LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Ukraine itakuwa Somalia ya Ulaya soon.....
1.Si silaha zote zitarudi hata baada ya vita kuisha, lazima vitazaliwa vikundi vingi vya waasi kama sio magang ya Uhalifu ( Ukizingatia uchumi utakuwa umeyumba)
2.Kuna mahala nimeona wapiganaji kutoka middle East wanakuja kujitolea ( Tunawajua hawa watu, na tabia zao za looting zinafahamika). Watalowea hapo Ukraine na kinachofuatia kinafahamika.
Ukraine ilishaanza kuwa na wahuni muda mrefu kuna battalion nilikuwa naisoma miaka iliyopita wale hawaongozwi hata na jeshi la serikali ila wanailinda mipaka ya Ukraine kule Donbass na wana spirit ya kupigana sana. Wale nao this time wamepewa silaha za EU wanazitumia, nadhani umewaona jamaa wana bendera za Nazi na skulls & bones. Wale wakiambiwa wajiunge jeshi la serikali wanakataa na hawataki kuwa chini ya mwongozo wa serikali
 
Hiyo ban hata yeye mwenyewe US
Mrusi ndo itamuumiza zaidi kwa sababu sio mrusi pekee anayezalisha mafuta,so nchi zingine zitafaidika zaidi pia kuuza.
ndo maana ameenda kujipendeza venuela

ndo maana ameenda kujipendeza venuela
Anafanya hivyo ili kumreplace mrusi katika soko,na atakuwa replaced kwa sababu hata huyo venezuela ataangalia maslahi ya uchumi wake hatajali na hatowanunia wamarekani,atakubali na mrrusi atakuwa replaced kidogokidogo.
na supplyer mkubwa wa hizo nishaati ni Russia
,Saudi Arabia, Canada, China na venezuela naye akikubali kusupply mafuta hawa wote wanamreplace mrusi kwa kiasi kikubwa sana ukiongeza na wairan pia ambao nao wakikubali kuuza mafuta yao katika soko basi mrusi ataumia
 
waliliona lkn ,imewabidi wakajipendekeza kwa maadui zao Iran,Syria ,Saudi Arabia ,maana hao hao malekani waliwawekeaga vikwazo vya kiuchumi,Sasa huu ndo muda wa hawa jamaa nao kupiga double standard [emoji1],hata hivyo haitatosha ,kum supless Russia kwenye volume ya mafuta aliyokuwa aki supply duniani.tushudie mafuta kupanda Bei zaidi !!
Weka data tuone kama hao hawawezi kureplace nafasi ya urusi.
 
Maduro atafaidi sana huu msimu... Siwaoni EU na Uk wakiban hii rasilimali
Deal likitiki Maduro ataula kuna uwezekano Venezuela akalamba kila mwezi zaidi ya dollar za kimarekani billion 5 hata na zaidi kama mrusi atawafungia ulaya Bomba la mafuta na gesi na vita ya Yukrein kuendelea. Kwasababu kuna uwezekano pipa moja la mafuta likafika dollars 300.

Enzi hizo za Hugo Chavez kabla ya vikwazo Venezuela hela ilkuwepo siyo mchezo hadi Chavez aliipa Haiti msaada wa dollars za kimarekani billion 2 nakuwasemehe wasilipe. Mungu amrehemu Hugo Chavez.

Colombia na Venezuela ni mahasimu na watani wa jadi ilivyo Kenya na Tanzania. Wakati wa neema kipindi cha Hugo Chávez wavenezuela walikuwa wanawacheka sana wacolombia kwasababu ya vita na hali ya kiuchumi nchini kwao. Baadaye Colombia ikatulia na uchumi kuimarika. Vikwazo vilipoanza Venezuela na uchumi kushuka wacolombia wakaanza kuwacheka Venezuela.

Sasa wanvenezuela watawaambia soon we'll be back.
 
Hii vita mpaka inaisha hakutakuwa na tank battle hata moja. Ile Gulf war Iraq walijichanganya eti wakaingia tank battle na Marekani walikuwa wanapigwa sana. Battle kubwa zaidi ilikuwa ni Medina Ridge ndani ya masaa mawili Marekani ilipoteza vifaru vinne na silaha nyingine ila Iraq ilipoteza vifaru 186 na silaha nyingine nyingi. Israel nayo ilikutana na vifaru vya Syria kwenye Yom Kippur iliviharibu sana ila Egypt walipambana. Hata uwe na vifaru vizuri ila training na experience ni muhimu mno kwenye crew yako.

