LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Hawezi kukwambia maana hana cha kusema Mkuu,hawa wanachojua ni "Putin anakiwasha Ukraine" lakini ukimjia na hoja kama yako,hana jibu la maana atakalokupa.
 
Unamaanisha Kwamba yeye alikuwa anamchokonoa Ukraine huku lengo lake kuu likiwa NATO na USA,jamaa wamemlia timing wakamwacha akauvaa mkenge,wao wakabonyeza kitufe cha vikwazo wakatulia,wakamwachia hangaike na maguvu yake Ukraine
 
Reactions: Tsh
Pro Ukraine mmelala,tulijua tu mtoto halali na hela analala na mavi tu. Tunamalizia kamji kale mda huu
Nimeamka kuangalia majivu ya Kyiv bado naukuta mji upo,tusogeze deadline mpaka lini tena ndugu Mrussi wa Kinondoni Moscow,wewe hauwezi kuwa Mrussi wa Shelui maana ni mjanja mjanja.😂
 
Na unakuta hiyo elimu anayojivunia kasoma kwa kudesa kila kitu kutoka google,muulize maswala ya msingi yanayohitaji critical thinking,utapewa jibu jepesi "nenda google utakuta kila kitu".
 
Muda utaongea mkuu.😀
 
Unamaanisha Kwamba yeye alikuwa anamchokonoa Ukraine huku lengo lake kuu likiwa NATO na USA,jamaa wamemlia timing wakamwacha akauvaa mkenge,wao wakabonyeza kitufe cha vikwazo wakatulia,wakamwachia hangaike na maguvu yake Ukraine
Watu wanawadharau NATO na USA. Wanasahau kuwa mule kuna binadamu wenye akili sana wanaoweza kuandaa mpango na ukamuumiza sana waliyemuandalia.
 
Hahahaaaaaa #kyivmajivubadotuuu# hahahaa mtu mzima Putin chaliiii
 

Unaachaje kuiongelea wakati wao ndio waliosababisha mpaka vita itokee,kyiv kuwa majivu ni swala la muda tu,,,ingekua Russia wanalengo lakuua na raia tungekua tunaongelea habari nyingine sasa!
 
Hii vita sio ya Ukraine na Urussi tu watu wanapigana indirectly humo.Urusi Vs USA na Nato.Wanachofanya Wamarekani ni kumtengenezea Puttin image mbaya kwanza,Kumuwekea vikwazo vya kiuchumi kwanza.Kwa sasa Urusi hataona madhara ila baadae atayaona.Na vita direct kati ya Urusi na wanachama wa Nato itaanza rasmi pale Putin atakapodorora kiuchumi.Ikumbukwe mabilionea wa kirusi nao wamepata sanctions wananchi wa kawaida maisha yao yataanza kuwa magumu usaliti utaanza ndani ya nchi yake mwenyewe na ndio mazingira wanayoandaa Wamerakani kwa sasa.Na Nato watakuja wakati Putin amedorora kiuchumi na hapo itakuwa rahisi kummaliza
 
ila ujue pia na yy ana gas ambayo juz tu kasign kuipeleka beijing.na 29% ya gas ulaya anayepeleka ni yeye.so maumiv yatakua kotekote.
btw mauaji yaliyofanyika donessk 2014 na ukraine uliyaona? unajua katika vita propanganda ni tool mojawapo,tunajazwa kuona selective news nenda RT uone jins documentary jins ukrain alivofanya mauaj donesk na luhans
 
Hutaki kujibu hoja umeng'ang'ania kyiv kua majivu, unataka Russia waue raia wasio na hatia? Alafu sikiliza malengo ya warusi wenyewe sio mashabiki kama wewe humu JF.
Malengo ya Russia according to president Putin ni 'special military operation' yenye lengo la ku demilitarize Ukrain Army ikiwa na lengo la kuondoa 'Neo nazism'

Urusi inahisi ujio wa vikosi vya EU na NATO pale Ukraine itakua ni 'threat' kwa usalama wa Russia, ikiwa haya yanafanyika au yatafanyika huo ndio utakua ushindi wa Russia, ikiwa itashindikana basi Russia watakua wameshindwa. Ushabiki maandazi unaondoa ladha jamani.
 
Kwa upande mwingine Ukraine itakuwa ndio uwanja uliotolewa sadaka ya vita kati ya Urusi na NATO maana ikumbukwe Marekani hapiganagi na adui nchini kwake hata siku moja sababu hapendi losses.Putin hii vita anatumia nguvu kuliko akili na meza yake imezungukwa na wale watu wa ndio mzee.Nao anaweza kuichukua Ukraine huku wao wapo kimya sababu now mkakati wao mkubwa ni kummaliza kiuchumi kwanza.Watu wanaona Wamarekani wajinga lkn hawa watu wanatumia akili kwanza sababu mtu akiwa na njaa nguvu ya kupigana na wewe ataitoa wapi?Pia Urusi kwa kuangalia nchi marafiki anaowategemea hajawaelewa vizuri hao watu anavibe nao lkn sio kwamba ana ushirika nao.Tangu lini China anaingia vitani na mtu?Kiduku mwenyewe hana rafiki he stands on his own na kwa maslahi yake binafsi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…