zaidi ya vifaa vya kijeshi kwa Ukraine.

Na taarifa zaidi zasema kwamba wamekuwa wakiisaidia Ukraine kwa miaka 20 sasa, kuijenga kijeshi na baadae kuikabili Russia wakiwa daraja kwa US na NATO.

Haiwezekani Zelenskyy aombe kukutana na Russia wazungumze inamaanisha kwamba hana maamuzi imara kutoka kwake yeye kama yeye.

Kwa maana moja ama ingine anashindwa aamue lipi.

Nae Balozi wa Russia UN pia ametoa kauli kwamba makosa ni ya Zelenskyy kukubali kuwa pamoja na mafashisti ambao ndio wanampoteza na kufanya mauaji kule Donbass kwa warusi.
 
Yes
Soma vizuri mkuu, nimekwambia kanusa plan ya Mmarekani na genge lake la NATO. Ikitokea kwa bahati mbaya au kwa kupanga kombora lake moja likaangukia Poland au Lithuania ambao ni wanachama halisi wa NATO, basi Putin na nchi yake watakuwa wakimbizi wa kisiasa huko China. Maana hatoweza kuhimili balaa la hawa jamaa.
Duuuh acheni ushabika wa maandazi basi tufanye comparison ya nuclear warheads baina ya nato versus russia
Russia ana nuclear war heads 6255
Usa 5558
Ufaransa 290
Uk 230
Israel 90
Yaan ukichukulia idadi yote ya nuclear aliyonayo mrusi kwa kulinganisha na nato na washirika bado kawazid parefu tu.
Tukisema tuweke na wachina hapo na north korea basi nato wanapigwa mchana kweupe.
Kuna wafuasi humu tumewasikia kuwa eti georgia ilimpiga urusi daah.kwanza tulale zetu maana tunakumbuka kisago kilichotembezwa mpaka nchi ya georgia ikapoteza majimbo yake mawili
 
Yes

Duuuh acheni ushabika wa maandazi basi tufanye comparison ya nuclear warheads baina ya nato versus russia
Russia ana nuclear war heads 6255
Usa 5558
Ufaransa 290
Uk 230
Israel 90
Yaan ukichukulia idadi yote ya nuclear aliyonayo mrusi kwa kulinganisha na nato na washirika bado kawazid parefu tu.
Tukisema tuweke na wachina hapo na north korea basi nato wanapigwa mchana kweupe.
Kuna wafuasi humu tumewasikia kuwa eti georgia ilimpiga urusi daah.kwanza tulale zetu maana tunakumbuka kisago kilichotembezwa mpaka nchi ya georgia ikapoteza majimbo yake mawili
vita ya nuclear haitakua na mshindi poyoyo wewe.
 
Kwa hivyo vikwazo walivyowekewa, Russia hawana jinsi itabidi tu wambembeleze Valodomyr Zelensky ili watete na Putin na ionekane kwamba wamefikia some sort of compromise ndio Russia wajifanye kuondoa majeshi yao Ukraine ili kuficha aibu inayowanyemelea Russia.
Sio mara ya kwanza anawekewa vikwazo, kipindi cha vita ya russo-georgia war aliwekewa vikwazo ila bado alitia ngumu mpaka akamega mikoa miwili ya georgia
 
Back
Top Bottom