Ukraine wameona hawawezi shinda battle ya tank vs tank, wala artillery hawatumii maana wako outguned na range ndogo. Wanapiga ambush kwa msaada wa ATM na raia
Nilishasema Cha muhimu.kwao sio hayo ma.APC bali ni missile za short range,anti aircraft missiles na wakiweza wapate drones plus mbinu zingine za medani.

Kwenye hii vita sijaona msaada mkubwa wa hayo ma tanks zaidi ya kuwa mzigo tuu.
 
Wewe unaongea nadharia wakati mimi naongea ambacho kilifanyika juzi. Juzi shirika la International Atomic Energy Agency (IAEA) imefungua ofisi zake rasmi Tehran kwa ajili ya ukaguzi wa vinu vya nyuklia vya Iran kwa Masharti ya Iran kuondolewa vikwazo vyote vya kiuchumi ilivyowekewa na Marekani.

Mpaka sasa kilichobaki ni Marekani kwenda kusaini Mkataba. Waziri wa mambo ya nje wa Marekani ANTONY LINKEN amesema Next Week wanasaini mkataba mpya na Irani Joint Comprehensive Plan of Action (JCPOA).
huo mkataba hatujui vipengele na mashariti yake yapo vipi ila fikra zangu zinaniambia kabisa kutokana nahali inavyoendelea sasa kule ukraine kama unalosema litatokea basi nauhakika 80% mkataba huo utakuwa in favour of iran nautakuwa nimkataba mbovu kwa marekani kusaini kuliko ule trump alioupiga chini nabila shaka utakuja kuleta balaa baadae sababu iran anadhamira za wazi kabisa zakutengeneza silaha za nyuklia toka kitambo na hata marekani analijua hilo ...tusiongee sana wakati hatujui nikipi kitakuwa kwenye mkataba huo ngoja tusubiri
 
Ukraine ilishaanza kuwa na wahuni muda mrefu kuna battalion nilikuwa naisoma miaka iliyopita wale hawaongozwi hata na jeshi la serikali ila wanailinda mipaka ya Ukraine kule Donbass na wana spirit ya kupigana sana. Wale nao this time wamepewa silaha za EU wanazitumia, nadhani umewaona jamaa wana bendera za Nazi na skulls & bones. Wale wakiambiwa wajiunge jeshi la serikali wanakataa na hawataki kuwa chini ya mwongozo wa serikali
Azov batallion nimewaona pia.....
Kwa sasa wapo Mauripol nadhani, ila kambi yao ni miongoni vya facility za mwanzo Russia kuzilipua.
Angalau hawa walikuwa wanabagua wanaongea kirussia, ila kama ni kweli hawa watu kutoka middle East wameingia. Basi sasa swala la amani lisahaulike.
 
Aisee.. Dunia inaenda ingia kubaya. Tunaenda kwenye hali ngumu haijawahi tokea.
 
waliliona lkn ,imewabidi wakajipendekeza kwa maadui zao Iran,Syria ,Saudi Arabia ,maana hao hao malekani waliwawekeaga vikwazo vya kiuchumi,Sasa huu ndo muda wa hawa jamaa nao kupiga double standard [emoji1],hata hivyo haitatosha ,kum supless Russia kwenye volume ya mafuta aliyokuwa aki supply duniani.tushudie mafuta kupanda Bei zaidi !!
Mbambe ni mbambe tu, hawana namna ya kukataa, hadi venezuela amekubali naye, kwa hili likitekelezwa ipasavyo Putin atakuwa amepata pigo kubwa sana, japo na yeye amesema ikipigwa ban kwenye mafuta na yeye anazuia gesi kwa nchi za ulaya!!
 
BREAKING NEWS

Sasa ni Rasmi. Marekani imepiga marufuku uagizaji wa mafuta kutoka Marekani. Marekani iliagiza wastani wa mapipa Milioni 20 kila mwezi kwa mwaka 2021.View attachment 2143676
Tulia Basi unavyoleta taarifa,haya Marekani imepiga marufuku uingizaji wa mafuta kutoka wapi?Maana maelezo yako yameumana
 
Back
Top Bottom